CHAGUO LA MOYO ❣️ SEHEMU YA 01--- 05
MTUNZI RITHA STORIES
WHATSAPP 0754380244 AU 0680992844
SONGA NAYO.................
Mpenzi msomaji Leo na kuletea kisa hiki Cha mapenz ambacho Kita kufunza mengi na kukusisimua,kukufurahisha, na kukuhuzunisha pia
Karibu tuende wote👇
Unaweza kuniita Sonia Arjun
Ni binti wa miaka 22 nilizaliwa mkoani songea,
Nikiwa na miaka 2 mama yangu alifariki hivyo nikabaki nikilelewa na Bibi yangu ambae nae alifariki nikiwa na miaka 10 baada ya bibi kufariki ndugu walikaa kikao ili kujadiliana Nani atakae nichukua na kuhusu huduma hasa shule.
Pacha wake mama (ma mdogo) alisema yeye atanichukua na atakuwa akinisomesha yeye mwenyewe ,
Kweli nilifurahi maana nilikuwa nampenda sana ma mdogo hivyo siku ya safari ilifika tukaondoka kuelekea mwanza ambako yalikuwa makazi yake,haikuwa Mara yangu ya kwanza kufika nyumban kwake kila Mara tulipokuwa tunafunga shule nilienda hivyo sikuwa mgeni kwenye familia yake,
Tulifika nyumban tukapokelewa na watoto wake pamoja namsichana wa kazi mamdogo aliniambia nikaoge Nile alafu nipumzike na mm nikatii na kufanya Kama alivyo niambia.
Kesho yake mchana alituita wote sebleni Kisha akaongea
"Nimewaita hapa ili kuwa mbia kuwa kwanzia leo Sonia atakuwa anakaa hapa na sisi"
Baada ya kusema hivyo mtoto wake wa kwanza(joy) aliongea
"Heee mama kweli ee nilikuwa nataka Nije kukuombea hilo hilo afadhali maana nampenda
Sana da Sonia"
"Aaaha! vizur sasa nataka muishi vizuri kwa upendo sawaee"alisema mamdoga
"Sawa mama"tuliitikia wote akaendelea kutuambia mambo mengine alipomaliza tulirudi kucheza,
Juma tatu walienda shule mm nikabaki nyumban na dada,jioni aliporudi kutoka kazi iliniita nakuniambia
Mwanangu naomba univumilie kidogo nikamilishe Mambo yako ili uweze kwenda shule sawaee "
Nikajibu "sawa "
SEHEMU YA 02
Baada ya kumjibu aliniambia sawa unaweza kwenda
Niliinuka na kurudi jikon
Wiki iliisha nikiwa nashinda nyumban
Siku moja alikuja mmama hivi akagonga nikaenda kumfungulia, aliingia ndani na kukaa Mimi nae huyo ni kaenda kumuita mamdogo
"Mamdogo Kuna mtu amekuja yuko sebleni"
"Mtu gani"
"Simjui
Okay nakuja.
Nilirudi na kummwambia amesema anakuja"
"Sawa binti"
Nilitoka na kwenda kwa wenzangu ambao walikuwa chumbani,kabla sijafika chumbani dada aliniita nakunipa nimpelekee mgeni mimi huyo nikapeleka na kumkuta mamdogo ameshafika
"Hee Martha kumbe umtoto mzuri hivi jamani,unajua sikuwahi kujua Kama umeolewa na mtu mweupe"
"Hapana huyu sio mtoto wangu ni wa marehemu dada yangu"
"🥺🥺ooo!jamani kumbe mama yake amefariki duh kanatia huruma bado mdogo Sana, Ila dada ako alizaa bwana khaa mtoto mzuri Kama nn ona unywele ona sura yake🥰aki nimempenda bure dada yako alikuwa ameolewa na mahindi au mwarabu maana sura yake ilivyo Kama muhindi alochanganya na mwarabu vile au nakosea" Sasa bwana nilivyokuwa kihele hele nikaropoka
"Hapana baba yangu sio mwarabu ni muhindi"weee niliona mamdogo kanikata jicho Hilo balaa mwenyewe nikageuza na kuondoka,
Sasa Yule mama Hadi anaondoka alikuwa akinisifia.
