MFALME KIPOFU 27
Sehemi..ya............ 27 (FINAL)
Whatsapp.............0748697173
Ilipoishia sehemu iliyopita........
Nawauliza Princess Nailet yupo wapi?
alipotazama Pembeni hakuamini kuona mwili wa binti yake.......
ENDELEA NAYO......
Mfalme Tengu alilia kama mtoto mdogo
"Pole sana mfalme kwa kipindi kigumu unachopitia Prince Yao aliongea"
Mfalme alipogeuka alimwona Prince Yao tena akiwa anaona kabisa hapo ndipo ukichaa ulipompanda.
"Yani umeniulia mwanangu alafu unanipa pole,wewe sasa ivi unaona mwanangu amelala usingizi wa milele?"
"Nimakosa yangu Mfalme na nipo hapa kuomba msamaha, na Nailet aliniomba nije nimuombe msamaha kwa kushindwa kukusikiliza"
"Unafikili itasaidia,mimi tayali sina mtu wa kulithi kiti changu mwanangu peke niliyekuwa namtegeme hayupo"
"Nisamehe mfalme".
"Msamaha peke hautoshi lazima ulipe kwa kusababisha nikampoteza mwanangu".
"Nifatieni karatasi ndani tuandikishane hapa",
"Tuandikishane nini???"
"Subri utajua tu"
Mfalme aliandika maandishi kwenye karatasi mbili na alipomaliza kuandika alimpa karatasi moja Prince Yao asome kilichoandikwa.
Prince Yao hakuamini baada ya kusoma kile kilichukuwa kimeandikwa na Mfalme Tengu.
Kwanini lakini unanifanyia ivi Mfalme??,Prince Yao aliongea baada ya kusoma kilicho kuwa kimeandikwa.
Nasoma kwa sauti kila mtu asikie na Mahiti ya binti yangu ikiwa kama shahidi namba moja kwa haya makubaliano, Mfalme Tengu aliongea.
"MTOTO WA KWANZA UTAKAYEMPATA KWA MWANAMKE WAKO WA NDOA ATAKUWA MLITHI WA FALME HII YA YUNDI"
"Umekubaliana na ninachotaka???".
Prince Yao hakuwa na cha kupinga na ukizingatia Princess Nailet alikuwa na upendo wa kweli kwake alikubaliana na Mfalme Tengu na taratibu za mazishi ziliendelea kufanyika.
**************
Upande wa General akiwa amekaa chini ya mti akitafakari njia sahihi ya kuuteka ufalme wa ADELI mawazo yakiwa yamemshika.
"General kimbiaa!! kimbia!!!!"
ilikuwa ni sauti ya asikari wake ikimtaka General kukimbia.
"Huyu amepata ukichaa mpaka anakimbia peke yake"
ila alisikia kitu kikimgusa mgogoni mwake alipogeuka hakuamini kile alichokiona.
Alikuwa ni nyoka mkubwa na General alivuta upanga wake ili amshambulie nyoka huyo lakini alikuwa ameshachelewa kwani alizungukwa na yule nyoka mkubwa na kubanwa kila sehemu ya viungo vyake baada ya hapo alimezwa mzima na yule nyoka.
Na huo ndio ukawa mwisho wa General, ndoto zote za kuwa Mfalme wa ADELI ziliishia tumboni mwa Nyoka yule.
*************
Katika Jumba la kifalme Mfalme Kojo anapata ahueni baada ya kulala kitandani kwa mda mrefu,
Malikia andwaa alifurahi kumuona Mfalme ameanza kurudi kwenye hali yake ya kawaida.
"Nani aliyenitibu mpaka nikapona??"
Binti Amma alikuwa maeneo yale alikuja mbele ya Mfalme na kupiga magoti na kumfanya Mfalme Koja kumshangaa mana ndiyo ilikuwa mara ya kwanza kumuona ,
Amma alisimulia kila kitu kilivyotokea kuanzia pale General alivyo mlazimisha baba yake atengeneze sumu mpaka pale alipouliwa baba yake kwenye mazingira ya utatanishi.
Na ata Princess Yanite ambae alikuwa na chuki na mtu aliyetengeneza ile sumu alimsamehe kwa moyo mmoja Amma
"Mfalme ila kuna habari njema ambazo ni lazima uzijue???",Malikia Andwaa aliongea.
"Habari gani izo???"
"Prince wa kweli tumeshampata".
Mfalme alijikuta akikaa kwenye kitanda kwa tarifa zile zilizokuwa ni tarifa njema kwake.
"Natamani nimuone Prince ameenda wapi??",Mfalme Kojo aliuliza baada ya kupewa tarifa zile mpya.
"Nipo hapa baba"
Prince Yao alikuwa amesharudi kutoka YUNDI.
"Mmmh unaona???"
"Ndio mfalme naona"
"Nani kakufanya uone???"
"Ni huyo binti aliyepembeni yako baba"
Mfalme alionyeshwa Amma kwa mara nyingine tena licha ya kumtibu yeye bado alimtibu mwanae,
"Binti sina cha kukulipa kwa ulichofanya kwenye familia yangu ila njia pekee ambayo mimi kama mfalme ningependekeza wewe kuolewa na kijana wangu ili uwe Malikia wa hili taifa kwa hapo badae, kama utakuwa tayali ila kama utaona haifai napo sitapinga maamuzi yako".,Mfalme Kojo aliongea.
Mfalme pia alimhurumia Amma baada ya kugundua hana ndugu yoyote kwenye hii dunia kwani ameshawapoteza wazazi wake wote wawili.
Amma alikubali kuolewa na Prince Yao na utabili wa yule mzee ukatimia kuwa Amma atakuja kuwa mtu mkubwa kwenye taifa la ADELI.
*************
MWAKA MMOJA(1) BADAE
Baada ya mwaka mmoja kupita Prince Yao na Amma walifanyikiwa kupata watoto mapacha na wote walikuwa wa kiume,
Prince Yao alimuelezea mke wake Amma makubaliano aliyokuwa nayo na Mfalme Tengu na Amma hakuwa na kipingamizi.
Prince Yao alitekeleza ahadi yake kwa kumchukua mtoto aliyetangulia kutoka ambae ni kulwa na kumpeleka kwa Mfalme Tengu na pia alifarijika sana kuona Prince Yao ametimiza ombi lake,
na kuanzia siku hiyo ukawa mwanzo mzuri wa falme zile mbili (ADELI NA YUNDI) kutengeneza mahusiano mazuri .
Kutokana na uzee wa Mfalme Kojo alimkabizi Prince Yao kiti cha kifalme na yeye kubaki kama mshauli wake pindi anapofanya maamuzi yasiyo sahihi bira kusahau upendo katika jumba la kifalme uliongezeka mara dufu na furaha ilirejea tenaaaaaaaaa.
MWISHOOOO
Shukrani zangu kubwa ni kwenu ndugu wasomaji mlipoteza mda wenu kufatilia simulizi hii na hatimae leo imefikia tamati
Sina chochote cha kuwalipa zaidi ya kuwaombea afya njema zaidi nawapenda sana ndugu zangu, TUKUTANE TENA WAKATI MWINGINE. Next ni FARASI MWEUPE itakuwa hewani siku ya Jumatatu.
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi



Maoni