ILA BOSS ANAJUA KUPELEKA MOTO 21------25 SEASON 2
SEHEMU YA 21
Nelly Nelly, niligeuka nyuma baada ya kuitwa alikuwa ni rafiki yangu Neema, Abeh umeniita kwa kunishtua una shida gani? Nilimuuliza. Nilisikia unatafuta tenda ya kazi? Ndio ila nishapata tayari nilimjibu.
Oh sawa nikajua bado dada yangu anafanya usafi kwenye hotel moja hivi sasa kwa siku ya kesho amepatwa na dharula kidogo hatakuwepo kazini ungeenda kushika nafasi yake then atakupa elfu arobaini... Ili tu bosi wake asijue kama hayupo kazini
Enhe kama ni hivyo nimekubali nipate hela ya kula tu kwa siku mbili hizi maana nimefulia hatari.
Basi shika namba yake hii wasiliana nae ili akupe maelekezo utakutana na mtu huko, sawa Neema akanipa namba ya dada yake nilivyotulia nikampigia simu akanipatia maelekezo muda wa masomo ulivyoisha nikarudi nyumbani kesho yake siku ya ijumaa sikuenda chuo nikaenda huko kwenye kazi..
Nilimkuta dada yake na Neema ananisubiri alinielekeza jinsi ya kufanya usafi chumba hadi chumba na kupanga vitu kisha akaondoka nikabaki mimi na wafanyakazi wengine.....
Mungu sio athumani si ndio napita kwenye korido ili niingie kwenye chumba kimoja wapo nikadeki si ndipo nakutana na mpenzi wake na Glavin anatoka kwenye chumba kimoja wapo wote tulishtuka baada
ya kuonana
Mara namuona na mkufunzi nae anatoka humo bahati nzuri mimi hanifahamu hapo hapo nikawapita nikawa nasogea mbele..
Baby vipi mbona kama umesimama hapo? Loreen aliulizwa, hapana nilidhani nimeacha simu ndani
kumbe ipo kwenye pochi
...
Hao wakaondoka zao mhh au nimemfananisha lakini ni yeye kabisa sasa wametoka kufanya nini humu ina maana anamsaliti kaka Glavin ila wanawake sie mbona tuna mambo mengi sana anakosa nini kwa kaka Glavin au hamridhishi kitandani mh mdomo koma mie hayanihusu nifanye kilichonileta... Basi niliendelea kufanya usafi hadi nilipomaliza nikapewa changu nikaona hapa ngoja tu niende kwenye kibarua changu sasa maana muda ushaenda saa sita hii naenda kusoma nini?....
Nilipanda zangu daladala hadi bunju nikaelekea nyumbani kwa Glavin... Kama kawaida mlinzi alinipa funguo nikaingia ndani nikaanza kufanya usafi.
Mara kaka Glavin akawa amerudi toka kazini akanikuta nipo nafanya usafi..
Oh kumbe umekuja nilijua bado upo chuo? Kaka Glavin aliongea, hapana leo sikuenda chuo kuna sehemu nilienda kufanya kazi.
Why hujaenda chuo hauna hela ya mahitaji ndio maana una overdose kazi Nelly Glavin aliongea kwa hisia.
Ndio kaka ila sitarudia tena kudodge chuo ni leo tu nilikuwa natafuta hela ya kula..
ILA BOSS ANAJUA KUPELEKA MOTO
SEHEMU YA 22
Nelly usifanye hivyo siku nyingine mimi ni kama kaka yako una shida yoyote ile nimesema uniambie kwani mimi hela ya kula inanishinda jamani ok isiwe shida, Kaka Glavin aliingiza mkono mfukoni akatoa wallet yake akatoa noti za elfu kumi tano jumla elfu hamsini akanipatia...
Shika hii utanunua chakula ukiwa na shida yoyote niambie nitakusaidia Sawa ila sio kukosa vipindi darasani..
Sawa kaka asante niliondoka nikaenda kuendelea na usafi... Kaka Glavin analalamika mimi kukosa vipindi huku nyuma demu wake anakosa vipindi anaenda kugeuzwa laiti angejua nahisi angeumia sana ila naomba Mungu amuumbue tu huyu Loreen mimi sitaki kuingilia mapenzi ya watu nimsemee mwisho wa siku waendelee kuwa wote aibu si itakuwa kwangu.
Nilimaliza kazi zangu nikampikia kabisa kama kawaida alinifosi nile kabisa ndipo niondoke nyumbani
.
Kaka leo Loreen haji niliuliza swali kimitego . Kasema haji anajisikia vibaya Leo, anhaa ndio maana nimeona kimya hadi sasa hajaja....
Nilimaliza kula nikaondoka zangu, kesho kwa kuwa jumamosi nilienda tu asubuhi na mapema
kufanya usafi
Nikiwa nafanya usafi taratibu nilisikia honi nje ya gari baada ya dakika mbili aliingia mpenzi wake na Glavin... Sijui unaitwa nani ila naomba niongee na wewe kidogo....
Naitwa Nelly ongea nakusikia niko bize nataka nifanye usafi haraka nataka niondoke....
