Menu






Simulizi za Maisha,Mafunzo,Mapenzi ,Chombezo Habari za Michezo na Burudani vyote kwa Kiswahili ndani ya – Gonga94 Semajambo

NAKUPENDA BILA MIPAKA 151 -- 157
Gonga94 · Stories

NAKUPENDA BILA MIPAKA 151 -- 157

Usimulizi huu ni wa watu wazima. Chukua muda wako, tulia, kisha usome kwa utulivu kama machapisho yetu yanayoendelea moja kwa moja.
:151
Kwenye akili yako vuta picha zile Abaya za kituruki, halafu ziwe tatu, nzuriiiiiii, rangi nyeusi, rangi nyeupe, na zambarau fulani imechanganyika, halafu kuna gauni mbili za ukali, eenh, eenh sijui nirudie tena kutoa ushuhuda wangu.

Natamani sana ila nitawezaje sasa mnielewe, ni Mr Gallen ameninunulia. Mimi sasa naangali nakumbatia, na viatu vya chinichini halafu mafuta ya kupaka, halafu na nguo za ndani. Ninatabasamu nikisema “oooh!!, oooh jamani, jamani.”

Nikaona tu bora nikaoge kwanza, nitoe kwanza msisimuko wa Busu. Tena busu lenyewe hata mswaki, nisiseme sana si mnajua sijaoga. Sijui hata amefurahia ila mimi nimefurahia balaa. Nilipoingia bafuni, mimi nafanya hata vitu sijawahi kufanya.

Nilijikuta napiga mswaki nawaza tu, hata nilipoanza kuoga nilisema “Nilikuomba Mungu, kibali kila mahali, najua maombi yangu uliyasikia, ni kazi sana kukumbushia kila siku. Nipo hapa nakukumbusha tena na tena. Mungu kwenye mahusiano, nipate kibali isivyo kawaida. Naomba ndoto hii iwe kweli. Nakuomba.”

Nilimaliza kuoga, nikatoka jamani kwanza ungeziona bra zangu za mwanzo halafu hizi nimeletewa unaweza kukaa chini ucheke. Kuna braaa nzuri jamani, mwanzo nilikuwa navaa kishikilia kifua tu halafu sasa hizi ndiyo braa.

Nilijiweka sawa halafu sasa nikaweka Abaya langu black, halafu mtandio ule nikajifunga mtindo fulani simple wa kupendeza halafu nikajiangalia kwa kioo.

Nimependeza sana, mimi kumbe mzuri ni nguo tu zinafanya usinizingati. Ndugu yangu nunua nguo, nguo hubadilisha mambo, nguo za kuvutia na nzuri huvuta neema nakuambia.

Nilikuwa kama sio Nazwi mimi, nimependeza balaa. Acha kabisa hata mimi najishangaa najiambia “kumbe mimi ni mzuri hivi jamani, sikuwa najua hili, nimependeza saana.”

NAKUPENDA BILA MIPAKA:152
Nikatabasamu, na kusema “wacha nikashtue watu sasa.”
Niliweka vitu vyangu vizuri kabisa halafu nikatoka.

Nilipofika jikoni Maria alishangaa akisema “wewe, ni wewe Nazwiiiiiii, Mungu wangu!!. Mdogo wangu ako kamwili chako kazuri, kaumbo chako sasa kalivyo, eenh Hii gauni usiwahi kuvua kama uvae kila siku. Umependeza sana, umependeza mno. Ujue nilikuwa nikusahau. Hapa nishaelewa dokta ana macho ya ndani, alielewa mapema sana.”

Nikacheka na kusema “dada Maria ujue una mdomo sana niache eenh, supu yangu si tayari.”

Alitabasamu akisema “Wallah umependeza kaka akikuona lazima atakusifia, hakuna mtu anakufahamu asikusifie. Hili gauni tamuuu.”
Nikacheka nikisema “dada tamu tena, halafu sawa gauni ila hili lina jina lake, linaitwa Abaya.”

Alitabasamu, ananitazama anatabasamu tu akisema “Mungu, Mungu aanh kuna watu ni wazuri. Wewe ni kazuri sana. Mungu wangu.”

