*MKAKA KAUZU HUYU JAMANI* *SEHEMU YA TISA* "Hellow Anaya, nimerudi kwaajili yako"
Hapo ndio nikashtuka Kuwa sikuwa nimekata simu hivyo kwa haraka nikakata na kumwambia.
"Ndio nini sasa Wala haifurahishi"
"Kwangu inafurahisha sana tu kwasababu nimesikia ni kiasi gani napendwa, anaya, hivi unaijua raha ya kujua unapendwa na unayempenda?"
"Nani anakupenda?"
Nilimuuliza nikiwa naangalia tu chini maana ni aibu sana kwa upande wangu, imagine Nimejiachia mineno yote hiyo halafu muhusika yupo
Frank akanisogelea Karibu kabisa na kushika mikono yangu kisha akazungumza.
"Hivi ndio unanipenda klasi hiko ?"
"Frank ata Sijui unaongea pumba gani kwa wakati huu, niachie nikafanye kazi"
"Una Uhakika unataka kufanya kazi ?"
Frank aliniuliza.
"Kwani Nimekuja kucheza hapa au? We Sijui ukoje jamani Basi Naomba unipishe please"
Frank ni Kama alipania kunichokoza kwa siku hiyo, kwa mwendo wa haraka akasogelea mlango na kuufunga kisha akaanza kunisogelea.
Jinsi ambavyo frank alikuwa akinisogelea, kuna Namna nilijikuta nikianza kuogopa, nilijikuta tu nikikumbuka siku ya kwanza Mimi kukutana na frank na kuutoa usichana wangu, Walahi wasiwasi ulikuwa wa hali ya juu sana, nikajikuta nikianza kurudi nyuma nyuma na mwisho nikafikia Ukuta, na sikuwa na uwezo wa kwenda. kulia Wala Kushoto
"Frank usinisogelee"
Nilimwambia frank nikiwa na wasiwasi sana, kWa upande wa frank hakuweza ata kunisikiliza aliendelea kunisogelea uku akiwa na tabasamu. pana usoni mwake.
"Frank nitapiga Kelele ujue"
Niliendelea kumsisitiza ilitu asiweze kunisogelea lakini ilikuwa ni kazi bure, Yaani frank alikuwa amejipanga sana na hakuwa akiogopa.
Frank alinisogelea na mwisho alinifikia, na
kwaajili ya kuniziba kidomo domo changu frank akaanza na kiss moja la kiufundi, Sawa Mimi sio mzuri kwenye haya mambo lakini ili kiss ni la kiufundi.
Nikaanza kumsukuma frank kwa style ya sitaki nataka, Yaani namsukuma uku moyoni nasema
ongeza kidogo baba fla nyie Mimi mmmh nastahili maombi, naitaji mniombee.
Basi frank Bwana kwenye haya mambo alikuwa mzoefu aswaaah, alifanya kila alichokijua
mwisho nilijikuta nikimpa sapoti ya kutosha, mwili wangu wote uliishiwa nguvu, Yaani Sijui niwaambie kitu gani lakini frank aliweza kuliona. ilo na hakuweza kupoteza muda chapu akajinyanyua.
Muda huo huo tukasikia sauti ya mlango ukigongwa, haraka frank akanishusha na kwa pamoja tukaanza kujiweka Sawa.
"We frank tangu lini umeanza kujifungia mlango
Ilikuwa ni sauti ya boss, Yaani baba mzazi wa frank.
"Sio Mimi baba ni Anaya huyo"
Alijibu frank kisha akasogelea mlango na kufungua.
"Kwanini mnajifungia miango muda huu?"
Alizuliza boss baada ya kuingia Ndani.
KWa upande wangu kwakweli sikuwa ata na cha kufanganya nilibaki nikimtumbulia macho frank, Walahi nilikuwa nikitilia huruma Yaani Kamal mchawi aliyenasa kwenye kanisa analosali kila siku.
"Baba ni Anaya ndio alifunga mlango kisa tu nilimtania Kuwa natoka na nitarudi kesho"
"Na ulikuwa unataka kwenda wapi na kuna kazi
muhimu nimekukabizi ?"
Baba frank alimuuliza Kijana wake.
Hapo kidogo nikapata Ka nafasi na mimi Nikadakia
"Bora useme wewe boss labda ata kuelewa, me nimemwambia Wala ajanielewa ndio maana nimeamua kumfungia tu umu Ndani.
Boss akaniangaukia kisha akanipa Tano na kuniambia.
"Good job Anaya, Yaani huyu asikufanye kazi zikakwama Sawa? Yaani ata ukipata muda wa kumchapa Viboko wewe chapa tu
Hapo wote kwa pamoja tukacheka kisha boss akafanya kilichomleta na kuondoka zake.
Siku hiyo Mimi na frank tukawa ni watu wa kuangaliana na kuchekeana tu Kama hatuna
akili nzuri Yaani Kama mtu angekuja ofisini kwetu na kutuangalia Mimi na frank lazima angeamini Kuwa Mimi na frank hatuna akili nzuri.
Majila ya kwenda Nyumbani siku hiyo nikapewa lifti na frank, nyieeee huyu kama ako na rangi Saba Jamani Yaani huyu frank ambave namuona siku ya Leo ni frank tofauti sana na
Yule ambaye nimeemzoea siku zote, jamani kaka Anajali huyu, kaka anajua kudekeza na
kubembeleza, frank yuko romantic kuliko Mimi mpaka inafikia hatua sasa mimi ndio najiona Kama mandonga mtu kazi
*SEHEMU YA KUMI*
Siku ziliendelea kwenda uku ukaribu wangu na frank ukia
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi
Maoni