VYOTE NDANI GONGA94
MR GENERAL : KUMBE ULINIPENDA EEE SEHEMU YA 8
Usimulizi huu ni wa watu wazima. Chukua muda wako, tulia, kisha usome kwa utulivu kama machapisho yetu yanayoendelea moja kwa moja.
Basi nikaanza kuwaza nifanye nini, kwanza nikajiambia kuwa nikaangalie ameacha shilling ngapi, nikakuta ameacha kama laki tatu hivi, nikaziangalia kisha nikatabasamu na kujiuliza
“Kwani huyu anafanya haya yote kwa sababu ipi, kwa sababu anaonekana hana hisia na mimi, ila amekuwa kama malaika na nuru ya maisha yangu, kwanini anafanya hivi, au ndio malaika ambao amewatuma Mungu kuja kuonesha nuru kwenye maisha yangu?
Nikawa najiuliza maswali ambayo binafsi hata sikuwa na majibu, ila nikajiambia kuwa “ atakuwa ananisaidia tu kama mdogo wake, natakiwa sasa nitafute na mimi mwanaume maana upwiru utakuja kuniua…
Basi nikapika nikala, kisha nikatafuta zangu kiwalo, huwa ana kawaida ya kuninunulia nguo hizi za kisasa sana kila wakati, hivyo nikawa nina viwalo vya kutosha ndani, nikapiga zangu kimoja, kikachonga vizuri kashape changu cha mchongo, kisha ikapiga wigi na makeup yangu ya uchwara, na baada ya hapo nikatoka…
Nimefika kwenye mgahawa mmoja hivi, ulikuwa ni mgahawa maarufu sana kwenye sehemu ambayo nilikuwa naishi, nikaagiza chakula na kuanza kula, na mara baada ya kumaliza kula, maana niliagiza visnaks tu, kwakuwa nilishakula nyumban nilikuwa nimeshiba, kisha nikaanza kunywa juice masaa, ili walau atokee mwanaume mmoja aje kunipa kampan, maana nilishachoka upweke, nilikuwa na mimi nataman kuwa namtu, ambae anaweza akanitumia sms asubuh, na jion, na akanipigia simu hata tukaongea lisaa lizima, nilikuwa nataman sana kuwa na mwanaume wa namna hio na mimi….
Basi nimekaa kama nusu saa, mara akaja mwanaume mmoja, alikuwa ni mweupe alafu anatabasamu flani hivi tamu sana, na baada ya hapo akakaa karibu yangu tukaanza kupiga story, nikiwa hata sijaanza kumjibu mara simu yangu ikaanza kuita, sikuwa najua hata kama Yule mwanaume ambae naishi nae alikuwa na namba yangu ya simu, nikapokea, kitu cha kwanza nilichoulizwa ni “Upo wapi?..
Nilikuwa nina uhakika kuwa yupo kazin, na namjua anaweza akaondoka nyumban na hata mwezi mzima usimuone, kwa sauti ya kujiamin nikajibu “Nipo nyumban..
“Upo nyumba ipi hio Happiness, mbona mimi nipo nyumban, kama unataka kuwa salama, naomba urudi sasa hivi..
Nilimuangalia Yule kijana ambaen alikuja kukaa na mimi, kisha nikamuomba namba za simu na kumuambia kuwa “Kaka yangu mkali sana, hapa nilipotoka nyumban nimetoroka, naomba nirudi ila tiutawasiliana, basi akanipa pale nikambip kisha huyo mpaka nyumban…
Nafika nakuta mwamba amejaa sumu balaa, akanikata jicho kisha kwa sauti ya ukali akasema
“Umetoka wapi happiness..
“Nilienda kunyoosha miguu, unataka nikae hapa ndani kama mfungwa wako si ndio? Nikajifanya na mimi ni mwamba namjibu kwa jeuri na wakati hata akisema anifukuze sina pa kwenda…
Akaniangalia kwa hasira kisha akaingia zake chumban kwake, nikawa nashangaa huyu vipi, ila kwa akili zangu mbovu nikajua kuwa ana mastress yake ya kazi na mimi hayanihusu hata kidogo…
Basi nimekaa zangu chumban nikaanza kuona namba ngeni inapiga, kwa akili zangu za haraka haraka nikajua ni Yule kijana ambae tulikutana nae muda mfupi uliopita, nikapokea kwa shauku, nashangaa nakutana na sauti ya shangazi, nikataman kukata simu, kwa kuwa nilishampigaga block muda mrefu sana, maana nilikuwa naona kama ananichanganyaga vile, ni kama alijua, akaniwah na kusema “Bosco amekuja na anahali mbaya sana, ameomba sana uje kumuona, kisha akakata simu…
ITAENDELEA …
MTAKATIFU GEMMA UTUOMBEE SHIRIKA LA MASISTA WA MT GEMMA WA DODOMA
Tunao Wapenda ndio wanao tuua baba
Sikiliza Wimbo Kamili
Umesoma kwa utulivu · dakika chache tu Asante Endelea kusoma chagua hapo chini
Umependezwa ?? Asante Soma Zaidi mr-general-kumbe-ulinipenda-eee-sehemu-ya