πΊπππππ πππ ππππππ ππππ ππ πππππ ππππ πππ: 68 Akaniuliza
Unajua hata nikajikuta nacheka nikisema βππhivi dada Martha unachanganyikiwa?, mganga yupi, kivipi mbona hata sikuelewi?β
Dada Martha akaniuliza βmnawasiliana vizuri, na anakupa pesa?β
Nikasoma tu ule ujumbe na kuona asinichanganye. Yeye ndiye ameniunganisha na nduguye na sasa ananitaka kunichimba. Kama yeye ndiye kuwadi wake anataka amtafutie mwanamke mwingine afanye asinichanganye mimi. Nikawa ninajisemesha.
My Boss akanitumia ujumbe, nikasoma, ujumbe ulikuwa unasomeka hivi βThank you my sweet person, I feel your love.. I feel you. I thank you for loving me. Even now at this moment I am confessing to love you totoo.. Nakupenda sana.β
Nikavuta pumzi na kutuma ujumbe βUna maanisha haya?β
Pale pale ujumbe uliingia akisema βsijawahi kuwa hivi kabla, popote, kwa yeyote hata mimi nashangaa kwanini kwako. Totoo, kweli kabisa nimezama kwenye kina kirefu sana cha bahari ya huba lako nakupenda.β
Nikamjibu kwa kifupi βAsante.β
Aliniambia kwa upole βNajua sio rahisi pengine wewe kunipenda, najua pengine unatamani unifahamu vizuri. Na najua utasikia mengi kunihusu. Ila Totoo, unaweza kuamini haya mapenzi hata kama sio kuniamini mimi. Please nakuomba usiyaache haya mapenzi. Mimi usinipende sawa, ila vipi kuhusu hisia zetu. Mimi Nakupenda kweli kweli.β
Nikasoma na kusema ndani ya moyo wangu βNakupenda ila naogopa sana. Nakuogopa.β
Na ndiyo nikaandika βNakuogopa.β
Alinipigia simu baada ya kupokea huo ujumbe, nilipokea nikiwa nipo kama nalia vile. Akaniuliza βtotoo!, kuna nini kwani, niambie nimekukosea pengine bila kujua nikuombe msamaha.β
Nikasema kwa upole βHapana hujanikosea kabisa.β
Akavuta pumzi na kusema βumesikia chochote kunihusu?β
Nikashindwa kujibu akasema βI knew this, Ndeana ni mapema sana. Safari yetu ndiyo inaanza. Please nakuomba usiyape nafasi ndani ya moyo wako maneno unayosikia kuhusu mimi.
ππππππ ππππ ππ πππππ ππππ πππ: 69
Nimekuambia nakupenda wewe amini haya maneno. Ndeana niamini, mimi kwako nimefika nakupenda sana, kila kitu kitakuwa sawa muhimu uniamini. Siwezi kukuumiza mimi. Sijawahi kupenda Ndeana.
Unaweza usinielewe, ila wewe ni mwanamke wa kwanza kunifanya nijue maana ya kupenda. Na unavyojua moyo unapenda sehemu moja, mara moja na hiyo sehemu ni wewe na kwako.
Naomba upumzike, kesho tutaongea vizuri ofisini. Nakuomba asubuhi nikuone. Siwezi kulala vizuri leo kama wewe unakua hivi mapema yote hii.β
Simu ilikata, kisha baada ya muda mimi nikapanda kitandani, dada yangu aliingia chumbani na kusema βwewe, mbona hata hujabadilisha nguo. si ukaoge kwanza?β
Nikamtazama tu, dada akasema βKuna tatizo kwani?β
Nikamtazama tena na kusema βnimesikia kitu kuhusu Boss, nashindwa kujizuia dada. Kwasababu ninampenda sana.β
Dada yangu alikuja karibu yangu na kusema βKitu gani mdogo wangu?β
Nikamwambia, sijui nipoje ila mimi kumficha kitu dada hata cha ovyo siwezi kasoro hivi vya aibu najiongeza tu. Basi dada yangu akasema βlabda ni kweli, na sisi hatuwezi kujua kwasababu hatujalala naye si ndiyo. Na ndiyo maana nilikuambia usiwe na haraka.β
Nikasema βwanasema pia ana dharau na wanawake hana muda nao ila mbona mimi muda wote anataka kuwa na mimi na hata huku ananifuata.β
Dada alitabasamu, alisema βMdogo wangu kwenye mapenzi kuna watu wengi. Pengine umekutana na mwanaume mbaya sana ila kwako huwezi ona ubaya wake kwasababu labda anakupenda sana kweli. Binadamu upendo wake wa kweli ni mara moja tu.
