NAKUPENDA BILA SEASON TWO 51 - 65
NAKUPENDA BILA MIPAKA:51
Nilitoka nikiwa nishapendeza hata mama alishtuka na kusema “kulikoni tena?
Nilishusha pumzi na kusema “Acha tu mama ndiyo nishaitwa.”
Mama alinitazama na kusema “huna namna nenda. Sasa vipi pesa ya watu.”
Nikamtazama na kusema “nna kidogo hapa, sasa Leo nusu siku sijui watanipa kiasi gani.”
Mama alisema “usijali mwanangu, Leo nitapata pia hapa tutamaliza tu.”
Nilitabasamu na kusema “Nashukuru mama.”
Nikampa ile pesa halafu nikataka kuondoka, nikakumbuka Yule mama alisisitiza kuhusu maandazi. Nilimgeukia mama na kusema “mama naweza kupata maandazi kumi.”
Mama alinitazama akisema “yote hayo mwanangu?”
Nilisema kwa upole “nakuomba mama.”
Mama alinitazama na kuanza kunifungia.
Alipomaliza nilisema “nashukuru mama, baadaye basi.”
Mama akasema kwa upole “kazi njema.”
Niliweka kwa mkoba wangu na nikaanza kuondoka. Yaani nimechoka Ila nitafanya nini.
Safari haikuwa rahisi eenh sio jirani. Lakini nilifika. Nilipofika dada Maria alisema “Karibu nesi, bora hata umekuja.”
Nikitabasamu kivivu na kuuliza “ni kwema lakini?”
Alinitazama na kusema “mmh, nenda kwanza anakusubiri ofisini.”
Nilimtazama tu na taratibu nilianza kwenda.
Baada ya kufika nilibisha hodi na kukaribishwa. Nilipofika nilikutana na Dokta pale na Boss. Dokta alinitazama kwa maringo na Kisha Boss aliniambia “Karibu.”
Nilitabasamu na kuwasalimia, Kisha Boss alinitazama na kuuliza “kwanini unafanya hivi?, hujafika kazini bila sababu yoyote ile.”
NAKUPENDA BILA MIPAKA:52
Nilimtazama dokta, halafu alitaka kuongea nikamuwahi na kusema “niliambiwa na dokta kuwa leo Atakuwepo siku Nzima hivyo nisifike.”
Boss alimtazama dokta na kuuliza “ulifanya hivyo?”
Akatabasamu na kusema “niliona sio mbaya nitashinda tu na mama maana leo sikuwa na kazı.”
Akamuuliza “na mpaka sasa umeonaje?”
Dokta alinyamaza maana sura ya dokta imechukia mimi hapo moyoni nasema “safi leo kimeumana.”
Boss alisema “unatakiwa kuelewa hii ni kuhusu mama yangu. Ni miaka, ni muda mrefu mama yangu hajawahi kuwa na furaha wala kuona tabasamu lake.
Sasa hivi anaendelea vizuri kwasababu anaelewana na nesi wake wewe tena unaleta maamuzi yako ambayo siyaelewi. Kumbuka nimekuajiri, vilevile na nesi. Unaweza kunichezea vyovyote unavyotaka lakini sio kwa upande wa mama yangu unaenielewa.
Nazwi sikia, unatakiwa kufuata maagizo ya dokta juu ya afya yake na namna ya kumtunza mama yangu. Naomba ufanye kıla namna mama yangu aendelee kufurahi. Nakuomba.”
Nilimtazama na mimi hapo sasa kichwa kama kipasuke, nilisema “sijaelewa, natakiwa kufuata maagizo ya Nani Kati yenu.”
Boss alinitazama na kusema “mimi ndiyo nawalipa ninyi, chochote kile nisikilize mimi kwanza. Dokta akupe maagizo ya dawa zenu na masuala ya afya mbali na hapo ni mimi mnanielewa.”
Nilimtazama tu kachukia, dokta aibu kainamisha kichwa chini kachukia balaa. Mimi nilisema “nimekuelewa naweza kwenda kwa mama sasa.”
Boss alitikisa tu kichwa, niliinuka kufika mlangoni akasema “hakikisha anakula tafadhali.”
Nilitabasamu.
Nimefika tu mlangoni, nasikia dokta analia huko na madeko yake “how dare, eenh unanifokea mbele ya mtoto mdogo Yule. Hivi ulishindwa hata kusubiri na kuniuliza kwa namna nzuri.”
Mr Gallen alisema “ni kuhusu mama yangu nataka uelewe, sitakumbuka wewe ni rafiki yangu, nitasahau kıla kitu kama huwezi nitii. Napenda mwanamke ambaye anajua mipaka yake unanielewa.”
Dokta sasa na kizungu chake “what do you mean?, unataka kusema sijui mipaka yangu. Hivi kweli huyu binti ndiyo atuchanganye.”
NAKUPENDA BILA MIPAKA:53
Nilitabasamu na kusema “niondoke hayanihusu, nyie endeleeni kugombana. Asante boss kwa kunichambia huyu dokta wako.”
Nilitabasamu na kuondoka zangu kuelekea chumbani kwangu ninapo badilisha nguo zangu.
Vile natoka tu, dada Maria akanivutia jikoni, Nikamtazama na kusema “dada ujue nna kazi, naomba sahanı kwanza.”
Dada Maria alinitazama na kusema “wewe nesi wewe, kwanini hukufika?. Ninavyokuambia mama kıla muda ni Nazwi, mpigieni nesi nesi. Boss Leo hata kazini hajaenda kwasababu mama hana raha mpaka sasa hajala chochote.”
Nilimtazama na kusema “usiniambie mama hajala kitu, naomba sahanı tafadhali.”
Alinipatia, Nikamtazama na kusema “tutazungumza baadaye.”
Akaitikia tu kwa kichwa. Nikarudi chumbani, na kuchukua maandazi yangu nikaweka vizuri na kuelekea chumbani kwa mama.
Nilifika mpaka mlangoni, nikatengeneza tabasamu na kuingia sahanı nikiwa nimeficha kwa nyuma nikisema “mama!!, mama yangu nimefika.”
Mama alikuwa amejilaza tu kama kawaida Ila ametazama kwingine. Alionekana amechoka sana na hakuwa na furaha. Niliita tena “mama ni mimi Nazwi, nimefika.”
Kwa taratibu alinigeukia na Nilitabasamu, nilikuwa tu nalazimisha ili mama asijisikie vibaya si unanielewa Tena vile najua mama kanuna.
NAKUPENDA BILA MIPAKA:54
Başı nikamwambia “mama otea nimekuletea nini!!”
Alitabasamu na kusema “msichana wangu, usirudie wewe ndiyo umekuwa rafiki yangu tunaelewana. Sasa kwanini hukuja kazini?”
Nilimtazama na Kisha alisema “nataka kujua kama utasema kweli au utadanganya kwasababu mimi tayari najua.”
Nilimsogelea na kusema “mama yangu, Subiri kwanza. Unatakiwa kula, tulikubaliana kwenye hili kwasababu dawa zako ni Kali sana. Sasa niambie, chai au juisi.”
Alinitazama na alinijibu “chai, chai yangu na chai yako.”
Nilitabasamu na Kisha nikamuonesha ile sahanı. Mama alitabasamu, alitabasamu akisema “mwanangu, usinambie umeniletea maandazi. Kabla hujaenda kuchukua chai Naomba moja.”
Sasa vile anaongea kiupole, napenda sana. Mimi natabasamu na kumpatia. Alipokea, nikaweka na kusema “nakuja mama yangu.”
Alisema kWa upole “nakusubiri.”
Nilicheka na kutoka, mpaka jikoni na kuomba chai. Dada Maria alinitazama, nikaongeza “vikombe viwili.”