Baada ya kuondoka mamdogo aliniita na kuniambia
"Wewe ninani aliye kwambia nikiwa nimakaa na mgeni wewe unakaa au kuongea kitu,hiyo tabia ikome kwanzia leo sawaee
"Sawa "nilijibu na kuondoka baada ya kuambiwa niende,
Sasa watu walifululiza kuja pale nyumban naona no kumfariji kwa msiba,Sasa kila aliye kuwa akija alikuwa ananisifia kuwa ni mzuri sana jambo ambalo halikumpendeza mamdogo.
Baada ya watu kupunguza kuja nyumban,siku hiyo aliniita na kuniambia
"Kwanzia leo huruhisiwi kutoka/kuja sebleni mgeni yoyote akiwepo unanisikia ?"
"Ndio mamdogo"
Basi ilipofika jioni mamadogo akaniita na kuniambia niende nje kwa kaka was getini aninyoe nywele,yaani nilijihisi moyo 💔 vile napenda nywele zangu sikutaka kunyoa Ila sikuwa na jinsi basi kinyonge nikaenda kwa kaka wa getini 🥺
Nifika nakukaa alichukua wembe kutaka kuninyoa Mimi nikamstopisha. Kwa kusema mjomba siunatumia mkasi maana unazipunguza tu akajibu
Hapana mama yako kasema nikunyoe kipara...........😭woii jamani 💔 nikanyolewa bhna baada ya kumaliza niliingia ndani ukweli sikuwa nimependa
Mamdogo alivyoniona tu akasema enhe...... unatakiwa kuwa hivyo na huo ndio utakao kuwamuonekano wako siku zote utakazo kuwa humu ndani. Sawa .........
Sawa 😭😭
Unalia Nini kuna mtu kakupiga au
Aliuliza kwa ukali nikajibu
"Hapana"
"Sasa kinachokuliza ni kitu gani
Nitakupiga sitaki mideko ya ajabu hapa kwangu Mimi sio bibi yako sawaee
"😭Ndio" nikajibu huku nikifuta machozi
"Haya toka mbele yangu"
Nilitoka na kuingia chumbani nilikokuwa na lala na Dada nikajiangalia kwenye kioo kichwa kilikuwa kinawaka bonge la upala nililia pale Hadi nikalala
Sijui ni kitu gani kilitokea Ila mama yangu mdogo alibadilika Sana tena saana allikuwa akinikaripia bila hata sababu yamsingi nilifanya kosa dogo napigwa kipigo Cha paka mwizi
Nilikaa miezi na miezi bila kupelekwa shule kwajinsi alivyokuwa mkali kwangu niliogopa hata kumuuliza
Baada ya mwaka mmoja alimuondoa dada wa kazi kwakusema Hana sababu ya kuajili mtu wakati Mimi nipo,😓
Kumbuka hata shule hajanipeleka.
