FROM BANGI TO BABY ππ SEHEMU YA 16
Usiku wangu ulikuwa mzito sana, maneno ya D kusema kuwa Veda anatembea na wanawake wengi, niliyaamini kabisaaa Bila shakaa kwa maana Yeye tu hana mwonekano mzuri ametuna tuna hovyo anakuwa na wanawake kibao vilee haya Huyo Veda mkaka wa maana kajazia kila kiungo cha mwili kinavutia ataacha kushambuliwa na wanawake ??
Basi Wivuuu mpaka machozi yalikuwa yananitokaa, Kukakucha asubuhi bado kuwa najua natakiwa kufanya nini, Huku Veda huku D daah kichwa inaniuma kweli haya mambo yameibuka ghafla sanaaa.
Asubuhi wakati najiandaa kwenda kazini nikahisi kichefu chefu kikali, Hii hali leo ni kama siku ya nne yaani asubuhi ile natapika kweli ...
Tinner akanikuta kule nyuma nipo natapika akashangaa "We kwani unaumwa??"
"Nahisi homa inataka kunivamia, tangu juzi ikifika tu asubuhi natapika nyogo ila leo naona imezidi huwa natapika tu kidogo, ndo maana hata kukuambia nasahau"
"We Veroo.... Embu niangalie" nikageuza uso kumtazama akanitazama kwa makinii kama sec kadhaa hivi sijuii alikuwa anatafuta nini usoni kwangu ..
"Kwahiyo mpaka sas hujui nini kinakusumbua??"
"Halafu sisikii kuumwa chochote zaidi ya kutapita tu hivi asubuhi "
"Hahaha hivi wewe ni Daktariiiii au mwenzangu umefoji vyeti??" Sikuelewa hata swali lake mie nikainuka zang nikachukua maji ninawe
"Una mimba....." hee!!! Yaani nilimtazama et mie na mimbaa?? Afu nikacheka nikainuka hata sikumjali
"Sawa Doctor " nikamjibu kimasihala
"We mwehu kwahiyo huniamini eeh embu kojoa hapo" akachukua kopo nililokuwa nimeweka maji akayamwaga et nikojoe humo
Tukavutana hapo mpaka mwisho ikabidi nikojoe tu maana alivyonigandaa duh, nikakojoa akaweka kipimo mie nikaingiza zangu ndani kujiandaa nisije kuchelewa bure kazini ..
Wakati najiandaa yeye akaja "Hayaa ni D au Veda??" Akaniuliza huku ananipa kile kipimo sikuwa na plesha et nina mimba nikakipokea bila wasi wasi nikatazama aloo!!! Nikahisi mpaka tumbo limekata baada ya kuona mistari miwili
"Mimbaaa.!!!???" Nilishtuka sanaaa, sanaaa..
"Ndio, mie nimekuona tu uso umekushuka dalili zote za mimba"
"Sio kweli, Embu naomba unuchukulie kipimo kipya sitaki hiki" nikampa hela Tinner yaani nilikuwa nishavurugwa Tinner ametoka nje mie nikabaki nazunguka nyumba yotee plesha ipo juu juu yaani ghafla tu nilihisi joto kalii ..
Tinner akarudi akanipa nikaenda tena kuutafuta mkojo kwa tabu sanaa nikaupata kidogo nikapima daah nilijikuta nakaa kitandani mwili hauna nguvu kabisaa
"Ni Veda!!!" Ndio mwanaume peke aliekuja kwenye akili yangu kwa wakati huu
"Kwanini?? Je kama D??"
"Hapana Tinner, D tulifanya mara ya mwisho anaondoka tangu alipo rudi mie nayeye hatujakutana kama ni mimba basi ingekuuwa ya miezi minne huko " nilijibu kwa uchovu sanaa
"Kwahiyo tunafanyaje??"
"Natoa..."
"Niniii weweee??"
"Natoa Tinner, mie sitaki kuwa single mother sitaki kabisa "
"Khaa!!! Hivi kumbe Vero na akili waga huna eeh ?? Kwanini usiongee na baba mtoto kwanza ukamsikiliza "
"Atanambia nizae kwani yeye ndie atakae lea yeye si ataendelea na starehe zake huko wakati mie nahangaika "
"Aisee kwa hili mie sipo upande wako kabisaaaa yaani sipo kabisa upande wako , Embu mtafute Veda muongee"
"Natoa mimba tena sasa hivi hata kazini siendi ngoja nikatafute vidonge" nikainuka haraka kuondoka swala la kuanza kusumbuana na mwanaume kwa sasa hapana jamani Mungu atanisamehe
Nikaenda moja kwa moja duka la dawa, Nikafanikiwa kupata dawa za kutoa wakati narudi nyumbani kabla hata sijalifikia Geti nikashangaa Piki piki nyuma yangu imekuja kasi kweli yaani hapa na hapa ikasimama kwenye miguu yangu , Nilishtuka kidogo nianguke nikageuka kwa hasiraaa, Nikapigwa na butwaa kumuona Veda..
Nikabaki nimesimama sasa kama sanamu, moyo unapiga kwa nguvu nikajikuta sijiamini tena
"Kaa....!" Akanambia kwa sauti kavu halafu amenikazia macho
"Wapi??" Namie nikamjibu kwa kiburi
"Kaa kwenye piki piki tunatakiwa kuongea"
"Veda, , , sina cha kuongea nawewe tafadhali endelea na maisha yako"
"Umedhamilia kumuua huyo mtoto kwa ujinga wangu?? Upo serious unataka kumdhuru mwanangu??" Heee nyiee hehehe walai nilihisi mkojo unataka kutoka enheee nikasimaa vizuri
"Mimbaaa....?? Mimba gani??" Kwanza nikajitoa ufaham maana hizi habar zilikuwa za ghafla kwangu naza kushtukiza sana
"Kaa kwenye piki piki tukaongelee nyumbani, Vero siwezi kuruhusu kabisaa ufanye unachotaka kufanya na unajua kabisa nini naongea sasa unakaa kwenye piki piki au hukai"
"Vipi kama sitakaa"
"Aiseee Veroooo..... Usitake kujua rangu yangu nyingine tafadhali usifukue upande wangu wa pili Veroo usinipindue ukanilazimisha mamboo sawa " Nikameza matee maana sasa Aliongea kama mwanaume, nikashika vizuri kamfuko kangu ka dawa nikapanda kwenye piki piki, moyoni najua huyu ni Tinner tu huyu sijui imekuwaje hadi Veda kayapata tena haraka hivi maana hata mzoea hawana ...
ITAENDELEA....
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi


Maoni