MY WANGU❤️ sehemu ya 78
Basi bibi mie nikaanza kujiandaa kwa ajili ya club. Na nguo nnazo kama zote. Kuna mda mlige ananinuliaga mpkaa nguo za ajabu . Ila nivae tu nikiwa na yeye. Na nguo kanijazia . Nna kabati la milango mitatu liko full kwa kujaa nguo. Yani nna nguo aswaaa . Wala sio shida zangu.angel akanipigia nijiandae. Nikamwambia niko kumpanga baby ila niko najiandaaa pia so tunaenda kama kawaida .akanmbia sawa . Basi kufika saa 2 mlige kapiga. Vp mama unaendeleaje .nikasema bado mume wangu kichwa kinauma .pia nasikia na mwili wa moto nahisi na homa.
Mlige akanambia basi agiza chakura kwanza ule na kisha .umeze dawa upumzike sawa mama.nikasema ndio . Basi akawa anianipa nipa moyo kumbe mie wala nna jamboa langu tu. Akakta simu . Mie nijajiandaaa zangu kwa ajili ya club. Nikavaaa kigauni cheupe cha kubana nyuma mgongo wazi . Na mtako wangu ulivyochora sasa wewe. Nikavaa na kiatu changu kirefu. Nikawa najifanyia make up pale. Mana kusuka nilishasuka.kila week mlige anatuma elfu 90 ya kusuka. So huwez nikuta na nywele fumu fumu mm.
Basi kufika saa 4 usiku. Mlige akapiga tena simu. Nikajifanya kma naongea kiusingizi. Akanmbia ulishakala kumbe mke wangu daah kweli unaumwa leo unalala huu mda mama.nikasema ndio sipo sawa . Napumzika kidogo. Akanmbia sawa lala basi mpenzi. Ila ntakuwa nakupigia pigoa kukuulizia mke wangu nishakuwa sina raha unaumwa. Nikasema usijali. Kanmbia sawa pumzika. Basi nikakata simu na shoga anafika. Akanisifia nakwambia. Akanmbia dada we ni mzuri bwana .uo mtako wako tu unapagawisha bwana. Nikacheka kweli. Tukarequest tax . Tukapanda ao mpaka masaki ndo iyo clup ilipo.
Mpak saa 5 tukaingia club bwana. Sie tukaenda sehemu tukakaaa pale bwana. Nyieee kulinogaa mnooo watu kama wote mziki nakwambia. Sie tukaagiza savaana pale. Hizi natumia ata nikiwa na mlige. Ndo ananinuliaga hizi. Ye anakunywa pombe ila sio mlevi. Na yeye ndo alianza kunifundisha kutumia hizi savanna. Kipindi iko ananambia nikinywa hizi ndo nakuwa nampa vizuri wala simuonei aibu. Basi tukawa tunakunywa uku mziki unaendelea aseee kulikuwa navibess kama loteeee nakwambia watu ni wengi mnoooo
Angel akwa anacheza nakwambia mnooo. Basi mie sikuwa mchezaji ila nilipenda lile vibes mnooo. Basi nikiwa pale. Akaj muhudumu wa kiume .akanmbia mabo nikamjibu powa akanambia kuna mtu anakuhita juu kule. Mh nikapangalia juu . Nikaon kuna watu na kumetulia alafu wanacheki mpira . Mie wala sikutaka kwenda nilijua ni usumbufu wa wanaume tu. Ila nilikuwa ntaka kuchangamsha akiri tu wala sijja kufata wanaume mie. Mlige wangu ananitosha sana. Mh mala akaja muhudumu wa pili akanmbia tena naitwa kule juu .sikutaka kwenda . Mh mala akaja mkaka wa makamo tu akanisalimia mambo. Nikasema powa. AkAsema daah mtoto mzuri mda wote unaitwa kule ju ndo umegoma kupanda . Nikasema yaa sitaki . Sijafata wanaume apa. Yule mshikaji akasema.sikia kule juuu kuna mtu speciala anakuuita wewe. Anaitwa kabaisa fanya uje utakosa bahati. Mh mie nikajinyamazia . Mh angel sindo akasikia akasema hee kabaisa ndo anamuita faridaah. Yule jamaa kasema yaa mwambie shoga yako atakosa bahati shauri yake
Nyie angel akanmbia wewe nenda uyo kabaisaha ana pesa mnooo. Shoga mkaka wa kiarabu ni handsome kisenge .ebu nenda bwana nikasema siend. Nikasikia sauti tamu na nzito kweli kwei. Ikisema aya kama hutaki kuja kule.mm ndo mwenye shida faridah nimekufata sasa.nyie nilistuka nageuza sula namuona zayd uyu hapa. Aseee amezidi kuwa mzuri . Bonge la handsome . Kaka jaeupe peee. Bado kabana nywele zake. Na kapendeza mnoooo. Alafu akawa anatabasamu mnooo . Nyie mimi nilihisii kama naota yani nimekutana na zayd tenaaaa.
🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi