*IN LOVE WITH ZURI* *SEHEMU YA 15*
SONGA NAYO.......
Ilinibidi niwe tu mpole, ila ushauri wa Ethan niliuona haufai kabisa kwa upande wangu, imagine nimempa zawadi jana tu harafu hizo siku za huko nyuma sijawahi kumfanyie hivi
Harafu eti jana tu kumpa zawadi leo nimepeleke hotelini, hata kama bwana ila kwa hili naona kama najivunjia heshima kabisa
"Me naongea na wewe harafu wewe unawwaza yako huko, walah me saivi sikwambii chochote.."
Nikiwa najiwazia zangu Ethan alizungumza ndio nikakurupuka sasa
'Sio hivyo bana, ila me naona kama namkosea yule binti.."
"Ila Frank kwa stail hii sizani kama utaoa wewe, yani mtu umekaa kioga oga bwana unanikera ujue.."
"Aya bana.."
Nilisema huku nikinyanyuka zangu kuondoka, lakini mara simu yangu iliita kuangalia ni wale wapambaji wangu niliowaagiza wanipamble.
Nikaitoa simu ili kupokea laki Ethan aliwahi na kuikwapua kisha akapokea yeye
Eh mnasikia nyie, acheni na kuoamba kule Beach, tafuteni hotel nzuri ambayo inavutia sana kisha mchukue chumba na kupamba humo, nataka mpambe na kupambika
Baada ya kila kitu mtume location, mnasikia.."
"Sawa boss.."
Simu ikakatwa, nikabaki namtazama huyu kijana natamani nimrukie nimpige ila kwa kuwa najua huyu fridge lake haligandishi nikaamua kuwa mpole tu
'Sasa sikia huku tumemalizana na hawa, cha kufanya wewe nenda saloon ukanyoe hizo ndevu ndevu hapo utengeneze vizuri, me naenda kutoka na Zuri saivi nampeleka saloon so harakisha muda ndio huu unatakiwa kufika kule
saa moja.."
Alisema Ethan huku akanirudishia simu yangu na bila kupoteza akatoka nje, akiniacha mie nimeganda kama barafu vile, nisijue nini cha kufanya kwa muda huo.
Baada ya Ethan kuondoka nilianza kumfatilia nyuma nyuma ili nijue ataongea nini na Zuri, maana huyu dogo me namjua vizuri kabisa
"Zuri mambo..??"
Ethan baada ya kufika seblen na kumkuta Zuri akiwa amekaa zake anaangalia movie yake pendwa, akamsalimia pale
"Poa tu za wewe..??"
'Me niko poa, ila zuri samahani kwa kilichotokea jana.."
"Mmh me mbina nishasahau bwana.."
"Kama ni hivyo sawa, but Zuri.."
Ethan alitaka kuongea ila akaniona mimi
nimejibanza kwenye nguzo iliyokuwa mle ndani nikiwa nawasikiliza, akacheka kwanza kisha akaendelea kuongea
"Zuri, unajua wewe ni mrembo sana ilal unachokosa wewe ni matunzo tu, maana wewe ungekuwa unatokea kwenye familia kama hii walah ungekuwa bonge la miss.."
Etha aliongea, me nilikuwa nasikiliza tu naishia kuguna chini chini maana hata sijui huyu ethani anampango gani
"Mh kweli..??"
Zuri aliuliza huku akiacha kuangalia kabisa TV na kumgeukia Ethan ili amsikilize vizuri, mnajua wanawake ni waajabu sana tena sana acha kwanza nicheka
Yani mwanamke ukimsifia kuwa yeye ni mzuri akili yake huwa inavurugika kabisa sasa hii frasa ndio Ethan aliitumia kumshawishi zuri
"Kwani we hulijui hilo??"
"Ethan acha basi hivyo, mbona sijaawahi kusikia mtu akiniambia kuwa me ni mzuri ndio nasikia kwako hapa na tena ni leo inamaana siku zote
hukuniona au..??"
'Sasa Zuri me huo muda wa kukwambia ulikuwa
unaniona nao wapi, jana napo nilikuwa nataka kuzungumza na wewe ukanifukuza.."
"Mh
"Sio muda wa kuguna huu twende nikupeleke salon walau ukasuke maana hizo nywele zako hazina mpangilio mzuri.."
"Lakin.."
"Nafahamu kuhusu hilo, usijali nishongea na mama nae hana tatizo.."
"Sawa basi acha nikajiandae kidogo.."
"Ouk wahi usichelewe sasa.."
Zuri aliondoka kwa kukimbia na kusahau hata kuangalia ile movie yake, upande wangu na mie
nikajiongeza nikaenda haraka haraka kuvaa nguo kisha nikatoka na kuongozana pamoja na Ethan lakini pia na Zuri..
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi

Maoni