MFALME KIPOFU 12 na13
Sehemi..ya............12
Ilipoishia sehemu iliyopita........
Pasipo kufikili mara mbili roho ya wivu ikamuingia hakuta kuona mwanamke yoyote anakaa karibu na Yao zaidi yake yeye,
Aliondoka mbiombio mpaka katika jumba la kifalme..........
ENDELEA NAYO....
Aliondoka mbiombio mpaka katika jumba la kifalme kwenda kutoa tarifa ambazo aliona ni sahihi kwa upande wake na alipofika tu tarifa zilimfikia mfalme Tengu juu ya ujio wake,
"Binti mbona asubuhi sana kuna tatizo??"
"Ndio mfalme nimemuona Princess akiwa na kijana yule kipofu asubuhi hii".
Alielezea kila kitu kwamba amemuona Princess Nailet akiwa na Yao na walikuwa kwenye mapozi yasiyo ya kawaida,
Habari zile zlimkasilisha sana Mfalme Tengu, kwa tarifa alizopewa hakuamini kama binti yake anaweza kufanya kitu kama icho na ukizingatia ni mtoto wa mfalme.
"Unachoongea unauhakika nacho???",Mfalme Tengu alimuuliza Yunde kwa mara nyingine.
"Ndio mfalme".alijibu kwa kujiamini mana alikuwa na uhakika na tarifa zake alizozileta mbele ya Mfalme wake.
Mfalme aliagiza walinzi waka muangalie Princess Nailet katika chumba chake na kumletea tarifa kama ni kweli binti yake hayupo katika jumba la kifalme.
"Mfalme Princess hayupo kwenye chumba chake".
Mfalme hakutaka tena kuuliza maswali zaidi ya kwenda kujihakikishia kama tarifa alizozileta na Yunde zinaukweli wowote.
"Aya binti ongoza njia".
"Sawa mfalme"
"Kuna vijana wengine mpaka wapewe fundisho ndio wakome kuchezea na watoto wa kifalme".
Yunde alianza kujilaumu baada ya kusikia maneno ya Mfalme na ndani ya nafsi yake alipingana na maamuzi aliyoyafanya ya kuleta tarifa zile kwa mfalme na safari ilianza ya kuwapeleka yalipo makazi ya Prince Yao.
Haikuchukua mda mrefu wakawa wamefika mahali husika na mfalme hakuamini kile alichokiona kwa binti yake Nailet,
"Ni ujinga gani huu unaofanya hapa??"
"Babaaaa!!!!!!!
"Yani umemshika mkono huna ata wasiwasi aya kamata huyu kipofu na mama yake haraka sana".
"Baba hawana kosa lolote lile mimi ndie mwenye kosa naomba uwaachie tafadhali"
"Wewe ni Binti wa mfalme inatakiwa iwe fundisho kwa vijana wengine kama hawa"
Yunde alikuwa akishuhudia yote yaliyokuwa yakiendelea pale,
Alijutia maamuzi aliyoyafanya na kwa macho yake aliwaona Prince Yao na Lindiwe wakipelekwa katika jumba la Kifalme aliamua kufatilia kuona mfalme atafanya maamuzi gani.
******************
Mandalizi ya sherehe katika ufalme wa ADELI ya kumpolea Prince Cheki au wamchongo yaliendelea kama ilivyo desturi.
Wakati huku gerezani napo mipango iliendelea ya kumtorosha General na temu hii Mlinzi Nzegi aliamua kuwa upande wa General.
Na mda maalumu ulifika wa Cheki kutambulishwa kama Prince, Mfalme Kojo alisimama kumtambulisha mbele ya halaiki,
"Huyu mnayemuona hapa ni Prince wa hili taifa na ndie atakayekuwa Mfalme wa hili taifa kwa badae, popote pale mtakapo muona naomba mumpe heshima yake".
Mfalme alimaliza na kuwafanya watu wapige makofi na kuanza kuimba....
"Princee,princee,mfalme ajaye Γ3,
Prince wa ADELI,Prince mwenye nguvu"
Malikia Andwaa alichukizwa sana na sifa alizokuwa anapewa Cheki ilihali haku sitahili kupewa sifa izo ila hakuwa na chakufanya zaidi ya kuonyesha tabasamu feki.
Wakiwa katika furaha viongonzi mbalimbali ya kumkalibisha Prince tarifa mpya zilifika,
"Mfalme!!mfalme!!! kuna tatizo maneno ha asikari yule aliyekuja kwa kasi yaliwafanya karibu kila mtu asitishe alicho kuwa anafanya na kumsikiliza asikari yule"
"General katoroka gerezani mfalme".
"Unaongea nini wewe na nyie mlikuwa wapi???"
"Mlinzi mkuu alitutoa pale gerezani akisema tuje huku kwenye jumba la kifalme kuna tatizo tulipokuja na kukuta hakuna tatizo tukaamua kurudi gerezeni na hatukumukuta General wala Mlinzi mkuu".
"Ujinga gani huu unaongea", Mfalme aliongea baada ya kusikia General katoroka aliona hatari iliyo mbele yake
"Hakuna cha sherehe......ITAENDELEA.
Mambo ndio yameiva sasa huku Prince Yao mikononi mwa Mfalme Tengu na huku General anafanyikiwa kutoroka nini hatima ya waziri mkuu baada ya kusikia General katoroka na alimsaliti tukutane sehemu ijayo.
MFALME KIPOFU
Sehemi..ya............13
Ilipoishia sehemu iliyopita....
"Ujinga gani huu unaongea,Mfalme aliongea baada ya kusikia General katoroka aliona hatari iliyo mbele yake"
"Hakuna cha sherehe.......
KUPATA MWENDELEZO ZAIDI WA SEHEMU INAYOFYATA BONYEZA LINK YA HAPO CHINI ππππ usisahau kunifollow ππ
https://www.facebook.com/profile.php?id=61550632115006
ENDELEA NAYO...
"Hakuna cha sherehe hapa General atafutwe haraka sana na inatakiwa apatikane kabra siku ya leo haijaisha", mfalme aliongea na kuwafanya asikari watowanyike kuanza msako wa kumtafuta General.
Cheki au Prince feki alichukia sana kuona sherehe imesitishwa,raha za kuwa mtoto mfalme alianza kuziona alikunja ngumi kwa hasira sana,
"Kaka nilikusubili kwa mda mrefu".
Cheki alishangaa ameshikwa mkono na kugeuka nyuma, hakuwa mwingine aliye mshika bali ni binti wa mwisho wa kifalme aitwae Yanni.
Cheki aliweka tabasamu feki mbele ya binti huyo mdogo,
"Usijali mdogo wangu nimekuja kaka yako"
"Princess Yanite alisema huwezi kuja mwangalie yule pale".
Cheki aligeuza macho yake nakumuona Princess Yanite aliyekuwa ameketi karibu na malikia,
Malikia andwaa alimuona Princess Yanni akiongea na Cheki kitendo kilichomchukiza sana na kuamua kuwafata walipo.
Malikia hakutaka kuona Yanni anakuwa karibu na cheki mana alijua sio kaka yake halisi alienda akamshika mkono na kuondoka nae eneo hilo.
"Mama mbona umenitoa nilikuwa naongea na kaka"
"Sasa ivi hapa sio salama yatupaswa tuingie ndani binti yangu".
Malikia hakutaka kujibu alichoulizwa na binti yake ila aliongea jambo jingine ambalo halihusiani na alichoulizwa.
Kila raia alirudi katika makazi yake baada ya sherehe kuingia tahaluki.
***********
"Hahahahahaha atimae nipo huru sasa, temu hii siachi mtu ata mmoja nitauwa wote"
"Ni kweli general hapa inatakiwa tuanze na mtu aliyekusaliti"
"Nzegi una akili sana kama ulikuwa kwenye ubongo wangu ulivyokuwa unawaza, naanza na waziri mkuu kisha anafata Mfalme"
"Ata mimi kuanzia sasa nitakuwa na hesabika kama mharifu niliyekutorosha wewe kutoka gerezani ivyo siwezi tena kurudi katika jumba la kifalme",
Nzegi aliongea na kumfanya General kuelewa zaidi.
Wakiwa katika mazungumzo walisikia sauti za watu wakija upande wao na kuwafanya kutafuta mahali pakujificha.
"Aya nyie pita huku na wengine mpite huku muwatafute haraka sana hakikisheni General anapatikana na Nzegi, ni sauti ya Asikari kiongozi akiwaelekeza wenzake"
Asikari walitii amri na kumuacha peke yake kiongonzi yule aliangaza huku na huku kama kuna asikari yoyote aliyebaki eneo lile na alipohakikisha hakuna aliyebaki aliongea,
"Aya tokeni nyie wapuuzi nimeshawaona tayali"
Nzegi alitoka bira ata kuogopa baada ya kumuona rafiki yake huyo waliyefanya kazi pamoja kwa miaka mingi katika jumba la kifalme
"Nilijua tu huwezi kunitenga ndugu yangu tumetoka mbali mimi na wewe".
"Kwanini umeamua kuwa msaliti kwa Mfalme????".
"Kwa sababu amechoka kuwa mtumwa rafiki yako,General alijitokeza na hakuona haja ya kuendelea kujificha".
"Mnatakiwa mwende msituni mkajihifadhi ni hatari kwenu kwa sasa asikari wamejaa kila sehemu"
"Ungana na sisi ubadilishe maisha yako,General alimwambia asikari yule".
"Itakuwa ngumu sana kuwa upande wenu"
Nani asiyependa maisha mazuri, General alimshawishi kwa maneno mazuri na kumfanya asikari yule awe upande wao na aliwaahidi atawaletea tarifa ya kila kinachoendelea katika jumba la kifalme.
*************
Prince Yao na Lindiwe wanafikishwa kwenye jumba la kifalme huku Princess Nailet machozi haya kuacha kufutika machoni mwake.
"Baba naomba uwaachie hawana kosa lolote lile makosa yote ni ya kwangu, mimi ndie niliye enda kwao kuangalia kama naweza kumsaidia Yao na kumfanya aone ",
"Naona umesahau mimi sio baba yako tu bali ni mfalme wa falme hii ya YUNDI na ni kosa kubwa sana kumdanganya mfalme".
"Hapana maneno yangu ni ya kweli baba"
"Wewe tangu lini ukawa daktari na umejifunzia wapi???,
Kwa makosa yako mwenyewe unamwingiza kijana wa watu kwenye matatizo ni kosa kubwa sana kukutwa kijana yoyote yule amemshika Princess bira ruhusa maalumu,
hukumu yake ni kifungo cha maisha gerezani".
"Hapana Mfalme naomba unifunge mimi na umuachie mwanangu aende,Lindiwe alipiga magoti mbele ya mfalme Tengu na kumuomba mfalme".
"Miaka iliyopita ulikuja ndani ya huu ufalme nikakupokea kwa mikono miwili utafute dawa ya mwanao ila ukayafanya makazi yako ya kudumu inaonekana ndio ilikuwa mipango yako hii"
"Hapana sio ivyo Mfalme"
"Sasa mbona uliamua kuishi kwenye huu ufalme tofauti na makubaliano yetu??"
"Ni kosa langu ilo mfalme ila naomba unikamate mimi umwachie mwanangu".
"Huyo hawezi kuishi bira wewe mana haoni na nafasi ya mwisho ni kuondoka katika huu ufalme nisione sura zenu tena hapa........ITAENDELEA
Mfalme Kojo atafanyikiwa kumshika General kwa mara nyingine?? Na vipi kuhusu Mfalme Tengu atafanya maamuzi gani juu ya Prince Yao tukutane sehemu inayofata
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi
