NAKUPENDA BILA MIPAKA SEASON FOUR 145 - 150
:146
Nilimtazama natabasamu, nakuambia uoga mimi sina, sina kabisa maana nishajua huyu Dokta anapambania mahali ahitajiki.
Kwanza angejua raha mimi nilikuwa naipata hapa ameniharibia mimi. Si unajua unampenda mtu huwezi kumwambia halafu kumbe na yeye ana hisia na wewe ndiyo kimetokea sasa.
Kwa huyu Muanko wangu mimi wakati mzuri na tulivu kama huu ningewezaje kukataa. Hizo nguvu mimi natoa wapi. Sasa ndiyo hivyo huyu bi mzuri amekuja kuniharibia jambo langu. Angeniacha walau hata dakika kumi tu amekuwaje sijui.
Nakwambia ukimuona sasa dokta, utasema puto linataka kupasuka. Hayo macho, mikono inatoa jasho. Amechukuia, amekasirika. mr Gallen aliuliza “kwanini bila hodi, unataka nini?”
Nilimtazama dokta alishadadia ile siku, alisahau ya kuwa dunia duara na sasa imefika zamu yake mimi hapo natamani hata asingekuja.
Nilimtazama Boss, si unakumbuka alivyo sema “Relax, am here for you.” Mimi hapa ndiyo nimeambiwa hivyo eti, na Mr Serious kama ndoto vile, kama ninaota ila ndiyo ukweli wenyewe huo.
Nilimwambia kwa upole “naomba niende sasa Mr Gallen.”
Alinitazama na kusema “Nazwi wait.”
Nilijitoa mikononi, halafu nikaanza kutoka. Dokta akanisukuma na mkono mmoja nirudi ndani halafu akafunga mlango. Nakumbuka Mr Gallen alimsogelea akisema “are you stupid?”
Dokta aliuliza “Whaaaaat!!”
Mr Gallen akamuuliza tena “Why are you pushing her?”
Mimi nawatazama tu na viingereza vyao, nasema mimi nishakula busu mpapaso hapa nyie endeleeni tu.
NAKUPENDA BILA MIPAKA:147
Dokta alisema “nakusaidia, najua hawa mabinti wa uswahili wana tabia mbaya sana. Usimuendekeze Mr Gallen. She is not your Type, unajua hilo eenh.”
Anaongea anatetemeka, anatetemeka mimi namshangaa, msichana wa uswahili kwahiyo ana maanisha mimi ndiyo nimemtaka, nimetega, nimemchawia, nimemchukua sio akili zake au anajua nini kuhusu waswahili sisi.
Mr Gallen alimtazama akauliza “Who are you?”
Mimi natamani kucheka, zamu yake kuulizwa yeye ni nani, Dokta alitoa macho akauliza “Whaaat!!”
Mr Gallen alisema “Dokta please, sijaomba msaada wako, I didn’t, na wewe sio mtu wa kunipangia nini nifanye na nini nisifanye. Wewe upo hapa kwaajili ya mama, mahusiano yangu mimi na wewe ni urafiki na sio zaidi.
Tafadhali linda mipaka yako nilinde mipaka yangu. Sitaki kusikia tena una msumbua Nazwi. Nazwi hapaswi kusumbuliwa kwa vyovyote vile unanielewa. Na siku nyingine bisha hodi, uruhusiwe ndiyo unaingia.”
Nikaona hii ya leo ya moto, mimi nikatoka zangu, nilitoka mpaka chumba changu cha kubadilisha nguo. Nilipofika huko nilijikumbatia, halafu nikasherekea bila sauti ila kwa furaha.
Si mmesikia amesema Nazwi hapaswi kusumbuliwa ni kudekezwa tu mimi. Umesikia amesema Dokta awe anapiga hodi. Leo anapumulia mashine, mimi kwangu shangwe.
Natamani nipige ukunga niseme “Wanachiiiiiii eeeeeeh, watu wa duniiiiiiaaaaaaaaa hiiiiiii, amkeniiiiiiiii, amkeniiiiii nina ushuhudaaaaaaaa, nina ushuhudaaaaaaaaaaaaa, nataka kusema yale maombi yangu leo yamekuwaaaaa, sitakiii ushauriiiii we kissed, am in love.”
NAKUPENDA BILA MIPAKA:148
Najiambia mwenyewe nacheka mwenyewe nikikumbuka kuhusu dokta natamani Dorice angekuwepo hapa. Nikakumbuka hata ule mtoko sasa. Nilitumia dakika huko chumbani, ndiyo akili sasa ikarudi kumbe mama alitaka supu.
Nilijawa na furaha mimi, kumbe mimi ni mtu wa furaha sana. Unajua saizi na nguvu hata za kuwatia moyo wale masingle girl, masingle mama, single boy, single baba, masingle singular tu wewe mapenzi yamekupita nisikilize mimi. Mama mgonjwa alisema na mimi
nakwambia “haijalishi unapitia nini, siku moja, mahali fulani utakutana na mtu. Mtu huyo atakupenda sana, atakupenda kuliko ulivyo wahi kufikiria. Atakupa heshima, atakujali, atakuhudumia, atakutunza, atakupa raha na kila kitu. Amini tu.Mapenzi ni heshima, kujitoa, huruma, kuaminiana, na mazuri mengi kama haya.”
Sitaki kuamini na mimi leo nimeanza kutoa ushauri leo leo tu jamani Nazwi tulia binti.
Nilienda zangu jikoni, nilipofika huko nilimuona dada Maria kama hana raha vile. Nikamuuliza “vipi dada yangu mbona umepoa?”
Akaniambia kwa upole “mama yangu, bado hayupo sawa. Nataka tu nikamwone walau liwalo na liwe tu.”
Nilimtazama na kusema “Si ulisema umekutana na Mungu. Sasa unaogopa nini?”
Alitabasamu, halafu aliniambia “subiri sana, leo uso wako una ng’ara sana. Ni kama umekuwa mzuri sana. Nini kimetokea.”
Nikajishika uso na kusema “una ng’ara ila dada Maria.”
Akacheka akisema “ni kazuri sana unajua.”
Nilitabasamu na kusema “mama anataka supu ya kuku, unaweza nisaidia niandae hapa.”
Alitabasamu akisema “bila shaka nesi wangu.”
NAKUPENDA BILA MIPAKA:149
Alikuwa ameanza kunitolea vitu na mimi nilisema “usiogope, ukimtegemea Mungu hupaswi kuogopa kabisa.”
Alitabasamu, na aliniuliza “umeongea vizuri. Hata maandiko yake yanasema hivyohivyo.”
Nilitabasamu, ghafla nikakumbuka nilipokuwa pale hospitali nilikuwa namuomba Mungu ning’are kama yeye, uso wangu upendeze na muonekano wangu uwe mzuri wenye kuvutia.
Nikajishika uso nikisema “Kumbe kweli, lakini mbona nipo vile vile mbona sielewi.”
Wakati huo alikuwa anatoka dokta, amechukia balaa, amechukia mno.
Maria alisema “maskini huyu dokta anateseka bure. Ni bora tu aachane na mapenzi. Kaka na hapendi usumbufu kabisa.”
Nilitabasamu tu, akasema “leo ni kama una furaha.”
Nilitabasamu na kusema “nina ushuhuda.”
Alitabasamu akisema “eenh.”
Nikacheka na kusema “tupike embu, dada Maria wewe.”
Akacheka na kusema “nacheka tu hapa lakini nawaza sana kuhusu mama. Naomba tu Mungu.”
Nilimtazama na kusema “Amen, atakusaidia.”
Alinitazama na kuniuliza “nyie mmezaliwa wangapi?”
Nilimjibu, akatabasamu.
Nikawa naendelea na mambo yangu ya mapishi eemh, siku hii ndiyo siku ya kuonesha ujuzi wangu haswa kwa upande wa jikoni. Na mimi sikufanya masihara. Nikahakikisha mambo yanakuwa vizuri.
Nakumbuka wakati naendelea na kazi zangu mlango uligongwa. Dada Maria alienda kufungua. Alikutana na mgeni, sikuwa najali. Lakini baada ya muda aliingia na mifuko akisema “haya mama, nimeambiwa mzigo wako.”
Nilimtazama na kusema “wangu mimi?”
Alisema kwa upole “eemh wewe.”
Nilipokea, kutazama kuna nguo. Nilitabasamu halafu nikasema “naweza kupata na mswaki mpya. Nahitaji kuoga sasa maana tangu asubuhi nimeamkia hospitali.”
NAKUPENDA BILA MIPAKA:150
Alitabasamu na kusema “pole kipenzi, pole sana nesi. Mswaki upo, sema nini kingine unataka.”
Nilimtazama na kusema “naomba tu niangalizie hapa maana najisikia uchovu. Nikioga nitakuwa sawa.”
Alinitazama akatabasamu tu, najua ana mengi ila hawezi niuliza chochote. Mimi hapo nasema eenh nimeagiziwa na nguo muanko huko ndani kama nikamchungulie ila siwezi.
Basi wakati ndiyo naingia chumba changu na yeye anatoka ofisini anaingia chumba chake. Macho yakagongana ndi!!, ndiiiiii!!. Nilitabasamu, akatabasamu. Mimi nikicheka nikaingia chumbani na yeye pia alifanya kama mimi.
Mungu muacheni tu, Mungu huyu wa mbinguni aanh muacheni. Ana fanya mambo mpaka una muuliza “nini nimefanya kustahili haya yote, mbona unanidekeza sana eenh, mbona unanidekeza.”
Nikuambie kitu ndugu yangu, Mungu ni Mungu wa haki, Mungu wa kutenda, Mungu wa wote, hana upendeleo yeye. Ni suala la Muda tu, muda wako lazima ufike, na ukifika Mungu yeye mwenyewe lazima atakuchagua. Hapo sasa ndiyo hata hutojua useme nini kushukuru. Sasa huo muda, muda wangu huu ndiyo wenyewe.
Si nilisema tangu awali, napenda mavazi ya heshima. Hata magauni yangu yana heshima ukiniona nilivyo vaa utajua tu binti ana jiheshimu. Hata kama fupi basi sio ufupi wa utisho, hata kama mpasuo basi wa heshima, sio kushika sana mwili.
Kuna wakati nilikuwa navaa viraba hata kama sio vya gharama ila vilinipendeza. Sio kwamba mimi ni wa zamani hapana, msichana tu wa kisasa, navaa kisasa ila tu pesa ya kununulia zile za heshima zenyewe ndiyo sina lakini hapa sasa, achana na hizi Abaya kila mtu anazo tena hata tutafute jina lake tuseme tu gauni za kujisitiri eenh nacheka, mimi mama mitumba na hizo Abaya zangu za mtumbani Mungu ndiyo anajua, sasa hizo ziache, hizo sahau, hizo achana nazo kabisa.
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi
Maoni