Kwingine unaweza kupenda ila kawaida hisia zisiwe sawa na zile za mwanzo kwa mtu fulani. Usikurupuke, usiwe na hasira. Kama anakupenda atakuelezea mwenyewe. Mwanamke silaha yake ni utulivu, usikivu, na maombi. Sio kelele, kumfokea na kumtukana au kumuona hafai.
Pengine kwa wengine alikuwa hivyo kwako kakupenda au itakuwa mbaya zaidi. Ndiyo maana nilikuambia kuwa makini na sasa mdogo wangu kama unampenda ingia vitani kwa maombi. Sali sana, kama ni wako atabakia, kama sio wako ataaondoka au utaona ishara mbaya za kukufanya umuache.
ππππππ ππππ ππ πππππ ππππ πππ: 70
Na ukiona hizo ishara mbaya au akiondoka usianze kulia tena kwa maana binadamu Mungu hutufanyia wema bali sisi hungβangβania. Usilazimshe awe kama alivyokuwa kwingine. Cheza nafasi yako kama mwanamke mwenye maadili.
Omba Mungu, jitofautishe na wengine na hata ikiwa mbaya basi utayaacha hayo mahusiano bila kujali maumivu yako. Niahidi mdogo wangu, maneno ya watu utayasikiliza na kuyachumbua, niahidi utaomba Mungu na ndiye atakuwa silaha yako katika mahusiano yako.
Vita yako haitwakuwa juu ya yeyote bali utakabidhi kila kitu mikononi mwa Mungu na hutongβangβania kitu hata ikikubidi uache kazi uwe tayari.β
Nilimtazama dada na kutabasamu, mara ujumbe ukaingia dada alisema βni yeye huyo.β
Nikamtazama na kusema βni kweli, ni yeye umejuaje.β
Dada alisema βzamani wakati wewe mdogo bibi alipokuwa hai. Aliwahi niambia ukimuwaza mtu unayempenda na yeye anakupenda au ukimfikiria na yeye anakuwa anawaza au kukufikiria. Kwahiyo mnawazana kwasababu mnapendana. Anakupenda pia sawa mdogo wangu.β
Nikamtazama na kutabasamu kisha nikataka nisome ujumbe wa Boss ambaye yeye ni kizungu anakipenda mpaka na mimi namzoea tu na sio kama najua sana kizungu, ila kwa huyu naona kabisa google itahusika. Maana bila hivyo atanishinda kwa utamu wake wa maneno.
Nikasoma nikitabasamu βHave a restful night Ndeana wangu, dream of us honey pot, sending hugs, cuddles, love and kisses to warm up your night.. I love you more each day than the previous day, I love you too much, please relax na uvute pumzi. Najua utaumia na unaumia ila usisikilize watu, nisikilize mimi. Nakupenda sana sana wewe ndiyo huba langu la kwanza kabisa.β
Dada akasema βanasemaje?β
Nikampa simu, dada akasoma kisha akasema βmbona kizungu?β
Nikacheka nikisema βndiyo maana nimekupa najua tu huelewi.β
Dada akacheka akisema βndiyo kasemaje sasa.β
Nikamwambia anasema βuwe na usiku mwema Ndeana wangu. Natuma kumbato, upendo na mabusu kuufanya usiku wako uwe mzuri sana. Nakupenda sana na huko mbele si umeelewa.β
ππππππ ππππ ππ πππππ ππππ πππ: 71
Akanitazama na kusema βSio kila kitu unachosikia lazima upeleke kwa mwanaume wako moja kwa moja. Wakisema malaya na wewe unaenda kusema nimeambiwa wewe malaya. Hapana mdogo wangu, mwanamke ulivyo tu wewe ni silaha.
Fanya uchunguzi wako kwa hekima, tulia mengine yameze. Wanaume hawapendi malalamiko, lawama, kuonekana hawafai. Kibinadamu kuwasha hasira ni kawaida. Ila kwa mwanaume unayempenda jitahidi. Utasema mbona wao wanatuambia hivyo.
Ndiyo ni kweli, ila sio kosa lao. Uumbaji ndiyo umewafanya kuwa hivyo. Kwakuwa wao wanatakiwa kuheshimiwa hila kujali umri wake. Basi hata akikosa anataka aambiwe kwa lugha nzuri, vinginevyo hamtoelewana.
Kuna muda unawaza kama tumeonewa, ila ndiyo hali halisi. Na wengi hupoteza watu wanaowapenda kisa kelele, gubu, malalamiko na lawama. Na wao huwa hawapendi kushushiwa ujasiri na imani ndiyo maana wanashindwana.
Katika vitu vinahitaji sana hekima na moambi ni mahusiano na ndoa. Mdogo wangu, sasa upo vitani. Kama unampenda jiweke karibu na Mungu yeye atajua akutunzie au akuondolee. Na akiwa akikuondolea ukingβangβania hasara kwako.β
Nikasema kwa upole βdada nakuahidi kufuata ushauri wako. Bora hata upo dada una akili. Tayari niliwaka ila maneno yako yamenifanya nitulie.
Mimi sio wapekee sana, sina umaalumu huo ila pengine ndiyo fungu langu nimpe nafasi. Na kama sio nakuahidi sitangβangβana. Nimefurahi sana dada na nitaanza leo leo kusali. Haya vipi na wewe na shemeji?β
Akanitazama na kusema βShemeji yako anataka nimzalie. Nami sipo tayari kuzaa na hajanioa. Nimemwambia walau aje nyumbani afuate taratibu anaona kama simpendi ninampangia.
Sitalazimisha mdogo wangu pengine ndiyo majibu yangu kwa maombi ninayoomba. Sasa akinitafuta namjibu bila kelele na asiponitafuta na mimi nakua mtulivu. Ndiyo mapenzi. Ila huo ndiyo msimamo wangu.β
Nikamtazama na kumkumbatia, nikisema βutakuwa sawa dada. Na yeye atakuelewa tu.β
Dada alisema βNinaamini hivyo mdogo wangu,
ππππππ ππππ ππ πππππ ππππ πππ: 72
Siku hii iliisha hivi kwa mtindo huu, dada yangu alinitoa wasiwasi. Ingawaje kitanda nilikuwa nakiona kikubwa kila nikikumbuka raha za ndani ya gari, muhogo wake ulioshiba na raha zake. Nyie mimi nampenda ila kumuonesha tu ndiyo kipengele. Ila ninampenda huyu kijana anahitaji maombi yangu tu. Pengine atanipenda zaidi au ataniacha. Ila mimi tayari nimefika. Akinigusa kama asiache, akinipigia ile sauti kama aongee tu mpaka asubuhi. I love my Boss. Ila siwezi kumuonesha, namuogopa, naona aibu, na sina hakika na huba hili.
Nikiwa kitandani nilipata muda wa kuongea na Mungu. Nilimwambia Mungu βUnanijua vizuri, sio mkamilifu ila nataka kuishi ndani ya kusudi lako. Sitaki kukosa sana Mungu wako. Ni bora nikose yote ila sio kukosa upendo, huruma, na hekima zako Mungu.
Naomba nisaidie kujua huyu mwanaume kama yupo hapa kwaajili yangu. Na kama sio kwaajili yangu basi Mungu muondoe mbali na maisha yangu. Na kama ndiye Mungu rekebisha tabia zake, nyoosha njia zake.
Awe mwanaume atakayefanya niishi ndani ya kusudi lako wewe mpaka mwisho wa maisha yangu. Nakuamini, nakupenda na nakutegemea Mungu wangu. Amina.β Kisha nikalala nikiamini Mungu atafanya heri zake.
Kesho yake asubuhi niliwahi kazini kama kawaida. Niliendelea na kazi baada ya kukutana na meneja. Kazi kubwa ilikuwa ni kuandaa ukumbi wa mkutano huo na kuutengeneza muonekano mzuri sana.