Ok naomba ulichokiona siku ya jana pale ukiache pale pale usije ukamwambia mtu yoyote yule nitakufanyia kitu kibaya...... Nilijikuta nacheka huo mkwara ninaopigwa na kimtu tena chembamba kama mti wa mnazi.. wewe huyo wa kunifanyia mimi kitu kibaya hapo umenoa bidada kingine mimi sinaga umbea wa kijinga hivyo siku yako ikifika tena wahenga wanasemaga za mwizi ni arobaini sasa kama jana nilikuona mimi ile ni thelathini arobaini coming soon .
Mtu unapendwa, unafanyiwa kila kitu na bado unachepuka na mkufunzi wako au kichwani ni kichwa boksi kwamba? Narudia nimekuja hapa kufanya kazi ili nitimize malengo yangu kuwa na amani sawa. Niliondoka sebuleni nikaelekea jikoni ili nipike chakula kabisa ndipo niondoke mdada wa watu alikuwa amesimama asijue cha kufanya.
Mtu unapendwa na bado unaruka ruka kama ndege mxieeew.
Glavin alirudi mapema akawa yupo chumbani na msaliti wake, mimi nikawa napika taratibu na hivi kesho ni weekend sikuwa na wasiwasi hadi mida ya saa mbili nilikuwa nimeshamaliza kupika.
Nikawa nataka kuondoka nikakutana na Glavin sebuleni, kaka mimi naenda. Why unaondoka bila kula hebu andaa chakula pale tule pamoja then nikupeleke nyumbani sasa hivi ushakuwa usiku
...
Itaendelea
ILA BOSS ANAJUA KUPELEKA MOTO
SEHEMU YA 23
Kaka usijali nitaenda kula nyumbani maana niliona huyu anataka kuniletea msala hapa na hivi huyo kisirani wake yupo.....
No huwezi kuondoka bila ya kula mdogo wangu fanya nilichokuambia... Sawa kaka ilibidi tu nikubali kishingo upande. Niliandaa chakula
kaka Glavin akaenda kumuita huyo mpenzi wake aje kula, dada alikuja ila alikuwa anaona aibu sana.. Loreen vipi mbona kama haupo sawa? Glavin
alimuuliza
I'm okay honey nimechoka tu na pilika pilika za siku nzima nataka nikalale
kwanza.. ………
Sawa pole mimi nitampeleka Nelly nyumbani kwao.. Kwani kuna ulazima wa kumpeleka si uite hata bolt tu honey..... Loreen aliongea huku akiwa na hasira .
Punguza kisirani sweet ninavyomjali Glad basi na huyu ni sehemu ya familia kuwa na amani...
Sawa mimi naenda kulala Loreen alinawa akaenda chumbani.
Tulimaliza kula mimi nikatoa vyombo nikasafisha kabisa nikatoka nje nikawa namsubiri Glavin aje anipeleke nyumbani .. Alitoka tukaingia kwenye gari safari ya kuelekea ubungo ikaanza... Tulikuwa kimya kwenye gari maana sikuwa hata na story nae alinifikisha hadi napoishi..
Hapa ndio napokaa kaka karibu ndani unywe hata maji uweke baraka niliongea huku nikishuka kwenye gari
... Glavin hakukataa wito wangu alishuka akaingia ndani.
Alikaa kwenye kiti pembeni ambacho nilichongesha na meza ili niwe najisomeaga usiku , ndani nilikuwa na kitanda zulia, feni, friji na tuvyombo kidogo sikuwa na mambo mengi. Nilifungua friji nikampa maji ya kunywa..
Glavin alikunywa kidogo kisha akaniaga
nilimsindikiza hadi nje
akaondoka zake mimi
nikarudi ndani kulala
niamke usiku
nijisomee...
Niliamka saa kumi
kujisomea hadi saa moja kisha nikarudi kulala zangu....
Niliamka mida ya saa nne nikawa nafanya usafi ndani kwangu nikawa nimeenda kutafuta vitafunwa ile narudi
nikakuta nje gari imepaki ilikuwa sio geni kwangu kumbe alikuwa ni
Loreen amekuja...
Nilimkuta amekaa kibarazani baada ya kuniulizia kwa wapangaji wenzangu... ILA BOSS ANAJUA KUPELEKA MOTO
SEHEMU YA 24
Karibu ndani nilimkaribisha, aliingia ndani kwangu hivyo alivyokuwa anapaangalia tu kama kaona uchafu..
Umepajuaje napoishi? Hilo ndio lilikuwa swali la kwanza kumuuliza.
Jana nilimtuma mtu awafuatilie mnapoenda na
Glavin.
Bado huna imani na mimi si nishasema ni kama kaka yangu au.....
Sio hicho kilichonileta Nelly niambie unataka kiasi gani ukae mbali na Glavin. Ili tu usije ukamwambia kuhusu ulichokiona..
My dear kuwa na amani mimi nilishasahau hayo hayanihusu mimi huu ni muda wa wewe kubadilika Loreen naweza mimi nisimwambie akaja kugundua yeye mwenyewe naomba uondoke ndani kwangu...
