WEWE NI WANGU SEHEMU YA 6
SONGA NAYO......
Nikashangaa amepiga magoti chini akafungua chupa ya maji akamaliza akjimiminia mdomoni, mimi kwangu yalikuwa mageni kabisa sijawahi kuona mtu anakunywa maji kwa staili hiyo
Basi alipomaliza kunywa maji akarudi kukaa na kuniambia asante huku akinikabizi chupa ya maji yale ambayo yalibaki kidogo
Nilichofanya ni kumwammbia akae nayo tu, basi akatabasamu tabasamu hafifu ila lilionekana vyema kabisa kwenye uso wake na kumfanya awe mrembo mashaallah 🥰
Eeeh umalaya huu acheni tu ndugu zangu walah hili jiji litaniua mimi kwa hizi pisi aiseee 😋
"Sasa Lizy nenda nyumbani kesho tutaongea vizuri hakikisha unakuja shule pia unakuwa msafi sawa..??"
Nilimwambia akabiki kuwa mnyonge mpaka nikashangaa binti alikuwa na nguo ambazo hazielewiki kabisa dah
"Vipi mbona hivyo..??"
Nilimuuliza
"Sir unajua mimi nakaa na shangazi yangu, na sio kama mimi ni mchafu hapana sir ni vile nguo zangu amepewa mtoto wa shangazi harafu mimi nikapewa hizi.."
Alisema, jamani nilimuonea huruma
"Kwani huyo mtoto wa shangazi yako anasoma kidato cha ngapi..??"
Nilimuuliza
"Anasoma pamoja na mimi ndio yule ambye ulimwambia after ubao.."
Eeeh nilichoka walah 😅 nikamtazama binti mara mbili mbili, kisha nikaangalia huku na huko kama kuna mtu ananiona kisha nikamwambia
"Si umwambie akupe nguo zako au ushtaki kwa mwalimu mkuu..."
"Sir me aiwezi maana kuna wakati niliwahi kufikisha hizi kesi kwa mwalimu mkuu ila dada akaingilia kati na kuanza kumtetea Leah..."
" kwani dada yako ana mahusiano gani na mwalimu mkuu..?"
"Aaah dada ndio huyu aliyekuwa hapa.."
"Nini..??"
Kakakaa kimya bila kunijibu, inamaana kumbe yule ni dada yake na yule anaejifanya slay queen kwa nguo za mtu mwingine ni binamu yake mbona sielewi eti au masikio yangu yameacha kusikia siku hizi
Wakati nikitaka kumuuliza swali jingine akawa ameningia Sir Joseph so nikaacha hata kuendelea kuzungumza nae zaidi ya kumwambia aende nyumbani
Kabinti ka watu kakanyanyuka na kuondoka, jamani kwa mara ya kwanza nilijikuta nikiingiwa na roho ya huruma ya kumsaidia huyu binti...
Basi baada ya Lizy kuondoka ndio na mimi pamoja na sir Joseph tuliongozana mpaka kwenye gari yake, eeh huyu kaka ana miliki gari na siku hiyo akanipa na lift kabisa
Njia nzima tulikuwa tunapiga story za hapa na pale kuna namna nikajikuta namziea huyu Joseph maanaalikuwa amechangamka sana sio poa
Basi ilibidi anipitishe mpaka kwangu kisha yeye aakaondoka zake, nikafungua geti na kuingia ndani, nimeingia ndakuta watu hapo nje wamekaa Kimbea mbea
"Habari zenu..."
Niliwasalimia, wakanijibu siktaka kusubiri chochote nikashika njia mpaka kwenye chumba changu nikafungua mlango na kuingia ndani, nilikuwa nimechoka sana kwa hekaheka za so nikaanzia kwanza kuoga
Mtoto wa kiume baada ya kumaliza kuoga sasa nikaanza kumuwaza Lizy, yani sikuweza kabisa kumtoa kwenye akili yangu yule binti aliitawala yote mpaka medulla oblangat 😂
Basi nikaa sana mule ndani, huku nikipiga mahesabu namna ya kwenda kununua chakula nije nipike, sasa bana napiga zanguajesabu mlango unagongwa
Nikanyanyuka na kutoka nikakuta mdada mwingine nayo ilikuwa pisi ikiwa imebeba sahani ya chakula
"Nikisaidie nini..??"
Nilimuuliza nikiwa nimeweka uso wa serious sana
"Ah aaah aah aaa oh yan nimeagizwa nikuletee chakula.."
"Kwamba nilikutuma au..??"
"Hapana lakini mi..."
"Ondoka..."
"Laki..."
"Nimesema ondoka, nilimwambia kwa ukali basi mdada akaondoka nikafunga mlango kwa nguvu kana kwamba mlango ndio umenikosea kisha nikarudi chumbani kwangu.....
*********
Siku nyingine ikashika nafasi kama kawaida yangu ni kupigilia pamba kali, siku hii nilipendeza zaidi ya jana 😂 maana nilipotoka nje nilipishana na tule mdada ambaye alinipa chakula baada ya kupishana nae alisababisha ajigonge kwenye mlango wa kuingilia
Kitendo cha yule dada kujigonga ndio nikajua kwamba nimependeza sana 🥰👌 basi nikatoka nje ile kufungua geti nakuta gari imepakiwa hapo nje
Katika kuitazama vizuri ndio nikajua ni gari ya Joseph, na kweli ilikuwa yake baada ya yeye kushusha kioo cha gari, bila kuchelewa nilipanda na safari ya kulelekea shuleni ilianza
Tulifika shuleni saa moja na madakika, moja kwa moja nikaingia ofsini, siku hii nilikuwa na majukumu mengi so nilianza kuandaa mapema ili nimalize mapema
Wakati yote yanaendelea huko nje sikuzingatia kabisa kwa kuwa na ubize nikasahau kabisa habari za Lizy......
ITAENDELEA ......
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi
Maoni