💋ILA BOSS ANAJUA KUPELEKA MOTO 💋 18
Mida ya jioni vipindi vilipoisha tuliongozana na Glad hadi kwa kaka yake ilikuwa ni saa kumi na moja za jioni hivyo alikuwa kasharudi toka kazini tulimkuta nyumbani 🏡. Karibuni wageni tena ndio naingia sasa hivi toka kazini muda sio mrefu, tulimsalimia tukaingia ndani ilikuwa ni nyumba 🏡 kubwa tu ina fence pamoja na mlinzi nje inaonekana kama ni mpya imejengwa hivi karibuni tu .
Glad wewe sio mgeni hapa nenda kalete vinywaji🍾🍷 kwenye friji mnywe na mwenzio , sawa kaka Glad alienda kuleta soda tukawa tunakunywa taratibu. Kaka nimemleta apaone ili kesho aanze kazi kama nilivyokuelezea hivyo vipindi vikiisha atakuwa anakuja kufanya usafi .
Sawa nimeelewa cha muhimu ni utiifu na uchapakazi tu kuna mtu alikuwa anakuja kunifanyia usafi ila nimemstopisha ili ufanye wewe ili uweze kutimiza malengo yako. Nashukuru 🙏 sana kaka yangu nakuhaidi nitafanya kazi vizuri , Ok ukija mlinzi atakuwa anakupa funguo mimi ngoja nitoke sijui nitawakuta 🤔 kuna mtu nataka nionane naye hapo mwenge . Sidhani kama utatukuta kaka tutakuwa tushaondoka hatuchelewi Glad alijibu , Hamchelewi nini hebu nipikieni msosi hapo mimi nina njaa ndio muondoke kila kitu kipo kwenye friji.
Kaka yake aliondoka tukabaki mimi na Glad kaka na yeye mtu nina miadi yangu anasema tupike tena atanikosesha hela mimi Glad alilalamika jiko liko wapi 🤔 tukapike basi , nilimuuliza Glad kaka naye naona anataka kunizoea mimi nishachoka habari za kupika jamani njoo jiko lipo huku njoo . Kwani hana mke kaka yako ? nilimuuliza hapana awe na mke sasa hivi aringe ana mpenzi tu tena anasoma chuo mwaka wa mwisho pale UDSM ila kozi tofauti na sisi kapuuzi tu , ooh sawa ni jambo zuri haya tunapika nini sasa? nilimuuliza Glad wewe ndio mama wa nyumba 🏡 tu assume ndio upo peke yako haya ingia kwenye friji pika unachoona kinafaa
Sawa nilifungua friji nikakuta kuna maini na mboga zingine nilichukua hayo hayo nikaanza kurosti.,muda huo Glad alikuwa sebuleni anaongea na simu 📱mara akaja jikoni . Nelly nimepigiwa simu na shemeji yako anataka kuniona sasa mimi nataka kutoka ila nitakuja kabla ya kaka hajarudi , Glad ufanye uwahi ujue hajaenda mbali kaka yako, Sichelewi sasa hivi narudi Glad aliondoka nikamkimbilia nje kumuuliza kama nikiulizwa ameenda wapi nijibu nini nilikuta kashaondoka tayari ikabidi tu nirudi ndani kuendelea kupika , nikiwa napika mlango ulifunguliwa nikawa naogopa sijui nani 🤔huyo.
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi


Maoni