CEO USINIVUE MI MCHUMBA WA MTU* * Chapter 13
"Wee nae nilikuwa nakwambia kila siku yule sio mwanaume, unaanza kusema ooh amenitolea barua, mimi nilijua tu hili litakuja litokee siku tuu yaani huyoo mkaaka ni mpuuzi sana kha! Mh na huyo shga ako ni mpumbavu, yaani muda wote. alikuwa anakulamba kisogoo na kukuinulia kisigino kwakweli mhhh ila nyiee, wewe ushawahi kuniona dada yako nina ushoga ? na mtu sinaga mazoea ya kijingaa mimi hao watu sio wazurii, kabisa
sasa dada itakuaje cheki maisha yangu yote yameharibika ona sasa dada nilikuwa naishi gizani muda mrefu siwaamini tena wana...." kabla sijamalizia sentensi akadakia dada angu hapana usiseme hivyo mdogo angu, wanaume wapo tena wanaojali na utampata huyoo mwanaume unaehitaji Mungu atajibu maombi yako kipenzi changu, nakuaminia sana tena natamani uolewe hata kabla sijaolewaa mdogo angu natamani hili litokeee sana mdogo wangu si unajua dada ako anavyokupenda eeh?" Nilijikuta natabasamu maneno ya dada yalinipa matumaini kidogo japo nilikuwa bado sipo saw
haya pumzika mdogo angu, usilie kichwa kitakuuuma sana yaani siku ya kwanza dada ako kuanza kazi wewe umepata matatizo ila ntakwambia kazi ilivyoenda ukitoka kazini kesho mdogo wangu, haya pumzika mdgo wangu sawa?" Nilijitahid kulala nisiwaze ila mawazo talinisonga sana kichwani kwangu nilijitahid kupata usingizi haukuja mpaka ikanibidi niinuke niende kuoga, ndio usingizi ukaja hapo huu usiku ulikuwa mzito sana kwangu Wallah
Hatimae asubuhi ilifika na niliwahi kuamka maana usingizi uliwahi kuishaa na niliwahi hata kufika kazini hii ilikuwa ni kam mgeni tena maana nimefika officine kila mtu ananitizama mimi uatadhani hawanijui vile wanavyonishgaaaa hadi nikawa naona aibu maan macho ya warning wote yapo mbele yangu nikaingia officine ghafla alikuaja Suzy akanambia
"Madam wewe hii sio office yako, office yako ni ile kule, kwa sasa wewe ni assistance chairman wa hii kampuni" nilishangaa kwa utendaji upi wa kazi mpaka niwe assistant chairman yaaani kuumanisha mimi ni CEO msaaidizi wewe nani kasem mimi ni huyo assistant chairman wa hapa?, utakuwa unaumwa Suzy mimi mbona sina taarifa za kupandishw cheo jamani?, mbona kila leo kuna suprise kwenye maisha yangu ?" Nilisema kwa namna ilivyoonekana kam nilikuwa nalalamika Fulani hadi Suzzy akawa ananishangaa yaani watu hii nafasi wanaitaka mimi naipata naanza kulalamika, kumbe mimi nina mambo yangu kichwani naona kila kitu kwenye maisha yangu kinakuja haraka haraka sana hata bila mimi kutarajiaaa nilikuwa nashangaa kila kitu kwenye maisha yangu nakiona kinaenda tofauti na mimi ninavyopanga yaani wiki moja tu imebadilisha kitu maishani mwangu hayo yalikuwa ni mawazo yangu.
Nilienda officine kwangu nilipoelekezwa nikawa. nimetulia tu mara mlango ukafunguliwa akaingia CEO na mfuko mkononi mwake akafika akakaa kwenye kitu kilichokuwa mbele yangu akanitizama kwa muda bila kunisemesha chochote mimi pia sikumjibuu maan hat mawazo yangu hayakuwa hapo maana hadi machozi yalikuwa yananitiririka tu usoni mwangu, nahisi hicho ndio kilimfanya anitizame kwa muda mrefu akainua mkono akanifuta machozi akaniinua uso kwa kutumia kidole chake hapo ndipo niliposhtuka
"Sitaki kumuona mwanamke wangu akiwa anatoaa machozi kwa ajili ya mwanaume mwingine, tena mpuuzi mmoja asiejua thamani ya mwanamke mzuri, na mwenye akili za maisha, ila naahidi nitatimiza hiloo" nilikuwa namshangaa tu anavyoongeaa maan kusema ukweli nilikuwa sielewi chochotee, akanikabidhi ule mfuko alokuja nao pale wewe utakuwa huvai hzii sare tena, kwa cheo chako sare ni hizi, kabadilishe kuna sehemu tunaenda" nilitamani kukataa, ila nilikuwa nina maswali nae mengi sana kwanini kaenda kwa wazazi wangu bila mimi kujua yaani hajanambia afu kafika kadanganya nilimtizama tu nikaenda kubadilisha nguoo maana mule mule officine kwangu kulikuwa hadi na choo yani ilikuwa kama chumba cha kuishi mtu, tena sio mtu kama mimi kabisa ni mtu wa hadhi zake, nilibadilisha na kutoka nilikuwa nimependezaa maan ilikuwa ni suti ya rangi ya kijivu nilipendezaa sana jamani, alinisifia ila sikusikiaa
Nilipita nae mbele ya wafanyakazi, na. Wote walikuw wananishangaa maan ilikuwa kuwa. karibu na huyo CEO ilikuwa ngumu sna tukaenda mpaka parking tukaondoka na gari lake...
Inaendelea.....
Chapter 14
Tuliendaa sehemu moja hivi magomeni, wanajiita mgalula ni kampuni kubwa wanayouza magari, nilishangaa tukashuka mwanzoni nikajua labda Ellias alitaka kubadilisha gari maan kwake ni kitu rahisi sana nilishangaa nilipoambiwa "madam chagua gari unalotaka?" alisema yule muuzaji wa pale nilishtuka nikamtizama Ellias aliniangalia akasema tu angalia inayokufaa hapa yoyote chukua
Nilibaki namshangaa tu maan niliona ajabu kwa kipi hasa mpaka nipewe gari na muda huo mimi sina lolote, hizo pesa Za kulipia gari nazitoa wapi? nilikuwa nawaz sana kupindukia ila Ellias alielewa hofu yanguu akanishika mkono akanambia kwa hadhi yako ya sasa hutakiwi kupanda daladala wewe hapo" nilizidi kumshangaa nikauliza " kwahyo hii ni kwamba kwasababu nimepandishwa cheo au kuna mengine? au ndio ntakuwa nakatwa kwenye mshahara wangu mimi au, mbona sielewi kwanza mimi maisha ya daladala nayapenda" nilileta sababu alinitizama akatabasamu "usijali sifanyi kwasababu, etty wewe umepandishwa cheo hapana, lla sitaki mwanamke wangu awe anatembeaa kwa miguu, na kuhusu kukatwa haiwezekani, mshahara wako upo pale, pale, ila bado unasababu utanambia hujui kuendesha gari ila nitakusaidia nishakutafutia dereva sawa, ila ntakuwa nakufundisha jinsi ya kutumia gari kama hutopenda kutumia dereva aliongea maneno yake kwa mpangilioo ulio makini kwenye maneno yake
"Haya chagua unalotaka sasa mrembo wangu" nilikuwa namshangaaa sana maan kaanza kujimilikisha hata kabla sijamkubali huyu vipi? aliamua kunichagulia yeye mwenyewe alichagulia gari aina la crown nyekundu lilikuwa nzuri sana na nilipenda nilitamani kumrukia ila nikasema nitaonekana mrahisi sana kwake. nikavunga tu akapiga simu hata dk 10 hazikupita akaja mkaka akaweka plate number, na akanipa lesseni, nilitambulishwa kwamba yule ndie atakae kuwa dereva wangu wa kila siku atakuwa ananipeleka popote ninapotaka alipewa address ya kupeleka lile gari, aliondoka nalo yule mwanaume
Tuliondoka kuelekea sehemu ya kula maana ilikuwa mchana, na tulienda sehemu yenye hadhi bhana mgahawa flani hivi upo jirani na palm village, kwanza mimi nilijiona ndio mshamba, ukiangalia ni waaarabu na wahindi ndio waliojaa jamani mpaka unaona haya mimi tena cheusi jaman mhhh aibu naonaa mimi , alikuja muhudumu akaleta menu ya chakula saaa mimi sielewi naona zangu vichina tu sielewi ila nikawa naona hay kusema pale mbele za watu kama sielewi Ellias alielewa hofu yangu ikabidi yeye ndio anichagulie chakula hakuna namna kwenye hili, nilikubali kililetwa chakula tukala, nikajua ndio tunaondoka sasa kumbe ndio kwanza tunaanza tukapanda gari tukaenda sehemu nyingine muda huoo sijamuuliza swali lolote. kwanini anafanya vile kwanini alienda nyumbani bila kuniambia yaani nilikuwa namshangaa tu maan kanifanyia mengi makubwa kwa muda mfupi sana
Tulifika kwenye nyumba moja kubwa nzuri sana, ilikuwa maeneo ya kinyerezi nilibaki napashangaaa maaana ni pazuri alifungua geti mwenyew na kuja kupanda gari ili kuingiza getini, mimi mwanzo nilijua ni nyumbani kwake, ila baadae nilijua sio penyewe kwasababu mazingira yalionekana mageni sana machoni mwangu tuliingia ndani tukaakaa sebleni nilitamani kumuuliza hapa ni wapi, ila nikaona nitulize komwe langu, niache ukiherehere miee,
Unapaonaje?" Aliuliza Ellias pazuri nilijibu kifupi " basi sawa hii ni nyumba yako, naomba upokee" akatoa funguoo na makaratasi akanipa, nilizidi kumshangaa" umeshanifanyia vingi inatosha na kwanini unifanyie hivi sasa huoni kam itakuwa ngumu kwangu kukulipa?" Niliongeaa kwa sauti ya utaratibu hamna mimi sitaki, chochote kutoka kwako ila nataka uuruhusu moyo wako tu unipende, mimi nataka utoe kule familia yako Ilipo na ije lishi hapa ndio maana nimenunua hii nyumba kwa ajili yako, fanya vyovyote unavyojua ila uje uishi hapa na wazazi wako" aliongea Ellias "sasa wewe familia yangu umeijuaje na kwanini uende kwetu bila mimi kujua jamni mbona unakuwa unakurupukka wew kwani mimi nilikuomba msaada nilisema mimi hapa nikimwambia Ellias ila nilikuwa simtizami usoni nilliinama chini naelewa ila ni upendo wangu kwako ndio umenisukuma nakupenda, na ninakuhitaji kwenye maisha yangu siku zote niwe na wewe nakupenda sana, pia nataka umuoneshe yule Baladhuli kwamba una nyota na huna mikosi" nilishangaa kuumbe Ellias anajua yote yaliyotea jana " lakini......" kabla sijamalizia hata sentensi nikaona mtu kanikatisha na juice
Itaendelea....
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi
Maoni