Alinipatia mimi nikaingia chumbani, mama aliponiona alisema “wewe Nazwi mama ana mgahawa, haya maandazi zaidi hata ya hotel kubwa nimewahi kwenda niongeze tena.”
Nilicheka na kusema “mama unasema kweli?”
Akasema kWa tabasamu “sasa Kumbe na kwanini nikutanie mwanangu, ni mazuri sana.”
Nilitabasamu na kusema “nikuambie sasa mama nimeandaa mwenyewe mama akachoma.”
Akanishangaa akisema “weee, Ina maana unajua kupika maandazi mazuri namna hii. Kumbe nikipona tutapika, utanifundisha.”
Nikasema kWa upole “kabisa mama, tena utakuwa mpishi mzuri kunizidi.”
Huyu mama alinitazama na kusema “wewe ni msichana mzuri sana.”
NAKUPENDA BILA MIPAKA:55
Nilitabasamu, akaniambia “pole binti yangu, mimi ni mama, ni mtu mzima naelewa. Najua Hampo sawa na dokta na najua kwanini, lakini nikuambie kitu mzoee, na usifanye vitu bila boss wako ambaye ni Gallen. Wewe upo hapa kwaajili yangu unanielewa.”
Nilitabasamu na kusema “usijali mama, tuendelee kula.”
Akasema kWa utani “hivi unafikiri mimi nitaacha haya maandazi, siwezi kuacha mwanangu nitahakikisha namaliza. Kula na wewe. Nikuambie kitu, nimefurahi sana kukuona.
Nilikuwa nawaza siku yangu itakuwa vipi bila kukuona, bila wewe kuwepo hapa kuna namna najisikia wewe ukiwepo hapa.”
Nilimtazama na kusema “nisamehe mama, sasa sitakosa tena.”
Alinitazama na kusema “nashukuru sana binti yangu, nakupenda sana.”
Hii kusikia Nakupenda kutoka kwa huyu mama ilifanya nijisikie raha sana moyoni. Nilimtazama na kusema “nashukuru sana mama, nakupenda zaidi.”
Unaambiwa hivi yaani kwa huyu mama watu wamekuja hapa , manesi na manesi lakini walikuwa hawaelewani na wengine Hali ya mama wanaacha kazı.
Pengine hata walipandisha malipo kwasababu ya kuona ugumu huo, lakini tazama mimi mtoto wa watu maskini ya Mungu, Mungu kasema Nazwi wangu ana mtoto, nyumbani maisha magumu kwanini nisimpendelee, mimi mama ananipenda, mimi na mama tunaiva, tunapika chungu kimoja.
Hata kama kazı ni ngumu, upendo katı yetu unafanya mambo yanakuwa rahisi kwangu na nafanya kazi kwa upendo sana. Nilikuwa namfurahia tu, mama amerahisisha mambo. ukisikia Mungu ana njia nyingi ndiyo kama hivi sasa.
NAKUPENDA BILA MIPAKA:56
Unajua mimi tena nilikuwa nimetoka kula nyumbani, sasa nitafanya nini nampa kampani mama. Mama alishiba, na mimi nikawa nipo vizuri. Yalibaki maandazi manne tu.
Basi nikawa natoa nirudishe jikoni. Mama alisema “Nazwi unataka kupeleka wapi sahani yangu, nawajua hao mimi, watakula maandazi yangu wewe weka hapo, tukiwa tunapiga zetu story nakula mpaka namaliza leo ni maandazi.”
Nikacheka na kusema “mama lakini, sasa ndiyo maandazi siku nzima.”
Akanitazama akisema “maandazi kanibebea mwanangu kutoka mbali wale wengine. Labda na supu si ndiyo eenh.”
Nilitabasamu.
Nikachukua vikombe na kurudisha, dada Maria anatamani tuzungumze lakini mimi sasa ndiyo nipo busy maana chumbani kwa mama bado ni kama nilivyo Acha jana, hata mama mavazi yake ya Jana jioni bado hajabadilishwa.
