NAKUPENDA BILA MIPAKA 141 - 144 MWISHO WA SEASON THREE
:141
Nikamwambia kwa ujumbe “Boss ni usiku sana, nenda nyumbani, tutaongea kesho naomba nipumzike.”
Akanijibu “sitaondoka hapa mpaka uje kunisikiliza.”
Nikamuonyesha Dorice, Dorice akasema “kamsikilize Labda ni muhimu.”
Nikamwambia Dorice “kusema kweli mimi roho bado inauma na unafiki siwezi. Nitaongea naye tu nikiwa sawa.”
Dorice alivuta pumzi na kusema “Muanko kanasa jamani.”
Nikatabasamu tu.
Sasa tukalala, sina hili wala lile. Ilikuwa ni asubuhi sana nasikia mama anaita sauti ya chini “Nazwiiii!!, Nazwiii!!, Nazwiiii!!! “
Mimi sasa na sauti ya usingizi “mama kuna nini tena mbona mapema.”
Mama aliniambia kwa upole “Una mgeni.”
Nilishtuka, nikauliza “mgeni?”
Mama alisema “amka mwanangu.”
Niliamka haraka haraka, mgeni gani mafungulia ng’ombe (asubuhi) yote hii. Nilivaa vizuri nikawa nafikicha fikicha macho yangu. Basi taratibu nikatoka.
Nimefika nje, niulize Nani, MR Gallen, inavyoonekana hajaondoka hapa kwani ana nguo zilezile za jana. Nikamsalimia “shikamoo.”
Akashusha pumzi na kusema “Marahaba Nazwi, tunaweza kuzungumza.”
Nilimtazama mama, na kisha nikamtambulisha. Mama alifurahi kumfahamu, na Boss pia alifurahia. Kisha tuliingia kwa gari. Nikamuuliza “Boss umelala hapa?”
NAKUPENDA BILA MIPAKA:142
Alinitazama, alinitazama kwa huruma na kusema “kwanini unanifanyia hivi?, kwenye akili yako kuna nini haswa eneh. Au kwakuwa ni mimi sio wewe unapitia haya. Nazwi hujawahi kukosea kwenye maisha yako yote na ukasamehewa.
Mama yangu Jana ameruhusiwa kurudi nyumbani lakini amegoma bila wewe, nakupigia walau uonekane tu tumtoe pale hujapokea simu. Nimekufuata mpaka hapa umegoma kutoka. Unasikia raha, unaona raha si ndiyo?. “
Nilimtazama na kusema “lakini Boss, Sio hivyo, nilikwambia nataka kuacha kazi.”
Aliongea kwa sauti “kelele, huwezi kuacha kazi nimeshakwambia.
Nikwambie Mara ngapi. Sahau kuacha kazi kwa mama. Na sio tu kwa mama huwezi kukaa mbali na mimi haiwezekani. Sasa sikia Leo hii sio Ombi ni lazima, tunaenda hospitali, tunamtoa mama na tunaenda naye nyumbani. Unanielewa?”
Niliogopa, Nikamtazama kwa hofu. Naona hataki hata kuniangalia macho yake yamebadilika. Nikasema “sasa nikabadilishe nguo, nioge hata.”
Alinitazama, akanifunga tu mkanda sasa vile ananifunga mkanda si ananiegemea jamani raha ni vipi, lakini yeye kachukia, akawasha gari sijaaga hata nyumbani nabaki tu sijui ndiyo utoto au ni nini “sasa ndiyo unaniteka?, Ona Ona na nilivyo hospitali kweli.”
Aliendelea kuendesha gari hasemi kitu, haongei chochote kile. Tulifika mpaka hospitali. Tulifika, tukashuka akanishika mkono ukimuona tu unajua kachukia na mimi nimetoka kulala. Tulifika mpaka chumba cha mama. Akaniambia “ingia hapo.”
NAKUPENDA BILA MIPAKA:143
Namtazama tu, nikashusha pumzi na kuingia. Mama aliponiona machozi yalimtoka, alisema kwa unyonge “mwanangu, mwanangu wewe ndiyo wakunifanyia hivyo ukaniacha kweli binti yangu. Ina maana hukunikumbuka mimi.”
Nilimtazama nikisema Kama nalia na vile anatia huruma “nisamehe mama, nisamehe sana. Siwezi kufanya kusudi na mimi nilikuwa naumwa.”
Mama alinitazama na kusema “mwanangu, najua mwanangu alikukosea, alikuja hapa analia kwasababu unaacha kazi. Nilimfokea sana. Lakini Nazwi nilikwambia mwanangu hayupo sawa kihisia. Msamehe mwanangu, msamehe sana. Eenh unaniacha mpaka mama yako unaacha kazi kweli. Nitapata wapi binti Kama wewe, nesi wakunipangusa, wakunisafisha wakunifulia kwa upendo eneh mwanangu.”
Nikajikuta nalia, na kusema “ni kweli mama, ni kweli nimekosea nisamehe sana, nisamehe sana mama nimekosa. Nipo hapa na wewe sitakuacha Tena .”