Sikuwa nimeona ujumbe wa boss siku hiyo kama ilivyo kawaida na ukifika kazini tena simu haziruhusiwi. Basi nikawa nafanya kazi ninatazama huku na kule labda nitamuona. Sikumuona. Nakumbuka Joan aliniuliza βunamsubiri mtu?β
Nikacheka na kusema βatoke wapi tena, hapana nipp tu nawaza namna hii kazi itakavyofanania.β
Basi tukaendelea na kazi. Ilifika mida ya saa nne hivi ndiyo tunatakiwa kunywa chai. Kuna dada alikuja na aliniambia βsamahani, unaitwa na meneja.β
Nikamwambia kwa upole βsawa kipenzi.β
Kisha nikamwambia Joan, βKipenzi nahisi kuna maelekezo, kwa meneja ameniita.β
ππππππ ππππ ππ πππππ ππππ πππ: 73
Akaniambia βsawa kipenzi, utanikuta ile sehemu tumekula jana. Na hapa kwa sisi tumemaliza. Watu wa mapambo watamalizia kisha mwenzetu ndiyo atasimamia sisi tutawahi kutoka leo ili tukajiandae na kukusanya nguvu ya kazi.β
Nikasema βwaao kumbe ndiyo hivyo?β
Akaniambia βNdiyo kipenzi, Meneja alikuja hapa muda fulani ulifuata vitu huko juu ndiyo akatoa maelekezo. Kasisitiza sana usafi pengine ndiyo maagizo hayo anaenda kukupa.β
Nikasema βbasi sawa nisubiri tutaondoka wote.β
Akaniambia kwa upole βsawa kipenzi.β
Basi mimi huyo mpaka kwa meneja. Nilipofika tu, alinitazama akatabasamu na kusema βkuna simu yako.β
Nikamuuliza βinatoka wapi meneja.β
Akasema βBoss anakupigia.β
Nikashtuka βBoss!!β
Akaniambia βpokea, ipo hewani.β
Nikapokea. Niliposema tu βHello Boss.β
Kwa sauti ya uchovu sana, alisema βTotoo, njoo ofisini tafadhali ni muhimu.β
Nikaitikia kwa nidhamu βsawa boss nakuja.β
Nikarudisha simu. Wakati natoka Meneja aliniambia βNdeana, anakupenda.β
Nikamtazama na kisha nikatoka bila kusema kitu, kwa maana sikuwa nataka kuongea zaidi.
Taratibu nilitembea, nilipofika nje ya mlango wake. Nilivuta pumzi ndefu na kukumbuka maneno ya dada yangu ya kuwa nisimlaumu, niwe mpole tu. Yeye mwanaume atajua namna ya kuongea na mimi na kuniweka sawa.
Nikabisha hodi. Nilisikia sauti ikisema kwa upole βIngia.β
Basi nikaingia. Alikuwa amelaza kichwa juu ya meza. Nikaita βBoss!!β
Haraka akainuka na kusema βNdeana!!, Ndeana umekuja!!β
Nikatabasamu. Akainuka na kuja kunipokea kisha akalock mlango wake. Alinishika mkono na safari hii alinikalisha kwenye kochi ambalo lipo ndani ya ofisi yake. Kisha aliniuliza βumenikasirikia Ndeana?β
Nikatabasamu na kumuuliza βkwanini sasa?β
Akanitazama kisha akaja mbele yangu, akapiga magoti na nikamwambia βunafanya nini sasa?β
Akanitazama kwa huruma akisema βusiondoke Ndeana, usiniache nakuomba sana. Ndeana nakupenda kutoka ndani ya moyo wangu. Siwezi kumpenda mwanamke mwingine ninavyokupenda wewe na wala sijawahi kupenda namna hii.
ππππππ ππππ ππ πππππ ππππ πππ: 74
Sikia sitaki kujua nani amekuambia kuhusu mimi kwa maana nilikuwa najua ipo siku utajua. Nimefurahi umejua mapema kwa maana haitakusumbua mbele. Ila nisikie, ni kweli, ni kweli mimi nimekuwa na wanawake wengi naona aibu hata kusema.
Ila wao ndiyo wananitaka mimi Ndeana. Hakuna mwanamke nimewahi kumpenda na hata nikiwaambia ukweli hawaelewi. Pamoja na kuwa nao, sijui kama unaelewa. Your my First love, wewe ndiyo upendo wangu wangu wa kwanza.
Ninavyojisikia na kujihisi kwako ni hisia ngeni, nashangaa sana, sijui umenifanya nini, kaa kama kuna kitu umekifanya fanya tena na tena maana ni raha sana kukupenda wewe. Nasikia amani kukupenda, nasikia raha, nasikia furaha.
Wewe ni mzuri kuliko wote, nakuona wa pekee sana na unatembea na hisia zangu. Nipe adhabu yoyote ila sio kuondoka. Ninakupenda sana Ndeana.
My sweet person, totoo Ninakupenda Wallah. Your the most amazing person I've ever met...You have been the most precious and wonderful gift of my life and I cannot thank God enough for blessing me with you... I know I don't say it but everything you do for me makes me fall for you again and again, when I am around you every moment feels so beautiful because you make me feel loved and wanted.
All your hugs, kisses and touches fills new life into my soul.. Thank you for being an amazing, kind, loving and caring person to me, Barikiwa tu siku zote mpenzi wangu, nasubiri hata siku nisikie neno Nakupenda from you, Nakupenda mno Ndeana, mno yaani, Nakupenda Ndeana wangu I love you so very much my sweet person
(Wewe ni mtu pekee nimewahi kukutana naye, umekua mtu wa thamani sana na zawadi ya kushangaza katika maisha yangu. Nashindwa hata kumshukuru Mungu kwa kunibariki mimi kuwa na wewe. Najua, sisemi hili ila kila kitu unachofanya kwangu kinanifanya nikupende tena na tena.
Nikiwa na wewe mara zote najisikia vizuri kwasababu unanifanya nijisikie kupendwa na kuhitajika. Kumbato lako, mabusu, mguso yanajaza maisha mapya ndani ya roho yangu. Asante kwa kuwa mtu mzuri sana kwangu, kuwa mwema, kunipenda na kunijali.)
ππππππ ππππ ππ πππππ ππππ πππ: 75
Nilikuwa namtazama vile anajisikia huzuni, na kunishika kwa hisia. Unajua hata alisema akitaka kulia βNdeana utasikia mengi kunihusu, ila wakati unayapa sikio unaweza ukayapa sikio la moyo wako na akili zako mapenzi yangu. Usiniache Ndeana, usiondoke kwasababu siwezi kuishi bila wewe. Love is a beutiful thing, i currently admit.β
Mwanaume huyu alianza kutoka na machozi akilia nisiondoke, nisimuache, ananipenda na amekiri ukweli mbele yangu ili nisiumie na watu watakayosema. Na nikajikuta namuonea huruma, nikajikuta namkumbatia huku wote tukilia. Mapenzi nyie hata ukilia husikii maumivu, haswa ukilia kwa furaha. Akanitoa mwilini na kusema βhutonifokea?, hutonisema?, hutoniuliza swali?β
Nikatikisa tu kichwa kukataa kuwa sitafanya lolote kwa maana tayari kasema yote. Ooh, ninatamani kama ningekuwa nimeyachukua mkanda wa video matukio yote muone nilivyokuwa nadeka hapa nakubembelezwa.
Tulikumbatiana tena na ubaya sisi wote tunapenda mabusu, ila zaidi mwenzangu ugonjwa wake kwangu ni mapenzi, ukimbusu tu anashindwa kujizuia kabisa, unajua kilichofuata pale tunapigana busu huku tunalia na kubembelezana.
Mimi na My handsome boss, Mwanaume wangu mzuri, hata yale maneno ya dada yangu yalinipotea kichwani, nikajikuta tena kwa mara ya tatu, kwenye kochi, baada ya hapo nikabebwa juu ya meza na hata yeye mwenyewe akiwa amesimama alinibeba na kunipa kitu roho inapenda nikiwa nimebebwa nami mikono yangu ikiwa imemkumbatia kwa shingo. Tulipokuwa hoi, tukajiweka sawa.
Tukatazamana na kucheka. Mimi nimeanza kuwa mlevi wa penzi la Boss wangu. Popote pale sisi sawa tu. Alitabasamu na kusema βTotoo, eti kukupenda ni haramu.β
Nikamtazama na kutabasamu nikisema βni haramu sana dini hairuhusu.β
Akacheka na kusema βHata penzi lako pia haramu eenh!!β
Nikacheka tena na kusema βni haramu dini hairuhusu.β
Akanivuta na kunikumbatia akisema βafadhali waniue, ila haramu vitamu.β
Tukacheka. Akanibusu nami nikasema βumeanza tena!!β
Soma muendelezo kwa sh 1000
Njoo WhatsApp 0743433005
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi

Maoni