Nilianza kazi na nikawa nasema “lakini mama hata nisipokuwepo uwe unakula jamani.”
Alinitazama na kusema “kwa uzuri usipokuwepo nitakula ila mtu akikuudhi nachukia sana.”
Nilisema kwa upole “usijali mama, dokta anajitahidi kukulinda umuelewe.”
Alinitazama halafu unajua aliniambia nini, aliniambia “naupenda moyo wako, moyo wa upole, huruma na unyenyekevu. endelea hivi hivi, nilishakwambia kuna neema kwenye unyenyekevu.”
Nilimtazama na kutabasamu.
Nilifanya kıla kitu safi kabisa, ndani ya muda mfupi mama alikuwa amependeza, hata aliniambia “wewe mwanangu kiboko, ndiyo maana nakupenda.”
Nilitabasamu na kusema “sasa hapa mama upumzike halafu baadaye tuendelee.”
Akacheka na kusema kama kawaida na sauti yake ya upendo “kwani leo mwanangu nataka kulala, wala hata silali sina usingizi, si unajua haukuwepo Kwahiyo tulipie muda wetu wa asubuhi. Kwanza niambie mjukuu wangu anaendeleaje?”
NAKUPENDA BILA MIPAKA:57
Nilimtazama na kucheka kidogo nikisema “Namshukuru sana Mungu mama, anaendelea vizuri.”
Akanitazama na kuniuliza “lakini baba yake si anawatunza?.”
Nilijikuta nainamisha kichwa chini, mama alisema “nisamehe mwanangu, nisamehe sikujua utajisikia vibaya.”
Nilimtazama na machozi kunitoka, mama aliniambia “ooh mwanangu, sikujua una maumivu namna hii, kwani nini kinaendelea, niambie mwanangu, mimi ni mama yako naweza kusema neno pengine likafanya usije kubali kutokwa tena na machozi zaidi unakuwa unatabasamu ukisikia kuhusu yeye.”
Nilimtazama na kushusha pumzi ndefu sana.
Kwa maumivu nilisema “nilikuwa mjinga mama, sikuwa na akili hata kidogo. Nilimpenda mwanaume hajawahi kunipenda. Mwanaume muda wote alinidharau, muda wote aliniumiza kwa kunipa matukio ya kutisha na nilivyo mpumbavu bado nilikuwa hapo nalia nikiomba ageuze moyo wake anipende.
Upo muda mama na umaskini wangu nilijimaliza kwake ili mradi anipe thamani lakini hakuwahi kuona. Hakuna uchafu hajawahi kunifanyia, hakuna mama, nimemfumania Mara nyingi kwa macho yangu, nimepigwa Mara nyingi hata na mimba yangu, bado alisema mimi sio ninayestahili, bado alisema mimi Malaya hata mimba Hana uhakika kama yake.
Sikujali hali ya nyumbani nikaongeza mzigo, lakini mama alinipokea, mama hata nilipojifungua mwanaume huyu nilimtafuta na nikamtumia picha bado alisema nisimtafute hana Mpango na mimi wala hatutambui sio mimi wala mtoto. Sijawahi kuwa na mwanaume mwingine, ni yeye tu tangu nimjue, nimeteseka nimeumia, naona kama nimepoteza kıla kitu. Sijui nikuambie nini mama.”
NAKUPENDA BILA MIPAKA:58
Huyu mama alinitazama na alisema “natamani sana mwanangu ningeweza kuinua hii mikono nikufute machozi yako lakini mama yako naumwa sasa ndiyo siwezi, Futa machozi yako nakuomba.”
Sasa na mimi hapo ndiyo nimefungulia machozi, ni kama vile nahangaika kumtafuta baba Priya, ugomvi wetu, matatizo yetu vile ananipiga vinajirudia kichwani. Yale matukio Mara condom, Mara picha na video zao za ngono yaani nalia sana. Ni mwanaume niliamini yeye ndiyo mume wangu.
