CHUO CHA MIHEMKO SEHEMU YA 1
SEHEMU YA 1
Mh! Bwana bwana wee, maisha ya chuo matamu sana kama yakifaana kinoma. Embu wacha nisiwe na maneno mengi wacha nikusimulie niliyapata huko chuo, hiki chuo chenye wanafunzi waliojaa mavitu na mavituziiii ya mihemko..
"Nilifika nikiwa bikira wa akili na mwili… nikarudi nikiwa na ujauzito wa hisia na kitumbo"
Waliosema “Chuo ni sehemu ya kutafuta elimu” walikuwa sahihi lakini hawakutuambia kwamba elimu nyingine huwa haifundishwi darasani.
Nilikuwa nimevaa sketi ya penseli, viatu vya chelsea, na nguo ya juu isiyoonyesha chochote isipokuwa tabia.
Hivi sijajitambulisha eee, sawa, naitwa Neema mtoto wa kwanza kwenye familia yetu ya watoto wanne, nina miaka 22 mpaka sasa ninapo anza kusimulia kisa hiki.
Nianze kwa kusema mimi nilikua mkorofi na mkali sana, maswala ya mkaka kuja na kunitongoza nilikua sipendi kabisa yani mkaka akijaribu alikuwa anakutana na majibu ambayo yatamfanya kesho kukaa kimya.
Tabia hiyo ilipelekea kuitunza bikra yangu bila kumpatia mvulana yoyote yule, tangu naanza kitado cha kwanza mpaka namaliza kidato cha nne, nikaingia kidato cha tano hatimaye sita hakuna mvulana yoyote aliye wahi kunibahatisha hata kwa kuniita beby, yaani hata beby ya bahati mbaya hakuna.
Hapo nikaamini kwamba nitaenda chuo, na nitatoka bila mjinga yoyote kucheza na mwili wangu hata kwa bahati mbaya.
Haya bwana sasa leo si ndio nimefika chuo, nia yangu kubwa ilikuwa kutafuta cheti bora na sio bora cheti, kwani mahusiano hayakuwa yananichukulia muda kabisaaa.
Moja mbili chuo hicho hapo mbele ya macho yangu, hatua kadhaa nikazipigia kusogea chuo, huku nikiwa nimepakata begi langu dogo maana mengine tayari yalikuwa nimeyapeleka hosteli.
Sasa bwana wakati natembea kwa haraka ili niwahi kwa viongozi wa chuo kusaini kuwa nimeingia chuo sasa, na nipewe utaratibu muhimu wa chuoni hapo, macho yangu yalikuwa kwenye simu nikichati Whatsapp kwenye magroup, huku hatua ndefu ndefu nikizipiga.
Sikumbuki ilikuwaje ila nacho kumbuka nilijikwaa, simu nikarusha kulee nikaanza kushuka chini kupigiza mwili.
Hapo kwa haraka nikafunika macho yangu nikusubiri maeneo ya mwili yatakayo umia.
Cha ajabu sekunde zikasogea bado sijaanguka chini, nikahesabu moja mpaka tano nikashangaa bado nimepanda hewani.
Kwambali nikaanza kuhisi kama vile nimekumbatiwa na mtu, na huyo mtu amenikumbatia kuzuia nisianguke.
Nikafumbua macho yangu ili kumtazama huyo mtu mwenye ujasiri wa kunishika.
"We vipi, nani kakuruhusu kushika mwili wangu" eti nikawa nauliza hivyo huku namuangalia kwa hasira.
Pale pale akaniachia, nikapigiza mwili chini,
"Mama weeeeee kiuno changu kimekatika mimi mwenzenu" nilijikuta nasema hayo baada ya kuhisi kama kiuno kimetoka na kwenda kando ya mwili.
Nikainuka huku nimekaandaa kamdomo kangu, kumsodoa huyo mkaka, yaani anasubutu kuangusha pisi kutoka Kagera, wacha nikuonyeshe, leo namsodoa mpaka akome kuangusha watoto wazuri kama mimi.
Nikainuka, nikajingunguta vumbi kisha nikaokota simu yangu na kumgeukia, nikashangaa mkaka simuoni, nilipotupa macho mbele nikamuona mkaka mwenyewe anawasha pikipiki yake ili aondoke, yote hiyo kuonyesha hana time na mimi.
Ila Pale nikawa nakumbuka kumbatio lake, sura yake iliyokuwa imenikaribia.
"Ila huyu mkaka ni hendsome jamani😜" nikawa NAWAZA mwenyewe.
Hata sijui nimeanza kumpenda!! Maana kamoyo kakawa kanajilaumu eti kwanini nimemjibu shiti, ilitakiwa muda ule nimkumbatie na niondoke naye .
Embu subiri, nyie ambao mnajua masuala ya upendo hivi itakuwa NIMEMPENDA au maana dada yenu kwenye mahusiano ni mngeni asee 🤣 🤣 😜
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi




Maoni