FROM BANGI TO BABY ππ SEHEMU YA 19
Basi mpaka sa moja inaenda na Nusu Veda hajaja, Moyo juu juu itakuwa tu kaenda huko kwenye ma club, moyo lipu lipu muda wote kama nimemezaa kaa la moto hajabu sasa hata namba yake sina, makubwa ..
Nikatoka mpaka kwa mama, ile nyumba ipo hivii kuna vyumba vya nyuma na nyumba kubwa Ni nyumba nzuri tu ila sio ya kifahari ni nzurii alijitahidi sana kujenga tena nilivyojua ni nyumba yake aah nilimpa salute mie nilijua mluga luga tu wa mtaani huko ...
Sasa veda yeye anakaa nyumba ya uwani huku ila hakuna wapangaji wapo wao tu tena sikuwakuta hata wale mapacha ile siku ..
Basii nikaenda kwa mama nikamuomba namba ya Veda mwenyewe alishangaa kweli et sina namba ya Veda yaani angejua haya mapenzi yameota ota tu asinge hata hangaisha kichwa kutufikiria ..
Akanipa nikarudi ndani nikampigia hapo nahasiraa hatari, simu haikuita sana ikapokelewa "uko wapii??" Niliuliza kama kuna ugomvi
"Veroo!!!?" Mwenyewe alishangaa kuona simu yangu
"UKO WAPIII??" Hata sikutaka kumjibu nikakaza sauti zaidi ya mwanzo
"Nakuja...."
"Upo wapiii....ushaenda kwa hao wanawake zenu wenye makalio makubwa hao wavaa uchi si ndio, Yaani mie s....." kabla hata sijamaliza kuongea naona mlango unafunguliwa anaingia yeye mweeh yakanishuka nikakata simu kimya kimyaa nikaitupia huko nikageukia pengine mana nilikuwa nimelala kitandani ...
"Sikia Vero....usije hata siku moja ukanifananisha na D mimi sawa, Sie ni watu wawili ambao hatuwezi kuwa sawa hata iweje ..." akachukua taulo akatoka baada ya muda akaja kaoga kumbe alibeba na nguo akaenda kuvaa huko huko mmh mbona kazi ninayo hapa, nikawa namkata jicho la chini chini, alikuwa kavaa penzi juu wazi nyiee nikajikuta natamani hata anikumbatie tu mmh ila kauzu hatariii anajifanya hanioni et
"Unakula sa hivi au baadae" nikamuuliza nimenunaaa hee!!
"Sasa hivi" Akanijibu huku anaendelea kupaka mafuta
"Kuna sehem unaenda" nilimuuliza baada ya kuona yuupo bize kujipaka mafuta wakati usiku muda wa kulala na mafuta wapi nawapi jamani ..
Hata hakunijibu, nikatenga zangu chakula yaani kama mke mwemaaa ukiniona mmh, yameni kuta Vero mieee ..
Wakati wa kula mwenzangu nampiga mjicho wa chini chini, labda hata atauliza hiki chakula nani kapika kimyaa mmh wakati mwenzie nilimaliza ufundi wote kwenye msosi jamani kwa ajili yake duh ..
Nikatamani hadi kuuliza unaonaje chakula sema nikakosa pa kuanzia , Baada ya kula nikasafisha zangu nikaenda kuoga tena najiachia mbele yake kuvua lakini hana hata moja namie yaani kama tu sipo hivii ...
Nimerudi kuoga namkuta amevaa anatoa hee nikamuuliza "unaenda wapi"
"Nakuja??"
"Nimekuuliza unaenda wapii??" Akashusha pumzi halafu akanionesha mkononi kipisi cha midude yake na kibiritu kwahiyo anaenda kuvuta nikavichukua
"Hakuna kuvutia hayo madude yako humu ndani na sheria ya pili hakuna Kutoka usiku kwahiyo lala tuone kama utakufa usipo vuta.." nikalibinya binya lile li kipisi nikatupa kule
Akacheka kidogo yaani anapindisha tu mdomo sijui alicheka au alitabasam afuu hakunijibu kitu akarudi akavua tishet akabaki na pensi akapanda kitandani , Na me nikajisaula mtoto wa kike , nikachukua simu nikamtext Tinner shoga huku mie hata sitazamwi, akanambia embu acha haraka bwana nenda Taratibu halafu we mwanamke embu mtege hapoo, Mmh nikasema hata nimemtega mpaka basi akanambia embu acha utoto hakikisha huu usiku leo hauvuki kabla hujamaliza hilo duku duku shoo ...
Mmmh sasa nitamalizaje mmh, nikaeka simu pembeni nikalala pembeni yake najigusisha gusisha hata halishtuki nina hamu hata hanikumbatie tu lakini wapi, We nikasema huyu asinitanie nikainuka nikakaaa kitandani nimenuna hadi nalia
Akashtuka akanitazama halafu akinuka nae akakaa "Vero.....vipi upo sawa, Unaumwa.??"
"Ndioo.." nikajilegeza , akaanza kuhamanika
"Ngoja nikamwite mamaa, sijui jinsi ya kukusadia."
Anataka kutoka mbio nikamvuta nimejinunisha kweli
"Mtoto anatakaa..." nikaongea kwa sauti ya puani kabisa yaani nimelegeza sautii yakumchanganya akili
βMtotoβ¦ anataka nini Vero?β akauliza kwa sauti ya chini
Nikavuta pumzi, nikajifuta macho kwa nyuma ya mkono kama mtoto yaani nimelegea nimevuta midomo, halafu nikamwangalia Jicho la hubaa
"Anakutaka wewe, sa we umenuna tu si bora utufukuze" nikajibu kwa sauti ya kulalamika, nikigeuza uso pembeni, ndo nazidi kuvuta mdomo
Akacheka kidogo yaani nikasikia kabisa sauti yake anacheka ooh ka moyo kaka pata hadi ahueni ..
"Acha masihara hali uliyo nayo haitaki utani sawa, utakuja kupata tatizo mie nitajua utani ohoo shauri yako" et akajigeza akalala khaa, Huyu kaka vipi
"Kwani hujasikia Veda mtoto anataka"
"Anataka ninii, Et babyyy unataka nini mtoto wangu, baba anakupenda sana roho inaniuma mama yako alichotaka kukufanya naumia sana hata sijui nikueleweshe vipi mwanangu" akawa ameinama anaongea na Tumbo langu
"Kwahiyo unataka huyo mtoto anilaani huko, ili we uonekane mzuri mie mbaya sio" akanitazama kidogo amekaza macho
"Vero....aaah hata sijui nikuambie nini lakinii naomba tulale akili yangu haipo sawa kabisa" akataka kulala nikamkumbatia, Taratibu baada ya sec ndio nae akanikumbatia nikawa nimejilaza kwenye kifua
''Nahisi kuwa naamani sana nikiwa hapa"
"Muongo wewe..."
"Veda nakupenda sana lakini nilikuwa naogopa utaniumiza mie sitaki kuumia'"
"Kwanini usinipe nafasi, kwanini una muhukumu mtu unajua umeniumiza kiasi gani Vero kwa hizo act zako!!"
"Basi nisamehe Ba mpenzi wanguu!!!"
Akanikumbatia vizuri mweeeh akanambia "Nimekusamehe muda sana nimefurahi sana kuwa una mtoto wangu Vero" waoooh nikajilaza vizuri, akanibusu kwenye paji la uso daah sikuamini kama msala umeisha
"Anataka nini mtoto" akaniuliza huku ananitazama na mie nilikuwa namtazama kwa ukaribu sasa Veda wangu aloo bonge la mkaka yaani So mwaaaah, waooooh Mungu sante yale macho yake nilijikuta na sisimkaa na lile swali alivyoniuliza huku ananiangalia wadudu mbio mbioo
"Tangu umuweke hajawahi kukuona tena kwahiyo tumpe pumzi!!" Alicheka huyoo hata hakuuliza swali lingine bwana akanipa mdenda huoo nyiee kaka msweeety hatari
ITAENDELEA.....
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi


Maoni