Nilifuta machozi na huyu mama alisema nitazame mwanangu nikuambie kitu, nilimtazama, alitabasamu akisema “hujapoteza, wewe sio mjinga, wewe sio mpumbavu. Yeye ndiyo kapoteza tena kapoteza mwanamke mzuri sana. Hujakosea kitu, yeye ndiyo kakosea kukubali uondoke. Ulifanya ulichotakiwa kufanya. Ukiwa na mtu unampenda, unamjali na una muheshimu. Yeye ndiyo ana makosa.
Sasa nikuambie Siri yangu Labda utajifunza kitu, mimi sasa ndiyo niliyakoroga haswa mwanangu kipindi cha usichana wangu.Nilikutana na mwanaume, mwanangu ukimuona unasema mwanaume si ndiyo huyu. Başı nakuambia alikuwa ananidekeza, pesa sio shida zake, alikuwa ananipa kıla ninachotaka.Mwanaume Yule alifanya wanaume wengine nione kama hawana maajabu mimi ni yeye tu.
Hapo penzi motomoto na ahadi za ndoa kibao utaniambia nini mtoto wa kike. Başı siku moja nikiwa kwake hapo tena mimi ndiyo najifanya mama mwenye nyumba mwanangu, kwenye kupanga panga tena Baada ya usafi si nikakutana na cheti cha ndoa. Nilichoka.”
Nilishangaa na kusema “mama usinambie alikuwa mume wa mtu?”
NAKUPENDA BILA MIPAKA:59
Huyu mama alinitazama na kusema “acha mwanangu, mume wa mtu na watoto zake wanne mwanangu. Namuuliza kwani anakataa, alikubali huku akisema “nisamehe sana, unajua nakupenda na sitaki kukupoteza hata hivyo mke wangu yupo mbali Hakuna kitu kitaharibika tuishi tu.”
Unajua kuchukia mwanangu, nililia nikisema “wewe ni mwanaume mbaya sana, ni katili kupita kiasi, nakuchukia sana wewe. Kuanzia Leo mimi na wewe başı, kıla mmoja apite njia yake sikupendi tena.”
Sikuwahi kutaka kuwa na mume wa mtu, kuharibu ndoa ya watu, mke wake ajue au asijue sikuwa nataka kuwa na mume wa mtu kabisa maishani. Başı nikaondoka pale nalia.
Nakuambia mwanangu, mwanaume alikuwa anapiga simu, ananifuata mpaka nyumbani anabembeleza anatuma zawadi mimi bado nilisema sitaki.
Kumbe nilikuwa nimechelewa, Baada ya wiki 2 tangu nimuache nikagundua Nina mimba ya miezi miwili. Nililia sana siku hii, ikabidi nimtafute na nimwambie.
Unajua namna alikuwa amefurahi, alifurahi sana, alifurahi kupita kiasi. Na hapo ikabidi turudiane. Wakati huo sasa tunaongea mengi ananiambia mengi kuhusu yeye na familia yake na namna anapanga kuishi na mimi.
Nilijifunza kutafuta furaha na kukubali hali. Unajua kilichotokea, huyu mwanaume mimba miezi 8 alinipotea, kwake hayupo, simu hapatikani, marafiki kıla mtu anasema lake.
Na mwisho wa siku alinitumia ujumbe kuwa nisimjue, na nisiharibu ndoa yake niishi maisha yangu. Mwanangu nilichanganyikiwa nitasema nini nyumbani eenh na wanajua naolewa na sikusema ni mume wa mtu.
NAKUPENDA BILA MIPAKA:60
Nikawa mtu wa kulia sana. Wakati huo wazazi wangu wakawa wafariji ingawa niliwauzi sana. Nikajifungua mwanangu ambaye ndiyo huyo Gallen. Nikaanza kulea, nilikuwa nahangaika huku na kule. İli mwanangu aishi.
Ajira sikuwa nayo, maisha magumu lakini Mungu alivyo wa ajabu alinikutanisha na mwanaume ambaye alinipenda, alibadilisha maisha yangu, alinijali, alinipa jina lake mimi na mwanangu, mwanangu alikuwa wake.
Haya maisha ni kwasababu yake. Alinipeleka nchi mbalimbali, akanifundisha biashara. Unajua kitu kingine, nilipata mtoto wa kike Baada ya kuoana naye alifariki. Unajua alikuwa anasemaje acha kukufuru mke wangu tunaye Gallen anatosha.
Hata nilipokuwa nahangaika nimpatie mtoto alinitia moyo na kuniambia Mungu anajua yote. Kila mtu alijua huyu ni kijana wake wa kumzaa na wanafanana na walipatana sana na mali alimwachia kijana wake.
Alipofariki niliona kıla kitu changu kimekufa, lakini ameniacha na kijana imara sana. Alinifundisha kuhusu Mungu ninayekuambia leo, alinipa heshima, alinijali na kunitetea nilikuwa malkia wake pamoja na yote niliyopitia, alifuta machozi yangu.
Naongea sana mwanangu lakini kuna mahali nataka uelewe. Kuna wanaume wapo tu kwaajili ya kutongezea idadi ya watu tuliowahi kuwa nao. Umekaa unaomba Mungu unahitaji mwenza wa maisha.
Kumbe wakati huo na shetani anasema huyu akipata mume wa maisha atafanikiwa sana. Analeta mfano wake, wewe unafurahia unajua ni Mungu bila hata kumpa Mungu mahusiano hayo unamuachia mwanaume huyo moyo anakutumia anakuacha unalia kesho anakuja mwingine unajua huyu sasa Mungu katenda kumbe walewale, na hawa ni kwasababu hawamjui Mungu, wala hawajalelewa katika malezi ya upendo wa Mungu.
NAKUPENDA BILA MIPAKA :61
Sikia msichana wangu, Acha kulia, Acha unyonge, Acha kujilaumu, koşa ni funzo, na wewe sio wa kwanza kukosea Ila usikubali kurudia koşa hilohilo tena na tena hapo utakuwa huna akili.
Nisikie sasa nakuambia sio kila mtu anayekuja mlangoni kwako kubisha hodi anakuja kwa Nia njema. kwenye maisha yako kıla hatua ndogo unayopiga leo ni mwanzo wa ushindi wako kesho.
Sikiliza msichana wangu mzuri, siku moja kuna mtu atakupenda sana, atakupa upendo mzuri uso mashaka.Mapenzi safi kabisa ambayo hutaojiuliza thamani yako, hutolia kuomba upendwe.
Utapata mapenzi utajihisi malkia, upendo wa kukuheshimu, kukujali, kukupandisha viwango, kukupa furaha, kukupa tabasamu, kubadilisha maisha yako, atakupa jina lake, atakupa kıla kitu chake hata usema kwanini sikukutanana huyu kabla ya yule.
kumbe ilikuwa lazima upitie maumivu ili ukimpata huyu ujue kumtunza na maombi , utoe ushuhuda kuhusu Mungu kama ninavyotoa mimi hapa.
Lakini kwanza unatakiwa ujifundishe kupona hayo maumivu ambayo aliyesababisha hana hata mpango wa kuomba msamaha, unatakiwa kukubali kuwa kuna watu wamepitia zaidi yako. Kwanza hata hivyo umebeba maumivu hustahili, unastahili heshima na mapenzi ya dhati sana.
Usijitese, kubali na Yule mtoto Yule ni zawadi yako na ndiyo maana Mungu anakubariki. Kuna vitu unavyo kwasababu yake, kuna mambo yanakuepuka kwasababu yake, kuna vitu vinakutokea hata hujui ni kwasababu yake.
Acha kujilaumu kwa kuwa na moyo mzuri, watu ni makatili sana huwezi kustahimili roho mbaya. Kıla ulichofanya kwa roho yako nzuri kitarudi Mara elfu hivyo hivyo wenye roho mbaya ni suala la muda tu. Jipende binti.
