REALLY LOVE* Chapter 19
muda ulisonga mbele hatimae jioni ya saa kumi ilifika seven akiwa ofisini alinza kujiandaa kitoka kisha akapitia ofisi ya john, aliingia na kumkuta yuko bize na compyuta
""nakuona upo bize jamaa alisema seven
"yes boss nawasilisha apa alisema john
"ok sawa mimi naenda zangu nyumbani maagizo yote nishamuachia secretary hakikisheni wale wapuuzi hawaingii hapa si cathe wala devi wala mwanasheria alisema seven
sawa boss lakini vipi mbona sahizi mapema sana sio mida yako hii alisema john
ndugu yangu acha tu alisema seven nakumfanya johna acheke kidogo
sasa unacheka nini alisema seven
amna nimecheka tu nahisi itakuwa shem huko. anakukazia hataki masihara kabisa alisema john huku akicheka nae seven akacheka
shem gani bhana hebu acha zako alisema seven
""mh niache zangu tena haya bhana msalimie sana ila asiwe anakubania hivo duh sahizi saa kumi hii alisema john
"John we humjui fahima vizuri apa nimechoka ngoja niwahi sitaki kelele zake sasahivi hapa. ataanza kupiga simu alisema seven na kifanya john acheke sana
"haya bhana kesho basi alisema john basi seven akaondoka akimuacha john anaendelea na kazi,
upande wa mama fatuma huku alikuwa na majanga matupu tu alikuwa amejifungia ndani kwake baada ya kufuatwa na wanawake wa kausha damu maana alishindwa kulipa
"nakwambiaje jifanye tu kutukimbia unatujua
vizuri sisi hatukimbiliki nyauba wewe yani leo
hatuondoki yunakaa hapa hapa halafu tuone kama utajinyea humo na kujikojolea humo alisema kiongozi huyo aliyejulikana kama mama
zena
hawa vipi yani asubuhi mtoto wake kaja
kichukua nguo zangu jioni wanakuja wao kha yani sitoi ela mimi karna kukaa mtakaa humohumo tu sitoi pesa hata kidogo nakwanza. sina ela apa kha alijisemea mama fatuma,
huki nje bado vichambo viliendelea na muda. huohuo akatokea fatuma ambaye ndo alikuwa anarudi kwenye mizunguko yake
ehe sogea hapa wewe mtoto kahaba mkubwa wewe sindio umefumaniwa asubuhi na mwanangu halafu ukajifanya kukimbia unadhani tunakimbilika yani wewe na mama yako wote
pumbavu sasa ngojea alisema mama zena kisha akauchukua mkoba wa fatuma ambao
ndani yake kulikuwa na simu smartphone na pesa kadhaa, fatuma alianza kuwaomba
wamrudishie
jamani nawaomba mnipe kuna simu yangu
humo sasa mimi nimefanya nini jamani mnanionea tu nipeni alisema fatuma huku analia, mama fatuma haraka akasimama.
dirishani
"weeee msimpe mshenzi mkubwa huyo mimi apa asubuhi zena kaja kuchukua nguo zangu na jiko kwa kosa lake la kutembea na waume wal watu sasa safi sana chukueni na hata mkitaka
mumvue nguo abaki uchi sawa tu chukua shoga angu mama zena ko hapo hatudalani kabisa. mpaka zipite wiki mbili alisema mama. fatuma
apo shoga angu tutaelewana haina shida alafu wewe mtoto siku nyingine ukome kulala na mabwana wa watu alisema mama zena kisha wakaondoka na wenzie wakamuacha fatuma
analia tu chini, bila kujua lakufanya
upande mwingine catherin alikuwa chumbani mudawote analia tu hakupata amani hata kidogo alikumbuka maneno machafu aliyokuwa
anaambiwa na devi hakuamini devi yule.
aliyekuwa anampa maneno matamu leo hii
anamulta kahaba hakuamini alitamani siku zirudi nyuma angalau arudishe mapenzi kwa seven alijutia sana
mara mlango wa chumbani kwake ukafunguliwa na mama yake akaingia ndani humo "wewe vipi devi ushaongea nae alisema. mama cathe
"ndio mama amesema atailea tu alisema. cathe kwa kudanganya alijuwa akisema ukweli
tu atafukuzwa kwao
sawa na vipi kuhusu ndoa mnatakiwa mfunge ndoa kabla mimba haijakua alisema mama cathe
"hilo swala nitaongea nae kesho mama nataka nipumzike alisema cathe
""sawa na unywe dawa za maumivu umelia sana. leo hutakiwi kuwa na mawazo tena kwakuwa devi kakibari alisema mama cathe
sawa mama alijibu, basi mama cathe akatoka chumbani humo bila kujua kafichwa ukweli
seven nae ndo aliwasili nyumbani ikiwa saa 11 na nusu, aliingia ndani na kuwakuta familia yake
na baba fahima wakiwa bize kwelikweli kupiga story, basi alifika na kuwasalimia wote
"karibu sana mzee sikupata taarifa kumbe ulikuja alisema seven
ndiyo nilikuja mda tu wala usijari kabisa alisema baba fahima
sawa mzee vipi fahima simuoni hapa alisema seven
"wifi ameenda chumbani kuoga alisema sarafina
"halafu we sara wewe hukuagi huo mdomo wako wewe alisema seven na kufanya wote wachek
"sasa seven unataka akue mara ngapi hapo jiandae tu mwakani kupata shemeji alisema. selina
heee dada selina sio vizuri hivoo alisema sarafina
ila unavotoa siri za wenzio ndo vizuri alisema selina aisee ilikuwa ni kituko familia
hiyo ilizoea sana kutaniana sana tu basi seven akawaaga anaenda mara moja kuongea па
fahima, alifika mpaka mlangoni na kugonga hodi akafunguliwa na fahima akiwa amenuna. kwelikweli seven akajuwa tayari kishanuka
samahani nilikuwa na kikao ndomana nimechelewa alisema seven
sawa endelea na kazi zako alisema fahima huku akijifunga vizuri mtandio wake
""hivi fahima mbona sikuhizi umebadilika hivyo muda wote visilani tu alisema seven
unamuuliza nani sasa alisema fahima
"kwani hapa naongea na nani alisema seven
hebu nipishe huko alisema fahima kisha akampushi seven na kufungua mlango kutoka. na seven nae akamfuata huku anaongea
fahima ujue sipendi nakwambia rudi tuongee fahima fahima usinivuruge alisema seven na wakati huo walikuwa washafika tayari seblen
""kuna nini tena jamani alisema mama seven baada ya kuona hali hiyo.
"hamna kitu mama alijibu fahima
"mama hebu mwambie fahima mimi nilivyo na majukumu kazini anakasirika kiasi hiki kisa tu
nimechelewa sasa nilikuwa na kikao ningefanyeje sasa alisema seven aiseee
mama seven bado kidogo tu acheke akajikaza kwelikweli maana alijua tayari hawal wanapendana sana na fahima anawivu sana
kwa seven
hebu fahima mwanangu rudini kwanza
mkaingee ndani sawa haya ni mambo madogo sana hebu kaongeeni ndani kwanza alisema mama fahima, mzee fahad alikuwa
anamuangalia mwanae akitabasamu tu alipata sana amani ya moyo
Itaendelea
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi

Maoni