UTAMU WA MABOSS 10 Linda Alikuwa amechoka sana na hataki kuleta vurugu yoyote MAANA mpaka muda huo Alex
"Ngoja.....Kwanini anataka niwe mpenzi wake na bado anilipe, alijiuliza Linda ila akaona haitosh hivyo akaona amuulize Alex ambae aliamin atampa majibu ya kueleweka.
"Kwanini unataka niwe mpenzi wako" Linda alimuuliza Alex
"Nilidhani hautaniuliza kwa sababu nakulipa ," alisema Alex
"Sawa, leo ni siku ya kumbukumbu ya wazazi wangu na wanataka nimlete mpenzi wangu na kwa vile sina...." Akasema Alex ila Linda akamkatisha
"Seriously?? Vipi kuhusu yule bibi niliyemuona akimbusu , Kwan hawez kufaa kuwa mwanamke wako? " Akaulzia Linda
"Lazima uingie kwenye mambo ya watu wengine" Alisema Alex kwa hasira.
"Nilijua nimesema kile ambacho sitakiwi kusema.
"Samahani bwana" Linda alisema
Hii ni kama mara ya tatu Linda akiomba msamaha MAANA bado anahofu kwa kitu alichomfanyia Alex na Alex mpaka muda huo hakuonesha reaction yoyote ile.
Bado walifika kwenye maduka ya fashion ambayo ni maarufu kwa jina la FM na hapo ndipo kunakouzwa vitu vya bei ghali ZAIDI.
"Anafanya hivi kweli???? Linda alijiuliza
"Je, UPO tayar tufanye manunizi" Alisema Alex na kumshika mikono Linda.
"Mbona anajali sana akajiuliza Linda
Waliingia ndani na Alex akasema kuwa Linda achukue nguo yoyote apendayo.
"kila kitu hapa ni ghali sana, Linda akawaza
Alichukua nguo tofauti za chapa tofauti.
"Nimemaliza" Linda alisema mara moja
.
"Unadhan umetosheka" Alex aliuliza na Linda akaitikia kwa kichwa.
Basi Alex alilipa na wakaondoka na kwenda sehemu nyingine ambazo wangeweza kununua vitu nyingine kama vile begi, viatu na vipodozi. Walienda hata kutengeneza nywele za Linda na muda wote Alex alikuwa akisubiri kama mtu mpole.
Linda alimaliza kutengeneza nywele zake na wakaingia kwenye gari baada ya kulipa.
"Linda" aliita Alex na Linda akamuangalia
"Adhabu yako ni kwamba utakaa nami, nyumbani kwangu na chumbani kwangu kwa wiki au ufukuzwe kazi" alisema Alex na Linda hakuamini alichosikia.
" Nini???" Aliuliza Linda kwa mshtuko .
"Ndio hivyo," alisema
"Mimi? Nyumba yako? Chumba chakokwenye kitanda kimoja? "Alisema Linda kwa uoga akawa anataman kuona Alex akiwa anatania.
"Nyumba yako? kwenye kitanda kimoja?" Aliuliza tena Linda kwa mshtuko
"Ndio, acha kunihoji tayari. Kwan Una mpenzi?" Alex aliuliza
"Hapana sijui" Linda Alisema na Alex akahema kwa furaha.
"Nashukuru Mungu sitakuwa nikipokea ngumi kutoka kwa mvulana yeyote kwa sababu niko na mpenzi wake, akasema Alex
"Sam naomba utupeleke kwenye jumba langu la kifahari" Alex alisema na Sam akaitikia kwa kichwa.
Walifika kwenye jumba la Alex la kifahari na walinzi wakawafungulia gari.
kijakazi alikuja kumsaidia Linda mabegi ya ununuzi na wakaingia ndani ya jumba hilo la kifahari. Wajakazi zaidi waliwasalimia huku Linda akiendelea kushangaa kila kitu.
Walifika chumbani kwa Alex na linda akajilaza kitandani kwa uchovu.
"Wow, chumba chako ni kikubwa sana," akasema Linda
.
"Asante"
"Hata kitanda ni kikubwa pia" alisema Linda akitabasamu
"Ndio ni hivyo na kumbuka ni kwa watu wawili TU kwa MAANA watu wawili pekee ndio wanatakiwa kulala hapo"
"Samahani nini??. Siwezi kulala kitanda kimoja na kijana mwenye kiburi" kama wewe Alinong'ona Linda.
"Kumbuka ninakulipa kwa hili na sio kama nitakugusa, zaidi ya hayo wazazi wangu wana akili sana na wanaweza kutushuku" Alisema Alex na Linda akapumua tu.
