Simulizi za Maisha,Mafunzo,Mapenzi ,Chombezo Habari za Michezo na Burudani vyote kwa Kiswahili ndani ya – Gonga94 Semajambo
Gonga94 · Stories
30 Nov 2025
195 views
VYOTE NDANI GONGA94
Jamani Kaka Cheni … Ndiyo Nini Sasa?! Sehemu Ya Kwanza (1)
Usimulizi huu ni wa watu wazima. Chukua muda wako, tulia, kisha usome kwa utulivu kama machapisho yetu yanayoendelea moja kwa moja.
Chombezo :
IMEANDIKWA NA : MAZUNDURU ATHUMANI
Sijui nini kiliendelea, nilipitiwa na usingizi moja kwa moja na kuja kushtuka saa kumi usiku nikiwa napitisha kumbukumbu kichwani, nikakumbuka mara ya mwisho ilikuaje. Nikakumbuka nilifikia sehemu moja na kaka Cheni na mwanamke wake, nikakasirika sana.
***
Asubuhi ilifika, kulikucha, nikatoka kufanya kazi za ndani uani huku nikiwa nalenga kuona kama yule mwanamke wa kaka Cheni aliondoka au alilala palepale. Nilifanya kazi kwa umakini wa macho. Muda mwingi nilikuwa nakazia macho mlangoni kwa kaka Cheni.
Saa moja, kaka Cheni alifungua mlango wake. Akatoka yeye akiwa amevaa bukta nyeusi tu, juu alikuwa kifua wazi. Akakutana macho na mimi, akaachia tabasamu. Mimi nilihisi aibu, nikaangalia pembeni, moyoni nikasema; ‘kaka Cheni bwana’.
“Mama ameamka?” aliniuliza.
“Kaenda kwenye maji,” nilimjibu nikiendelea kuangalia pembeni.
“Hujanijibu swali. Nimekuuliza mama ameamka, unajibu kaenda kwenye maji.”
“Sasa kaka Cheni anaweza kwenda kwenye maji akiwa amelala?” nilimjibu ki hovyo maana hata yeye alijua kwa nini nilimjibu vile.
“Yamekwisha…kwenye maji wapi?”
“Kwa mama Tabu.”
Kaka Cheni akarudi chumbani kwake. Nikajua kwa nini aliniuliza vile. Nikajua alilala na yule mwanamke wake sasa alitaka kujua alikoenda mama ili amtoe mwanamke wake.
Baada ya dakika tatu, kaka Cheni alitoka akiwa amevaa traki suti, nyuma yake akafuatiwa na mwanamke. Jamani! Ninaposema mwanamke nieleweke kwamba ni mwanamke. Sijui kama Cheni alimpendea nini maana si saizi yake. Muwowowo huo, mpaka nikacheka mwenyewe moyoni.
Nikasema loo!
Akitembea sasa, mbengenyu… mbengenyu…mbengenyu. Hapo alikwenda chooni. Akiwa bado chooni, baba akatoka na kiti, akakaa nje…
Nilimwona kaka Cheni akishtuka sana. Hata mimi nilishtuka kwani nilijua baba ameshakwenda kazini kwake, kumbe alikuwepo bwana.
“Shikamoo baba,” kaka Cheni aliamkia huku wasiwasi wake ukiwa umegundulika na baba.
Jamani Kaka Cheni … Ndiyo Nini Sasa?! Sehemu Ya Kwanza (1)
Chombezo :
IMEANDIKWA NA : MAZUNDURU ATHUMANI
Sijui nini kiliendelea, nilipitiwa na usingizi moja kwa moja na kuja kushtuka saa kumi usiku nikiwa napitisha kumbukumbu kichwani, nikakumbuka mara ya mwisho ilikuaje. Nikakumbuka nilifikia sehemu moja na kaka Cheni na mwanamke wake, nikakasirika sana.
***
Asubuhi ilifika, kulikucha, nikatoka kufanya kazi za ndani uani huku nikiwa nalenga kuona kama yule mwanamke wa kaka Cheni aliondoka au alilala palepale. Nilifanya kazi kwa umakini wa macho. Muda mwingi nilikuwa nakazia macho mlangoni kwa kaka Cheni.
Saa moja, kaka Cheni alifungua mlango wake. Akatoka yeye akiwa amevaa bukta nyeusi tu, juu alikuwa kifua wazi. Akakutana macho na mimi,...
👉 Soma zaidi hapa: https://www.gonga94.com/semajambo/jamani-kaka-cheni-ndiyo-nini-sasa-sehemu-ya-kwanza-1
Maoni