*NIMEKOMA MIMI 🙌* *SEHEMU YA SITA* Bishop hakuja peke yake, Alikuja na wanaume wengine watano
vibaya mno
Bishop macho yake yakatua kwangu nikasema Nafwaa leo. Hakua ananijua ivyo Akauliza kwa sauti nzito "huyu jamaa ni nani?"
Mmoja akajibu haraka "Boss Bishop hatumjui. Alikuja tu ndo tukawa tuna mhoji"
Bishop akaongea akiwa amekasirika sana. "Mtu anaingia bila nyinyi kujua? How?? Na kwanini mliacha geti wazir
Wakajibu kwa sauti ya hofu, tulisahau boss, na unajua hakuna mlinzi wa getini, tulisahau kweli. Tusamehee boss, tusamehee"
Lakini Bishop si mtu wa utani na hapendi makosa. "mnajua jinsi gani polisi wanani winda alafu mnakua wazembe kiasi hiki?? Spy wako kila kona wanasubiri saa ngapi niteleze wanidake Alivua koti akaliweka pembeni akakunja mikono ya shati lake taratibu bila haraka.
Wale jamaa walijua kinachofuata ni kipi. Haraka walilala chini wakaanza kumuomba msamaha
Ila sifa nyingine ya Bishop ni kutokusamehe. Alifungua buti ya gari lake akatoa mjeledi flani mweusi alafu mrefu. Nilipo uona nilijua kabisa hapa lazima wachezee washawasha.
Lakini yote ni makosa yangu, mimi ndiye niliyeingia bila ruhusa "Samahani lakini ni Ni kosa langu Sijui hata nguvu ilitoka wapi nikajikuta nasema ivo
Bishop akanigeukia kwa macho makali mpaka nikabanwa na mkojo. Aliniangalia weee bila kusema kitu kisha akanipuuza na kuanza kugawa dozi.
Aliwapiga wale jamaa mgongoni kwa mijeledi kama anaua nyoka. Na walivyo kuwa wamejilaza kifudi fudi aliwa faidi kweli kweli mpaka akatoka Jasho
Wallah nillumia kuona wanavyo lia kwa kupigwa. Nilijikuta namchukia sana Bishop na kumuona
mwenye roho mbaya na mkatili mno. Utawapigaje binadamu wenzako namna lyo
Basi Baada ya kuwapiga, akaniangalia akasema kwa sauti wewe??? kali ulikuwa unasema nini
"aaaah saah samahani mimi ni mgeni hapa..... nimekuja kufanya kazi kama mlinzi wa geti
"mlinzi wa geti? akamgeukia msaidizi wake ambapo niliweza kumtambua kama ndie Tobias.
Tobias akajibu kwa haraka "Boss nilitafuta mlinzi mpya ila nilisahau kukuambia, leo ndo alipaswa kuripoti kazini
Bishop hakumjibu Tobias badala yake alirudisha macho kwangu akaniangalia kuanzia juu mpaka chini akasema "ukitaka kufanya kazi hapa,
lazima ujue sheria. Sheria namba moja, nikimwadhibu mtu hakuna anayeingilia. Umelielewa hilo??"
Nikasema kwa uoga "ndio Boss nikiwa natetemeka maana macho yake yalikuwa ya kutisha
Baada ya kuniambia hivyo aliingia ndani huku Wale jamaa wakimfuata nyuma. Aliyebaki ni Tobias na mimi
"Shege, si ndiyo?" Tobias akauliza. "Ndiol"
"Si nilikuambia usubirie nje?? Unajua izi hekaheka zote ni wewe umesababisha?? Alikua
mkali kidogo
"Nisamee tu! Naomba radhi"
Tobias alishusha pumzi "anyways uwe makini, Bishop hataki mchezo hata kidogol Also unadhani utaweza kweli kazi?? Tumeshafukuza
walinzi 20 kwa huu mwakal Watano walikatwa
ulimi, sita wali katwa masikio na walio bakia ni chongo
"nitaweza nitaweza
"Okay! All the best! Nitamtuma mtu akuelekeze kazi na sheria za humu ndani nikiwa free tutasaini mkataba
"Asante" nikamwambia.
"sasa nenda kwenye chumba cha mlinzi, weka mizigo yako. Pia vaa uniform za kazi, utazikuta kitandani
"Ok" Nikachukua begi langu nikaenda kwenye
chumba cha mlinzi karibu kabisa na geti. Ndani Nilikuta uniform zimenyoshwa vizuri. Nilivaa haraka haraka zikanikaa vizuri.
Cha kufurahisha, nilifanikiwa kabisa kuigiza kama mwanaume. Kuanzia Bishop, Tobias na wengine wote hawakufanikiwa kujua kama mimi ni demus
Lakini ukweli ni kwamba nilikuwa ria hofu sana. Siku yangu ya kwanza tu nimeona mambo
mazito. Siku nikijulikana kuwa ni mwanamke si ataniua kwa kudhani mimi ni mpelelezi kumbe nimekuja kutafuta hela za kumuhonga Labubu wangu. Na ivi jamaa ana roho ngumu, nachoka mimi binti wa Banza
Nilipokuwa mule ndani mmoja wa wale jamaa akaingia ghafla bila kubisha hodi. Ni yule yule aliyenitisha mwanzo.
"Eeh, unaitwa nani? akauliza kwa sauti ya juu. "Shege Shege Banza"
Akanitazama "sikiliza Shegel Umeshajua Boss wetu alivyo, Kwa hiyo lazima ufanye kazi zako kwa wakati Kazi zako ni kufagia, kufungua na kufunga geti, kusafisha nyumba na kupika"
Nikashangaa "lakini kupika na kusafisha nyumba si kazi yangu
hapa mambo ni tofauti. Hizo ni kazi alizoagiza Boss. Akisema usafishe, unasafisha. Akisema upike, unapika"
Nikamuuliza "na wewe kazi yako ni ipi?"
"kila mtu hapa ana kazi yake maalum. Sisi hatufanyi kazi za wengine na hupaswi kuuliza kuhusu kazi zetul Hii ni sheria nyingine ya hil
nyumba. Chochote unacho kiona na kukisikia
kibaki hapa hapa! Ukitoa siri kwa polisi au mtu yeyote basi upo kwenye hatari ya kupoteza jicho, sikio, ulimi au uhail Tuachane na hayo, unapaswa kupika chakula, Tuna njaa na muda
unakimbia, jioni kuna kazi ya kwenda kufanya" "Mhhhh sawa
Kwakua sikua najua ni wapi jiko lipo nikamfuata
nyuma nyuma hadi jikoni. Nyumba kwa ndani
kuwa safi sana lakini haina vitu vingi. Kulikuwa na sofa mbili tu na TV kubwa, Dinning room ilikua nyeupee zaidi kulikuwa na jamvi kubwa tu chini. Hilo lilinishangaza, lakini sikuuliza maswali mengi.
Tulipoingia jikoni, Niliona nyama nyingi kwenye sufuria, unga pamoja na viungo vyote vya kupikia
Dennis akaniambia "tupo watu kumi na mbili ila leo upikie chakula cha watu kumi. Boss nа Tobias hawatakula. Harakisha, maana jioni tuna safari
Nikajibu sawa" alafu akaondoka zake Sasa nikaangalia jiko nikiwa nawaza, nitapikaje
ugali na mchuzi nyama kwa watu kumi? Lakini nikakumbuka enzi zangu za kufanya kazi kwa mama ntilie Kwa hiyo hakuwa ngumu sana
japo nilihitaji msaada
Haraka haraka Nilianza kuandaa, nikakata
nyama, nikaichemsha huku nikiendelea kuandaa
viungo vingine. Nilijiambia lazima nimalize kwa wakati, la sivyo nitapokea mijeledi ya Bishop mwenyewe.
Unajua nini kilitokea baada ya hapo??? Subiri
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi
Maoni