"Nenda ujisafishe" akasema Alex
na kusimama kabla ya kutoka nje ya chumba.
Sihitaji kueleza mahali bafu lilipo naamin utaliona.
Alex alishuka na kuwaona wazazi wake wakitazama sinema
"Halo mama, habari baba," alisema Alex na kumnyanyua mama yake Kisha kukaa kando yake.
"Oh mpenzi wangu" Mama yake Alex alisema huku baba akitabasamu tu
"Kwahiyo yule binti yuko wapi" aliniuliza mama yake Alex na Alex akatoa macho MAANA aliamin kuwa hakuna ambae aliewaona.
"Sawa...yuko chumbani kwangu anaoga" alisema Alex na mama yake akatabasamu
"Ngoja niende nikamchunguze" Alisema mama yake Alex na kusimama.
"Mama tafadhali usimsumbue kwa maswali" akasema Alex kwa sauti ya uoga maana anakijua kichwa Cha Linda asije akaharibu mambo.
"Sawa" alisema mama na kuelekea chumbani kwa Alex .
"Hatimaye umemleta msichana wako nyumbani. I'm proud of you son" Alisema baba yake Alex na yeye akaachia tabasamu
"alisema anajivunia mimi kwa sababu nilileta msichana nyumbani
Mambo gani jamani.
, wananipelekesha sana Hawa wazaz wangu, Alex aliwaza......
****
Linda alimaliza kuoga na na kuingia chumbani akakutana na mwanamke pale amekaa
"Habari za mchana mama, nawez kukusaudia, akasema Linda
Na mama yake Alex akatabasamu
"Mungu wangu, mwanangu kweli ameleta msichana mzuri nyumbani," alisema na Linda akamtazama akiwa na hofu
.
"Mwanao? Alex ni mwanao" Linda alimuuliza na akaitikia kwa kichwa kama mtoto.
"Oh Mungu wangu, samahani mama" Linda alisema haraka na mama yake Alex akacheka na kumfanya Linda atabasamu.
"Nakupenda, wewe ni mrembo, unajali, mtamu na mcheshi. Alisema na Linda akatabasamu.
"Jina lako nani" aliuliza
"Linda, naitwa Linda, nina umri wa miaka 22 na nimpenzi wa mwanao Linda alisema .
"Natumai sijasema kile ambacho sitakiwi kusema, akawaza linda
"Wow, una akili sana pia. Vipi kuhusu wazazi wako?" Aliuliza mama
"Wamekufa mama"
"Oh..samahani sana kwa kufiwa na wazaz" Alisema na kumkumbatia Linda.
"Nini! Mke wa top 10 ya matajiri hapo na mwenye mvuto ananikumbatia Ahh!! Bahat gani hii Linda akawaza.
"Tutaongea baadae baby" Alisema na kumshika Linda shavuni kisha akatoka nje.
Linda alichukua gauni jepesi na kulivaa, akafunga nywele zake na kibanio. Alichukua simu yake na kuanza kuperuzi kwenye mtandao na ndipo Alex alipoingia.
"Nini jamani, ningekuwa bado navaa je, Kwann unaingia bila kubisha hodi" Linda alisema.
"Nilijua utakuwa umemaliza sasa hivi," alisema Alex n Linda akamkazia macho.
Alex Alikuwa karibu kuongea jambo mara mtu akabisha hodi
"Ingia" Alisema Alex na mwanamke aliyevaa sare akaingia
"Mheshimiwa, chakula cha mchana kipo tayari," alisema na kumpa ishara ya kuondoka na akaondoka zake.
"Lunch is ready, let go" Alisema na wote wakashuka.
Meza ilikuwa tayari imewekwa na wazazi wa Alex walikuwa tayari wameketi
"Habari za mchana bwana" Linda alimsalimia baba yake Alex, na yeye akatabasamu na kusema
"Habari za mchana, habari yako"
"Sijambo bwana"
"Wow mwanangu kweli umeleta msichana mzuri" Alisema na Linda akatabasamu
"Asante baba" Linda alisema na baba akaitikia kwa kichwa kisha wakaanza kula
macho ya mimi na Alex yaliendelea kugongana na Bi Shaws ambae ni mama yake Alex akatabasamu ..
"Baada ya chakula cha mchana nyie mnapaswa kufurahiya, sherehe bado ni usiku," Bi Shaws alisema na Linda akaitikia kwa kichwa
NAKUJA
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi



