Simulizi za Maisha,Mafunzo,Mapenzi ,Chombezo Habari za Michezo na Burudani vyote kwa Kiswahili ndani ya β Gonga94 Semajambo
Gonga94 Β· Stories
17 Jan 2026
83 views
VYOTE NDANI GONGA94
MZUNGU TULIA MOYO HAUNA RANGI SEHEMU YA 5
Usimulizi huu ni wa watu wazima. Chukua muda wako, tulia, kisha usome kwa utulivu kama machapisho yetu yanayoendelea moja kwa moja.
Sikusubiri Sada aniulize nilizama ndani ya gari nae akanifuata.
"Love, kuna nini lakini?" aliniuliza baada ya kunikuta mule
"Ah! da Sada jamaniπ€¦! hii kazi balaa! dereva ebu ongeza mwendo basi!" nilisema kwa upole. Yule kijana alitabasamu kisha akalipiga gari fimbo. Punde tuliwasili hapo kazini. Tukashuka na kuanza majukumu yetu sasa. Niwe mkweli, maandazi yangu yaliopendwa sana kiasi ya kwamba nilikuwa napika hadi napika tena. Ila kulikuwa na wanaume wanakanda unga, ni mimi nawaelekeza viungo. Sasa kuna mdada akaja, Zai kama mnakumbuka alinikuta jikoni.
"Love, samahani! naona una kazi lakini kuna mtu anataka kukuona" Zai alisema akiashiria kule nje
"Zai nani tena na unaona kabisa kuna wateja bado wanahitaji maandazi" nilisema nikimuonyeshea maandazi
"Nae pia ni mteja ila ameshakula tayari" alisema Zai. Nikatoka hivo hivo na dera langu. Lakini kumbuka msomaji kuwa: boss alinisainisha mkataba, kisha akasema kama nataka kubaki na dera kazini, nijitahidi nsitoke jikoni hadi nitakapo maliza kazi. Sasa hapo masharti shwaaa yanavunjika.
"Ndio, nimeitikia wito" nilisema baada ya kumfikiliza mteja huyo. Alikuwa mzee hivi wa kizungu. Akanisifia pale kwa kingereza kisha akanipa pesa. Nilikataa ila baadae nikachukuwa. Nikarudi zangu jikoni.
Nikiwa naendelea na kazi, simu yangu iliita namba ngeni, nikapokea.
"Njoo haraka ofisini" alisema boss, na ndie alikuwa kanipigia simu. Tena hakusubiri jibu langu, alikata moja kwa moja. Nishaanza kumzoea boss wangu hivo hakunipa shida. Nilimkuta ofinisi, akiwa na Sonia tena Sonia, alikuwa kamkalia boss mapajani.
"Wewe tena! unaingia bila kubisha hodi" kilisema ki Sonia. Yaani jibu ningekuwa hili: sasa boss wako si aliniita na alikuwa anajua kuwa nakuja. Hapo nilijibu kimoyomoyo, sikutaka kujibu kwa sauti mwisho nigombezwe na hili li boss.
"Samahani madam haitajirudia tena!" nilisema kwa upole
"Okey. Baby umemwita huyu au?" Sonia alimuuliza boss
"Yeah tuna kikao kidogo" alisema boss. Sonia alituacha, tukiwa na boss. Jamani fanyeni maombi sasa.
"Naam boss, nakusikiliza" niliketi nikiwa mwoga sana lakini hata hakuongea, zaidi alinisogelea akiwa na mfuko; akanikabidhi.
"Ya nini hii boss?" nilimuuliza huku nikimtazama
"Nimechoka kukuona na hizo dera mbili kila siku, haya kuanzia leo uniform zako ni hizo" alisema hivo kisha akaendelea kuangalia laptop yake. Nilifurahi kupata nguo mpya, nikamshukuru kisha nikaondoka zangu. Sada alinikuta nabadili mavazi, kwenye chumba husika.
"Haya naona ndio unajiandaa, mi naondoka" alisema akiwa anasubiri jibu langu
"Sawa ila uniwekee ugali kipenzi" nilimwambia hivo Sada. Nilimsindikiza hadi zilipo boda, akaondoka ndio nikarudi.
Nilijielekeza moja kwa moja hadi kwenye chumba nilichoelekezwa kuna mgonjwa...natakiwa kumfanyia massage.
Niliingia moja kwa moja bila kubisha hodi maana niliambiwa kuwa ni mgonjwa kalala tu kitandani. Ghafla namkuta Sonia.
"Khaaa! we binti, mbona unanifuata sana?" aliniuliza Sonia
"Mimi nakufuata wewe? kwa lipi hasa?" nilimjibu kwa jeuri sasa.
Tuliendelea kuzozana hadi tukasikia kitu kinaanguka chini kama mzigo. Tukageuka kutazama tobaaaaπ³ bibi!
To be continued.....π₯
Maoni
You're not logged in
X
Login
X
signup
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa
+ Endelea kugundua zaidi
SHAMIRA Sehemu ya58&59
Wassap; 0742443214 Mwandishi; lissa wa huru media nikanunua chakura kwanza ndani.kisha kesho yake niliamkia hopitali sa...
πππππππππππππ Mwandishi; 0742443214 Mwanangu alifika mwaka ila ata kutembea alikuwa hawezi husna akanambia wewe uyu mtot...
*AFANDE MILLANπ* *season 3* *SEHEMU YA HAMSINI NA SITA*
π¦π¦π¦π¦π¦π¦π¦π¦π¦π¦π¦π¦π¦π¦π¦π¦π¦π¦π¦π¦π¦π¦π¦π¦π¦π¦π¦π¦π¦π¦π¦π¦π¦π¦π¦π¦π¦π¦π¦π¦π¦π¦π¦π¦π¦π¦π¦π¦π¦π¦π¦π¦π¦π¦π¦π¦ Daaah basi mwanangu ibraaa ndo akanipanga hivyo kwamba, nitafut...
48 MWISHOOO πΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌ Mwandishi; lissa wa huru media Kesho yake ...
46 MPAKA 47 πΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌπΌ Mwandishi; lissa wa huru media Yani niliba...
Sikusubiri Sada aniulize nilizama ndani ya gari nae akanifuata.
"Love, kuna nini lakini?" aliniuliza baada ya kunikuta mule
"Ah! da Sada jamaniπ€¦! hii kazi balaa! dereva ebu ongeza mwendo basi!" nilisema kwa upole. Yule kijana alitabasamu kisha akalipiga gari fimbo. Punde tuliwasili hapo kazini. Tukashuka na kuanza majukumu yetu sasa. Niwe mkweli, maandazi yangu yaliopendwa sana kiasi ya kwamba nilikuwa napika hadi napika tena. Ila kulikuwa na wanaume wanakanda unga, ni mimi nawaelekeza viungo. Sasa kuna mdada akaja, Zai kama mnakumbuka alinikuta jikoni.
"Love, samahani! naona una kazi lakini kuna mtu anataka kukuona" Zai alisema akiashiria kule nje
"Zai nani tena na unaona kabisa...
π Soma zaidi hapa: https://www.gonga94.com/semajambo/mzungu-tulia-moyo-hauna-rangi-sehemu-ya-5
Maoni