Dada Maria tu sasa anataka kichwa kipasuke sio kwa sifa hizi. Mimi nilisogea na kuanza andaa chakula kisha nilisema “Boss ana njaa muhudumie supu hii na ndizi hizo hapo, hii napeleka kwa mama sasa.”

Alitabasamu, nilianza kwenda. Dada Maria aliita “nesi!!”
Nilisimama na kumtazama, alisema “tumefurahi upo hapa asante. Ilikuwa mbaya.”
Nilimtazama na kutabasamu tu halafu nikaendelea na safari.

Nilifika mpaka chumbani kwa mama, mama alikuwa ameamka, ile naingia mama alishangaa hata aliachia mdomo. Nikasimama na kusema “mama jamani.”
Alishangaa akisema “ni wewe binti yangu Nazwi?”

Nilicheka kidogo na kusema “ila mama, haya jiandae supu nzuri ipo tayari.”
Mama alinishangaa bado na alisema “mwanangu umependeza. Weka supu hapa simama hapo.”

NAKUPENDA BILA MIPAKA:153
Nilitabasamu na kufanya alichotaka, akasema “ebu zunguka, eenh zunguka. Eenh Mungu nna binti mzuri sana. Hii nguo imekupendeza mno. Uzuri wako umeonekana vizuri kabisa. Mwanangu jamani, wewe ni mrembo sana. Nafurahia kukuona hapa. Nashukuru sana mwanangu.”

Nilitabasamu na kusema “mama nashukuru sana kwa upendo. Tule sasa.”

Mama alitabasamu, halafu alisema “ukweli lazima niseme, mwanangu wewe aaah wewe chombo tena chombo saafi. Nashindwa hata niseme nini. Nishushie tu supu, vipi mwanangu amekuona?”
Nilitabasamu tu nikisema “mama lakini upoje.”

Akacheka na kusema “nitakupa umbea nile kwanza.”
Nikacheka huku nikisema “mama ushaanza mimi sitaki. Nakulisha huku unaniambia eneh niambie.”

Mama akasema akicheka “dokta kabale nikiwa hospitali walifikiri nimelala. Akawa ana mshauri Gallen. Tutafute nesi mwingine, huyu naona mjuaji sana anaweza sababisha tatizo.”

Gallen sasa anasema “hapana, Nazwi hapaswi kuacha kazi ni mtu pekee anaongea lugha moja na mama.”

kabla Dokta hajasema kitu nikafungua macho na sauti ikatoka nikisema “sitaki yeyote, binti yangu arudi na mna maelezo ya kuniambia kwanini sio yeye. Namtaka Nazwi.”

Dokta niliona sura yake, ikawa inatisha ila anatabasamu. Nikacheka na kusema “ila mama, kwahiyo umbea umeishia hapo?”

Akacheka na kusema “najikaza mwanangu, kwasababu wewe upo. Ila sipo vizuri.”
Nikamwambia kwa upole “kula mama ndiyo utapata nguvu.”

Mama alitabasamu na kusema “umependeza sana mwanangu. Nitakununulia nyingi kama hizi. Nazwi asante upo hapa. Nashukuru kwa msaada wako binti.

NAKUPENDA BILA MIPAKA:154
Hakuna kiwango cha pesa nitakupa kitatosha. Lakini mwanangu nataka ujue ya kuwa nakupenda sana. Nitahakikisha una furaha wakati wote.”

Nilitabasamu na kusema “asante sana mama.”
Aliniambia kwa upole “niahidi hutoniacha binti yangu.”

Nilitabasamu na kusema “Nakuahidi mama. Sitakuacha hata iweje.”
Alitabasamu na kusema “Supu tamu, asante sana. Na nakupenda mwanangu.”
Nikatabasamu pia na kusema “Nakupenda mama.”

Huyu mama anaumwa, ukimtazama tu unajua kabisa anaumwa ila ni mtu Imara sana. Ni imara. Alilala tena nikiwa namtazama huku natabasamu tu, nikamuweka sawa, nikatoa vyombo na kurudi kumtazama.

Nimekaa pale kwenye kochi, na nguo yangu mpya. Najitazama natabasamu tu, siamini, siamini kila kinacho nitokea.Sijui ni ndoto naota, sijui ni ukweli huu au nijizabue ndiyo nijue haya yote ni ukweli na sioti ni uhalisia.

Mambo mengi sana yametokea, mengi sana. Nikisema mambo mengi namaanisha mambo mengi sana. Lakini katika mambo mengi yaliyotokea hili la leo, hili la busu ni jambo kubwa kuwahi kutokea kwangu tangu dunia yangu iumbwe.

Hata natamani nifanye tangazo maalumu lakini nafanyia wapi hili na wewe likufikie eenh. Hahahahaaa!!, hahahahahah!!, hahahahaha!!!, eenh nachoka mimi jamani, kila ninachowaza kuhusu busu na Mr serious wangu ni uchizi. Ni uchizi naona kabisa mwenzenu naenda kuchanganyikiwa.

Lakini kadri muda ulivyokuwa unazidi kwenda, kadri nilivyokuwa nazidi kukaa hapa ndiyo nilikuwa nazidi kuumia moyo wangu juu ya ndugu yangu, rafiki yangu kipenzi Dorice. Anateseka sana, anapitia maumivu, anaumia juu ya mama yake, mama yake na matendo yake. Roho yangu ilikuwa ina hangaika hata nikawa nakumbuka vile analia, vile anaumia, vile anasimulia. Ushirikiano wetu, umoja wetu namna tunaishi nilijikuta napoteza hata furaha. Nilikuwa tu natamani nirudi nyumbani nikamuone.

NAKUPENDA BILA MIPAKA:155
Mama alitumia muda mwingi sana kulala, muda wote huo sikuwa nimemuona Boss kabisa. Ni wazi na yeye alienda kupumzika. Ana stahili kupumzika. Amechoka sana. Siku zote hizi ana hangaika juu ya mama yake mpaka analala nje kwetu mchezo. Nilitulia tu.

Ulifika muda nilimwamsha mama, mama alipoamka niliona tu nimsafishe ili azidi kuchangamka. Nilianza kumuhangaika. Mama alikuwa tu ananitazama na aliniambia “pole sana mwanangu.”

Nilitabasamu na kusema “mama wewe ndiyo unastahili pole hii. Unaonekana umechoka sana mwanangu.”

Mama alinitazama akisema “ni kweli mwanangu, ni kweli nachoka. Dawa za safari hii sielewi kabisa. Lakini jambo zuri ni kuwa wewe upo hapa.”

Nilitabasamu, mama aliendelea tu kunitazama huku mimi nikifanya mambo yangu. Sikutaka hata kusema lolote niliacha tu yeye ndiyo ataongea. Mama yangu alisema “Nazwi mwanangu upo sawa kweli?”
Kwa upole nilimjibu “nipo sawa mama yangu.”

Kabla hata mama hajamaliza, dokta huyu hapa. Hajafa tu jamani. Nikajua leo ni kusafirisha maana kwa mbwembwe zake zile na kilichotokea. Aaaah dada ana roho ya paka huyu. Tena anatabasamu kabisa na alinisalimia “Hujambo nesi?”
Nilitabasamu na kusema “Shikamoo Dokta.”

Tena kaja kapendeza, eenh sijui ndiyo ameenda kujiupdate. Au ndiyo sijui tuseme amejipanga upya. Huwa anapendeza. Safari hii. Amependeza kupitiliza.Na hapa nisiwe muongo anapatia sana. Mimi haya sio mambo yangu, sio mambo yangu mimi tu nioge nivae masuala ya kujipodoa hata pakuanzia mimi sijui bora hata rafiki yangu Dorice.

Alitazama na kusema “umependeza nesi.”
Nikatabasamu na kusema “umependeza sana dokta.”
[3/28, 2:51 AM] faraja simulizi nunua: 156 - 165 SEASON FOUR
NAKUPENDA BILA MIPAKA:156
Akapiga hatua akisema “mama yangu mzuri. Unaendeleaje. Nilikumiss sana na sasa uniambie, kwanini ukaondoka hospitali hujaniambia mwanao.”

Mama alimtazama akisema “nisamehe tu binti yangu. Sikutaka kuendelea kukaa pale. Ilipotokea nafasi nikaona tu niondoke zangu.”

