CEO USINIVUE MI MCHUMBA WA MTU* * *16&17*
Sikujua kam nililala pale mpaka asubuhi, tena nimelala kana kwamba pale ni nyumbani kwetu jamni nilikuja kushtuka tena baada ya kupigiwa simu, jamni si ndio naamka najikuta nipo kwenye chumba tofauti na kile nilichokizoeaa mtume wangu mimi nimekufa hivi hivi najiona uwii, ndio nikakumbuka kilichotokeaa Mungu wangu nilikurupuka kana kwamba sjui nimemwagiwa maji ya baridi kitandani kuangalia anaepiga ni dada yooo nilichanganyikiwa nikaitizama sikupokeaa make ndio kuangalia nakuta missed calls kam 45 hivi yaani toka jana ananipigia. Mara anaingiaa Ellias na kikombe cha maji ya moto na kuniambia nikunywee, nilikunywa ila nikawa nasubiri da mariam apige, na kweli haukupita muda dada mariam alipiga, nikataka kuacha kupokea "pokea, usipopokeaa atazidi kuwa na wasi wasi juu yako kwa sababu hujawahi kutokulala nyumbani wee pokea na mtoe hofu mwambie kwamba upo sehemu salama sawa mke wangu alisema Ellias kwa hekima sana nilikubali kwa kichwa na kupokea simu
"Wewe upo wapi mdogo wangu hupokei simu shga angu me hadi nimeanza kupatwa na wasi wasi shgaaa." Dada angu alivyopokea tu alisema hivyo, nikaanza kujuta kumbe nimemtesa dada angu makusudi jamni "usijali dada nipo sehemu salama kabisa wala hata usihofiee dada angu kipenzi, ni jana tu kulikuwa na kikao cha bodi kiliisha usiku sana, nikaamua tu...." nilisem hata kabla sijamalizia akadakia dadaa kwahyo umelala officine na kwanini, hicho kikao. kilivyoisha hukunitafuta weee mjinga" dada alisema alikuwa anaongea kwa panic ndio Ellias alipochukua simu
"Usiwe na wasi wasi hata hivi nakupa maelekezo kuna sehemu uje sawa?, ndio yupo nakutumia dereva akufate hapo uje huku, ukifika kila kitu kitaongeleka, usiwe na hofu" Ellias aliongea machache yenye kueleweka sana. dada alikubali na haikupita hat masaa mengi alikuwa kafika pale, akaaingia ndani kwasababu ile nyumba haikuwa hata na mfanyakzi wa kumuelekezaa, alifika sebleni akapiga simu akaelekezwa sehemu ambayo tupo akaja
"Enhee wewee kimekukuta nini? Tena shga angu mbona sielewi najionea mauza uza tu hapa unaumwa ama vipi? Mbona sielewi?" Alisema dad Mariam sikuwa na jibu la kumpatia moja moja nilikuwa hata kumtizama siwezi ila Ellias hakutuacha wenyew alikuwepo, dada alikaa kimya akabaki ananichunguza kwa macho tuu na alikuwa haongei, dada ni kama kuna kitu allinotice, yeye ni mtu mzima akamgeukiaa Ellias
"Mmnefanya ujinga gani?, na umemfanyia nini Salma wee mgalatiaa?" Alisema akimtizam kwa jicho kali kweli Ellias hakuwa na jinsi ila kumueleza ukweli wa kila jambo, na akasema samahani kwa unyenyekevuu kwahyoo wewe huoni kam ni dini tofauti na hauwezi kumuoa huyuu, kwa akili zako mdgo angu yupo tayari kubadili dini wewee mjinga?" Dada alimuuliza Ellias kwa hasira, ila Ellias alikuwa mpole sana na mnyenyekevu si alikuwa anataka mzigoo, "kwahyoo wewee, umetumia vipesa pesa vyako kumpata mdgo ang sio?, najua huna malemgo naeee ya kumuoa kwasababu haiwezekani," dada akanigeukia na mimi" Hivi na wewe wakati unafikiria kufanya huu ujinga hukuwaza about wazazi wako watalichukuliaje hili?, mbona unakuwa mpuuzi wewe bintii" dada aliongeaaa na alikuwa mtata sana Ellias alijaribu kumuelewesha mpaka akajaa kwenye mfumooo alikuwa mgumu mwisho akalanika na kwenye dini alikubali kubadili yeye mwenyew, asijali, dada hapo alipoa ila alisema haamini mpaka
athibitishe hili.
Ellias alikubali kwamba atathibitisha, ila alitaka kwanza kwenda kushirikisha wazazi wake kuhusu ndoaa, na alituelezeaa kwamba kwao ni amezaliwa mwenyew hana dada wala mdogo na wazazi wake wapo Marekani, jamani nilikuwa nimelala na mwanaume hata sijui familia yake Ipo wapi mimi jamani sa angekuwa jini jeee, alisema atasafirii ili kwenda kuongea na wazazi wake, tulikubali na alisema atarudi baada ya wiki tuu maana wazazi wake ni wazungu wazungu kuhusu yeye kubadili dini hawatosumbuaa, tulikubali
Alituachia maagzio kwamab akirudi akute wazazi wangu, washakuja huku na alituachia pesa nyingi za matumizi plus na dada anavyopenda hela akaona shemela ndio huyuuu jamani, pia aliacha maagizo kwamba mdgo wangu akifika atapelekwa shule ya kusomea udereva па atamtafutiaa kazi kwenye makampuni ya magari, tulielewa na CEO aliondokaa....
Itaendelea....
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi

Maoni