MFALME KIPOFU 19 -- 20
Whatsapp.............0748697173
Ilipoishia sehemu iliyopita......
Ni mapenzi ya ajabu aliyokuwa nayo Princess Nailet kwa Yao licha ya kumfahamu kwa mda mfupi tu lakini aliteka sehemu kubwa ya moyo wake...
ENDELEA NAYO.......
Aliendelea na safari ya kumtafuta mwanaume wa ndoto zake licha ya upofu aliokuwa nao mwanaume anaye mpenda ila bado aliamini ndie mtu sahihi kwake.
***************
Ni majira ya jioni Cheki akiwa anamtafuta mlinzi ili ampe tarifa kuwa yupo tayali kufanya kile alicho kuwa anakitaka,
"Nimekutafuta sana kumbe umekaa huku", Cheki aliongea.
"Nilijua utakuja tu,na nilikusubiri hapa kwa hamu".
Walianza kuondoka kutoka katoka jumba la kifalme.
Na safari ilianza ya kuelekea msituni kuwa tafuta General na Nzegi na mwongonza njia alikuwa rafiki yake Nzegi au asikari wa jumba la kifalme,
"Nisehemu gani hii unanipeleka au unamipango mibaya na mimi??"
"Jiamini wewe ni mwanaume".
Cheki alianza kupata wasiwasi baada ya kuona wanazidi kuingia msituni na walipofika sehemu husika asikari yule alipiga mluzi kama kawaida yake kuwaita General na Nzegi.
"Umefanya kitu cha maana sana kumleta Prince"
General aliongea na kumfanya Cheki aanze kujiona kweli watu wana mtambua kama Prince wa ADELI.
"Wewe sio Prince na ndio mana uko hapa"
Kibao kiligeuka na kumfanya Cheki atambue kuwa ata General anajua kuwa yeye sio Prince.
"Nikweli mimi sio Prince ila mnashida gani na mimi???".
"Vizuri kama umekili mwenyewe , tunataka ufanye kazi ndogo tu na utapata malipo mazuri zaidi ata ya yale ambayo Mfalme amekuahidi kwanza kabisa, utaendelea kuwa Prince wa hili taifa, na kitu cha pili hautotoka kwenye jumba la kifalme ata kama mfalme akiwa mwingine".
Cheki aliyetafakari maneno aliyoambiwa na General ...
"Mnataka nifanye kazi gani???"
"Kazi yako ni kushika kichupa hichi,humu kuna sumu kali itakayo weza kumu angamiza mfalme taratibu ndani ya siku tano ili watu wasi shituke zaidi, mfalme anapenda sana kunywa kahawa, basi kazi yako ni kuvizia na kuichanganya sumu hii kwenye kahawa ya mfalme".General aliongea.
"Ni hatari sana kwa upande wangu hasa niki kamatwa".
"Wewe ni mwanaume utaangalia jinsi ya kuepuka hili"
General alifanyikiwa kumshawishi cheki nae haku pingana na kazi aliyopewa, alipatiwa kichupa nakuelekea katika jumba la kifalme,
Kazi ilibaki moja tu ya kuichanganya ile sumu kwenye kahawa ya mfalme.
***************
Lindiwe pamoja na rafiki yake wakiwa wanapiga stori mbalimbali baada ya kupotezana kwa miaka mingi sana.
"Rafiki yangu baba wa huyu handsome wako ulimtoa wapi nikamwambie na mimi anizalishe???"
"Yu....le alikufa miaka iliyopita".
Lindiwe alipata kig'ug'umizi kidogo cha kujibu swali la rafiki huyo na hakutaka kuendelea na stori zinazomhusu Prince Yao,
"Kuna habari gani katika jumba la kifalme??", Lindiwe aliamua kubadilisha mada.
"Hakuna habari za maana zaidi ya sisi kutambulishwa Prince siku kadhaa zilizopita"
"Kwani mfalme alikuwa hajamtambulisha Prince miaka yote iyo???"
"Wapi sasa, huku Prince mwenyewe inasemekana amekulia nje ya jengo la kifalme na mfalme ana watoto wa kike tu wawili,wananchi walipo lalamika kuwa wanataka wamuone Prince mfalme ndio akakubali kumtambulisha".
"ila makosa yote ni ya kwangu".