hivyo nikawa mtu was kazi tu nakumbuka wakati nakuja pale hawakuwa wamelima mboga mboga Ila baada ya dada kuondoka aliniambia natakiwa kulima mboga mboga na kila. Nywele zikikuwa kidogo tu napigwa kipala ........😭😭
SEHEMU YA 03
Maisha yalikuwa magumu upande wangu so kwasababu ya kufanya kazi no Bali matusi navipigo vya mara kwa mara,
Nilikuwa napika chakula lakin sikuruhusiwa kula hadi wao washibe so mara nyingi niliishia kushinda bila kula nilitamani niwe basi na kula jikon wakati napika Ila sikuweza maana aliweka. Camera hadi jikon Sasa ole wako akuone utaomba mbingu zifunguke
Nilimkumbuka Sana Bibi yangu na kumwambia Mungu kwann ulimchukua Bibi yangu 😭😭
Kila siku ilikiwa bora Jana yaani Kama nisipopigwa basi ujue nitatukanwa au sitokula siku hiyo
Chaajabu hata watoto wake nao walinibadilikia wakawa wakirudi shule wanavuruga vitu makusudi mda mwingine kama nimepika chakula nikatoka kumwagilia mboga nje wao wanakuja na kujaza chumvi Sasa mama yao akirudi😭ni matusi na kipigo juu
Hakuna kitu kilikuwa kikiniuma Kama alipokuwa alisema kuwa mama yangu alikuwa Malaya akajiona mzuri na kumpanulia miguu boss wake akidhani atamuoa mwisho aliishia kupata ukimwi 😭
Wakati huo alipokuwa anaongea maneno hayo nilikuwa na miaka 12 tu Mara ooo utakuwa Malaya Kama mama yako na utakufa na ukimwi mbwa wewe ,
Yaani alikuwa akikasirika anichagulii tusi linalomjia ndio Hilo anatoa
Niliendelea kuishi hivyo Hadi nilipofikisha miaka 20
Wakati huo moyo wangu ulikuwa unavuja damu yaani nilitama kuokolewa katika Yale maisha Ila wapi Nani aniokoe Sasa wakati huo nilikuwa nimeshakuwa binti na bado niliendelea kupigwa kipala tu nguo nilizokuwa navaa ukiniona unaweza 😭 nilikuwa nimezishona Shona Sana bila kusahau vilaka vilikuwa vyakutosha nilitolewa kwenye nyumba kubwa n kuhamishwa nyumba ndogo ambayo alikuwa analala mlinzi nyumba yenyewe ilikuwa ya chumba kimoja hivyo mm ndio nililala sebleni kwenye mkeka na shuka liliochakaa Sana huku mlinzi alikuwa analala kwenye godolo tena zuri
Lakini pamoja nashida zote hizo nilikuwa mzuri bhna 🥰 nakipala changu nikatunukiwa shepu ya mama weee nilikuwa mwembamba ndio Ila Kama nimecholwa vile 😁 sio kwamba najisifia hapana bwana ndivyo nilivyo
Basi nilikuwa navaa minguo mipanaa hatari
Nilikuwa kila siku namuomba MUNGU anitoe katika yale maisha Ila Hadi nafika miaka 22 sikuona mwanga au dalili ya kutoka nje 😓 nilikata TAMAA hata ya kuomba tena maana sikuona umuhimu wa maombi maisha yangu yalikuwa ya maumivu kiasi ambacho nilikuwa najiuliza kwann nilizaliwa kwann mimba isinge haribika tu kuliko kuja dunian kuteseka hivi nilivaa nguo ambazo zilikuwa zimeisha yaani nilikuwa naweka vilaka vya kutosha sikuwa hata na nguo ya ndani ,😓 (nadhani utakuwa unapicha ya maisha yangu Kama mtoto wakike kukaa bila nguo ya ndani inakuwaje hasa kipindi cha siku za hedhi)
siku zilienda hatimae ikafika siku ambayo Joyce alikuwa anasheherekea kuhitumu chuo kikuu.........ilikuwa siku ambayo kila mmoja kwenye familia alikuwa na furaha ya kipeke yake nakumbuka niliambiwa nipike chakula Cha watu 100 watakuja kwenye sherehe sikuwa na pingamizi nilipewa vitu vya kupika na kikapewa mda kuwa wakitoka kanisani wakute chakula tayari .......basi niliamka saa kumi nakuanza kuandaa vitu ....mida ya saa moja alikuja mmama moja hivi alikuwa ni rafiki yake mamdogo
"Shikamoo mama Anethi"
"Marahabaa hujambo?"
