Menu






Simulizi za Maisha,Mafunzo,Mapenzi ,Chombezo Habari za Michezo na Burudani vyote kwa Kiswahili ndani ya – Gonga94 Semajambo

NAKUPENDA BILA MIPAKA  36 - 45
Gonga94 · Stories

NAKUPENDA BILA MIPAKA 36 - 45

Usimulizi huu ni wa watu wazima. Chukua muda wako, tulia, kisha usome kwa utulivu kama machapisho yetu yanayoendelea moja kwa moja.


:36
Sijapenda kabisa, binti alisema wanapika kwao, ina maana wewe huli kabisa huko nje kwasababu una uwezo au ni kwasababu gani. Kumbuka na wewe hapa umeajiriwa kwaajili yangu, kwanini haujali hisia zangu.”

Nikaona eenh kumbe mama ana maanisha, nikasikia dokta anasema “lakini mama sikujua kama una hamu namna hiyo na maandazi. Sio kwamba hutakiwi kula lakini kwa usalama wako mama yangu.

Kama unapenda sana bora tuone hapa wanapika kwa usafi. Nisamehe mama, sikujua nitakukwaza na unajua hutakiwi kukwazika si ndiyo mama.”

Nikaona nisije sutwa mie nikaondoka zangu. Sijui waliongea nini zaidi ila baada ya dakika kadhaa dokta alitoka amekasirika hata macho yake naona kabisa amekasirika.

Halafu alinitazama na kunipa Ishara nimfuate. Nilimfuata kwa hofu, alikuwa anaelekea chumba changu cha kubadilisha. Nilipofika alisimama kwa hasira akanitazama akisema “umemwambia nini mama?”

Nilimtazama na kusema “sio kitu dokta, aliulizia maandazi nikamwambia sijabeba.”
Alishusha pumzi na kusema “Nazwi upo hapa kikazi. Fuata kilicho kuleta.

Habari za umbea maneno na mgonjwa wangu sitaki sijui unanielewa. Yule ni mgonjwa hatakiwi kusumbuliwa unanielewa binti. Umekuja kufanya kazi sio kugombanisha watu.”

Nikamtazama na kusema “nimekuelewa dokta ndiyo nipo nafuata kilicho nileta.”

Akanitazama, akanipandisha, akanishusha halafu akanisonya akawa anatoka. Eenh mimi hapo nasema “ya leo kali, ya moto haswa sasa kwani nimekosea wapi. Mboba jeuri sana huyu dada.”

NAKUPENDA BILA MIPAKA:37
Nilijikuta najisikia tu vibaya hata ile hali ya kazi nayo ikanitoka. Nikawa sasa sina la kufanya natakiwa kurudi tu chumbani kwa mama.

Niliporudi, nikawa sio yule mchangamfu tena ingawa nikawa najitahidi sasa. Nilianza kumuweka mama sawa. Nikamvalisha nguo nzuri na kusema “umependeza sana mama.”

Alinitazama tu ni wazi aligundua sipo sawa, nilitabasamu na kukusanya pale nguo na kuweka kitanda safi kabisa. Baada ya hapo nikamrudisha mama kitandani vizuri na kuweka kiti mwendo mahali pake.

Baada ya hapo nikawa naendelea na mambo mengine na hapo dokta aliingia. Alipoingia alisema kwa furaha “sasa mama kuna sindano inabidi nikuchome ndiyo niende.”

Nipo hapo naendelea na kazi, yule mama alisema “usijali binti yangu, Nazwi atanichoma wewe kaendelee tu na kazi.”

Niligeuka kutazama, unajua jicho nimepigwa, nilipigwa jicho ambalo sijawahi kupigwa, alinitazama kwa jicho la ukali na uchungu. Ikabidi nijifanye najali mambo yangu tu kwa maana haya yanaendelea hapa hayanihusu ndewe wala sikio(hayanihusu kwelikweli).

Nilisikia Dokta ananiita kama hajachukia vile, hapo kama naona moyoni anavyosema “huyu nesi ananichukulia nafasi yangu kwa mama.”
Nikaitikia kwa adabu “abee dokta.”

Nikafika pale na yeye alinipa maelekezo juu ya hiyo Sindano, halafu akamuaga mama kwa upendo kisha alipogeuka na kunikata mimi hilo jicho, mpaka naogopa. Aliondoka zake.Nami nikashusha pumzi nikijiongelesha pale ili tu mama asijue lolote linaendelea pale.

NAKUPENDA BILA MIPAKA:38
Mama alinitazama akisema “mwanangu unachoma sindano vizuri sana, akinichoma yeye hapa nitaumwa mkono wiki zima unichome mwanangu.”
Nilitabasamu tu.

Nilimchoma mama sindano, akanitazama akisema “sasa je umenichoma hata sijui kama umenichoma. Nashukuru sana mwanangu.”

Nilimtazama na kusema “usijali mama, nitakuchoma mara zote nitakazo kuwa hapa.”
Mama alitabasamu tu, nikaendelea na mambo yangu. Basi nikahakikisha mama anakuwa sawa.

Nilihakikisha amekula vizuri, amepata dawa zake, yeye alikuwa anafurahia. Sasa wakati tumemaliza kila kitu mama alinitazama na kuniuliza “Upo sawa mwanangu?”
Nilimtazama na kusema “nipo sawa mama wala usijali.”

Alinitazama na kusema “amekufokea na kukutisha eenh?”
Nilitabasamu na kusema “hapana mama, ni sawa kila kitu kipo sawa.”
Huyu mama alitikisa kichwa na kusema “Unajua mwanangu nikuambie kitu?”
Nilimtazama na kusema “niambie mama yangu.”

Alitabasamu na kusema “hakuna kitu kizuri kwenye haya maisha kama unyenyekevu na hekima. Vitu hivi unaweza kuona ni vya kawaida sana hata havina maana na mbaya zaidi hivi vitu huwezi kuigiza hata ukijaribu ni kwa siki chache sana.

Unajua ni ngumu kwasababu vitu hivi vinaleta neema nyingi sana kwenye maisha yetu. Neema nzuri za kupendeza machoni pa watu na Mungu. Lakini mbaya zaidi watu wengi hawana hivi vitu.

NAKUPENDA BILA MIPAKA:39
Wote hatufanani kila mmoja ameumbwa kwa namna yake na hii ndiyo inatufanya tuwe tofauti. Usijali kuhusu Dokta.Chochote akikuambia usiweke moyoni kabisa, ni mtu wa kujiona yupo sawa muda wote. Ni binti yangu wa muda mrefu sana, namfahamu hanisumbui akili.”

Nilitabasamu na kusema “nimekuelewa sana mama. Nashukuru sana kwa maneno yako mazuri. Lakini mimi nipo salama kabisa.Nakuahidi sitasumbuka kabisa.”

Akatabasamu na kusema “sasa kesho ole wako usilete maandazi. Nitakasirika. Sitakula kabisa. Nakuambia.”
Nilicheka nikisema “mama jamani, nitakuletea usijali.”

Mama alitabasamu na kusema “nilale kidogo sasa.”
Nilimtazama na kusema “ni kweli mama, pumzika kidogo.”
Basi nilisogea kwa mama na kumlaza vizuri halafu nikawa natoka sasa kwenda kupeleka sahani kwa dada Maria.

Aliponiona alitabasamu, nikamuuliza “dada Maria mbona tabasamu hivyo kuna nini?”
Alinitazama na kusema “Mdogo wangu, natamani ungekuwepo jana. Boss aliponiuliza kuhusu wewe na utendaji wako kazi.”
Nilimtazama na kusema “eenh ikawaje?”

Alitabasamu na kuendelea “kitendo cha kusema mama amekula asubuhi, amekula mchana na jioni hajaamini. Unajua amebaki anatabasamu, akaenda kwa mama yake kuzungumza naye wametumia muda kweli. Alifurahi sana.”

Nilitabasamu nikisema “weee usiniambie, ina maana huwa hafurahi?”
Dada Maria akasema “weee, hivi unaona ile sura ndugu yangu au unaongea tu hapa. Ananuna balaa.”
Nikacheka, halafu akatazama huku na kule akisema “vipi dokta naye.”
Nilishusha pumzi sikutaka mengi nikasema “mambo ya kazi tu.”

NAKUPENDA BILA MIPAKA:40
Alitabasamu akisema “namfahamu vizuri, Na wivu balaa. Dokta utasema hapa ndiyo kwao. Anavyompenda Boss sasa humwambii kitu, unajua nini sasa. Boss hata muda naye hana.

Basi yeye pale ndiyo aonekana anamtunza sana mama, mara hivi mara vile si unajua tena aonekane ana jali eenh. Kwahiyo kuwa mvulimivu maana mwenzako kwa jino na ukucha (kwa kila njia)anatamani aolewe hapa.”

Nilimtazama Da maria nikisema “wee usiniambie!”
Alicheka akisema “ndiyo hivyo mdogo wangu.”
Nikashusha tena pumzi ndefuu ili nipate afua.
Akanitazama na kusema “Kiukweli jana Boss alifurahi sana. Mimi pia tunashukuru sana. Tafadhali usimzingatie huyo Bi mzuri.”
Nikatabasamu na kusema “dada Maria lakini.”
Tukacheka tu.

Basi nikaweka vitu jikoni nikiwa na amani kabisa.Nikarudi zangu sehemu yangu ya kazi kuhakikisha namalizia kila kitu. Nilikuwa nafanya kila kitu vizuri sana. Nikafua nguo za mama.

Nikamuweka safi kabisa na baada ya hapo mama alipata chakula cha jioni, na bado alipata na dawa. Sasa ile jioni aliniuliza “Nazwi mwanangu umejiandaa vipi kuhusu suala letu.”
Nikamtazama na kumuuliza “suala letu, suala lipi tena mama?”

Alitabasamu na kusema “ushasahau jamani, kuhusu kusali.”
Nikatabasamu na kusema “mama jamani, nakumbuka. Na jana tu nimefikiria. Nitajifunza, nitakaa karibu na Mungu nakuahidi.”

Alinitazama na kusema “mama yako lazima atakuwa anajivunia sana wewe. Ni binti mzuri sana. Mwanangu, ukitaka kuishi siku nyingi, maisha marefu sana na furaha kuwa karibu na Mungu.”
Nilimtazama na Kumuuliza “ina maana wewe mama unampenda sana Mungu.”

Alinitazama akaniambia “ninampenda mwanangu, sio mara zote nakuwa karibu naye. Upo wakati kwasababu ya maumivu, mateso ya magonjwa na mambo mengi ya maisha nakaa mbali naye.

NAKUPENDA BILA MIPAKA:41
Lakini Mungu ana mambo mengi sana. Ukiwa karibu naye na ukijiweka kwake hakuachi upotee kirahisi. Mara zote hunifuata popote pale na kunirudisha kwake. Unajua mimi peke yangu ndiyo naamini hivi. Mwanangu kipenzi wakati mwingine anachoka na kuniona napoteza muda.

Na kabla ndugu zangu walikuwa wananichukua na kunipeleka kwa waganga eenh wakati huo hali ilikuwa mbaya zaidi. Siku moja niliona namkosea tu Mungu leo huku kesho kule. Niliamua kusimama na Mungu ndiyo kupata hii nafuu hata sasa nipo hapa. Unajua nilikuwa siongei kabisa.”

Nilimtazama na kusema “ooh jamani mama, kumbe umeteseka sana.”
Akasema kwa upole “ndiyo maana sasa nakuambia, kaa karibu na Mungu utajiepusha na mengi sana.”
Nilimtazama Kisha nikatazama saa ya ukutani.

Huyu mama aliniuliza “umechoka kukaa hapa?”
Nilimtazama na kusema “nawezaje mama ikiwa unanipa elimu nzuri namna hii. Kusema kweli mama, Nina hofu sana kuhusu mtoto wangu.”

Alinitazama na kusema “hii ndiyo nguvu ya mama. Muda nao umeenda naona dokta wako hajafika mpaka sasa ili ukamuone. Kachukue simu yako emu.”

Nilishusha pumzi, na haraka nikainuka na kufuata simu yangu Kisha nikarudi chumbani kwa mama. Nilikuta simu imeita sana. Alikuwa ni mama yangu.

Halafu akanitumia ujumbe “mwanangu ilikuwa ni homa. Tumepumzishwa hapa jirani na nyumbani. Lakini sio muda natoka.”
Ujumbe ulikuwa ni wa saa 12.

NAKUPENDA BILA MIPAKA:43
Muda huu ilikuwa inaenda saa mbili. Nilipiga hakupokea. Mama mgonjwa akauliza “eenh kuna nini?”
Nikamwambia mama huyu “walimpumzisha lakini saa 12 alisema wanajiandaa kutoka.”

Akaniambia kwa upole “Tulia sasa, mama anajua anachosema. Kila kitu kitakuwa sawa.”
Nilikaa kwa upole, wakati huo Dokta aliingia, niliinuka na kumsalimia akawa anatabasamu huku akimchangakia mama.

Na mama naye anamjibu vizuri tu. Kisha aliniuliza Mimi kuhusu maendeleo ya mama. Vile namjibu tu simu yangu iliita. Mungu wangu, dokta aliacha alichokuwa anafanya akanitazama na kuniuliza “Nazwi Ina maana hukuelewa?, unawezaje muhudumia mama na ukiwa busy na simu yako. Chuo ulichosoma ndiyo walikufundisha hivyo?”

Nilimtazama kwa upole na kusema “nisamehe sana Dokta. Sitarudia tena.”
Akanitazama na kusema “nachukia sana kuombwa msamaha, unajua kwanini?, watu kukosea makusudi na Kisha kuomba msamaha. Msamaha bila mabadiliko sio msamaha.”

Yaani mpaka nakosa la kusema hapo ni simu tu imeita, hata mama alisema “Nazwi Binti yangu, Mimi ndiyo nilimruhusu atumie simu Baada ya kuona mnachelewa kurudi na ameacha mtoto anaumwa.”

Alishusha pumzi, alinitazama na kusema “mama yangu, usijali lazima nimuelekeze.”
Mama alinitazama, Kisha alimtazama akisema “taratibu sawa mwanangu.”

NAKUPENDA BILA MIPAKA:44
Alitabasamu na kusema “Unaweza kwenda kubadili sasa umuwahi mtoto.”
Haraka nilitoka, Nilifika kwa chumba cha kubadili nikashusha pumzi na kujiambia “Siku ya Leo aiseee.”

Nikampigia simu mama yangu. Mama alipokea akisema “mwanangu ondoa hofu tushatoka nipo naye hapa nyumbani. Alikuwa anacheza cheza saizi naona tena amelala. Vipi bado tu.”
Nikasema kwa upole “ndiyo natoka mama.”

Akaniambia kwa upole “jitahidi uwahi Labda akikuona atafurahi.”
Nilitabasamu, na haraka nilianza kubadili nguo zangu.

Baada ya kumaliza Mimi nikaenda chumbani kwa mama.
Nilipofika nilikuta mama, dokta na Mr Gallen. Nikasalimia “Shikamoo Boss.”
Alinitazama na kusema “marahaba.”
Sikutaka maneno mengi, nilisema “mama uwe na mzuri, Mimi naenda.”
Mama alinitazama na alisema “usisahau ulichoniahidi na sasa kesho ukija uje nayo si ndiyo?”

Nilitabasamu, Mr Gallen akawa haelewi, Dokta ananitazama kwa dharau Mimi hata najali sasa. Nikasema “nakuahidi mama.”
Mama alisema “kesho uwahi mwanangu.Uwe na mwema msalimie sana mama.”
Nilitabasamu na kuanza kuondoka.

Natoka huku nasema kimoyomoyo “huyo Mr Gallen ndiyo alifurahi mbona sioni hiyo furaha.”
Wakati najisemesha Dada Maria akasema “nesi ndiyo unaondoka?”
Nikatabasamu na kusema “Uwe na usiku mwema dada.”
Akaniambia kwa upole “Amen mdogo wangu, usiku mwema.”
Basi vile natoka na muamala ushasoma nikawa na furaha kwelikweli. Nilianza safari huku Naomba Mungu mwanangu asiwe tu amelala.

Safari haikuwa rahisi nilichelewa kweli kufika, Ila kwa bahati nilikuta mama yake Dee na Dee wapo nyumbani na Dee anambembeleza mwanangu alikuwa analia. Nilipofika tu nikamchukua mwanangu huku nikimbembeleza, alikuwa Hana raha lakini homa ilikuwa imeshuka.

Basi nikasalimia huku nabembeleza mwishowe Priya alilala. Mama na rafiki yake walikuwa nje Mimi nikasema “mama wacha nilale naye tu Leo.”
Mama alinitazama akitabasamu na kusema “ni sawa mwanangu.”

Nikaingia chumbani, mama alinifuata na kuniambia aliazima pesa mahali hivyo tunadaiwa nikasema “sawa mama hakuna shida.”
Wakati anatoka na Dee aliingia.Nilisema “Karibu kipenzi, Asante kwa kumsaidia mama.”

NAKUPENDA BILA MIPAKA:45
Akatabasamu akisema “niliposikia anaumwa hatujaweza kukaa nyumbani. Vipi lakini upo sawa?”
Nilimtazama na kusema “nimechoka, nimepata tu kazi na mwanangu anaanza kuumwa kweli?”


Alinitazama na kusema “rafiki yangu Mungu akikupa Neema anakupa na majukumu yake. Kwahiyo usijisikie vibaya furahia vipi angeumwa huna mia.”
Nilisema kwa upole “usiseme hivyo.”
Akanitazama akisema “nakujua wewe, shida nini?”

Nilimtazama na kusema “Acha tu si huyo Dokta Leo Ana foka bila hata sababu yaani hata simuelewi. Naona ananipa wakati mgumu kweli.”

Rafiki yangu akasema “unajua hawa watu wenye pesa wana matatizo sana. Usiwe karibu naye sana, Fuata vile anataka kaa naye mbali muhimu kazi yako.”

Nilishusha pumzi, Mara ujumbe ukaingia kwa simu. Alikuwa dokta kabale, alichokiandika sasa rafiki yangu hapo ananitazama kaandika “kesho usije kazini nitakuwepo mwenyewe mpaka nitakapo kujulisha.”

Dorice akaniuliza “kuna nini tena?”
Nikajisemea “Kumekucha shooo, huyu dokta Kama chawi.”
Basi Nikampa simu Dorice akaanza kusoma Kama Hana meno vile “kejo usije kazhini nitakuwepo mpaka nitakapo kujulisha.”

Nikacheka na kusema “Ana hekaheka.”
Dorice akasema “au ana mtaka boss huyu?”
Nikacheka nikisema “haswaaaa nacho kasema dada wa kazi.”

Tukacheka sana huku Dorice akisema “ana hofu utamchukua au, mbona kazi anayo na mama tunaye tunatamba naye.”

Nikacheka na kusema “rafiki yangu huyo boss na ukauzu ule, ule utu uzima ingawa mzuri Ila apambane sio kuniharibia ugali.”

Dorice sasa alivyonijibu “Una kichaaa?, utu uzima upi, hata ubaba bado, uanko tu atushindwe akitupenda hatumchukui?”
Nilimtazama Dee kwa jicho Fulani halafu, 😂😂😂sijui mpoje siku hizi hamlike wala comment Nisameheni basi mlike na mkomenti kesho nipost😂😂😂

Maoni

You're not logged in


Tangazo - from bangi to baby fully stories 1 to 21
from bangi to baby fully stories 1 to 21
   
X
SHARE TO SOCIAL MEDIA

NAKUPENDA BILA MIPAKA 36 - 45



:36
Sijapenda kabisa, binti alisema wanapika kwao, ina maana wewe huli kabisa huko nje kwasababu una uwezo au ni kwasababu gani. Kumbuka na wewe hapa umeajiriwa kwaajili yangu, kwanini haujali hisia zangu.”

Nikaona eenh kumbe mama ana maanisha, nikasikia dokta anasema “lakini mama sikujua kama una hamu namna hiyo na maandazi. Sio kwamba hutakiwi kula lakini kwa usalama wako mama yangu.

Kama unapenda sana bora tuone hapa wanapika kwa usafi. Nisamehe mama, sikujua nitakukwaza na unajua hutakiwi kukwazika si ndiyo mama.”

Nikaona nisije sutwa mie nikaondoka zangu. Sijui waliongea nini zaidi ila baada ya dakika kadhaa dokta alitoka amekasirika hata macho yake naona kabisa...

👉 Soma zaidi hapa: https://www.gonga94.com/semajambo/nakupenda-bila-mipaka-36-45

#Nk #gonga94 #trending #simulizi #hadithi #viral #fictionwriter
#ShortDrama #fblifestyle #BeautyBattle #AfricaVsWorld #Tanzania #Kenya #Congo #Rwanda #Burundi #SouthAfrica #USA #VoteNow #DebateTime #Trending <br>

Share on Facebook
Share on Twitter
Share on LinkedIn
Share on Pinterest
 
Umesoma kwa utulivu · dakika chache tu Asante Endelea kusoma chagua hapo chini
Umependezwa ?? Asante Soma Zaidi nakupenda-bila-mipaka
NAKUPENDA BILA MIPAKA 1 - 12
NAKUPENDA BILA MIPAKA 1 - 12
NAKUPENDA BILA MIPAKA 26 - 35
NAKUPENDA BILA MIPAKA 26 - 35
Tafuta Simulizi,Hadithi,Michezo
Andika unacho taka.

Top 10 Kali za Leo

AFANDE MILLAN😎 Sehemu ya 66 na 67

AFANDE MILLAN😎 Sehemu ya 66 na 67

751
AFANDE MILLAN😎 Sehemu ya 68

AFANDE MILLAN😎 Sehemu ya 68

703
MY HOT PILOT* (rubani wangu🔥) 17 to 18 final

MY HOT PILOT* (rubani wangu🔥) 17 to 18 final

304
SHAMIRA 87 MPK. 91      (SEASON FOUR)

SHAMIRA 87 MPK. 91 (SEASON FOUR)

283
SHAMIRA 94 Hadi 96

SHAMIRA 94 Hadi 96

235
JOGOO WA KIENYEJI sehemu ya 7

JOGOO WA KIENYEJI sehemu ya 7

199
SHAMIRA 92 kwa 93

SHAMIRA 92 kwa 93

193
NAKUPENDA BILA  13 - 25

NAKUPENDA BILA 13 - 25

179
JOGOO WA KIENYEJI sehemu ya 6

JOGOO WA KIENYEJI sehemu ya 6

176
NAKUPENDA BILA MIPAKA 26 - 35

NAKUPENDA BILA MIPAKA 26 - 35

143

ZIMESOMWA ZAIDI

‎TUNDA LA  DADA ‎ ‎SEHEMU YA KWANZA

‎TUNDA LA DADA ‎ ‎SEHEMU YA KWANZA

11.79K
RUNGU LA KIPOFU 22.

RUNGU LA KIPOFU 22.

7.5K
🙄 NILIONA MWENYEWE DADA YANGU ANAGEUZWA🔥  sehemu ya tisa.  👉 Akaanza kunipamp sasa...👇

🙄 NILIONA MWENYEWE DADA YANGU ANAGEUZWA🔥 sehemu ya tisa. 👉 Akaanza kunipamp sasa...👇

3.85K
🔥 UTANI WA SHEMEJI KAICHOMEKA..6..10  KWELI...Aaaaaaaaa chomoa🔥  Sehemu ya sita.  👉 Aaaaaaaaa chomoa...👇  Shemeji inauma utanichana.

🔥 UTANI WA SHEMEJI KAICHOMEKA..6..10 KWELI...Aaaaaaaaa chomoa🔥 Sehemu ya sita. 👉 Aaaaaaaaa chomoa...👇 Shemeji inauma utanichana.

3.34K
MY WANGU❤️ sehemu ya 119 na 120.

MY WANGU❤️ sehemu ya 119 na 120.

2.96K
MY WANGU❤️ sehemu ya 108

MY WANGU❤️ sehemu ya 108

2.93K
MY WANGU❤️ sehemu ya 116 na 117

MY WANGU❤️ sehemu ya 116 na 117

2.76K
 UTANI WA SHEMEJI KAICHOMEKA KWELI...Aaaaaaaaa chomoa🔥  Sehemu ya 20.  👉 Nikatanua mwenyewe miguu manuu..kazi kwake tu...👇

UTANI WA SHEMEJI KAICHOMEKA KWELI...Aaaaaaaaa chomoa🔥 Sehemu ya 20. 👉 Nikatanua mwenyewe miguu manuu..kazi kwake tu...👇

2.74K
MY WANGU❤️ sehemu ya 106 na 107

MY WANGU❤️ sehemu ya 106 na 107

2.68K
🔥 UTANI WA SHEMEJI KAICHOMEKA..16..20  KWELI...Aaaaaaaaa chomoa🔥  Sehemu ya 16.  👉 nakupenda pia...👇

🔥 UTANI WA SHEMEJI KAICHOMEKA..16..20 KWELI...Aaaaaaaaa chomoa🔥 Sehemu ya 16. 👉 nakupenda pia...👇

2.61K

RATIBA ZA MAKALA ZETU

Hakuna Ratiba kwa sasa

Machapisho Mapya
Vijipost vilivyotangazwa karibuni (yamekatwa hadi maneno 30)
NAKUPENDA BILA MIPAKA  36 - 45 Post Mpya
NAKUPENDA BILA MIPAKA 36 - 45
@majario LIVE

:36 Sijapenda kabisa, binti alisema wanapika kwao, ina maana wewe huli kabisa huko nje kwasababu una uwezo au ni kwasababu gani. Kumbuka na wewe hapa umeajiriwa kwaajili yangu, kwanini haujali hisia...

AFANDE MILLAN😎 Sehemu ya 68 Post Mpya
AFANDE MILLAN😎 Sehemu ya 68
@majario LIVE

IMETOKAAAAA SEASON YA MWISHOOO SEASON 4 Nikasema ahaa kaka nipo busy sana na nabanwa na kazi, na kuna mda nalala kazini, kka akanmbia au sio unanidanganya na mm mdogo wangu, we...

AFANDE MILLAN😎 Sehemu ya 66 na 67 Post Mpya
AFANDE MILLAN😎 Sehemu ya 66 na 67
@majario LIVE

🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈 Mwandiishi; LISSA Na kesho yake mapema sana mimi.niliamkia kazini , na nilipofika tu job,nikaongea na uyo afande mnige, ni mshikaji wangu tu uyu baba ,na huwa ananiitaga boss, mana nimempita...

SHAMIRA 94 Hadi 96 Post Mpya
SHAMIRA 94 Hadi 96
@majario LIVE

SHAMIRA Sehemu ya 94 Wassap; 0742443214 Mwandishi; lissa wa huru media Nikasema hapana mimi sijawah.akasema basi mimi niliwahi kuza mwenzio ila kwa bahati mbaya nilikosa il uchungu niliuona aswaa. Unauma sana shoga...

MY HOT PILOT* (rubani wangu🔥) 17 to 18 final Post Mpya
MY HOT PILOT* (rubani wangu🔥) 17 to 18 final
@majario LIVE

* * MTUNZI: SMILE SHINE EP 17. Mikononi mwake nilikuwa sarama, siku ya ndoa, ilifika na vicram tulimualika na familia yake, kama wao walivyofanya, ila hii ndoa nilijua kupendeza jamani, nilipaka na Hina yangu...

SHAMIRA 92 kwa 93 Post Mpya
SHAMIRA 92 kwa 93
@majario LIVE

SHAMIRA Mwandishi; lissa wa huru media Sehemu ya 92 Basi bwana siku zikapita kidogo nikawa nipo apa naendelea na kazi zangu ili iki kitoto hapana . Kina tabia mbaya jamani mh...

NAKUPENDA BILA MIPAKA 26 - 35 Post Mpya
NAKUPENDA BILA MIPAKA 26 - 35
@majario LIVE

:26 Nikacheka na kusema “Muanko ana muda sasa, hacheki na yeyote, yaani tabasamu lake tangu nifike pale sijaliona dada hivi unanielewa.” Alinitazama akisema “eenh chaupole wangu nipe nipe.” Nilimtazama na kusema “wewe tena...

NILIKUTANA NA MAREHEMU MKE WANGU AKIWA KWENYE GARI LA TAJIRI MKUBWA  ​Episode 1 Post Mpya
NILIKUTANA NA MAREHEMU MKE WANGU AKIWA KWENYE GARI LA TAJIRI MKUBWA ​Episode 1
@majario LIVE

​Mvua ya rasha rasha ilikuwa ikidondoka jijini Dar es Salaam, ikichanganyika na moshi wa magari na kelele za wapita njia. Nilikuwa nimesimama kando ya barabara ya Ali Hassan Mwinyi, nikisubiri...

BILLIONS OF LOVE💓💓   SEHEMU YA "6"💓😽 Post Mpya
BILLIONS OF LOVE💓💓 SEHEMU YA "6"💓😽
@majario LIVE

"BY BABIE LOVE" Basi bwana kakabaki ka laki na nusu nikasema hatakama kesho sipiki lazima tu niende road nikatafute chakuniinguzia pesa Mnakuja nn 😂😂😂 vitoto vya mskini sisi akili ni...

JOGOO WA KIENYEJI sehemu ya 7 Post Mpya
JOGOO WA KIENYEJI sehemu ya 7
@majario LIVE

🐓 Mwandishi:lissa mwalla Reyhan kwel ananifanyia mm hiv?niliumia sana huku nikimuangalia ivan anaonfoka zake.reyhan akasema imeisha hio huwez nifanyia mm umalaya ww,unanijua unaskia?sasa uneshakua malaya kweli washkaj malizaneni nae m najikataa.aliongea huku...

NAKUPENDA BILA  13 - 25 Post Mpya
NAKUPENDA BILA 13 - 25
@majario LIVE

MIPAKA:13 “Keti tafadhali.” Nilimtazama, yeye hapo hata hajainua uso wake. Nilimeza mate nikaketi hapo moyoni najisemesha “wenye hela wana ringa jamani kwani si anitazame hata.” Nilipoketi aliniinua uso wake na kunikabidhi karatasi akisema...

SHAMIRA 87 MPK. 91      (SEASON FOUR) Post Mpya
SHAMIRA 87 MPK. 91 (SEASON FOUR)
@majario LIVE

🏀🏀🏀🏀🏀🏀🏀🏀🏀🏀🏀🏀🏀🏀🏀🏀🏀🏀🏀🏀🏀🏀🏀🏀🏀🏀🏀🏀🏀🏀🏀🏀 SHAMIRA Sehemu ya 87 Mwandishi; lissa wa huru media Siku iyo sasa nimeenda kazini. Ile nimefika tu asubuh love akainiita mh nikaogopa nikahisi au nimeharibu sehemu.mana kufika na kufika nimeitwa.nijaenda kisha ...

JOGOO WA KIENYEJI sehemu ya 6 Post Mpya
JOGOO WA KIENYEJI sehemu ya 6
@majario LIVE

🐓🐓🐓🐓🐓🐓🐓🐓🐓🐓🐓🐓🐓🐓🐓🐓🐓🐓🐓🐓🐓🐓🐓🐓🐓🐓🐓🐓🐓🐓🐓🐓 Mwandishi:lissa mwalla Sasa hapo ndio nimekwisha sasa,uwiii,niliogopa nikamsukuma ivan,akasema nani huyo?nikasema ni ticha,akasema ticha wako ndio anakufata mpaka huku?mm nikatoa tu macho,ivan akasema subir hapa,nikasema sawa,akanyanyuka akavaa nguo akatoka mm name...

SHAMIRA 82 MPK  86   Post Mpya
SHAMIRA 82 MPK 86
@majario LIVE

(SEASON FOUR) (HURU MEDIA) 🏀🏀🏀🏀🏀🏀🏀🏀🏀🏀🏀🏀🏀🏀🏀🏀🏀🏀🏀🏀🏀🏀🏀🏀🏀🏀🏀🏀🏀🏀🏀🏀 SHAMIRA Sehemu ya 82 Mwandishi; lissa wa huru media Basi shoga yenu maisha yakaanza dodoma sasa. Nikawa nipo na kiakiba changu ndo kinanisapoti naendesha maisha mdogo mdogo. Apo...

ISABELA NA WATOTO WA BOSSLADY 1 ---- 5 Post Mpya
ISABELA NA WATOTO WA BOSSLADY 1 ---- 5
@majario LIVE

SEHEMU YA KWANZA Ni majira ya jioni ikiwa ni muda mfupi tokea ametoka bafuni kuoga kwa ajiri ya kujiandaa aweze kurudi nyumbani mara baada muda wa kazi kuisha, Isabela akiwa...

Home Login Signup
Top 20 Privacy Policy Contact us
Terms & Conditions About us Latest