NAKUPENDA BILA MIPAKA:62
Nakuombea sana Mungu ukutane na mwanaume mzuri, na naamini wapo wengi sana kwasababu hata mimi shahidi, sasa niambie mwanangu ukikutana na mtu mzuri wa kukupenda upo tayari kupendwa?
Nilimtazama tu huyu mama, aliongea maneno mazuri sana. Maneno ambayo Hakuna mtu amewahi kuniambia. Naikumbuka sana hii siku, Nakumbuka maneno ya huyu mama kwenye hadithi ya maisha yangu yeye ni Kama usukani wangu. Ni mgonjwa wangu, nimekutana naye Kama mimi ni nesi wake lakini amegeuka kuwa wa maana sana kwenye maisha yangu.
Akaniita akisema “Nazwi utaendelea kulia Baada ya yote haya binti yangu, hustahili kulia. Mungu anakupenda sana unanielewa mwanangu.”
Nilifuta machozi na kusema “najilaumu kwanini siku zote nilikuwa nalia mama Kumbe sijapoteza kitu na zaidi mimi ndiyo nimefanikiwa sana. Nashukuru sana kwa maneno yako mama, nimefurahi sana. Wewe ni mama mzuri sana. Maneno yako yamefufua maisha yangu mama. Sijui niseme nini unielewe lakini nataka ujue kuwa kuanzia Leo mimi sio Nazwi Yule wa zamani, nimebadilika, nimekubali, na nitakuwa mpya mpaka siku yangu ya mwisho mama. Nakupenda sana mama yangu.”
Mama huyu alitabasamu akisema “sasa haya ndiyo maneno ya msichana shujaa. Nakupenda sana nesi wangu, wewe ni furaha yangu. Sasa mwanangu Leo nilikuwa na siku ngumu kidogo, nimeongea sana. Nimechoka, nataka kupumzika.”
NAKUPENDA BILA MIPAKA:63
Nasemaje mimi, nafanya nini tena bada ya mambo mazuri mama huyu ameniambia. Nilikuwa nafurahia hata kumlaza nikisema “ni kweli mama, ni kweli umeshachoka. Nisamehe mama nimekuchosha.”
Mama alikuwa anatabasamu tu, Kisha nikamlaza vizuri na Mimi. Nikakaa kwa kiti nikimtazama mama hata alilala.
Nilikuwa Namshukuru Mungu kimoyomoyo, vile nilikuwa mpumbavu sijamuachilia mtu ambaye hata kusema nimekosa hawezi. Nilishusha pumzi yangu na kutabasamu, nikafuta machozi yangu nikisema “nimebadilika mimi, mimi ni mpya, sitalia kwaajili yake kamwe, mimi ni Nazwi mpya.”
Nikavaa tabasamu pana usoni.
Unajua sasa ukikaa huna cha kufanya eenh si nikaanza kukumbuka dokta kafokewa mbele yangu hadi analalamika kwanini mbele yangu. Nikajikuta nacheka na kusema “Leo boss umeninyooshea slay queen, safi sana.”
Basi nikawa natabasamu, namkumbuka Mr Gallen natabasamu.Yale maneno ya mama, halafu picha inakuja Kama Mr Gallen, vile Dee anasema akikutaka kubali. Mimi sasa naona Kama ndiyo amenitaka. Ni anavutia jamani mimi naona nampenda huyu Tajiri, Ila yeye Hana huo muda, hata kuniwaza sijui maana hatuendani hata kidogo.
Subiri kwanza, embu mniambie kwani mapenzi ni nini?, mapenzi ni kukaa unamuwaza mtu halafu unatabasamu, au ni kila ukikaa unachekacheka tu. Mungu wangu, Mungu wangu!!, na vile mimi napenda kutabasamu basi hapa nishatabasamu mpaka nachanganyikiwa.