Sawa kama umeghairi mimi kukupa ofa ila nikuambie tu nampenda sana Glavin nimetoka nae mbali sitapenda kuona tunaachana kirahisi hivyo kama umeamua kunifichia hiyo siri nashukuru sana...
Sawa ..... Nilimjibu kifupi akatoka nje akaondoka zake kuna watu wana mambo ya ajabu sana kuchiti uchiti wewe uanze kusumbua
watu wengine
Kashaniharibia siku tayari ananifuatilia hadi nimeanza kuogopa. Asiponielewa akizidi kunifuatilia nitamwambia Glad.
Kesho yake mida ya asubuhi jumatatu nikiwa nimekaa mwenyewe mara nikashangaa mtu ananishika bega.Wewe ndio Nelly , Ndio nilijibu huku moyoni nina hofu. Nimepata habari zako kuwa unataka umsemee Loreen kwa kaka yake kuwa umetuona tuko pamoja hotelini ....
Nilibaki nimeshangaa binti huyu kwa kubadilisha maneno kutoka kwenye mpenzi hadi kaka tena....
Unashangaa nini mimi nikuombe tu kitu hapa ni chuo kila mtu ana maisha yake usilete mambo ya o level hapa, umebakisha miezi mitatu umalize chuo jitahidi umalize kwa amani fanya mambo yanayokuhusu mengine achana nayo sawa..
Sawa niliitikia hivyo tu mkufunzi akaondoka zake nilibaki nimesimama nimeduwaa tu alikuja kunishtua Glad we vipi mbona umesimama muda hapo unawaza nini? Hamna kitu nimesahau calculator nyumbani ndio nakumbuka hapa .. oh usijali tumia hata yangu shika hii hapa siku nyingine uwe makini..
Asante sana, kumbe hata sikusahau wala nini niliamua nibadilishe maada tu ili asijue kitu chochote kile.
Vipindi vilipoisha nilimfuata Loreen nilimkuta amekaa na rafiki yake nikamuomba rafiki yake atupishe kidogo nina mazungumzo naye kidogo...
Naona Loreen unavuka mipaka sasa naomba kwenye ujinga wako usiniingize sijui unanielewa sitaki uniweke kwenye wakati mgumu sinaga mambo ya kufuatilia ya watu basi naomba uache kunifuatilia.....
ILA BOSS ANAJUA KUPELEKA MOTO
SEHEMU YA 25
Ndio nini unaongea bila kituo halafu kwa sauti unataka watu wasikie nilikuwa nakupa tu onyo usije ukamwambia Glavin ni hicho tu....
Ndio uniwekee mikwala kwa lecture kisa na mkasa nishindwe kusoma vizuri hebu naomba uniache tafadhali wewe ndio utasababisha ujulikane mwisho Glad aone nina ukaribu na wewe aanze kuniuliza maswali sidhani kama tutaluongelea hili suala tena naomba yaishie hapa sijui unanielewa....
Ndio nimekuelewa, tunza ahadi yangu tu.
Nilimuangalia Loreen kisha nikaondoka zangu .
Nikaenda kazini kwangu kufanya usafi, nikawa nasafisha chumbani kwa kaka Glavin nikakuta nguo chafu kwenye dustbin ina maana huyu Loreen anashindwa kufua nguo za bwana wake hawa mabinti wa kuwalea kimjini mjini kazi tupu...... Nilizichukua zile nguo nikaenda kuzifua nje mara kaka Glavin akawa amerudi akanikuta nipo namalizia kufua na nguo zilikuwa nyingi hadi boksa
duh
Shikamoo kaka, nilimsalimia marahaba umekuja muda mrefu aliniuliza.
Hapana sio sana, nilimjibu huku naendelea kufua, Mbona umepata shida kufua na mkono wakati mashine ya kufulia ipo........ Sijui jinsi ya kutumia niliogopa nitaharibu ok basi ukimaliza kufua hapo njoo nikuelekeze jinsi ya kutumia ili siku nyingine usipate tabu...... Sawa kaka.
Glavin aliingia ndani nilivyomaliza nikaenda kumwambia anielekeze jinsi ya kutumia mashine, alikuwa amelala aliinuka akaja nje alikuwa amevaa bukta tu juu hajavaa shati nikaomba Mungu asije tu kutokea kivuruge wake
atukute hivi patachimbika.. mbona
Alinielekeza kisha akarudi
kulala mimi nikaenda kupika, nilimaliza nikaenda kumuita ili ale nilimuaga akaniambia nile ndio niondoke...
Unajua kupika umesomea wapi mapishi? Kaka Glavin aliniuliza, hapana ni nyumbani tu marehemu mama yangu alikuwa
akipika na namuangalia... mimi
Oh very sorry huna
mama kumbe? Ndio
nilimjibu
Dah unajua maisha bila ya wazazi au mzazi tena hasa mama ni changamoto sana ila usijali tupo sisi ni kama ndugu zako if you need anything please let me know..
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi



Maoni