NAKUPENDA BILA 46 - 50 MWISHO S1
NAKUPENDA BILA MIPAKA:46
Nilimwambia “nina kichukulio?, Dorice natamani unielewe huyo mwanaume alivyo kwanza Hapana sitaki, na unajua mimi kwasasa akili ni mwanangu tu na hata hivyo hawezi kunitaka mimi. Kwa kipi Labda, yeye na huyo dokta wanaendana.”
Dorice alinitazama na kusema “una shida gani sijui.Mwanaume mmoja kukuumiza basi unachukia wote. Na Nani amekuambia kuwa huna uzuri. Tuachane na yote ni Nani amesema kuwa mama ndiyo mwisho wako hakuna wa kukutongoza.
Sikia nikuambie kipenzi, umri wa huyo muanko usikutishe Hana üzee kwanza wenye pesa hawazeeki kila mtu anataka nafasi ya kuishi vizuri. Kuzaa ni baraka, tunakosea tunainuka tena.
Watu wameolewa na hawana watoto kukicha wanakesha kwa waganga, wengine watu wazima hawana hata namna ya kupata mtoto sikia mshukuru Mungu usikute bila huyu mtoto hata hii kazi usingepata.
Hata hivyo huyo dokta mpaka amekuwa mkubwa kwetu hajaolewa ana kazi ya kumendea tu mpuuzi kabisa, mimi tu na umri huu 30 sina hata huyo mtoto Kama wako sio Kama sitamani Ila ndiyo nabembeleza penzi.”
Halafu alianza kucheka akisema “wewe si amesema usiende kazini tuliaaa tulii, maombi yangu Leo mama huko awasumbue wakome wajue umuhimu wako.”
Nilitabasamu na kusema “tena ni kazi rafiki yangu, si unajua mtu mzima yule, umtoe kitandani umuweke kwa kiti, umbadilishe nguo zake, hawezi chochote.”
Dorice alinitazama na kusema “nakuelewa Ila wewe ndiyo kazi yako sasa jikaze.”
Nilitabasamu na kumtazama mwanangu, Dorice alisema “anaita huko wacha niende.”
NAKUPENDA BILA MIPAKA:47
Nilitabasamu na kusema “hakuna shida kipenzi, kesho nitakuja ukitoka kazini.”
Dee alitabasamu akisema “uje ndugu yangu maana na wewe sasa ushakuwa adimu.”
Nikacheka nikisema “unafiki tu kazi siku 2 nishakuwa adimu.”
Tukacheka huku akitoka.Alipofika mlangoni akasema “Sikia binti, huo upole wako na unyenyekevu achana nao wewe sio sista unanielewa. Huyo Muanko akijaribu tu hata Kama hajasema wewe kubali.”
Nilijikuta nacheka nikisema “hivi una kichaa.”
Alicheka akisema “Nani hataki kuwa wa kishua sasa, changamka mjini hapa na mimi niwe na ndugu tajiri Labda utaniambukiza.”
Nilijikuta nacheka, anawaza vitu ambavyo kichwani hakuna kabisa.
Alitoka, mimi nipo tu hapo na kiswaswadu changu naangalia ule ujumbe halafu nasema “sasa itakuwaje mimi sina pesa zaidi ya hii ya Leo. Anapenda sana kuharibu mipango huyu Dokta.”
Nilimtazama mtoto wangu na kusema “Usiku mwema Priya wangu. Utakuwa sawa.”
Nikajiandaa nikaoge maana kusema kweli nilikuwa nimechoka sana. Kazi ya kumtunza mama sio rahisi kumbuka ni mtu mzima halafu hajiwezi Kwahiyo ni mimi tu uzuri vitu vyake ni vya kisasa sana, vinanisadia muda mwingine bila hivyo ilikuwa ni ngumu sana.
Baada ya hapo nilirudi zangu kitandani, Nikajikaza Kama mzigo nilikuwa nimechoka. Sasa hapo nipo nawaza tu kuhusu maneno ya Yule mama halafu nasema “Mungu, sasa nitajua vipi. Nikipata nafasi ya kukutana naye nitamuuliza maswali zaidi.”
Nilijilaza.
Nililala usingizi huo Kama siamki tena. Mama alikuja niamsha akisema “mwanangu, mwanangu amka kazini huendi Leo?”
Huku nalalamika nilisema “mama lakini, Niache mwenzako nilale kidogo nimechoka sana unajua. Kazini Leo mapumziko.”
NAKUPENDA BILA MIPAKA:48
Mama aliniuliza “mapumziko?, kwani Leo juma ngapi?. Kama huendi kazini amka basi tusaidiane kazi maana Leo Ukiachana na kuuza kuna mahali wana shughuli wanataka maandazi Kwahiyo bado tutapika mpaka basi Leo.”
Nikalalamika nikisema “mama lakini?”
Mama alinivuta shuka akisema “wewe kulala tu, amka upesi.”
Basi niliamka, Nikamtazama Priya bado alikuwa amelala na nikamsalimia mama.Mama aliendelea kuongea Kama unavyojua tena mama zetu, ooh mtoto wa kike mvivu, kalienda kakarudi mimi nilinyamaza tu kimya.
Tulifanya kazi kwa kusaidiana, Baada ya muda mwanangu na yeye aliamka nilimpa dawa na kumuhudumia kwa chakula na kuoga. Namshukuru Mungu mwanangu aliamka na Afya njema tofauti na ulegevu wa Jana. Wakati mama anaendelea na mambo yake niliandaa chai na mimi nilikaa ili ninywe. Vile nakunywa chai kaka Baraka alifika.
Nilimwambia kwa upendo “karibu kaka yangu.”
Aliniambia kwa furaha “dada yangu kipenzi, nina njaa balaa.”
Nilitabasamu nikisema “wewe tena na kula.”
Akacheka kidogo, alikaa nikaandaa chai na kusema “haya karibu.”
Alikunywa na kusema “ankali wangu anaendeleaje?”
Nilimtazama na kusema “anaendelea tu vizuri Namshukuru Mungu.”
Akanitazama halafu aliniambia “sister kusema kweli naona aibu, najua una vipengele vyako lakini Leo nimekwama. Nina shida na elfu 5 tu.”
Nilimtazama na kusema “lakini kaka?”
Aliniambia “dada usiseme kitu najua, najua umeanza kazi Jana tu hapo, najua mtoto anaumwa na unajua huwa sio tabia yangu tafadhali.”
Nilimtazama na kusema “najua kaka, lakini kaka yangu Baraka. Jitazame ulivyo mzuri, jitazame ulivyo na afya njema, jitazame kaka yangu. Mimi ni mdogo wako, unajua nakupenda na najivunia sana kuwa na kaka Kama wewe.
NAKUPENDA BILA MIPAKA:49
Tafadhali kaka, muonee mama huruma, tuonee huruma. Tangu baba alipofariki wewe ndiyo mwanaume tupo naye. Unaonaje ukatafuta kazi, tukasaidiana majukumu. Mimi nikileta unga wewe unaleta mboga.
Haitoshi kaka kesho na kesho kutwa umepata mtoto, huyu ni baba unataka mtoto wako ajivunie. Naomba usikasirike kaka Nakupenda sana. Tazama marafiki zako, Kama mnakaa mnajivunia tabia mbaya badilisha kaka.
Wewe ni baba yetu, mwanangu baba Hana ana wewe tu, huoni Hilo lakini. Natamani ungejua mama anavyokuwa anakuombea, unataka kusema Mungu Hana maana ameshindwa kubadilisha kiumbe alicho kiumba?”
Kaka yangu machozi yalikuwa Kama yanamtoka, na mimi pia. Nilimwambia “usinijibu kitu kaka, tule halafu tukimaliza tuongozane mpaka kwa wakala.”
Kaka yangu kweli alinyamaza, hakusema kitu chochote kile alikaa kimya.
Hatukula hata vizuri, niliondoa vyombo nikamwambia kama yangu “twende kaka.”
Kwa upole maskini maneno yangu yanaonekana yalimgusa. Nikamwambia “nisubiri naingia ndani sasa.”
Nikaingia, nikachukua simu na kutoka. Sasa simu yangu nilikuta na missedcalls Kama 10 hivi, kutazama namba mpya. Moyoni nikajiuliza “sijui hata atakuwa Nani namba mpya hii.”
Kwakuwa kaka yangu alikuwa ananisubiri Ilibidi niongozane naye. Mama aliita akisema “mnaenda wapi Tena wanangu?”
Nikacheka nikisema “hapo anataka kujua roho inarukaruka.”
Baraka alicheka na kusema “tunarudi mama.”
Mimi Nikacheka tu na kusema “muangalie mjukuu wako, mimi na kaka yangu tunatoka.”
Niliona tabasamu la mama yangu, ni kila mzazi anapenda kuona watoto wake wanaelewana.
NAKUPENDA BILA MIPAKA:50
Basi nilifika kwa wakala, nikatoa pesa na kumpa kaka yangu elfu kumi. Alinitazama na kusema “Mungu akubariki sana dada. Sitaki kuzungumza sana. Lakini dada nakuahidi nitabadilika.”
Nilijikuta namkumbatia nikisema “nakuombea kaka yangu kipenzi.”
Alitabasamu akisema “wahi nyumbani sasa, Mimi naenda mishe.”
Nilitabasamu na kusema “kuwa makini kaka yangu.”
Alitabasamu na kunipungia mkono. Ukiona sasa alivyo vaa kipensi kimechanika ovyoovyo, kaka yangu mzuri sana Ila sasa alivyo ukimuona unajua tu huyu muhuni, ukimuona unajua kabisa huyu ni bamtu.
Ilikuwa mida ya saa 6 mama bado anachoma maandazi mimi nikaona nioge kwanza nipate nguvu.
Nikawa nimeingia bafuni, nimerudi chumbani ile nakaa tu ile namba inapiga tena. Nilitazama na Kisha nikapokea. Vile napokea tu nikasikia naitwa “Nazwi!!”
Nilishtuka, hii sauti sijaisikia Mara nyingi lakini Nina uhakika ni boss. Niliitikia kwa upole “Abee.”
Aliniambia tena kwa kunyooka “Unaongea na Mr Gallen, Tafadhali fanya unavyofanya nahitaji ufike hapa haraka sana.”
Nilishusha pumzi na kusema “lakini!!!”
Kabla sijamalizia alisema kwa kumaanisha “Hakuna cha lakini, nakusubiri.”
Simu ilikata, nilishusha pumzi na kusema “ni nini tena mbona nazungushwa Kama mtoto mdogo. Leo Nikienda huko wana majibu ya kunipa sitaogopa.”
Nilijikuta nimechoka, unajua vile unaambiwa Leo usije mahali umeshaandaa akili yako na mambo mengine halafu ghafla unaambiwa tena uende hiyo sehemu wakati hukuwa na akili hiyo. Basi nikawa tu najiuliza maswali na kujijibu. Ndiyo natakiwa niende maana kazi kuitaka naitaka Ila bosi wangu sasa ni huzuni.
NAAAAAAAAAAAAM
HAPA NDIYO MWISHO WA SEASON ONE
SEASON TWO INAPATIKANA
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi

Maoni