"Makosa ni yako kivipi ??,
Lindiwe alikulupuka kutoka kwenye mawazo baada ya kujisahau na kutamka kuwa yeye ndie mwenye makosa na kumu weka njia panda rafiki yake huyo ambae nae alimuuliza swali ila Lindiwe aliamua kupindisha mada.
Lindiwe alitambua sababu iliyo mfanya mfalme amtambulishe mtu mwingine kama ndio Prince badala ya Prince Yao.
******************
Ndani ya ufalme wa ADELI Cheki anaingia katika kasili la kifalme akiwa na chupa ndogo yenye sumu ndani yake alielekea jikoni na kumkuta mpishi mkuu wa kifalme,alipewa heshima mana bado alitambulika kama mwana wa Mfalme,
"Mfalme umeshampelekea kahawa yake??:
"Hapana Prince bado tunaiandaa hapa".
"Jambo zuri fanya haraka umpelekee, alafu nimekumbuka kitu Yanite aliniambia umpikie chakula ila nimesahau nichakula gani nenda ukamliza yupo chumbani kwake".
ilikuwa ni njia ya kumtoa mpishi maeneo yale,alipotoka tu Cheki akaichanya sumu kwenye kahawa ya mfalme na kuondoka zake.
"Prince kaniagiza nije nikuulize ulimwambia unataka upikiwe chakula gani binti mfalme??"
Mpishi yule alimuuliza Yanite
"Mbona sijamwagiza chochote!!!".
Mpishi alishaga aliamua kurudi jikoni kwake kuendelea na kazi yake ila alichukia sana kwa kitendo cha Cheki kumfanya kama mtoto mdogo.
Mfalme akiwa ametulia kwenye kiti chake akitafakari mambo yanavyo endelea kwenye utawala wake,
Mtumishi wake alimletea kahawa kama ilivyo desturi ni lazima aonje kwanza ndio mfalme nae anywe alionja bira kujua kama kuna sumu na mfalme nae baada ya kijihakikishia ipo salama kahawa ile..........ITAENDELEA.
Je? Mfalme Kojo atakunywa ile kahawa au atagundua kuna sumu ndani yake? Sehemu inayofata si ya kukosa
[12/12/2025, 6:40 AM] zooper simulizi2: Story.....................MFALME KIPOFU
Mtunzi...................Zooper
Sehemi..ya............ 20
Whatsapp.............0748697173
Ilipoishia sehemu iliyopita........
Mtumishi wake alimletea kahawa kama ilivyo desturi ni lazima aonje kwanza ndio mfalme nae anywe alionja bira kujua kama ina sumu na mfalme nae baada ya kujihakikishia ipo salama kahawa ile....
ENDELEA NAYO.............
Baada ya kujihakikishia ipo salama kahawa ile nae alikunywa bira kujua kama itaanza kumzulu baada ya masaa manine yajayo.
Cheki hakuwa mbali alikuwa anafatilia kila kitu alichokuwa anafanya Mfalme, na alivyoona mfalme amekunywa ile kahawa alifurahi na kuona mipango yao imeenda sawa kama alivyopewa maagizo na General Tengeli.
"Wewe mbona unamchungulia mfalme??"
Alikuwa ni Princess Yanite aliyemkuta cheki maeneo yale,
"Aaaah nafikilia jinsi ya kwenda kuongea na baba tu".
"Emu rudia tena, umemwita nani, baba??".
"Mfalme ni baba yangu na mimi ndio Prince lazima uniheshimu kama kaka yako",Cheki aliongea bira kujua kama Princess Yanite ameshafahamu ukweli wote.
"Tangu lini ukawa Prince wewe??"
Yanite aliondoka na kumuacha Cheki kwenye mawazo juu ya kile alicho kisema.
"Hapa lazima niungane tu na wale jamaa tarifa zimeshavuja tayali nisipokuwa makini nitakosa kila kitu" .
****************
Princess Nailet anafanyikiwa kufika kwenye ufalme wa ADELI na anakuwa na kazi kubwa ya kumtafuta Prince Yao pamoja na Lindiwe ni wapi walipo.
Upande wa ufalme wa YUNDI,
Mfalme Tengu, jumba la kifalme linashindwa kukalika kutoka na upweke aliokuwa nao juu ya kuondoka kwa binti yake,
Uvumilivu unamshinda Mfalme wa kumuacha binti yake afanye anachotaka anaita walinzi nakutoa maagizo,
"Nendeni katika ufalme wa ADELI mkamrudishe Princess Nailet awe anataka au hataki".