Akawa anacheka cheka na mama. Mara Boss akaingia. Alipoingia tu alitabasamu, tukatazamana mimi haraka nikakwepesha macho na kusema “Nimeondoka nyumbani mapema sana bila hata kuaga yeyote. Lazima watakuwa na wasiwasi sana. Kama hamtojali naomba kuondoka sasa.”

Mama alinitazama na kusema “upo sahihi mwanangu, lakini unaonaje unipe supu tena halafu ndiyo uondoke.”
Nilisema kwa upole “bila shaka mama, bila shaka.”

Nikatoka, baada ya kutoka nikaingia jikoni, na dada Maria alinisaidia. Nikarudi chumbani bado Dokta alikuwa hapo, mimi kimya kimya nilianza kumpa mama ile supu. Mama aliinywa vizuri sana, nikampa na maji alimaliza ile niliyokuwa nimeweka.

Alinitazama na kusema “Binti yangu sasa unaweza kwenda, lakini kesho uwahi sawa eemh.”
Nilitabasamu na kusema “upo sahihi mama. Kesho nitawahi.”

Alisema kwa upole “nashukuru sana, nashukuru.”
Nilitabasamu na kuaga. Dokta na yeye alisema “Uwe na siku nzuri nesi eenh.”
Dokta mnafiki huyu, mnafiki kama nini. Nilitabasamu tu huku moyoni nikisema “unaniletea sanaa THT hapa ndiyo jumba la sanaa. Tutanyooshana mnafiki sana wewe.”

Nilitoka mpaka kwa chumba changu cha kubadilishia nguo. Nilikusanya vitu vyangu na kuanza kutoka. Nilipita kumuaga dada Maria maana na yeye hakuwa sawa.

Hivyo niliagana na yeye na kumtaka tu aniambie kama akihitaji msaada hata mtu wa kuongea naye nipo kwaajili yake. Alitabasamu na kusema “Nakupenda mdogo wangu, wewe ni mkarimu.”

Nilimwambia kwa tabasamu “Nakupenda dada maria wangu, cha umbea wangu.”
Angalau akacheka, nilimkumbatia na kuondoka zangu.

NAKUPENDA BILA MIPAKA:157
Sasa naondoka rohoni naumia mimi, naondoka ondoka vipi Mr Gallen hata hajaniambia nimependeza, hajanisifia kweli ni haki jamani. Sasa nifanye nini sina namna inabidi tu niondoke zangu tu. Unajua ile eneh umependeza mwenyewe halafu hukutani na uliyemlenga, au umejiandaa mwenyewe akija akukute umependeza halafu haji. Basi yale maumivu moyoni sasa hapa ndiyo nayahisi.

Nakwambia sasa, nimetoka nje naelekea getini nifunguliwe mimi niondoke zangu. Nimetoka tu getini, ndinga hii hapa.

Nilitabasamu, halafu sio amekaa huko ndani ya gari, ameshuka, amekuja upande wangu kunifungulia. Kwanza sasa tangu nimfahamu sijui ana nguo ipi haijampendeza. Bana ana pendeza huyu, muanko ana vaa huyu mimi ni tabasamu tu.

Subiri!!, subiri taratibu kabla hatujaendelea, eenh nakukumbusha kwanza ni Tajiri, Ni boss, ni mkubwa, ni mtu mwenye misimamo lakini linapokuja suala la mimi, hivi vyote sivioni, anashuka na kunifungulia. Nilipoingia alinitazama na kusema “Hey, naweza kukukumbatia.”

Nilitabasamu, alinikumbatia kwa muda, akanifunga na mkanda wa gari mimi hapo natetemeka kindanindani asijue tu maana niseme ukweli kwake mimi sijiwezi kabisa. Baada ya hapo aliwasha gari hakukaa kimya alitabasamu na kusema “Nazwi umependeza mno.

Hivi si umeelewa, amesema mno, mbele ya sana unajua eemh, nilitabasamu na kusema “nashukuru sana. Nguo zote ni nzuri, lakini Boss ni gharama sana.”

Akatabasamu na kusema “Gharama haina maana kulinganisha na umuhimu wako Nazwi. Umependeza sana.”

Nilitabasamu, unasikia maneno haya, mimi ni bichwa linanielemea kama linapasuka.Ukiniona sasa natabasamu tu nasema “asante sana.”

