CHAGUO LA MOYO ❣️ 6 -- 7
NO 06
Niliamka na kwenda sebleni nikakuta johari haha amka naona itakuwa nimeamka mapema sana ilibidi nikae nimsubiri maana sikuwa najua vifaa vya usafi vinatoka wapi .........nilikaa mda mrefu hatimae akaamka na kunikuta nimekaa ........
"Hee wewe ulikuwa kuwanga au "
"Shikamoo da johari"
"Shika yako Kama nimali alafu siongei Mara mbili hiyo dada ukamuite daa yako huko shamba sio mm"
"Samahani nimesahau"
"Haya nifate nikupe vutu uanze usafi"
"Alinipa vifaa vya kufanyia usafi nikaanza kufanya kazi pale mda huo yeye yuko anapika .......
" Nilimaliza kazi za asubuhi mda mfupi watu wanaanza kuamka ........ Nicole ndio alikuwa wakwanza kushuka.........."mambo soni"
"Poa umeamkaje"
"Salama"....... ......
"Sinimemaliza kufanya usafi"
"Ndio "
"Haya fanya haraka basi maana tunakula pamoja "
"Haya"
"Alafu johari utampa mwenzako nguo basi maana Hana nguo"
"Nimpe nguo kwamba huko alikokuwa alikuwa anashinda uchi au kaona anakuja kiwandani "
"Sema moja unampa au haumpi nasio maneno mengi"
"Mpe wewe mm sivaliani na mtu kwanza mtu mwenyewe amekaukiana kama mgonjwa wa kisonono "
"Johar kauli gani hizo"alikuwa mama mwenye nyumba...... johari alinyea huyo
"Nifate"aliniambia Nicole ......tuliongozana Hadi chumbani kwake ........mmm humu analal mtu au malaika maana sio kwa chumba hiki
"Haya chugua nguo unayoona inakufaa hapa "alisema Nicole baada ya kufungua kabati la nguo
Mmmmh hizo nguo ni fupi balaa .......
Nilichagua lakini hazikunitosha
"Heee pole, ngoja nikaongee na mama ukanunue baadae sawaee"
"Sawa"
Tulishuka chini na kukuta watu wako mezani ....... Aloo
Hawa ni watu au majini .......niliwaza baada ya kuona waka watatu wamekaa mezani huku kila mmoja Yuko bz na sm yake......
Tulifika mezani Nicole akakaa....... Mimi nikabaki nimesimama
"VP mwanangu mbona umesimama,kaa"
Aliposema hivyo nikisogeza kiti ili nikae mda wote wale wakaka wako bz na sm zao,
"Nyie wekeni sm zenu pembeni ni mda wa chai"alisema Yule mama na wote wakaweka sm pembeni Kisha wakanigeukia alafu wakamuangalia mama yao,
"Sonia"aliniita yule mama
"Abee boss"
"Niite mama inatosha, Sasa Hawa unaowaona hapa ni wanangu,na tunaishi nao hapa wote isipokuwa huyu alievaa blue sawae "
"Na nyie big boy's huyu ni Sonia ni dada mpya atakuwa anahusika na mambo yote humu ndani isipokuwa kupika maana hiyo ni kazi ya johari , hope mtaishi nae vizur sawae"
"Nice to meet you"alisema mmoja wa wale vijana Mara Nicole akadakia............"alafu ni mhindi mwenzio".........
Aliposema hivyo nikakumbuka kuwa alisema kaka (Rahul)yake atafurahi kupata mwenzake.........so huyu ndio Rahul (niliwaza)
"Asante"
"Nimefurahi kusikia kuwa na wewe una damu ya kihindi so Nani muhindi Kati ya baba yako na mama yako"
"Baba"nilijibu mkato
"Okay vizur unamacho mazuri hongera sana"
"Mmmmmmmmmmmm Mara hii"waliguna wote tena kwa pamoja
Nilihisi aibu nikaangalia chini
"What kwani uongo "
"No sio uongo,Ila Mimi nimependa kila kitu 👌"aliongea Nicole
"Mimi nimependa pua"alisema (mkorea) lee
"Mimi lips"alisema (Wang)mchina
"Mimi sauti"(Salim) mwarabu
"Haya inatosha "aliongea mama
"Mara akaja mkaka mwingine nyie huyu alikuwa handsome kuliko wote pale alishtuka akiwa kaweka uso wambuzi blaa,alipofika wote wakaa kimya alivuta kiti na kukaa
"Berat,huyu ni Sonia mdada mpya ndio anashika nafasi ya Victoria".......mama alimwambia Yule kaka aliefika
"Okay"alijibu na kuanza kula
Mmm mbona kauzu hivi na kafika tu watu wote wamekaa kwa adabu ,.......