Naona nishapotea mwenzenu, huyu Mr Gallen ni Kama ananikaba moyo wangu sipumui vizuri. Naona Kama nampenda vile lakini sasa si ni mkubwa sana kwangu. Mimi sijui Ila mpaka hapa nilipo nahitaji maombi tena tatu kavu.
Huyu mama alilala sana, alilala mpaka jioni imefika hakuwa ameamka na anatakiwa kupata dawa.
NAKUPENDA BILA MIPAKA:64
Nikawa tu namtazama, natazama muda naona sasa bora nimuamshe. Taratibu nilianza kufanya hivyo. Baada ya muda mama aliamka na kunitazama akisema “nimelala sana.”
Nilitabasamu na kusema “ni kweli mama, sasa unatakiwa kula na kupata dawa.”
Alinitazama tu, na mimi nilianza kazi zangu. Nilihakikisha na yeye amekuwa safi kabisa. Sasa mpaka muda huo dokta hajafika. Nilisubiri bila mafanikio, Baada ya kuona muda unazidi kwenda niliwaza tu niende kwa boss. Hata sijaenda yeye ndiyo alifika pale ndani. Alinitazama na kuniuliza “mama anaendeleaje?”
Mimi na kutabasamu tena nikimuona muanko wangu ndiyo nachanganyikiwa, Nilitabasamu na kusema “naendelea vizuri.”
Mama alisema “mwanangu, njoo ukae karibu na mimi.”
Alikuwa ana mwita kijana wake.
Mr Gallen alipofika kwa mama yake alimshika mkono, akanitazama na kusema “unaweza kwenda , kesho uwahi.”
Nilitabasamu tu.
Sasa niliona sijui Kama ananitazama vizuri kwa upendo, nilivyotoka natabasamu tu. Mara nikaona dada Maria ameniita kwa ishara. Nikamfuata, aliniambia “nesi Leo dokta katoka kwa hasira hapa Kama ungemuona.”
Nilimuuliza Kama sijui vile “kwanini tena?”
Dada Maria akasema “Nadhani wamegombana.”
Nilishusha pumzi na kusema “ndiyo maana hajarudi. Watajua wenyewe mimi najiandaa niondoke kesho tutaongea dada.”
NAKUPENDA BILA MIPAKA:64
Nikawa tu namtazama, natazama muda naona sasa bora nimuamshe. Taratibu nilianza kufanya hivyo. Baada ya muda mama aliamka na kunitazama akisema “nimelala sana.”
Nilitabasamu na kusema “ni kweli mama, sasa unatakiwa kula na kupata dawa.”
Alinitazama tu, na mimi nilianza kazi zangu. Nilihakikisha na yeye amekuwa safi kabisa. Sasa mpaka muda huo dokta hajafika. Nilisubiri bila mafanikio, Baada ya kuona muda unazidi kwenda niliwaza tu niende kwa boss. Hata sijaenda yeye ndiyo alifika pale ndani. Alinitazama na kuniuliza “mama anaendeleaje?”
Mimi na kutabasamu tena nikimuona muanko wangu ndiyo nachanganyikiwa, Nilitabasamu na kusema “naendelea vizuri.”
Mama alisema “mwanangu, njoo ukae karibu na mimi.”
Alikuwa ana mwita kijana wake.
Mr Gallen alipofika kwa mama yake alimshika mkono, akanitazama na kusema “unaweza kwenda , kesho uwahi.”
Nilitabasamu tu.
Sasa niliona sijui Kama ananitazama vizuri kwa upendo, nilivyotoka natabasamu tu. Mara nikaona dada Maria ameniita kwa ishara. Nikamfuata, aliniambia “nesi Leo dokta katoka kwa hasira hapa Kama ungemuona.”
Nilimuuliza Kama sijui vile “kwanini tena?”
Dada Maria akasema “Nadhani wamegombana.”
Nilishusha pumzi na kusema “ndiyo maana hajarudi. Watajua wenyewe mimi najiandaa niondoke kesho tutaongea dada.”
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi
Maoni