Maoni

You're not logged in


Tangazo - Tume toka mbali na nyumbani kuja kwenye miji ya watu kutafuta maisha
Tume toka mbali na nyumbani kuja kwenye miji ya watu kutafuta maisha
Tume toka mbali na nyumbani kuja kwenye miji ya watu kutafuta maisha
Mwanangu Mungu ndio anae jua
Sikiliza Wimbo Kamili
   
X
SHARE TO SOCIAL MEDIA

NAKUPENDA BILA MIPAKA 151 -- 157

:151
Kwenye akili yako vuta picha zile Abaya za kituruki, halafu ziwe tatu, nzuriiiiiii, rangi nyeusi, rangi nyeupe, na zambarau fulani imechanganyika, halafu kuna gauni mbili za ukali, eenh, eenh sijui nirudie tena kutoa ushuhuda wangu.

Natamani sana ila nitawezaje sasa mnielewe, ni Mr Gallen ameninunulia. Mimi sasa naangali nakumbatia, na viatu vya chinichini halafu mafuta ya kupaka, halafu na nguo za ndani. Ninatabasamu nikisema “oooh!!, oooh jamani, jamani.”

Nikaona tu bora nikaoge kwanza, nitoe kwanza msisimuko wa Busu. Tena busu lenyewe hata mswaki, nisiseme sana si mnajua sijaoga. Sijui hata amefurahia ila mimi nimefurahia balaa. Nilipoingia bafuni, mimi nafanya hata vitu sijawahi...

👉 Soma zaidi hapa: https://www.gonga94.com/semajambo/nakupenda-bila-mipaka-151-157

#Nk #gonga94 #trending #simulizi #hadithi #viral #fictionwriter
#ShortDrama #fblifestyle #BeautyBattle #AfricaVsWorld #Tanzania #Kenya #Congo #Rwanda #Burundi #SouthAfrica #USA #VoteNow #DebateTime #Trending 🐓 Follow the ommy khan Tanzania channel on WhatsApp: https://whatsapp.com/channel/0029VbCg0JyFsn0hCN1ByD44

Share on Facebook
Share on Twitter
Share on LinkedIn
Share on Pinterest
 
Umesoma kwa utulivu · dakika chache tu Asante Endelea kusoma chagua hapo chini
Umependezwa ?? Asante Soma Zaidi nakupenda-bila-mipaka
NAKUPENDA BILA MIPAKA 131 - 140 SEASON THREE
NAKUPENDA BILA MIPAKA 131 - 140 SEASON THREE
NAKUPENDA BILA MIPAKA 141 - 144 MWISHO WA SEASON THREE
NAKUPENDA BILA MIPAKA 141 - 144 MWISHO WA SEASON THREE
NAKUPENDA BILA MIPAKA: 109 - 120 SEASON THREE
NAKUPENDA BILA MIPAKA: 109 - 120 SEASON THREE
NAKUPENDA BILA MIPAKA 96 - 100 MWISHO SEASON TWO
NAKUPENDA BILA MIPAKA 96 - 100 MWISHO SEASON TWO
NAKUPENDA BILA MIPAKA 1 - 12
NAKUPENDA BILA MIPAKA 1 - 12
NAKUPENDA BILA MIPAKA 121 - 130 SEASON THREE
NAKUPENDA BILA MIPAKA 121 - 130 SEASON THREE
NAKUPENDA BILA MIPAKA 76 - 86 SEASON TWO
NAKUPENDA BILA MIPAKA 76 - 86 SEASON TWO
NAKUPENDA BILA MIPAKA  36 - 45
NAKUPENDA BILA MIPAKA 36 - 45
NAKUPENDA BILA MIPAKA 26 - 35
NAKUPENDA BILA MIPAKA 26 - 35
NAKUPENDA BILA MIPAKA 66 - 75 SEASON TWO
NAKUPENDA BILA MIPAKA 66 - 75 SEASON TWO
NAKUPENDA BILA MIPAKA SEASON THREE 101 - 108
NAKUPENDA BILA MIPAKA SEASON THREE 101 - 108
NAKUPENDA BILA  MIPAKA 87 - 95 SEASON TWO
NAKUPENDA BILA MIPAKA 87 - 95 SEASON TWO
NAKUPENDA BILA MIPAKA SEASON FOUR 145 - 150
NAKUPENDA BILA MIPAKA SEASON FOUR 145 - 150
NAKUPENDA BILA MIPAKA 158 -- 160
NAKUPENDA BILA MIPAKA 158 -- 160
NAKUPENDA BILA MIPAKA  161 -- 164
NAKUPENDA BILA MIPAKA 161 -- 164
Tafuta Simulizi,Hadithi,Michezo
Andika unacho taka.

Top 10 Kali za Leo

NAKUPENDA BILA MIPAKA 151 -- 157

NAKUPENDA BILA MIPAKA 151 -- 157

319
NAKUPENDA BILA MIPAKA SEASON FOUR 145 - 150

NAKUPENDA BILA MIPAKA SEASON FOUR 145 - 150

300
ZARA❤️ Sehemu ya 8 na 9

ZARA❤️ Sehemu ya 8 na 9

164
ZARA❤️ Sehemu ya 6 na 7

ZARA❤️ Sehemu ya 6 na 7

159
BILLIONS OF LOVE💓💓   SEHEMU YA "16_17"💓

BILLIONS OF LOVE💓💓 SEHEMU YA "16_17"💓

142
💋ILA BOSS ANAJUA KUPELEKA MOTO 💋 (MWISHO SEASON 1) 19 -- 20

💋ILA BOSS ANAJUA KUPELEKA MOTO 💋 (MWISHO SEASON 1) 19 -- 20

101
IN LOVE WITH ZURI* *12&13*

IN LOVE WITH ZURI* *12&13*

95
*IN LOVE WITH ZURI* *Sehemu ya 11*

*IN LOVE WITH ZURI* *Sehemu ya 11*

70
ZARA❤️ Sehemu ya 10

ZARA❤️ Sehemu ya 10

54
Zamani kidogo nilikuwa darasa la saba siku moja mama aliongea na Mimi akanambia baba ako anarudi leo

Zamani kidogo nilikuwa darasa la saba siku moja mama aliongea na Mimi akanambia baba ako anarudi leo

33

ZIMESOMWA ZAIDI

‎TUNDA LA  DADA ‎ ‎SEHEMU YA KWANZA

‎TUNDA LA DADA ‎ ‎SEHEMU YA KWANZA

12.06K
RUNGU LA KIPOFU 22.

RUNGU LA KIPOFU 22.

7.74K
🙄 NILIONA MWENYEWE DADA YANGU ANAGEUZWA🔥  sehemu ya tisa.  👉 Akaanza kunipamp sasa...👇

🙄 NILIONA MWENYEWE DADA YANGU ANAGEUZWA🔥 sehemu ya tisa. 👉 Akaanza kunipamp sasa...👇

3.92K
🔥 UTANI WA SHEMEJI KAICHOMEKA..6..10  KWELI...Aaaaaaaaa chomoa🔥  Sehemu ya sita.  👉 Aaaaaaaaa chomoa...👇  Shemeji inauma utanichana.

🔥 UTANI WA SHEMEJI KAICHOMEKA..6..10 KWELI...Aaaaaaaaa chomoa🔥 Sehemu ya sita. 👉 Aaaaaaaaa chomoa...👇 Shemeji inauma utanichana.

3.7K
MY WANGU❤️ sehemu ya 108

MY WANGU❤️ sehemu ya 108

3.14K
MY WANGU❤️ sehemu ya 119 na 120.

MY WANGU❤️ sehemu ya 119 na 120.