Berat:"thanks"...... aliongea na kuondoka. Baada ya kuondoka tu Nicole alishusha pumzi Kama vile mtu aliyekuwa amebeba mzigo mkubwa
"Uuuuuuuu"
SEHEMU YA 07
"Nyie mtu Kama Askari wa motoni yaani akija tu kunakuwa na joto"aliongea Nicole
"Afadhali amenisaidia kuwanyoosha".....mama mtu alijibu
"Amesaidia kutunyoosha?badala umuombee awe mtu was kwaida eti unafurahia, nakwambia usipoangalia atakufa single huyo maana hakuna mwanamke mwenye akili zake akaolewe na jitu Kama Hilo"........ alijibu Nicole
"Nicole acha kumuita kaka yako jitu sawa"
"🙄Okay mamy sorry"
Aliinuka na kuondoka,......basi na wengine waliinuka nikabaki Mimi Rahul na johari, Sasa mda huo Johari akaanza kujichekesha pale
"So Sonia unajua kuongea kihindi"
"Hapana kaka"
"Okay nitakufundisha Kama ukipenda"
"Namm utanifundishae"aliongea Johari
"Ili uongee na Nani? Rahul aliuliza
"Jamani sininaongea na wewe "
"Tutaongea nn Mimi nawew ?"
"Kama tunavyoongea hapa "
"Sonia byee tutaonana baadae "
"Sawa kaka baadae"
Aliinuka na kuondoka basi Johari alibaki amevimba Kama andazi lililozidi amira 😏 niliamka nikaondoka akabaki amekaa pekee yake...........
Basi mida ya jioni wote walirudi kutoka kazini
Mimi mda huo nikiwa bz na kazi zangu
"Mamboo Nia"alinisalimia Lee
"Poa shikamoo kaka"
"Wewe ukijibu poa inatosha sijawa mzee kiasi hicho"
"Sawa kaka"
Akaondoka kuelekea chumbani kwake
Walipita wang, Salim. Nao wakanisalimia na kwenda chumbani kwao
Mara Rahul alirudi na kuja mahari nilipokuwa napasi
"Hi Sonia"
"Shikamoo kaka"
"Marahabaa hujambo😁"aliitkia na kucheka,
🤔Sasa kwann anacheka au nachekesha
"Aaaa nimekuletea zawadi hope utaipenda"
Nilipokea na kumshukuru
"Asante"
"Karibu"alijibu na kuondoka
Sasa nilifungua ilikuwa ni chocolate nilitabasamu na kufungua mdomo ili Nile alikuja Johari akanikwapua na kuiweka mdomoni kwake
😳😳
"Unashangaa Nini, sinilikwambia ukae mbali na mwanaume wangu"
🙄 Mwanaume wangu miguu yangu angekuwa mwanaume wako siangekuletea mwenyewe 😏(niliwaza hivyo)
"Kama hauta sikia nitakunyoo......kabla hajamaliza kuongea alipita uso wambuzi aka Berat na ukauzu wake akatupita shwaaa
Alitupita na Kama upepo bila hata salamu ............wote tukibaki 😦😦
"Yaani huyu kauzu utafikili bluce Lee sijui hata nani ataolewa na kauzu hivyo"
Aliongea Johari na kuondoka
Mda wakula ulifika wote tulikaa mezani mda huo hamna hata anae kohowa kila mtu kainama kwenye sahani yake ,........Kama kawaida kauzu akawahi kumaliza na kuondoka yaani aliinuka tu watu wakashusha pumzi na kuonza kuongea
Mmmm🤔kwani nin huyu kaka anaogopeka hivi (nilijiuliza)
"Nicole inabidi kesho uende na Sonia kununua nguo"
"Mama nitaenda nae Mimi"alidakia Rahul
"VP hauendi kazini au"
"Nitaenda Ila nitawahi kurudi"
"Sawa"
"Mama na mm nimeishiwa nguo"aliongea Johari
"Haya na wewe utaenda"mama alimjibu
"Ataenda mwenyewe sianayajua maduka yalipo"
"Heee kwaiyo tutatoka tofaut"
"Hilo sio swali ni sentence, asanteni kwa chakula"
Alijibu na kuondoka Sasa Johari alinigeuki na kunipiga jicho hilo
Mimi nikajifanya biz kula
Tulimaliza kulamm nikaenda kuosha vyombo mda huo Johari akaja
"Kesho ukatae kuwa hautaki kwenda na Rahul"
Heee huyu dada vp
"Kwanin"
"Wee kam unataka kukaa humu ndani fanya ninachokuambia laaa sivyo utarudi polini kwenu
🥺🥺 Jamani
Nilimaliza kazi nikaenda chumbani kwangu nilifika na kujitupa kitandani Mara nikaona kikaratasi kimeandikwa (good night)sikuwa najua kusoma kilichoandikwa hivyo nikaishia kukiweka pembeni tu na kulala zangu
Asubuhi na mapema niliamka na kuanza usafi kama kawaida mara kauzu akaja nilipo na kusema.........."ufue nguo zangu na ubadilishe mashuka"
Mimi nikajifanya najua sana heshima nikamwamkia
"Shikamoo kaka" hakuitika badala yake aligeuka na kuondoka
Hivi huyu kaka anamajini au sio mtu wa kawaida ...........mara nikasikia mtu ananijibu nyuma yangu
"Hana majini ila sio mtu wa kawaida huyu"niligeuka alikuwa Nicole
"Mamboo"nilimsalimia
"Poa, yaani Kati ya mtu unaetakiwa kumuogopa na kukaa nae mbali ni Berat huyu kiumbe Hana matani wala hataki mazoea na mtu yoyote kwanza haoni ajabu kukufukuza
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi

Maoni