"Sijambo "
"Nani yupo nyumban"
"Nipo mwenyewe'
"Sasa nisikilize nimekuja kukutorosha kwahiyo vaa hii nguo tuondoke"....😳kutoroka tukikamatwa je sinitauliwa mm
SEHEMU YA 04
Nilifikilia nikikamatwa wataninywa supu😔 Ila siko tayari kuendelea kukaa humu ndani..........nilizama kwenye dimbwi la mawazo mwisho nilistuka baada ya mama Anethi kunivutia ndani ....."hembu vaa hiyo nguo haraka bila hata kuongea niliingia nilikokuwa na lala nikavaa na kuchukua picha ya mama na ya bibi Kisha tukatika nduki mda wote mlinzi alikuwa nyuma ya nyumba akifua nguo zake hivyo alikuwa hajui kinachoendela ....... masikini sijui wakija na kukuta sipo atakuwa kwenye Hali gani Ila Sina jinsi😓........niliacha baadhi ya vyakula jikon watajiju 😏........ tuliingia kwenye gari na kuondoka Hadi stendi kuu ya mabasi .......tulifika akasimama na kuniambia....."Sasa sikia unaenda dar es salaam huko utakuwa mfanya kazi wa ndani kuhusu mshahara ntaelewana wenyew, hakikisha unafanya kazi yako vizur na uwe na malengo najua maisha yako unayajua hivyo ukiharibu huko sitakuwa na msaada tena"...... "Asante sana mama kwa msaada wako" ......... usijali Mimi ni mama nimeshindwa kuona ukiumia kila siku........hakikisha hauvui hicho kitambaa usoni wasije kukuona sawa.......sawa......alishtuka akanikatia ticket na Kisha akaongea na kinda ili alifika ampigie mwenyeji wangu.....niagana nae kwa machozi Kisha nikapanda na safari ikaanza .......na baada gari kutembea kwa mda mrefu hatimae tulifika dar watu walishuka na Mimi nikawa wamwisho nilisubiri mwenyeji wangu nilimkumbusha konda akasema kuwa bado hajafika nilikaa pale Hadi konda akaanza kufoka kuwa anachelewa sana hivyo ataondoka........niliogopa na nikawaza vipi Kama hatokuja😓
Baada ya kusubiri lisaa hatimae alifika alikuwa ni mdada mmoja hivi mrefu mwembamba kiasi mweupe na alikuwa na nywele ndefu Hadi mgongoni ....niliwaza huyu ni mzungu au Ila hapana Hana sura ya kizungu labda kachanganya. ....hello dear sorry nimechelewa kulikuwa na na foleni Sana..... aliongea Yule dada........haina shida shikamoo...nilijibu na kumuamkia........acha zako Mimi sio mkubwa hivyo vo uko wap mzigo wako....... hapana Sina mzingo (sikuwa nimebeba nguo kutokana na nguo nilizokuwa nazo zilikuwa zimechakaa Sana hivyo nilichukua picha tu) nilivyomjibu hivyo hakutaka kuuliza maswali mengi zaidi tuliongozana Hadi kwenye gari safari ikaanza mada wote huo nilikuwa bado nimevaa nikabu ......
Inaitwa Nani(aliuliza)
"Naitwa Sonia"
"Oo! hongera unajina zuri mimi naitwa Nicole"
"Asante"
"Wewe ni mwarabu au mpemba au mhundi, usishangae nimeona rangi yako pamoja na macho yako walivyo ndio maana nimeuliza"......
"Ni mchanganyiko wa muhindi na mtanzania"......wow hatimae Rahul kapata mwenzake".....
(😳 Rahul kapata mwenzake 🤔 Mungu wangu usikute naenda kuuzwa🥺)......."Rahul nikaka yangu yeye baba yake ni muhindi ndio maana nasema kapata mwenzake so usihisi vibaya😊"....... (afadhali maana nilikuwa nimeanza kuwaza)
"So una miaka mingap"
"Nina 22"
"Wow mwezi wangap".
"Wapili"
"Tarehe ngap"
(Huyu dada vp mbona maswali mengi)"tarehe 14"
😲😲 What so tunalingana namm nimezaliwa mwezi wapili tarehe hiyo hiyo wow nimeipenda hii🥰"
Nilitabasamu maan sikujua nijibu nn
SEHEMU YA 05
"Mmezaliwa wangapi"aliendelea kuuliza
"Niko mwenyewe"
"Duh pole, sisi tulizaliwa 7 Ila Sasa tuko 6 na wakike ni mimi tu last born wamama,. Kaka yangu wakwanza baba yake ni mkorea,wapili baba yake ni mturuki,watatu baba yake mchina,wanne baba yake ni muhindi,watano baba yake ni mwarabu,wasita ni mm baba yangu ni mzungu wa marekani yakusini na wamwisho Bab yake alikuwa mtanzania (mpare)....😳😳huyo mama alitaka kuzaa na kila nchi au ...."najua unawaza nn Mimi mwenyewe kila siku nilikuwa namuuliza hivyo hivyo"........huyu dada anaongea hata hachoki Mambo mengine hata sioya kuyaongea ukitegemea tumeonana dakika chache tu huyu siwezi kukwambia Siri yangu anaonesha fliji lake bovu haligandishi😒
Yaani njia nzima alikuwa anaongea tu 😏 baada ya mda mrefu tulifika nje ya geti ..... Alipiga honi na geti lilifu nguliwa 😲nilitoa macho baada ya kuona jumba sio nyumba hili ni jumba palikuwa pazuri kama anaishi mfalme vile,...... Sonia..nilistuka baada ya kuitwa bhn ...abee .......twende ....haraka nilimfuata huku nikishanga sangaa .......wow ndani nikuzuri balaa hembu subiri humu wanaishi watu au majini maana kulikuwa kumepambwa vitu vya thamani Sana ....... Karibu hapa ndio nyumban kuwa huru kabisa..alisema baada yakufika sebleni ...Mara alikuja mmama na kusema mmefika ?.... hapana bado hatujafika .....😁alimjibu Nicole sijui ni Nani yake maana anamjibu Kama vile wanamatani....karibu binti ... Asante shikamoo......
Marahabaa hujambo.......... sijambo...... karibu sana, we johari njoo umpeleke mgeni chumbani kwake......😳 Johari Tena huyu siamesema yuko pekee yake Sasa inakuwaje"...
Alikuja huyo johari mwenyewe alikuwa mrefu mweusi alafu bongee
Shikamoo.... nifate
Hee mbona hajaitikia Sasa au ni mdogo Ila hapana mbona sura imekomaa hivyo...
Waooo chumba kilikuwa kizuri balaa "samahani dada johari hiki ndio chumba changu"
"Hapana Cha Bibi yako,alafu Mimi sio dada yako ukiniita Johari inatosha"
Alinionesha bafu na vitu ngine Kisha akaniambia namna ya kutumia
"Sasa ukatumie vitu tofauti na nilivyokwambia utarudi kijijini kwenu ukalime huko,alafu kingine hiyo minija huruhisiwi kuivaa humu ndani hatutaki uchulo sawae"
"Sawa" nilijibu Kisha akaondoka nilibaki niakuangalia chumba kilivyo kizuri ......... nikaenda kuoga nakushuka chini nilikuta johari anaangalia tv ........
"Chakula Kiko hapo mezani "
" Haya Asante"
............
Nisogea mezani nakufungua hotpot 😋mate yalinijaa baada ya kuona nyama ya kuku kitambo Sana sijala zaidi ya kula harufu yake
Nilipakua na kuanza kula wow chakula kitamu balaa........ Sasa wakati niliendelea kula alipita mkaka mmoja hivi bonge la handsome hatari nilibakia nakijiko mdomoni nikimshangaa Hadi akaishia
Nilimaliza kula nikamshukuru akanielekeza jiko lilipo nikaenda na kuisha vyombo ..........Nyie hapa nipazuri kwanzia ndani hadi nje .........kutokana ni uchovu niliamua kwenda kulala ....... Wakati usingizi ikiwa unanipitia mlango wa mchumbani ulifunguliwa nilishtuka na kukaa ......... oooh kumbe ni Johari ......
"Unashtuka nn au unadhani Kuna wabakaji "
"Hapana "
"Sasa nimekuja kukwambia kitu kimoja kabla kesho haijafika ,humu ndani Kuna wanaume 5 saa unaruhusiwa kucheza na hao wa 4 Ila mmoja kaa nae mbali narudia tena kaa nae mbali "
"Samahani mbona sikuelewi"
"Usichoelewa nn hapo nakwambia kaa mbali na Rahul Ila hao wengine unaweza pita nao "
Alimaliza kuongea na kuondoka Mimi nilibaki nashangaaa tu
Sijui usingizi ulinipitia sangap Ila nilikuja kushituka kumekucha
Itaendelea.......
Full 1000
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi
Maoni