AAAAH IMETOSHA BOSS ππ N0 51...52ππ
Uwe na usiku mwema mke wangu mimi nitakwenda kulala kwenye chumba changu kingine natumaini hili jambo litabakia kuwa la siri kati yetu sisi wawili..... natumaini hautamwambia mtu yeyote yule Acha ibakie siri kama vile nilivyoificha aibu ya kile ulichokitenda..... heeπ³π³ huo ndo ujumbe alioniachia mme wangu pale kwenye muto..... baada ya kuusoma nilihisi kuchanganyikiwaπ΄π΄ hivi huyu mwanaume hana tena hisia na mimi kwa hiyo simvutii tenaπ€π€ si tuko honeymoon jamani ni kwanini asiyaweke pembeni makosa yangu tufurahie kwanza mapenzi ya ndoa yetuπ€π€ ataninyanyasa mpaka lini lakini mimi naye nilikurupuka sana kwenda kufanya mapenzi na hemedπ₯Ήπ₯Ήlakini tayari nilishakosea ataninyanyasa mpaka lini.... angalia adhabu ninayoipitia kwa ajiri ya ujinga wangu wa kujitakia...... hivi hii ndoa itakuwa ndoa ya aina gani etππ nilipanda kitandani kwa hasira nikalala kesho yake mapema alfajiri niliamka nikaingia bafuni nikaoga nilivaa nikapendeza sana baada ya hapo nilichukua notebook nikamwachia paschal ujumbe...... nilikukosea sana huenda ni kweli sisitahiri kusamehewa na weweππ sioni kama kuna umuhimu wowote wa kuendelea kuact kama watu tulioko kwenye ndoa hii itatumaliza kisaikolojia sisi bado ni vijana wadogo ambao tunatakiwa kuishi katika ndoa halisi na siyo hii ya maigizo iliyopo kati yetu sisi hapa, paschal ukweli ni kwamba mimi ninakupenda sana wewe lakini ninaona kabisa moyo wako umeshanitema sioni kama kuna umuhimu wowote wa kuendelea kuwa karibu na wewe nitaondoka mimi na mtoto wangu tutaelekea sehemu yoyote ile ilimradi tu tupotee machoni kwako make naona ni kama ninakupa tabu sana ya kukaa unanikwepa kila muda ....... kwa heri mme wangu ubaki salama niliivua ile Pete ya ndoa nikaiweka juu ya ule ujumbe nilizitoa line zangu kwenye simu nazo nikaziacha pale nilichafukwa sikutaka kuondoka na line zikaja nishawishi kumtafuta au yeye kunitrac kimtandao ili kujua sehemu niliko ni wapi..... nilimuandaa mwanangu nikaitisha tax tukawa tumeondoka kule hotel tukahamia mji tofauti ambapo huko nililipia chumba hotelini nikakaa na mtoto wangu......
Haikuwa rahisi kwangu kuamua uamuzi mzito kama ule.....lakini ilinibidi tu hakuna kitu kinauma kama umtege mwanaume wako alf asitegeke yani ujiweke fresh kwa ajiri yake alf yeye akikukuta hivyo achukue nguo kukufunika kisha akuache na kwenda kulala kwenye chumba kingineπ alf nilimkumbuka et niliyamis mapenzi yakeπsasa kaniowa ili iweje kama hataki kuniduu..... nilichokifanya nilimtafutia nice shule ni day care nilikuwa nampeleka asubuhi then jioni naenda kumchukua..... ilikuwa ni shule ya watoto wenye umri wa kuanzia mwezi mmoja hadi miaka miwili...... kwa kipindi hicho nice alikuwa na miezi 10 kuelekea 11..... nilimlipia nice huko kwa sababu sikuwa na mtu wa kumwangalia Isabella alienda kwao kusalimia baada ya kuwa sisi tumeondoka kuelekea paris kwa ajiri ya honeymoon...... mwanangu alianza shule nami nilitafuta kazi nilipata kazi katika super market moja ni katika kitengo cha cashier......ilikuwa ni kama bahati tu siku hiyo naenda kuomba kazi pale super market nilikuta wana uhaba wa cashier mmoja na nafasi ya kazi ilikuwa imebakia hiyo hiyo moja nilichukuliwa siku ileile na kuanza kufanya kazi.....
Nilikuwa natoka kazini saa 12 jioni naenda mpokea mtoto kwenye kituo cha school bus tunarudi hotelini kupumzika..... siku zilizidi kwenda mwilini kwangu nilianza kuona mabadiriko maziwa kifuani kwangu yalianza kunyauka hadi mtoto akaanza kukosa maziwa ya kunyonya mmhhh kizungu zungu cha hapa na pale uvivu nilianza kuwa nasinzia hadi kazini nilijiuliza hii hali ni kwanini inanikutaπββοΈπββοΈ sikuliwazia sana swala la ujauzito japo nilikuwa nimepitiliza siku zangu za period lakini tarehe zangu za period huwa zinabadirika kila mwezi nilihisi tu huenda ni stress za mapenzi ndizo zinazonichanganya...... siku moja nikiwa kazini nilidondoka kutokana na kuvamiwa na kizungu zungu kikali sana nilikimbizwa hospital nikachukuliwa vipimo majibu yalitoka kuwa mimi ni mjamzito nilishtuka sana kutokana na yale majibu ya vipimoπ΄π΄niliyaona kabisa matatizo yanavyozidi kuongezeka katika upande wangu niliwaza kumbambikia paschal ule ujauzito lakini ni miezi sasa imepita bila kushiriki naye tendo.....nakumbuka tangu niliporudi Tanzania kwa ajiri ya ndoa sikuwahi kabisa kuduu na paschal na hata siku tuliyokuwa safarini kuelekea Tanzania mimi nilikuwa niko period na paschal alilijua hilo kumsingizia huu ujauzito siyo rahisi ni bora hata ningekuwa nimejamiaana naye kwa siku za hivi karibuni........
Habari za ujauzito nilizipokea kwa masikitiko makubwa sanaπ€¦ββοΈπ€¦ββοΈ kusema kweli nililia machozi nilikuwa najiona single mother wa watoto wawili ambao wana baba tofauti......hey miss mbona unalia ujauzito ni jambo la kheri unatakiwa kulipokea kwa furahaβΊοΈβΊοΈaliniambia Mom Elizabeth hahahaa ni kweli mom lakini ninalia machozi ya furaha etπ₯²π₯² hospital nilisindikizwa na mama Elizabeth huyu ni boss wangu kule ninakofanyia kazi...... baada ya kuruhusiwa hospital jioni mida ya saa 1 Mom Elizabeth aliniuliza.....
""Vipi naweza nikakupeleka nyumbani kwako?!""
""Ni sawa Mom""
""Unakaa wapi na unakaa na nani?!""
""Nakaa Hotel Mom ninaishi na mtoto wangu mdogo....""
""Why kwanini usitafute nyumbaπ³π³""
""Nipo kwenye harakati za kutafuta nyumba Mom ndo najipanga et""
""Mwanao ana umri gani?!""
""Ana miezi 10""
""Whatπ³π³ mwenza wako yuko wapi?! Samahani lakini kwa maswali najaribu kutafuta namna ya kukusaidiaπ€¨π€¨""
""Mwenza wangu tumetenganaπ₯Ήπ₯Ή""
""Ni sawa usilie basi mimi nitakupatia sehemu ya kukaa wewe na mtoto wako twende hotel umchukue mtoto wako na vitu vyako then nitawapeleka nyumbani kwangu mpumzike utakaa na mimi hadi pale utakapopata pesa za kujitegemea..... kwa hii hali yako unahitaji uangalizi wa mtu.....pole sana kwa matatizo yaliyokukumba kwenye mahusiano yako lakini hutakiwi kukata tamaa unatakiwa kuwa strong kwa ajiri ya watoto wako""
Mom Elizabeth alinipeleka hadi kule hotelini nilimkuta mwanangu yuko kule reception na wahudumu wa kule hotelini baada ya kuchelewa kwenda kumpokea nilipigiwa simu na uongozi wa shule nikawaelekeza wampeleke kule hotel pale hotel kuna dada nilikuwa nimeshaanza kutengeneza urafiki naye huyo ndiye aliyempokea mwanangu akabakia naye hadi huo mda niliorudi kutoka hospital ....nilimbeba mwanangu niliwashukuru kwa msaada wao niliwaomba radhi kwa usumbufu mom Elizabeth alikwenda chumbani kwangu akanisaidia kutoa mabag yangu na ya mwanangu alitupeleka nyumbani kwake alitutambulisha katika familia yake pale kwake nilimkuta kijana wake ambaye alijitambulisha kwa jina la Tristan.....Father house ambaye ni Mr philipe pamoja na wasaidizi wa kazi za pale nyumbani nilipokelewa vizuri nice alimchangamkia sana Tristan hahahaaaa alimbeba et Tristan alionekana kumpenda sana nice alimchukua akaanza kumbembeleza mom Elizabeth alinionyesha chumba vitu vyangu vikawa vimewekwa huko niliingia nikapanga nguo zangu na za mwanangu kabatin nilimshukuru sana mom Elizabeth kwa ukarimu wake kwangu...... baada ya kupanga vizuri..... nilijilaza kitandani nikapumzika make kimimba kilikuwa kinanipeleka siyo mchezo...... mlangoni nilihisi kama kuna mtu anagonga niliamka kwenda kuchungulia ni mama Elizabeth alikuwa kaniletea matunda ya kuongeza damu mwilini kwangu ni mazuri kwa wajawazito yatakupa nguvu mwilini kwako samahani kwa usumbufu lakini unahitaji kuyala hayaππ asante sana momπ nilipokea yale matunda nikarudi chumbani kwangu niliyala taratibu hadi nikayamaliza usiku mida kama ya saa 4 tulikutana dinning table kwa ajiri ya kupata msosi wa usiku
Hahahaaa kilichonishangaza ni vile ambavyo nice na Tristan walivyozoeana kwa karibu sana nice alianza kumuita Tristan daddy πΉπΉπΉ nilijikuta nacheka vile Tristan alivyogeuka kuwa mtoto kulingana na vile alivyotaka nice wacheze..... Tristan alimlisha mwanangu chakula huku akiwa anamuimbia nyimbo duhπ₯² nilijikuta kinanijia kisura cha simanzi usoni kwangu mawazo yalienda mbali zaidi nikaanza kumuwaza paschal vile alivyokuwa generous kwa mtoto wake baada ya chakula mimi na mtoto wangu tulikwenda chumbani kulala wanafamilia walibakia kule sitting room niliona niondoke pale ili angalau niwape muda wa kuniteta kidogoπ€£π€£π€£ si mnajua mgeni lazima ajadiliwe kidogo adadavuliwe kama anastahiri kubakia au laa!
Itaendeleaaaaaaaaa.......
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi