MMMH DADY NIKIKUPA UTANIOA SEHEMU YA 15 ,16 Kingston alisimama baada ya kuisikia ile kauli ya kuogeshwa😂😂😂akageuka akaniangaliaaaaaa...
Then akaniambia hiyo siyo kazi yako ninaweza kuoga mwenyewe...
Mxiiiwww mbona ananikazia😔😔😔...kwa hiyo nimwambie mama kuwa unaweza kujiogesha peke yako siyo😒
What is your problem zarina 🥺🥺 are you out of your mind??...
Alianza kunifokea kizungu ata sivielewi nikaamua kuondoka zangu kuelekea jikoni..
Nilimwandalia chakula utafikili namwandalia rais wa nchi😂😂
Nilikuwa nafanya hivyo at least kijana wa watu aone kitu kwangu maana ni mgumu huyo watu wa arusha sijui wakoje😂kuwashawishi si kazi rahisi..
Nilipika haraka chakula anachokipenda The Boy nikamwandalia mezani..
Alishuka chini baada ya kuoga akakuta chakula tayar kiko mezani🤩
Alionja kisha nikaona ananiangalia😂😂Mama weee au nimeboronga🙈
Wakati natetemeka mara nikasikia ananisifia💃🏼💃🏼chakula ni kitamu sana sijawahi kula menu yenye taste kama hii😀❤️
Hongera unajua kupika....nyieeeeeee nilitamani kama nipae hivi😂😂😂😂yani kama niruke juu mawinguni💃🏼basi pale nikaanza kucheka cheka🤗🙈
Mshikaji akaendelea kula wala hana habari namimi😂😔... the way anavyotafuna uuuwwww lisura lake sasa nilikuwa nachanganyikiwa nikimuona...
Ile sura yake na sura yangu nilikuwa nafananisha the way tutazaa watoto wa cute🤣🤣🤣..
Kingston alimaliza kula akapanda zake chumbani mi nikabaki naondoa vyombo mezani💃🏼💃🏼
Kale kachakula kidogo alikobakiza nikakala kwa kutumia kile kile kijiko chake💃🏼💃🏼💃🏼..
Wakati naviosha vile vyombo alivyltumia the Boy ghafla nilimsikia akiwa anatembea kuja kule niliko..
Atakuwa anahitaji kitu gani sijui 🙄🙄... alifika pale jikoni The Boy akafungua fridge akachukue energy badae akaniuliza vipi uko bize sana,?..
Nope hata siko bize nilikuwa namalizia tu kuvisuuza hivo vyombo..
Ohhh OK....fungua fridge uchukue kinywaji chako then uje chumbani kwangu..
Heeee😀😀😀mbona chumbani😂😂😂nilijiuliza tu kimoyomoyo huku mdomoni nikiwa nimebanwa na smile la hali ya juu🤣🤣🤣
Nilijua jamaa ndo anaenda kunitongoza💃🏼💃🏼💃🏼nilichukua kinywaji haraka nikaelekea chumbani kwangu..
Nilibadili nguo nilizokuwa nazo nikavaa zingine nzuri nzuri😂😂😂yani nilihisi zile nilizokuwa nazo hazivutii🤣🤣🙌
Ni vimarash nikaenda kuiba chumbani kwa mama nikajinyunyizia nyieeee🤣 nilipomaliza sasa ndo nikaenda chumbani kwa Kingston kama alivyoniomba...
Nini kitafuata??..
MMMM DADDY NIKIKUPA UTANIOWA KWELI?!*
*16
*__________*
*SEHEMU YA 16*
Niligonga mlango Kingston akaniruhusu niingie🤗🤗... nilifungua mlango taratibu nikaingia na kinywaji changu mkononi..
Ile harufu ya marashi niliyojipulizia si ikamfikia Kingston 🙂🙂🙂akanitizama huku akiwa ameshika pua🥺
Akaniambia kabla hujakaa nenda kabadili hizo nguo sijaipenda hiyo pafume🥹nilitamani kulia😰😰
Nilitoka kwenda kubadili nguo na sikuwa na nguo ingine nzuri ninayoiaminia kama ile niloivua😰😰
Sa nitavaa nini jamani haya maronya ronya💔💔😔any way nitajifunga kitenge na hii tisheti ya rangi ya pink...
Kweli nilivaa hivo nikarudi chumbani😔😔nilikuwa nimenyong'onyea sina ata raha na tule tunguo nilitovaa tubaya tumepauka..
Kingston aliniomba niketi tuzungumze... yeye aliketi kitandani mie kwenye sofa..
Hapo nilikuwa nang'ata vidole wacha kabisa😀😂 nilishajenga imani kwamba mshikaji leo ananitongoza hata kumwangalia machoni nikawa nashindwa😂
Wakati najihangaisha na mawazo yangu ya ndoto za mchana ghafla Kingston akaniita zarina are you hiaaa.???😂uko hapa?..
Ndiyo kaka🥰🥰🥰...okay vizuri... nimekuita hapa kwa jambo moja..
Najua ni wewe pekee unayejua kuwa mimi siumwi kitu chochote right?...
Ndiyo kaka ni kweli😔😔..okay leo nataka nikwambie kwanini nafanya haya yote ili kuwaaminisha watu wengine kuwa mimi ni mgonjwa...
Uuwwww kumbe siyo kama anataka kunitongoza🥹🥹ilibakia kidogo machozi yanitoke😂😂😂😂niliumiaaaa...
Lakini sikuwa na budi kumsikiliza...
Kingston aliniambia yeye ni mzima wa afya tele haumwi hata kipere mwilini kwake....
Anadai alipotimiza umri wa miaka 28 alikuwa tayari na Degree moja ya hiyo taaluma anayoisomea na hivo alianza kusimamia miradi kadhaa ya kifamilia kwa sababu tyr alikuwa ni kijana mkubwa...
Miradi yao ya kifamilia ilizidi kufana sana na kuingiza mapato mengi sana na jambo hilo liliwafurahisha sana wazazi wa Kingston..
Kingston anadai alipotimiza miaka 29 alianza kupenda😔😔moyo uliniuma nyie🥹🥹🥹...
Anadai huko nyuma wakati yuko chuoni alishakuwa na mahusiano kadhaa lakini hakuwa serious alikuwa anapita tu...
Kwa mara ya kwanza anakuwa serious na mahusiano ni hiko kipindi alipokuwa na miaka 29 anadai alimpenda mdada mmoja hivi mzuri sana msomi classic na ni mfanya kazi wa kampuni moja ambayo iko jirani na kampuni ya kina Kingston..
Kingston anadai baada ya kumuona huyo dada kwa mara ya kwanza alichanganyikiwa sana maana moyo ulimuenda mbio kama kaona kitu ambacho hajawahi kukiona tangu azaliwe...
Alianza kutumia muda mwingi kumfukuzia huyo mlimbwende na huku nyuma bidii ya kazi ikapungua hivyo biashara za kifamilia zikaanza kuyumba..
Wazazi baada ya kufanya upelelezi waligundua kuwa kijana wao ameshaingia kwenye ulimwengu wa mapenzi hivo wakapanga kumuozesha haraka kabla hajaharibikiwa...
Kingston anadai wazazi wake walikuwa na chaguo Lao la binti waliye mpendekeza aolewe na kijana wao na hapo ndipo mambo yalipoanza kuharibika....
Nini kilitokea?.?.
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi

Maoni