CHUO CHA MIHEMKO SEHEMU YA 3
SEHEMU YA 3
Tulipoishia...
“Neema, sijui kama ni kusema hivi, lakini kuna kitu najisikia… na nahisi naweza kukupenda.”
Twende nzetu..
Maneno yake yalinikata mifupa kama vile nipo kwenye X-ray ya hisia.
Moyoni nilisikia kitu kinaanguka sio mguu, si nini, ni bikira ya kihisia ilivunjika kimyakimya. Japo sikumwambia, kwani nilijua kitu ndani yangu kilikuwa tayari kimesalimu amri.
Mara Ohoo sitapenda mimi, mara hoo mimi nitamaliza chuo bila kuwa kwenye mahusiano, kipo wapi????, mapenzi shikamoo..
Lakini, bwana eeh! Hii dunia ya chuo ina siri. Na midomo ikiongea mapenzi, macho yapo bize kuchunguza viashiria vya hatari.
Nikamuangalia Kelvin… sura yake ilikuwa kama ya mtu asiye na hila, lakini tabasamu lake lilikuwa na mkorogo wa upole na ujanja.
“Mwanamume wa hivi haonekani mara mbili kwenye maisha ya mwanamke,” moyo wangu ukaongea, hapo hadi nafasi nayo ikakili kwamba nimekwisha penda.
Tulisimama kwa muda pale juu ya jengo la Engineers, mvua ikaanza kunyesha taratibu kama mziki wa ki-romantiki. Watu wakaanza kukimbia, wengine wakaanza kupiga mayowe, lakini sisi tulibaki pale pale. Kama vile mvua ilikuwa sehemu ya ratiba ya usiku ule. Ila mapenzi bana.
Mimi naye kupenda tu, kusimamia ahadi ahaaaa????
Basi bwana Akanisogelea taratibu. Akavua koti lake akanikinga nalo.
“Neema, nataka tukimbie mvua,” akasema.
Nikacheka, "Unajua navaa weave na mvua haipatani nayo? Kabisa, "
Akanikazia macho, "Nataka ukumbuke usiku huu miaka mingi ijayo."
Nikakubali. Hatua za haraka tukakimbia hadi kwenye hostel za Engineers. Tukaingia chumba kimoja cha rafiki yake Kelvin, ambaye kwa bahati au mpango alitoka mapema na kusema, "Mimi naelekea kwa demu wangu." Yaani kwa lugha nyepesi, waliandaa uwanja kabla ya mechi.
Chumba kilikuwa kimepangwa kama 'bachelor pad' mwanga mdogo wa bulb moja, kiti cha mbao kimoja, kitanda cha futon, na harufu ya deodorant za bei ghali. Kelvin aliketi kitandani, nami nikaketi upande wa pili. Tulikuwa wawili, mvua inanyesha nje, roho zetu zina chemka ndani. Mh! Nikitoka salaama leo mh!
“Mimi ni msichana ambaye sijawahi kuwa kwenye mahusiano…” nilianza kusema kwa sauti ya chini.
"Najua," akajibu taratibu.
"Najua unataka kuwa makini… lakini pia najua kuna kitu kinaanza kujengwa hapa kati yetu."
Akasogea, mikono yake ikishika pole pole mkono wangu. Sikupinga. Si kwa sababu nilitaka, la hasha, ni kwa sababu mwili ulishaanza kuutambua uwepo wake. Ule ukaribu, ile harufu yake, ile namna alivyoniangalia ilikuwa ni kichocheo tosha cha kuua uoga wote wa mwanzo.
Kilichofuata ni dakika za ukimya, lakini kilio cha mioyo kilikuwa kikubwa – hatukuzungumza, lakini miili yetu ilielewana. Macho yakakutana. Mdomo ukakaribia. Kisha… BAM! KITU HICHO.
Mlango ukagongwa kwa nguvu.
"Kelvo! We jamaa upo?" Ilikuwa sauti ya kijamaa mwingine, muongeaji sana, mwenye vituko vya hostel.
Haraka tulirudi kwenye akili zetu. Kelvin akatoka na kunong’ona naye nje. Nikabaki ndani nikihisi mchanganyiko wa kitu kilichokaribia kutokea na kingine nilichokizuia kimoyomoyo.
Aliporudi, akaniambia ni bora turudi kila mmoja kwake kabla usiku haujapinduka. Hatukutaka kuharibu ladha ya muda wetu wa kwanza kwa papara. Ilibaki kumbukumbu ya ukaribu wa hatari. Ilibaki hisia ya tendo ambalo halikutendeka lakini lilijengeka vizuri kwenye kiwanja cha akili.
Alinisindikiza mpaka hosteli. Tulitembea taratibu, chini ya mwanga wa taa za barabarani.
"Neema..." akasema kabla hatujafika.
"Naomba unipe nafasi ya kukujua vizuri. Sitaki tukimbilie kwenye mwili, nataka twende kwenye moyo."
Nilihisi kama mtu aliyenyweshwa wine ya maneno matamu. Nikatikisa kichwa na kutabasamu.
Alinibusu kwenye paji la uso. Sio midomo. Sio shingo. Kwenye paji eneo ambalo wanawake huitunza kwa ajili ya wanaume wa heshima.
Niliporudi chumbani, nilianguka kitandani nikasema:
“Huyu mwanaume si wa kawaida. Lakini je, ni wa pekee au wa hatari?”
Siku zilivyoenda, uhusiano wetu ulikua kama mimea yenye mbolea ya mawasiliano. Kelvin aliniandikia ujumbe kila asubuhi, akanitafuta kila baada ya lecture, akanisindikiza kwenye library, akawa sehemu ya ratiba yangu kama vile timetable ya chuo.
Lakini kila kitu kizuri huwa hakikai kimya kwa muda mrefu… Mambo yalianza kubadilika wiki ya tatu, nilipoanza kuona Kelvin anazungukwa na mademu kama asali ya nyuki.
Nilimuuliza, “Kelvo, kwanini kila msichana anakuchekea?”
Akanijibu kwa utani, “Hivi ukikaa na jua halafu ukapata rangi, ni kosa la jua au ngozi yako?”
Majibu ya kipumbavu. Lakini kwa sababu mapenzi yalikua yamenikolea, nikayameza kama vidonge vya malaria vyenye ladha mbaya lakini vinahitajika.
Siku moja jioni, nikiwa nasoma somo la Psychology of Emotions, nilisikia mlango wa hosteli ya akina Kelvin ukigongwa kwa nguvu, kelele, makelele…
"Mwanamke mmoja alikuwa analia, akisema, 'Kelvin si umeahidi utaniacha lini?! Leo ndo unanishika shati na kunifokea?!’"
Nikajifuta macho vizuri.
Moyo wangu ulianza kutetemeka kama simu ya mkononi ya mtu aliyeweka vibration mode.
Kwa hiyo ananisaliti.
SEHEMU YA 4
Inakuja:
Unahitaji niendelee sasa hivi? Moto bado uko juu!..
Nishawishini sasa kwa like
FOLLOW PAGE YANGU KWANI HUO HUO UPENDO...
????????
Layman Donsue Simulizi
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi



