Simulizi za Maisha,Mafunzo,Mapenzi ,Chombezo Habari za Michezo na Burudani vyote kwa Kiswahili ndani ya – Gonga94 Semajambo
Gonga94 · Stories
06 Dec 2025
143 views
VYOTE NDANI GONGA94
mtoto wa mchepuko nimeona nikusimulie na maswaibu yangu
Usimulizi huu ni wa watu wazima. Chukua muda wako, tulia, kisha usome kwa utulivu kama machapisho yetu yanayoendelea moja kwa moja.
Mambo mchaga,nimesoma kisa cha huyo dada mwenye mtoto wa mchepuko nimeona nikusimulie na maswaibu yangu maana ni miezi tisa sasa ila naona km nipo ndotoni bado.Mimi nimeolewa ndoa nzuri kabisa na takatifu ya kanisani 😂mimi na mume wangu tumejaaliwa kupata watoto watano.Namshukuru Mungu kwa hilo
Mume wangu tulianza chiniiii chiniiii na tumenyanyuka wote mpk leo hii tunaona neema za Mungu kwenye maisha yetu.
Nilipokuwa na ujauzito wa huyu mtoto wa tano mume wangu alikuwa ansafiri sana yaani sana madai akisemaa anafatilia biashara tulizofungua mikoani na mimi sikuona shida sababu namuamini ni mume wangu
Sasa kuna siku ukweni kukatokea msiba na mahala naishi na ukweni kwangu sio mbali kabisa kwahyo msiba huo ulipotokea nilikuwa nimejifungua tayari na mtoto alikuwa na miezi mitatu kwahiyo nikajibeba walau ile siku ya kuaga nikaenda msibani hapo
Sijui niseme ni machale au ni nini kuna dada alikuwa pale msibani pia na alikuwa karibu sana na mama mkwe wangu na mawifi me nikawa najiuliza huyu ni nani mbona simjui,basi tukazika salama nikarejea nyumbani na hiyo siku mume hakurudi kabisa
Kesho yake akarudi me nilikuwa jikoni kwahiyo alipitiliza chumbani akaenda kuoga,basi me nikaingia chumbani nikasikia yupo bafuni na simu ikawa kitandani,nimesogea tu msg ika pop juu ukirejea usisahau diapers na wipes,mmmmh nilishtuka sana yaani sana ila nikajikaza na sikuuliza
Kesho yake akaniaga asbh sasa alipokuwa kwenye gari akaniita kasahau chaja yake,nimempeleka chaja nafika kwenye gari kwenye siti ya nyuma nikaona kinguo cha mtoto na kile kinguo sio cha mtoto wangu
Manca ujue nikaanza kupata uwoga flani ambao sijawahi kupata nikawa natetemeka,nikajiambia sasa nifanye uchunguzi wangu
Nikaanza kumfatilia sasa looooh huwezi amini mume wangu kazaa nje na watoto wetu wamepishana week tu
Niliumia sana na ikabidi nimuulize akakiri kweli ndiyo kazaa nae na anatupenda wote hataki kutuacha na hawezi kutuacha ndo maana kamtambulisha hadi kwao
Hapa nilipo nilikuwaga nimeanza ujenzi ila nilikuwa naenda taratibu,sasahv nimeongeza nguvu sana nataka mpk mwakani mwezi wa tano niwe nimmemaliza kila kitu nimuachie nyumba yake aishi kwa uhuru na mwanamke wake.Kuhusu watoto ntajua nikishatoka ila sina amani tena,simpendi tena,namchukia sana sana sana.Nachomshukuru Mungu maisha yangu ya kipato nilishayatengeneza siku nyingi kwahiyo siogopi kuanza kujitegemea.Huyu mwanaume amejua kuniumiza sana.
Nimemaliza
Maoni
You're not logged in
X
Login
X
signup
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa
+ Endelea kugundua zaidi
SHAMIRA sehemu ya 34&35
Mwandishi; lissa wa huru media Basi nikajiiinua taratibu tukaingia bafuni. Mwanaume akanikumbatia uku tunaoga. Aseee uy...
mtoto wa mchepuko nimeona nikusimulie na maswaibu yangu
Mambo mchaga,nimesoma kisa cha huyo dada mwenye mtoto wa mchepuko nimeona nikusimulie na maswaibu yangu maana ni miezi tisa sasa ila naona km nipo ndotoni bado.Mimi nimeolewa ndoa nzuri kabisa na takatifu ya kanisani 😂mimi na mume wangu tumejaaliwa kupata watoto watano.Namshukuru Mungu kwa hilo
Mume wangu tulianza chiniiii chiniiii na tumenyanyuka wote mpk leo hii tunaona neema za Mungu kwenye maisha yetu.
Nilipokuwa na ujauzito wa huyu mtoto wa tano mume wangu alikuwa ansafiri sana yaani sana madai akisemaa anafatilia biashara tulizofungua mikoani na mimi sikuona shida sababu namuamini ni mume wangu
Sasa kuna siku ukweni kukatokea msiba na mahala naishi na...
👉 Soma zaidi hapa: https://www.gonga94.com/semajambo/mtoto-wa-mchepuko-nimeona-nikusimulie-na-maswaibu-yangu
Maoni