UTANIITA SHEMEJI. SEHEMU YA 18
Basi bwana wiki kadhaa zilipita maandalizi yakaanza kufanyika na mwisho kila kitu kikawa tayari nikaanza kazi rasmi๐ฅฐ.
Kutokana na mazingira tuliyokuwepo ililazimika duka liwe kisasa zaidi, vitu vilivyowekewa kwaajili ya biashara vilikuwa vya kishua kishua na sio unga wa kupima sijui mafuta ya kupima au vitu vidogo vidogo.
Kiufupi ilikuwa ni min Market, ili kuboreshwa zaidi akaweka na huduma zote za kifedha kwa hiyo pakawa mwaaa๐ ๐.
Mtoto wa bukoba nikashika usukani ๐ Mungu huwa hamnyimi mtu vyote bhna , kaninyima elimu ila nyota ya biashara kaiwasha inang'aa mwee๐.
Basi biashara ilianza kwa kishindo ,wateja wakamiminika kutoka kila pande, yule kijana wakununua mayai kila wiki ndo akapata njia ya kutengeza ukaribu vilivyo๐.
Japo haikuwa rahisi ila kutokana na kuja kila siku mdogo mdogo tukaanza kuwa tunapiga story hadi ikafikia kipindi tukazoeana na kuwa marafiki.๐ฅฒ
Daria alishangaa sana imekuwaje Samuel kuwa karibu na mimi kiasi kile ila hali haijawahi kutokea kwa binti yoyote wa pale mtaani , nikawa namwambia sijui๐โโ๏ธ
Eeeh sasa najua nini mimi ๐ฅฒ maana mazoea yenyewe yalivyoanza yalianza kimasiala tu kwanza sikuwahi kupenda kuwa karibu nae .๐
Ni vile tu Mungu ana mipango na njia zake ๐, basi bwana ukaribu wangu na Samuel ulikuwa haushikiki yaani ninavyo sema haushikiki namaanisha ๐ฅฒ
Mtu ulikuwa ukituangalia kwa mbali unahisi au kuona sisi ni wapenzi ukisogea karibu unatuona kama mabest ๐ ukigeuka na kutuangalia kiupande upande tunaonekana kama tuna crashiana vile ๐.
Yaani tulikuwa kimvurugano tu wala hakuna alieelewa kuwa tuko katika kundi gani ๐ฅฒ, na ukiniuliza mimi namuona je nitakwambia namuona kama mshikaji tu.๐
Eeeh huo ndio ukweli jamaa namuona kama mshikaji wala hakuna hata siku moja niliyowahi kumuona kama mwanaume au kufikilia lolote yenye hisia za mpenzi.
Kwa hiyo msije kusema oh kutakuwa kunakitu maana haiwezekani watu wawahisi kuwa wapenzi ,akuuu kwenye mapenzi nae sipoo๐ โโ๏ธ.
Na sio kwamba nikimtaka siwezi kumpata naweza sana ila sipoo na staki ๐ฅฒ mpoo? , haya bwana maisha yaliendelea miezi mitatu ikapita tukiwa bado lelele๐.
Bwana weee nakumbuka siku hiyo alitoka job kama kawaida akaja dukani mimi mda huo niko nacheza game la nyoka kwenye kiswaswadu cha boss ambacho alinipa kwaajili ya kazi.
Basi akawa amepita bila kunisalimia na kuingia ndani , kwakua nilikuwa bize na simu sikuweza kumuona ila baada ya kusikia geti lao likifunguliwa nikachomoka chap na kwenda kuchungulia.
Kupiga jicho hivi naona gari lake ndo kinaishia ,nikaona ooooh huyu mbwa kapita bila kunisalimia leo fresh ๐, nilivuta domo likafika kuleeeโน๏ธ .
Kwa hasira nikarudi na kukaa game halikuchezeka tena ,nikabaki nasubiri aje nimsuuze vizuri ๐.
Ajabu hadi inafika mda wa kufunga hajaja , nikataka kumtumia meseji ila nikaona hapana nitakuwa najipendekeza ngoja nikaze fuvu๐.
Basi kinyonge nikafunga na kuingia ndani , kwakua ilikuwa ni siku ambayo mama huwa anarudi na chakula niliingia ndani tu na kuingia bafuni nakuoga chap kisha nikaungana na wengine tayari kwa kupata chakula.
Na baada ya kula niliweka mazingira sawa nikaaga na kwenda chumbani kulala,uliza nililala ๐? Yaani kila ninavyo jitahidi kutuliza akili ili nilale wapi usingizi unagoma kuja.
Moyo nilihisi kama umeingia uzito ambao hata sikujua umetoka wapi๐, niliendelea kujitahidi kuusaka usingizi mwisho nikaona eeeh siwezi kujiua .
Nikaamka na kutoka kibalazani labda naweza kumuona ,lakini hakutoka wala hata taa ya chumba chake haikuwa on ๐ swali likabaki kichwani .
Huyu mtu kalala au kaamua leo asiongee na mimi ๐ค na kama ni kweli kwanini afanye hivyo ๐ค , maswali hayo hayakuwa na majibu , basi kinyonge nikarudi kitandani na kuulazimisha usingizi uliogoma kuja.
Kama Mungu zilipita dakika tano tu simu yangu ikaita kuangalia mpigaji ni Alvin ๐ฅฒ afadhali rafiki yangu wa milele kanikumbuka ๐ฅฒ.
Na huyu ndo rafiki sasa sio hili gume gume linalojifanya dunia yote yake ๐ na ole wake kesho anisemeshe ๐ yaani nitamchamba hata amani shwain yeye ๐๐.
Basi nilipokea simu ya Alvin na kuanza kupiga story, unajua bhna moja kati ya watu wanaojua kunifanya nifurahi hata nikiwa na huzuni au hasira kali ni Alvin.
Aaah huyu kiumbe nampa salute ๐ ananijua na kunijulia hadi anakera๐ yaani dakika moja tu ilitosha kunisahaulisha yote yaliyokuwa yakininyima raha na kunifanya niwe mchangamfu ๐๐
Story na umbea wa hapa na pale ulienda hadi saa Saba kasoro ndo tukaagana na kila mmoka akalala ๐ด๐ด.
Kesho asubuhi na mapema niliamka na kufanya majukumu yangu ya kila siku , nilivyo maliza nikajiweka safi ,kisha nikakaa zangu sebleni na kuangalia tv.
Unaweza kuuliza leo siingii kazini? Jibu ni kwamba naingia ila navuta mda ili Samuel aondoke maana sikutaka kumuona kabisa so nitakaa na akiondoka tu nitaenda kufungua.
Kweli dakika zilisogea lisaa likapita hatmae mda wake wa kwenda kazin ulifika akaondoka ,na baada ya kuondoka tu nikajiinua na kwenda kufungua.
ITAENDELEA
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi

Maoni