LETICIA 15:16
LETICIA
Sehemu ya 15
Mwandishi;LISSA
Yule dada alikuwa mcheshi dakika mbili tushazoeana ,nilikuwaga namuona tu kijijini ila hii siku ndio nikamjua vizuri .alinambia anaitwa rehema. Tulipiga story mno akanipa na namb yake ya simu nikipata simu nimtafute ,nikaichukua tuliongea ongea adi nikachekewa kulala yaani nijilaza lisaa tu, mama tele akaja kuniamsha nijiandae ,bas kweli nikaamka kujiandaa nilipomaliza ,nikashangaa rehema ananip nguo et yeye hamtosh nyingi tu ,nikamshukuru mno maana zilikuwa nzuri tena zote za dukani. Basi mama tele akanichukua akanipeleka adi stendi na uko akanipakiza gari la kwenda dar na alichukuwa mawasiliano ya konda maana mimi simu sikuwa nayo . Nilikuwa naumia jamani kumuacha mwanangu ila nikaona bora niende tu nikatafute maisha , nilifika dar na nikaja kupokelewa na kijana tu alikuwa yupo kwenye gari akashuka akanipokea tumizigo twangu akapakia kwenye gari
Basi akaendesha gari adi hiyo sehemu wanayokaa ,kiukweli nyumba ilikuwa nzuri mno apo ni kwa nzje ata geti hawajafungua ila nikaona nyumba ni nxuri mno . Basi akapiga honii geti likafunguliwa nyie hamuwezi amini si namuona polela ndio anafungua geti ,moyo ulifanya paaaah . Daaaah nilijikuta napata tu hasira yaani mtu ndio kaja kujificha uku miaka yote iyo ata kusema amtafute mtoto wake amjulie hali hamna.yeye hakuwa ameniona ata basi tumeingia ndio akaja ety kutupokea ,lloooh aliponiona nikaona kashituka kuniona naona hakutegemea kabisa kuniona pale. Ila hakutaka kuonesha kuwa ananijua wala kushituka ,na mimi wala sikuangaika kumsemesha , maana nilikuwa namchukia tu polela miaka mi 4 ata kutuma salamu. Bas yule kaka akamwambia polela uyu mgeni wa madam naona ni dada wa kazi mpya . Polela akasema aaah kalibu dada , nyie ata kumjibu sikutaka nikatikisa tu kichwa changu. Bas akatoa mzigo yangu akapeleka ndani . Nikafika kule ndani nikapokewa na mdada mzuri jamni mweupe mwili mzima yaani.
Msafi hadi rahaa ,japo hanifikii mimi nivile tu sijaoga vizuri, na matunzo aweeeh mimi ni kisu.basi yule dada akanambia kalibu leticia . Nikasema asante, naona jina langu aliambiwa na mama tele ,akasema kalibu apa ndio nyumbani na mimi ndio boss wako nadhani kazi zangu utafanya vizuri. Nikasema ndio boss haina shida . Akasema aah na mimi sina shida kabisa ukinifanyia kazi zangu vizuri na mshahara nakuongezea umesikia, nikaitika nikasema ndio . Akasema sasa mimi apa naishi na mume wangu japo kuwa yeye hashindi hapa kazi zake nyingi ni zakisafiri kama apa kusafiri kurudi mwisho wa mwezi . Na ninakaa na uyo mlinzi na dereva wangu aliyekuleta basi . Kwaiyo kazi sio nyingi kufua mashine zipo . Labda usafi tu na nyumba yangu sio chafu sana maana hamn mtoto wa kuchafua ,akawa ananielekeza pale mambo ya nyumba yake nikawa namsikiliza tu .
ππππππππππππππππππππππππππππππππππππππππππππππππππππππππππππππππππππππππππππππ
LETICIA
Sehemu ya 16
Akanionesha na mazinfira na jinsi ya kufanya kazi zake adi nikaelewa ,alipomaliza akanipeleka sasa chumbani kwangu nitakakokuwa nalala .daaah yaani chumba ni kikubwa mno daah kweli watu wanaishi ,nilipokiona nikajiuliza tu kama chumba cha dada wa kazi kipo hivi cha kwake je si ndio baraa uwiih. Basi akanambia nikaoge basi alafu nipumzike yeye anaagiza chakula kikifika atanishitua ,nikamwambia sawa ,akataka kutoka akarudi tena akasema alafu nilitaka kusahau leticia ukitaka kuishi mda mrefu hapa na kwa amani ,umbeya sitaki utakachokiona baki nacho moyoni na utakachosikia sitaki kukisikia kokote apo ndio tutaelewana umu ndani ,nikasema sawa boss nimekuelewa ,akasema safi alafu. Sipendelei uniite boss niite madam prisca. Nikasema sawa ,basi akaondoka zake
Mimi nikabaki nashangaa bado uziri wa kile chumba ,daah chumba ni kizuri mno ,nikazunguka chumba kizima ,nikaruka ruka kwenye godoro, nyiee ushamba huu nilishangaa mno ,nilipomalizq kushangaa ndio nikaenda kuoga sasa oyaa ni balaa choo kama ulaya jamani unaweza ata ukalia wali chooni π€£π€£π€£π€£π€£π.kufungua bomba siwezi ,nikawa nabinya binya tu mule bafuni adi nikapapata nikashangaa tu maji yanatoka,basi nikaoga nilipomaliza nikafunga bomba kisha nikaenda kuvaa na nilivaa nguo alizonipa shoga angu rehema na niilipendeza angalau nikaona nafanana na ile nyumba ,nilipovaa nikaka kitandani nikawa nawaza nyumbani sijui ilikuwaje na vip kuhusu mwanangu. Nilipomuwaza mwanangu nikamkumbuka baba yake polela ,yupo tu dar anakula raha anakazi kumbe mshahara sijui anapeleka kusema ata niwatafute ahudumie mtoto sijui alikuwa anapeleka wapi ela daah .
Basi nilikaa pale nikawaza mno adi madam prisca ,akaja na chakula ,naona aliagiza nje tu ,maana anamikucha uyu ata kupika uyu sidhani ,yaani uyu inaonesha ni mama wa nyumbani na nyumbani kwenyewe anafanya kazi ya kula raha tu ,maana mfanyakaz wa ndani nipo ,bado getini ,wakumuendesha yupo yaani ni anaraha mno tu. Basi nikachukua kile chakula nikaanza kula aliniagizia chips kuku na soda ,oyaaah siku ya kwanza tu napokelewa na maraha daaah. Basi nilikula adi nikamaliza ,nikatoa vyombo nikapeleka jikoni ,nikakuta nao washakula mimi nikaanza kuosha vyombo sasa . Madam prisca akanambia ningeacha nipumzike ,ila mimi nikaona bora npunguze kazi na kulal na vyombo vichafu ndani jau daah .basi snilipomaliza kuvipanga vizuri , ndio nikaenda sasa kulala nikamwacha madam na yule dereva sebleni wanaangalia movie.basi nimefika chumbani ,nikapanda kitandani nikalal hata haikupita mda nikapitiwa na usingizi na vile nilichoka nililala mapema
ππππππππππππππππππππππππππππππππππππππππππππππππππππππππππππππππππππππππππππππ
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi

Maoni