Mama huyu alisema “Sitaki kukaa hapa, tutaongea tukifika nyumbani. Tuondoke.”
Ndiyo sasa Mr Gallen aliingia, mama alisema “mwanangu, niitie Dokta tunaondoka hapa sasa hivi.”
Niliona tabasamu usoni kwa mtekaji, nilimtazama mama na kusema “mama si kaniteka.”
Mama akacheka kidogo kwa upole akisema “Kwa nilivyokuwa nimemkasikiria anakufokea vipi binti yangu na wakati ulikuwa unanipa mama yake furaha. Lazima akuteke.”
NAKUPENDA BILA MIPAKA:144
Tukacheka mama akisema “futa machozi sasa, nataka tukifika uniogeshe vizuri maana hawajui hata chochote si unaona hata sipendezi.”
Nikatabasamu nikisema “Upo sahihi mama, kweli.”
Basi mimi huyo, nikawa napanga pale vitu, Dokta na Gallen wakaingia. Sio kabale lakini. Alimuangalia mama, na alituruhusu.
Tukamkalisha vizuri mama, hataki hata kusukumwa na mtu mwingine Ila mimi. Nikasaidiana na wauguzi wengine pale tukaondoka mpaka kwa gari na safari ya mjengoni ilianza. Mimi nimekaa na mama tu huko tumetulia. Tulifika nyumbani.
Niliandaa vizuri chumba cha mama na kusaidiana na Gallen. Tukamaliza, tukasaidiana kumlaza mama. Alitutazama na kusema “Asanteni sana wanangu.”
Tulitazamana na kutabasamu, mama akasema “Nazwi mwanangu, niandalie supu ya kuku nzuri sana. Mimi sijala hata vizuri na sasa nataka nilale kidogo.”
Nikatabasamu, nikasema “sawa mama.”
Mr Gallen alitabasamu akasema “na mimi hiyo supu tafadhali nesi, najisikia kuumwa usingizi.”
Nikacheka huku moyoni nasema “lazima uumwe chezea kulala nje wewe.”
Alikuwa anatoka, wakati anatoka aliniambia “naomba upitie ofisini tafadhali.”
Nilitabasamu na kusema “sawa boss.”
Basi Baada ya kuhakikisha mama yupo sawa na mimi nilitoka na kumfuata ofisini. Nilikuta amesimama anatazama dirishani.
Nilipoingia tu aligeuka na kunitazama kwa uso wake serious “Nashukuru upo hapa, thanks for everything, thanks for my mom, for Me. Nazwi sijui nikushukuru vipi. Una maana kubwa sana kwenye maisha yetu.”
Nilitabasamu na kusema “nashukuru sana. Usijali tuachane na hayo. Lakini sasa sijaoga, sipo vizuri. Najisikia vibaya. Naomba nirudi nyumbani halafu nirudi tena.”
Alicheka kidogo, akapiga hatua kunifuata, halafu akanisogelea mimi tena naona eneh vipi tena huyu.
NAKUPENDA BILA MIPAKA:145
Akanifikia na kushika mikono yangu akaniambia hivi “Ukiwa hapa ondoa shaka kuhusu jambo lolote, utapata kila kitu as long as upo na mimi hapa. Hakuna kitu kinashindikana mimi nikiwa hapa.”
Nilitetemeka.
Mr Gallen alinitazama na kuniuliza “naweza kukukumbatia kama kusema asante.”
Natamani kusema “nikumbatie sasa hivi ila nimeumbwa na haya. Nilimtazama tu. Si akanisogelea na alinikumbatia kwa nguvu, kama katoto.
Halafu nikawa sasa mwili nasisimka jamani, mikono yake si ikashuka kwenye makalio, mimi ndiyo nasidizi sogea mwilini mwake, akadondokea kukaa kwa kiti, akanivutia karibu. Tukatazamana. Hapo natetemeka, sina hamu.
Alivyo na nguvu, alininyanyua, akaniweka mapajani mwake miguu huku na kule, halafu akaingia mikono yake kwenye shati langu kwa ndani huku nyuma. Akanipa midomo yake, nikajikuta naifuata nampa yangu. Alivyoishika midomo yangu jamani hapa ninachoweza kusema ni “we kissed am in love, i can’t get enought of him.”
Anajua kukiss, anavyonishika, tena ni kama alinipania. Tukiwa kwenye hali hiyo, mlango ulisukumwa, vile tunatazama, niligongana uso kwa macho na uso wa Dokta tena akiwa amechukia anatoa machozi. Nilikuwa nataka kushuka pale juu. Unajua Muanko alisema “Hey relax, am here for you.”
NAAAAAAAAAAAM
HAPA NDIYO MWISHO WA SEASON THREE
SEASON FOUR inakuja nikili tu ndugu zangu mchango wenu unahitajika sana 0768304821 jina omary luambano 🙏
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi


Maoni