"Sawa mtukufu Mfalme"
"Hakikisheni mnatekeleza maagizo yangu sitakuwa na msamaha na mtu yoyote atakayefanya makosa"
Kundi la vijana wa Mfalme Tengu linaondoka na kwenda kumtafuta Princess Nailet.
**************
Lindiwe aliona hakuna sababu tena ya kuendelea kuificha ile siri aliona ndio mda mwafaka wa Prince Yao kujijua yeye ni nani na rafiki yake pia alikuwepo kwenye yale maongezi,
"Yao mwanangu,hii siri nimeficha mda kwa mrefu uliopita ila leo ndio mda mwafaka wa kukwambia najua huwezi ukakumbuka vzuri kwa sababu ulikuwa bado mdogo sana".
"Mmmh siri gani iyo rafiki yangu uliyomficha mwanao??".
Lindiwe aliwaelezea kila kitu Prince Yao pamoja na rafiki yake na hii kuwafanya wote wasiamini walichokisikia.
"Unataka kuniambia wazazi wangu walinitenga kisa mimi ni kipofu????"
"Hapana sio kama unavyofikilia Prince Yao wanakupenda sana na......"
"Wananipenda kivipi yani wanipeleke mbali kisa mimi kipofu alafu useme wananipenda??"
Alinyenyuka kwa hasira na kusahau kuwa haoni alipo jaribu kutembea alijikuta anajikwaa na kuanguka chini ila hakutaka mtu yoyote amshike siku iyo.
"Wewe Prince Yao unaenda wapi huko huoni na huwezi kutembea peke yako???",Lindiwe alimuongelesha.
"Niacheni sitaki mtu yoyote anifate na wala sitatumia fimbo leo kutembea".
Alikuwa na hasira ambazo zilimfanya Lindiwe ajute maamuzi aliyoyafanya ya kumwambia ukweli ule.
"rafiki yangu naomba ukaonge nae wewe huenda atakuelewa".
"Hatutakiwi kukaa hapa inatakiwa tumfatilie kuangalia usalama wake mana haoni yule".
Walinyenyuka na kuongozana kumfatilia Prince Yao sehemu aliyoenda.
******************
Baada ya masaa manine kupita mfanyakazi aliye ionja kahawa kabra ya mfalme kuinywa alikuwa kwenye hali mbaya iliyopelekea, watumishi wenzake wambebe na kumpeleka katika chumba cha kupumzikia.
Upande wa Mfalme Kojo nae akiwa anaongea na Malikia Andwaa gafra alianza kutapika damu hali iliyopelekea Malikia kupiga kelele.
Watumishi mbalimbali walifika na kumwita daktari wa jumba la kifalme aliyefika na kuangalia tatizo la mfalme,
Alifika mtumishi mwingine nakutoa tarifa kuwa kuna mtumishi amepatwa na hali mbaya kama aliyo nayo mfalme.
"Hii inawezekanaje watu wawili waumwe ugonjwa unao fanana tena kwa pamoja??", Dakitari aliuliza na hamna mtu aliyemjibu.
"Daktari fanya unavyojua mfalme apone"
Malikia aliongea huku machozi yakimtoka.
Uchungunzi ulifanyika katika jumba la kifalme na iligundulika ni sumu kali ambayo ina msumbua mfalme pamoja na yule mfanya kazi wa jumba lile la kifalme,
Na waligundua baada ya kupima kikombe alichotumia Mfalme kunywea kahawa.
"Hii sumu aliyopewa mfalme ni kali sana na inaonekana imetengezwa na watalamu wa dawa za hasili".
"Dakitari hatuwezi kupata tiba ili mfalme apone???".
"Tiba pekee nikumtafuta mtu aliyetengeneza hii sumu na yeye ndie anayejua njia ya kumponyesha".
Malikia alichanganyikiwa baada ya kusikia maneno yale ya dakitari Malikia aliita walinzi na kuwapa maagizo ya kuwakamata matabibu wote..............ITAENDELEA.
Je? Malikia Andwaa atapata tiba ya kumtibu Mfalme na vip kuhusu Nailet atafanyikiwa kumpata Prince Yao ??? Huu mkasa sio wa kukosa
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi



Maoni