CHUO CHA MIHEMKO SEHEMU YA 2.
SEHEMU YA 2.
Siku ya pili ya chuo ndiyo ilinikamua akili kuliko hata ile siku nilianguka mikononi mwa yule mkaka wa pikipiki.
Unaweza usiamini Usiku mzima nilijigeuza kitandani kama maandazi ya Morogoro yakikaangwa kwenye mafuta ya baridi.
Sura ya yule jamaa ilinichezea akili kama beats za Konshens , hasa kila nikifumba macho naona dimple zake, kila nikikumbuka kumbatio lake najikuta navuta blanketi kama nasaka joto la mapenzi yake.
Mh, bado NAWAZA nimependa au, nimemtamani au nimefanyaje mimi, kumlisha na ule ushamba wangu kwenye mahusiano noma sana.
"Neema, usilewe mapenzi ya mtu ambaye hata jina lake hulijui," nilijikumbusha mara kadhaa. Lakini moyo ulikuwa umeshikika kama mbegu ya parachichi kwenye ganda, ushaingia, hutoki????????.
Asubuhi ikafika, nikaamshwa na makelele ya wasichana waliokuwa wanapiga picha na madude yao ya iPhone kwa staili ya "first day vibes." Nilipojitazama kwenye kioo nikaona mwanadada mmoja wa nguvu na wa maana kinoma sketi ya jeans, top ya off-shoulder, viatu vya block heels, na mwonekano wa “usinikosee bro, sijakuomba.”
Nikajipulizia manukato ya "Temptation," nikahakikisha kila nywele umelala na kisha nikashika pochi yangu nikaelekea CAFETERIA kupata breakfast kabla ya orientation.
Nikiwa kwenye mstari, mara nikasikia sauti ya kiume nyuma yangu, sauti laini kama imetoka kwenye redio ya classic. Mh! Mbona ninaisifia sauti hiyo asije akawa yule mkaka jamani..
"Excuse me, hivi hii foleni inaenda haraka au tuandike CV tukisubiri?"
Nikacheka kidogo, si kwa sababu ya utani wake, la hasha, bali kwa sababu ya sauti yake ilikuwa ni yake yule!!????, kwa sauti hii nzuri awee lazima niangalie ninani.
Niligeuka taratibu kama mlango wa ofisi ya mkuu wa shule. Alikuwa ni YULE YULE mkaka wa pikipiki aliyenibeba kama malaika wa msaada wa dharura. Lakini sasa alikuwa amevalia suruali ya jinzi, t-shirt nyeupe iliyomkaa mwilini kama muvi ya Netflix na perfumu yake ilikua inachokoza matamanio kama DJ anavyochokoza beats kabla haijalipuka.
"Wewe ndo yule…?"
"Wa pikipiki?" akakata kauli huku akitabasamu. "Ndio mimi Neema."
Nikastaajabu, "Unanijua?"
"Niliona ID yako ilipoanguka wakati wa ajali yetu ya mapenzi," akasema huku akitabasamu kwa maringo.
Nilijikuta nikipoteza mwelekeo. Nikapokea chakula kama robot kisha tukakaa meza moja.
"By the way, naitwa Kelvin," akasema. "Ni mwanafunzi wa mwaka wa pili pale engineering."
Engineering. Hapo hapo moyo ukawa kama ka-taulo kaliko loweshwa, kajisikie vibaya kujificha.
Mazungumzo yakatupeleka mbali tukacheka, tukagawana juice, hadi chips zangu akaomba kipande. Nani angeamini? Mimi Neema ambaye nilikuwa na roho ya chuma, ghafla na smile kwa Kelvin kama nimesukumwa na upepo wa mihemko, au nimelogwa jamani????
Baada ya kifungua kinywa, tukatembea hadi uwanja wa orientation. Kila mtu alikuwa makini kumsikiliza Dean of Students, lakini mimi nilikuwa makini na tabasamu la Kelvin. Kila alipotazama upande wangu, macho yetu yaligongana kama risasi na silaha.
Nakwambia, ni kama kuna sumaku kati yetu bana, roho zilianza kuzungumza kabla hata ya midomo.
Wakati wa mapumziko, Kelvin akanifuatilia mpaka pembeni ya jukwaa.
"Neema, kuna kitu kimoja nataka kukuambia…"
Moyo wangu ukaanza kudunda kama ngoma ya jandoni. Nikajiuliza, “Hivi anataka kuniambia ananipenda? Na kama akichanganya sikwepeshi namkubalia”
Basi bwana Akanitazama kwa makini, akasogea karibu, pumzi yake ikihema karibu na shingo yangu. Halafu akasema:
"Leo kuna bonge la party pale hostel za Engineers… sitaki uikose."
Nikakenua. "Party? Mimi? Mimi sipendangi hivyo vitu."
"Ndio maana nakutaka uje – uone tofauti," akasema.
Sasa ningefanya je jamani, ndio hivyo tayari nilikuwa mtumwa wake kwenye maswala ya upendo, mh! Ila mimi jamani????
Usiku ulipofika, moyo ulikuwa unanishawishi kwenda, lakini akili ikawa inasema “Utaharibu record yako Neema. Umesema huwezi daiwa na mwanaume.” Lakini kiukweli, moyo ulishawahi, yaani kama asilimia mia moja, nafsi ilikuwa na asilimia 10 huku moyo ukiwa na asilimia 90, sasa hapo naimani umeshajua ni upande gani utashinda, kwenda au kubaki.
Basi bwana, Nikakimbia, nikaivaa ile gauni nyeusi ya kuonyesha shape, nikaweka perfume ya “midnight magic,” nikaangalia kiooni na kusema, “Leo sitoki kumlaumu moyo.”
Baada ya hapo nikaondoka huku wadada baadhi ambao walikuwa Hosteli siku hiyo wakinishangaa sana.
Nilipofika kwenye party, Kelvin alikuja kunipokea mwenyewe. Akanipeleka sehem ya juu ya jengo, mahali walipochoma nyama na watu wachache waliokuwa na nidhamu ya kula, si wale wa kuruka na kupiga kelele.
Tukaanza kuongea… juu ya maisha, familia, ndoto zetu… Kelvin alikuwa tofauti. Hakuwa wa kawaida. Hakuwa kama wale wanaume wa mtaa waliokuwa wakitoa like kwa mapaja ya wanawake mitandaoni. Alikuwa na mvuto halisi, na heshima ya mwanaume aliyelelewa kwa mikono ya mama mwenye maadili, sio wale wa mtoto kua unipe pesa????
Usiku ulipochafuka, alinipatia koti lake kunikinga na baridi. Tukakaa kimya kidogo. Kisha akanishika mkono na kusema:
"Neema, sijui kama ni mapema kusema hivi, lakini kuna kitu najisikia… na nahisi naweza kukupenda."
Aweeeeeeeeeeeeeeeee, huyu makaka kayakanyaga aseeee, ananiambia je????
Mh! Ahaaaa!
Nilinyamaza. Sauti yangu ikakosa sauti. Unajua sauti kukosa sauti ndio leo bana????
Ndani ya moyo wangu nikasema, “Hivi huu ni mwanzo wa mihemko, au ndio mwisho wa bikira yangu ya hisia?” niliendelea kujisemea mwenyewe ndani ya moyo
---
GONGA LIKE TWENDE SAWA..
FOLLOW PAGE YANGU, MAANA HUO NDIO UPENDO BURUDANI ZIENDELEE..
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi




Maoni