MIMI SIKUACHI🥰 Sehemu ya 36 na 37
Basi bwana kuanzia apo rasmi mi nikavunja mkataba na princess kabisa. Nikawa busy na maisha yangu kabisaa. Lemi aliniulizaga we ndo unahusika na mimba ya princess nikasema hapana siusiki kivyovyote na mimba yake na wala mm sio muhusika wa ule mzigo kabisaa. Nilikataaa .si amenambia sio yangu basi fresh. Mi nikawa busy na shule sana. Na familia. Si unajua tena nna kabinti sasa. Asee mwanangu alikuwa mzuri kama mama yake . Na kanapenda kucheka sana. Yani mnooo. Alafu alikuwa ananipenda mnoo uyu mtoto . Yani ananipenda aswaa na ananijua mie baba. Mana kilivyofikisha miez 3 . Kalianzaa kutambaa .basi nikilidi anatambaa ananifata uku anacheka . Yani anajua kabisa kuwa baba anaingia sasa. Ilikuwa ni rahaa mnoo.
Basi bwana ikapita miez 3. Nina princesss tumbo limemchomoka kabisa. Na ikawa sio siri tena . Kila mtu anajua kabis kuwa princess ana mimba. Wengine wakawa wananihisi mm. Washikaji wananaitania kuwa mi noma mpaka nimemtia mimba princess. Mi nawaambia sihusiki itakuwa michael. Ila kwa kipindi iko sikuwa namuona tena na michael .ata princess namuona kwa nadra sana chuoni. Yani nimbahatishe sana. Na tukikutana hatukuwa tunaongeleshana kwa chochote ata salamu sisi hatukuwa nayo.kila mtu ni busy na maisha yake. Basi mimi nikawa napambana na maisha yangu na ile stationery ikawa inanisaidia sana . Apo nakimbiza sana chuo. Yani napasua mnoo. Unakuta napata mpaka madeals ya kufundisha njee uko wananipa maleacturer. So vihela nikawa napata. Ndani kwangu nikanunua vitu vyote vya ndani yani. Basi mke wangu akawa anapendeza .na ananenepa japo ana lea. Mana vipesa vipesa nilikuwa napata tu nashukuru
Basi bwana ikapita mdaa nikawa sijamuona princess pale chuo. Kama miezi 3. Sikumuona kabisa. Na kwa mda uo alikuwa mwaka wa 3 .so ulikuwa ni mwaka wake wa kugraduate. Ila sikuwa namuona akija kabisa chuo. Na mpaka wenzie waligraduate ila yeye hakufanikiwa kumalaiza chuo. Na kila mtu alijua na watu wengi walimzungumzia . So unajua ukiwa maarufu shuleni. Wengine wakaanza kumsema na vibaya kuwa aliendekeza sana mapenzi chuoni mpaka kapata mimba kashindwa kuendelea na masomo. Yani story zilijuwa nyingi sana. Kuna siku lemi alinambia kuwa ata kwenye simu now hamuoni. Yani hajipost ata. Nilitamani kumpigia ata nimuulizie tu. Kuwa ana shida gani ila nikaona ntakuja kuanzisha mawasilino nae baadae ikaniletea shida. Nikaamua kukausha tu.
Na finally nikaingia mwaka wa 3. Apo kabinti kangu kana miez 9. Na tuna furahaa. Sana.ni katundu na kashakuwa kanasimamia. Akiniona ananiita baba kabisa . Bsi maisha yakawa yanaendelea. Nikatulia mno zipu nilikuwa nafungia kwa mke wangu tu. Na mke wangu nae hakuwa na shida. Ana heshima sana fatuma ..na huruma na upendo mpaka rahaa. Basi nikapambana sana chuo mpaka nikaaingia mwaka.wa 3 yani mwaka wa mwisho wa masomo. Apo ndo nikakaza zaidi mana mzumbe chuo ni kigumu hakitaki lele mama..basi nikakaza buti.. na finally nilimaliza chuo. Yani apo sikuwa kabisa kuonana na princess wala kuongea nae . Na kichwani nilishamtoa kuwa sina plan nae tena . Yani nilishamove on na maisha yangu. Apo sasa nilishadevelop kimaisha nilipanga chumba na sebure. Na ndani nikiwa na furniture zote japo za kawaida ila nnazo. Na mtoto wangu alikuwa na miaka 2. Anatembea kabisa. Baada ya kumaliza . Mim sikuwa na plan za kuondoka mzumbe. Ile stationery ilikuwa inanisaidia sana. So nilimwambia mke wangu kuwa sie tutabaki uku na maisha yetu yatakuwa uku mpaka nitakapo pata kazi . Hatuna plan za kurudi babati. Mke wangu wala hakuwa na shida akakubalina na mm tu.
Basi nikatulia nasubiri graduu. Uku najishikiza katika vibarua vya kufundisha tutions. Mana tulifunga chuo na wengi waliludi makwao ata lemi ya aliludi kwa dar. Mi nikakausha nikawa napamabana na life. Basi bwana nikajichanga changa na finally mahafari yetu ikafika. Apo sasa mama na dada walisema wanakuja kwenye mahafari yangu na kutuona. Tukawakalibisha sana na tukafurahi sana . Asee mama na dada waktupongeza sana kuwa tumeweza na tumejitahidi. Mana ndani kwetu kulikuwa pazuru tu. Kila kitu cha muhimu mke wangu nilimuekewa. Basi ikawa rahaa sana hii siku walofika wazazi . Ilikuwa ni story tu. Hatukulala.. yulipiga sana story yani sanaa uku mama akicheza na mjukuu wake. Akamsifia sana kuwa arina kafanana sana na mama yake kwa kila kitu . Fatuma akawa anacheka tu . Na kesho yake ndo ilikuwa siku yangu ya kugraduate
Basi mapema sana mke wangu ndo aliniandaa .nilipiga suti ya atari .niliwaka sana . Apo chini nna kiatu kizuri ilikuwa unyama sana. Basi bwana asubuh na mapema mi nikaingia chuo uku familia yangu ikija nyuma. Na mpaka saa 4 graduu ikaanza bwana . Kulichangamka sana. Nashukuru nilikuwa best student wa chuo kwa uo mwaka.na pale pale nilipata offer ya kuajiliwa katika bank moja kubwa sana . Katika tawi lake la morogoro mjini. Nikapata schoolar ship ya kwenda china kuongeza elimi nikitaka. Nikapata chance ya kuwa leacture wa mzumbe kama nitahitaji. Bado kuna kampuni nyingi zilinipa offfer aseee nilikuwa na rahaa sana . Ilikuwa ni hatua kubwa sana kwenye maisha yangu. Nilimshukuru sana mungu. Na mimi ndo nilisoma hotuba pale. Ilipendeza sana jamani . Yani nilifanikiwa kumuona mpak baba mkwe si ni mbunge bwana wa moro mjini alijuwepo . Yani baba yake na princess. Akawa ananipigia na makofi kabisa. Nafikiri hakuwa anajua kuwa nilishawahi kudate na mtoto wake uko nyuma.
Basi baada ya kumaliza graduu chuo .nlipokeag sana pongezi ple.washikaji ndo usiseme. Yani nilipata raha sana. Basi mke wangu alinikumbatia kwa nguvu. Nikamkumbatia pia kisha nikamnyanyua mwanagu. mam na dada walinipongeza sana kwa htua kubwa ya maisha yangu niliyoipiga. Aseeee ilikuwa rahaa sana. Hatukukaa sana chuo tulikija kumaliza nyumbani kwangu. Apo ndipo nilikataaa keki..na tukala chakura kwa pamoja .mama akijivunaia sna mimi.
Na usiku nilishauliana na mke wangu . Nifate offer gani . Mke wangu anaelewa sasa ananmbia mi ata sijuh bwana. Nikasema.sawa nakubali kufanya kazi katika iyo bank iliyopo moro mjini . NA nitakiwa nasoma apa mzumbe kupata masters yangu. Mke wangu akanambia sawa. Basi wazazi walikaa kama week 1 nyumbani kwangu wakaaga..aaseee kabla ahawajaondoka niliwafanyia shopping kubw sana. Mana ile siku pia nilipewa kama milion 5 kama.zawadi. basi niliwafurahisha tu mama na dada yangu. Mana wamenipambania sana mpaka leo nafika apa. So niliona ata kwa iki kidogo wafurahi. Basi wakafurahi kweli na nikawasafirisha wakarudi babati sasa.
🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi