CEO USINIVUE MI MCHUMBA WA MTU* * Chapter 8
Asubuhi ilifika sasa ila leo nilichelewa sana, japo huwa nachelewa ila leo ilijulikana dhahiri kwamba siendi kazini, naaamka hivi ilikiwa saa 4 inaelekea saa tano namuona dada bado yupo pale nyumbani mh leo huendi kazini na sio Jumapili? Hyo ilikuwa salamu ya kwnza kutoka kwa dada angu nilikaa kimya wewe mimi sinakuliza au unajishauaaa wewe mtoto, wewe kunijibu huwezi ntakuwasha mmbao wewe nikodolee mimacho tu, enheee kwanini hujaenda kazini wewe mshenzi"? Yaanj dada angu licha kwamba ana mdomo ila ni anatukana mpaka yaani afu akikaa mbele za watu
"Naumwa dada najiskia vibaya, nimeomba ruhusa kazini" nilikuwa namwambia dada Mariam naumwa nimeomba ruhusa kazini nyooo mbona toka jana hujasema au unataka ufie humu? Haya ushaenda huko hospitali, maaan nina kichambo chako wee mwanamkee msiri kam nini?" Nilishangaa ana maongezi gani na mimi mpaka aniite mie msiri "enhe maongezi gani dada yangu?" Nilimuuliza kwa unyenyekevu
"Enhe kati yako wewe na huyo Ellias kuna nini?"nilishtuka maan huyo Ellias anamtaja dada ninae mjuaa ni CEO wa kampuni ninayofanyia kazi, nikawa nawaza asiwe kamwambia dada kwamba etty mimi na yeye tuna mahusiano wakati hamna chochote? si nina kuuliza wewe komwe hunisikii au?" aliuliza dada Mariam nilibaki namshangaa tu 'kwani kuna nini sister?" niliuliza mh kuna kitu kanambia Zakia kwamba wewe uliletwa na gari juzi na hilo gari ni la sijui nani yako seo sijui sio mimi sielewel ila anaitwa James nilishusha pumzi nikasema moyoni Zakia nae cha umbeaa yulee" mh dada alinipa tu lift ile siku umesahau nilikuambia dala dala zilikuwa shida sna shga angu?" Ikanibidi nianze kumpamba ili ajae kwenye mfumo mambo mengine yaendeleee maan cha mdomo yule hatomaliza kuongeaa haya hukoo utajua mwenyew mpendane mwisho mpeane mimba, yule hawezi kukuoa yule hata angekuwa anakupenda vipi wewe uliona wapi Ellias kama Salma?, me naenda zangu miee baadae,ugua pole, nikasema haya poa, kumbe siumwi wala nini drama tu zimenijaa sina lolote kichwa kilikuwa kinaniuma nikaamuaa zangu kulala
Nimekuja kuamka hivi saa 12 jioni kwa jinsi ninavyoupenda usingizi kulikoo kulaa uwiii mimi Mungu ananiona nashika simu nakuta missed call 34 hapo Hussein kapiga mara sita na text juu hizo 28 zote alikuwa kapiga CEO na text juu pia nikampotezeaa huyo CEO nikaamua kumpigia Hussein napokea tu kwahyo simu zangu huzioni au dharau?, kwani wewe mdada toka umeanza hyo kazi unatak kututawala sio?, mbona unarusha wee?" aliongea Hussein kwa panic kwani shida nini jamani mpaka unanifokeaa hivyoo jamani yaani hujaniuliza nina tatizo gani basi tu unaanza kufoka jaman hivi ni kweli?"
Me hizo shda zako zingekuwa unaona zinanuhusu ungenipigia mapema haya pole, ule mpango wa kila siku vipi? Mbona unatisha mamy unaanza kupepea afu ile ishu ya jana niliipokeaa sawa?" Aliongea yule mwanaume" sasa kam naumwa, nawezaje kwenda kwa Wakala etty? Mbonaa hunihurumii wewe Jamani?" Nilikuwa nalalamika nikijaribu kumpima kama ana huruma na mimi kwani salma umekuaje wewe, mdada una shindwa kujitahid hapo ukainuka acha zako basi mbona hivyoo?" Nikamjibu mimi siwezi kuinuka kama unaweza njoo ufate mwenyew kwahy Hussein wewe 15k kwa siku moja una maliza mbona na wewe ni mkaka Tu unaweza kutafuta? Lakini mhh...mbona unakuwa hauna huruma? Leo niliongeaa kwa kujiamani mpaka nahis alikuwa anashangaa maana nilikuwa simuoni kwa macho yangu poa si umeamua kunipangiaa masharti fresh tutaonana alisema Hussein na kukata simu, niliumia sana yaani namwambia naumaa ananijibu shirt nilikaasirika na kuumia hii ilikuwa moja ya uthibitisho kwamba mimi ndie naempenda na yeye hanipendi nililia saan maan nilikuwa nimechanganyikiwa mno nikikumbuka kwamba mimi yeye akiumwa ninavyohangaika sana juu yake lakini yeye hajajali kuhusu mie wala nini
Niliamua kuangalia missed call za CEO, sikumpigiaa maan najua wazi ningemjibu vibaya nikasoma text zake ilikuwa ni muamala takribani kam ml 4, nilishtuka maan sikutegemea na sms juu ulikuwa inasema kwamba ile ni pesa yangu ya matumizi madgo madogo kwa hiki kupindi mimi nipo nyumbani, jamn nilishangaa sana yaani sijawahi kuhongwa mimi hat mia mbili leo kiutani tu natumiwa 4 ml ilinishangaza sana, nikaamua nimpigie hakupokeaa na mimi nikaachana nae COZ hakuwa moyoni nakurudisha pesa sio kwel me mwenyew akuu mwenzangu shida ninazonukia bintii akuu sikufundishwa kukataa mapene...
Ila niliamua kwenda Zakia, yeye ni mtu pekee niliekuwa namwambia hadi vitu ambavyo sikuwahi kumwambia dada angu, nilimuhadithia kila kitu ila kuhusu pesa sikumwambia kabisa maana nilikuwa najiona kama vile ni bahati tu na kwa imani yangu hat zakia hajawahi kukutana na mwanaume tu mara ya kwanza akampa ml 4, hivyoo sikumwambia ila yaliyotokea kwenye gari nilimwambia yotee, sikumficha kitu kabisa
Hee sasa wewe hapo unafeli wapi? Maana huyo Hussein wako hana lolote ila hata usimuache kwakuwa unampenda na huyo CEO wako mkubaliee maana unakuwa unamchuna unamuacha kwani shingapi? Kumpa kidude tu yaani miezi miwil umetoboaa hee we vipi shtuka" nilimshangaaa sana Zakia nilitegemea sijui anishauri nini nikasahau kam rafiki yangu mwenyew chengal balaa katika watu waliopagawa wa kwanza ni huyu dada afu fridge lake haligandishi kabisa asiropoke hee mwenzako bwana wangu kanifungulia duka...." nikamuuliza nani huyoo mara akaniambia nipotezeee, nilimlazimisha hakusema nikaamua kumchana sijawahi kumuona kanificha nikajuaa labda Kuna sababu maan huyu anaweza date hata na mtu mwenye miaka 70 imradi awee na pesa inatosha......
Tuliongea mengi hatimae nilirudi nyumbani kwa dada, ambapo naweza sema ni kwetu ila nilirudi na wazo. La kufungua biasharaa maana hii plan niliitoa kwa Zakia aliporopoka kuhusu kufunguliwa duka, nikasema hapa nina ile 4ml + vipesa vyangu vya mshahara vya hii miezi mitatu mbona nina mtaji mkubwa nikawa namsubiri dada angu, ili nimshaurishee aseme ni biashara
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi
Maoni