Simulizi za Maisha,Mafunzo,Mapenzi ,Chombezo Habari za Michezo na Burudani vyote kwa Kiswahili ndani ya – Gonga94 Semajambo
Gonga94 · Stories
21 Mar 2026
105 views
VYOTE NDANI GONGA94
IN LOVE WITH ZURI* Chapter 7
Usimulizi huu ni wa watu wazima. Chukua muda wako, tulia, kisha usome kwa utulivu kama machapisho yetu yanayoendelea moja kwa moja.
SONGA NAYO.....
Kitendo cha mimi kuongea kwa ukali kiasi hicho kiliwashtua sana Idress lakini pia na Ethan, Ethan yeye mpaka alinyanyuka na kuja sehemu niliyokaa kisha akachukua hiyo chai ambayo nasemea haina sukari na kunywa
"Mbona chai ina sukari hii, tena nyingi balaa we Frank leo umeamka na nini..??"
Ethan alizungumza, nikamkata jicho maana aliniharibia mipango yangu
"Me nimesema nataka sukari basi.."
Nilisema na kutulia, nikamuona Zuri akipiga hatua kwenda jikoni lakini Ethan alimzuia kwa kumshika mkono
"Hebu acha na hata usiende kuleta hiyo sukari, huyu na wivu wake usiokuwa na maana atajua mwenyewe.."
"Ethan....!!"
Nilimuita kwa ukali lakini hakusikia ila akendelea. kuongea
"Ethan kitu gani, we unapenda kumchosha mwenzio huoni amechoka huyu, we kama unataka hiyo sukari nenda kafate mwenyewe..."
"Ethan me unanijibu hivyo..??"
"Ndi..."
"Achaneni tu nitafata mwenyewe, kaka Ethan we nenda ukakae maana hii ni kazi yangu.."
Alizungumza Zuri kwa upole kisha akaondoka, nikamsindikaza kwa macho namna alivyokuwa anatetemesha huku nyuma, amejaaliwa mzigo wa maana walah huyu binti
Tena yeye hakuwa na ule mzigo mkubwa sana, no yeye alikuwa na ule mzigo wa size yaan ameumbika kiaina flan hivi sijui mnaitaje me hata hayo mambo siyajui
Baada ya muda kidogo Zuri aliweza kurudi akiwa na kopo la sukari, akaniwekea kwenye ile chai ambayo ninalalamika haina sukari, ukweli ni kwamba ile chai ilkuwa na sukari ila kwa kuwa mimi wivu wangu unakaa kwenye magoti, nikasema chai haina sukari
"Na ole wako uibakize.."
Ethan aliongea, ila huyu dogo nitakuje nimpige yani anaona kabisa me namzidi umri ila ananiletea ujuaji wake huo ye ngoja, nilichofanya ni kumuangalia kwa hasira kisha nikamwambia Zuri
"Nenda kafue zile nguo.."
Zuri akaondoka zake nikaichukua ile chai na kwenda kuimwaga kisha nikaweka chai nyingine
"Ila we Frank unajitafutia mabalaa, badala ya kufanya vitu vya kumfanya akupende ila wewe unafanya akuchukie kweli wewe sijui kama utaoa kweli...
Ethan alizungumza kwa kulalamika yani
"Ila we Ethan nitakuja nikupige siku moja, we unajua nafanya vyote hivi kwa sababu gani?? Kwa sababu yule ni mke wa mtu na ni mama wa mtoto mmoja so tulia.."
"Ni mke wa mtu..??"
Ethan na Idress wakauliza kwa pamoja, nikabaki kimya tu moyoni najua mwenyewe namna nilivyokuwa naumia
"Ndio ni mke wa mtu yule.."
Nilisema huku nikitaka kulia kabisa, ila mapenzi acheni kabisa
"Dah, so hapa tayari nimekosa shemu aisee.."
ila Ethan huyu ndugu yenu akili zake anazijua mwenyewe
"Ethan muda mwingine uwe serious, huoni mwenzio hapo anapitia wakati gani we unaweka matani tu.."
Alizungumza idress Akimwambia Ethan, Ethan akakohoa kwanza kisha kwa sauti iliyojaa
userious akasema....
Itaendelea.......
Maoni
You're not logged in
X
Login
X
signup
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa
+ Endelea kugundua zaidi
IN LOVE WITH ZURI* *Sehemu YA SITA*
SONGA NAYO..... Kimya kifupi kilipita hii ni baada ya mimi kusikia kuwa Zuri ni mke wa mtu nilikuwa naumia sana sio sir...
Kitendo cha mimi kuongea kwa ukali kiasi hicho kiliwashtua sana Idress lakini pia na Ethan, Ethan yeye mpaka alinyanyuka na kuja sehemu niliyokaa kisha akachukua hiyo chai ambayo nasemea haina sukari na kunywa
"Mbona chai ina sukari hii, tena nyingi balaa we Frank leo umeamka na nini..??"
Ethan alizungumza, nikamkata jicho maana aliniharibia mipango yangu
"Me nimesema nataka sukari basi.."
Nilisema na kutulia, nikamuona Zuri akipiga hatua kwenda jikoni lakini Ethan alimzuia kwa kumshika mkono
"Hebu acha na hata usiende kuleta hiyo sukari, huyu na wivu wake usiokuwa na maana atajua mwenyewe.."
"Ethan....!!"
Nilimuita kwa ukali lakini hakusikia ila akendelea. kuongea
"Ethan kitu gani, we unapenda kumchosha...
👉 Soma zaidi hapa: https://www.gonga94.com/semajambo/in-love-with-zuri-chapter-7
Maoni