3.05K
MY WANGU❤️ sehemu ya 116 na 117

MY WANGU❤️ sehemu ya 116 na 117

2.91K
 UTANI WA SHEMEJI KAICHOMEKA KWELI...Aaaaaaaaa chomoa🔥  Sehemu ya 20.  👉 Nikatanua mwenyewe miguu manuu..kazi kwake tu...👇

UTANI WA SHEMEJI KAICHOMEKA KWELI...Aaaaaaaaa chomoa🔥 Sehemu ya 20. 👉 Nikatanua mwenyewe miguu manuu..kazi kwake tu...👇

2.88K
MY WANGU❤️ sehemu ya 106 na 107

MY WANGU❤️ sehemu ya 106 na 107

2.78K
🔥 UTANI WA SHEMEJI KAICHOMEKA..16..20  KWELI...Aaaaaaaaa chomoa🔥  Sehemu ya 16.  👉 nakupenda pia...👇

🔥 UTANI WA SHEMEJI KAICHOMEKA..16..20 KWELI...Aaaaaaaaa chomoa🔥 Sehemu ya 16. 👉 nakupenda pia...👇

2.73K

RATIBA ZA MAKALA ZETU

****

  • NAKUPENDA BILA MIPAKA 161 -- 164 29-03-2026 00:00
Machapisho Mapya
Vijipost vilivyotangazwa karibuni (yamekatwa hadi maneno 30)
IN LOVE WITH ZURI* *12&13* Post Mpya
IN LOVE WITH ZURI* *12&13*
@mjukuu LIVE

* SONGA NAYO....... Nilisema huku nikimkabizi ule mfuko, zuri alinitazama sana mpaka ule ujasiri wote niliokuwa nao ulianza kupotea kidogo kidogo "Unasema..??" Aliniuliza "Am nimekuletea hii hapa zawadi.." "OH my God ni yangu..??" Aliniuliza tena huku akitabasamu,...

*IN LOVE WITH ZURI* *Sehemu ya 11* Post Mpya
*IN LOVE WITH ZURI* *Sehemu ya 11*
@mjukuu LIVE

SONGA NAYO...... Haraka haraka nilitoka nje ambako nilimkuta Ethan akiwa ananisubiri, bila kusubiri chochote niliingia kwenye gari na safari ya kurudi nyumbani ilianza, ni mida ya saa moja na nusu hivi "Dah...

ZARA❤️ Sehemu ya 10 Post Mpya
ZARA❤️ Sehemu ya 10
@mjukuu LIVE

__________ Mwandishi; LISSA WA HURU MEDIA ila sasa ni alijuwa na heshima sana na mimi, yani alijirejebisha kweli kweli , waha hakuwa annifanyia ujeuri kabisaa,yani ata kidogo hapana ,...

ZARA❤️ Sehemu ya 8 na 9 Post Mpya
ZARA❤️ Sehemu ya 8 na 9
@mjukuu LIVE

__________ Mwandishi; LISSA WA HURU MEDIA Nikasema.dady sio kuhusu mama ni kuhusu yule dereva melvin, baba aksema ahaa yule derebaa si tumeshamfukuza jamani zara nn sasa, nikasema baba mi nimemuonea huruma ,nahisi...

ZARA❤️ Sehemu ya 6 na 7 Post Mpya
ZARA❤️ Sehemu ya 6 na 7
@mjukuu LIVE

__________ Mwandishi; LISSA WA HURU MEDIA Khaaaaa nilichukia nikamuangalia uyu kaka kwa dharau na hasira kwli kweli, kwanza nikampandisha kisha nikamshusha , nikamuuliza eeeh umesahau nn, au unadai mshahara apa ulikuwa...

NAKUPENDA BILA MIPAKA 158 -- 160 Post Mpya
NAKUPENDA BILA MIPAKA 158 -- 160
@mjukuu LIVE

:158 Aliendesha na kuniambia “nisamehe kwa kukuteka asubuhi, nisamehe maneno yalinitoka asubuhi lakini ilikuwa lazima nifanye vile. Wewe katoto ni kabishi sana. Huna hata huruma unataka mtu mzima mpaka nipige ukunga.” Nilimtazama,...

NAKUPENDA BILA MIPAKA 151 -- 157 Post Mpya
NAKUPENDA BILA MIPAKA 151 -- 157
@mjukuu LIVE

:151 Kwenye akili yako vuta picha zile Abaya za kituruki, halafu ziwe tatu, nzuriiiiiii, rangi nyeusi, rangi nyeupe, na zambarau fulani imechanganyika, halafu kuna gauni mbili za ukali, eenh, eenh sijui...

NAKUPENDA BILA MIPAKA SEASON FOUR 145 - 150 Post Mpya
NAKUPENDA BILA MIPAKA SEASON FOUR 145 - 150
@mjukuu LIVE

:146 Nilimtazama natabasamu, nakuambia uoga mimi sina, sina kabisa maana nishajua huyu Dokta anapambania mahali ahitajiki. Kwanza angejua raha mimi nilikuwa naipata hapa ameniharibia mimi. Si unajua unampenda mtu huwezi kumwambia halafu...

BILLIONS OF LOVE💓💓   SEHEMU YA "16_17"💓 Post Mpya
BILLIONS OF LOVE💓💓 SEHEMU YA "16_17"💓
@majario LIVE

( alikuja kama muuza chai kumbe ni Billionea) Alikunywa dawa zake akatulia 🥹nilikuwa namuonea huruma sana yule mkaka jmn 🥹 Muda huo huo wateja wakaja watatu , mimi sasa bize...

Zamani kidogo nilikuwa darasa la saba siku moja mama aliongea na Mimi akanambia baba ako anarudi leo Post Mpya
Zamani kidogo nilikuwa darasa la saba siku moja mama aliongea na Mimi akanambia baba ako anarudi leo
@majario LIVE

toka safari(Hawa ni mama na baba angu wa kunizaa) mama alinambia baba akifika tuu chochote atakachokwambia kubali nikamwambia Kuna nini akanambia Nisikilize Mimi nikamwambia nakusikiliza akasema leo utalala chumbani...

💋ILA BOSS ANAJUA KUPELEKA MOTO 💋 (MWISHO SEASON 1) 19 -- 20 Post Mpya
💋ILA BOSS ANAJUA KUPELEKA MOTO 💋 (MWISHO SEASON 1) 19 -- 20
@majario LIVE

19 Aliingia kaka yake na Glad Mimi ndio nilikuwa namalizia kupika jikoni, G nimekuletea ice-cream 🍨🍦 unayopenda nilinyamaza kimya hadi alipokuja jikoni. Glad ametoka mara moja nipo mimi peke yangu nilikuwa namalizia...

NAKUPENDA BILA MIPAKA 141 - 144 MWISHO WA SEASON THREE Post Mpya
NAKUPENDA BILA MIPAKA 141 - 144 MWISHO WA SEASON THREE
@majario LIVE

:141 Nikamwambia kwa ujumbe “Boss ni usiku sana, nenda nyumbani, tutaongea kesho naomba nipumzike.” Akanijibu “sitaondoka hapa mpaka uje kunisikiliza.” Nikamuonyesha Dorice, Dorice akasema “kamsikilize Labda ni muhimu.” Nikamwambia Dorice “kusema kweli mimi roho...

JOGOO WA KIENYEJI sehemu ya 15 Post Mpya
JOGOO WA KIENYEJI sehemu ya 15
@majario LIVE

Mwandishi:lissa mwalla Simu ilikatwa,nilichanganyikiwa,iv nimeskia kweli au ni mawenge yangu?keanu ananisaliti?yani maneno yake makavu yote aliyoniambia hayakua na maana sikuyajali kabisa nilijali mwanamke alieongea.nikasema hapana ngoja,nikapiga simu iliita ikakatwa,nilipiga tena ikakatwa,nikapiga...

Kinachomtisha Mgosi ni kuwa Edna Lema anawachezaji walioonekana wa kawaida Simba Post Mpya
Kinachomtisha Mgosi ni kuwa Edna Lema anawachezaji walioonekana wa kawaida Simba
@majario LIVE

ila sasa wapo kwenye kiwango cha hali ya juu kiasi cha baadhi kuitwa timu zao za taifa. Diana Mnally Ritticia Nabbosa Precious Christopher Wincate Kaari Aisha Djafar Edna Lema...

JOGOO WA KIENYEJI sehemu ya 14 Post Mpya
JOGOO WA KIENYEJI sehemu ya 14
@majario LIVE

Mwandishi:lissa mwalla Mmmh nilihisi utumbo unacheza, kwa nn haruhusiwi ndoa sasa? Au ameoa? Nilijiuliza sana, keanu akasema sijakuelewa kwa nn siruhusiwi kuoa sasa? Akasema kuna mashart katika kila kanisa ili...

Home Login Signup
Top 20 Privacy Policy Contact us
Terms & Conditions About us Latest