FROM ONE NIGHT TO TRUE LOVE*๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐โจโจโจโจโจโจ SEHEMU YA 4_5 Baada ya mazungumzo ya muda mrefu na Adam, Damian alimwangalia Adam
โChukua kijana huyu mpeleke kwenye chumba cha michezo, ajiburudishe.โ
Adam alitabasamu na kumwangalia mama yake. โUsijali, mama. Nitakagua kama huyu boss ni baba mzuri kweli,โ akasema huku akitoka kwa utundu.
Mara tu mlango ulipofungwa, Damian aligeuza macho yake makali kwa Amina. Ofisi nzima ilijaa ukimya mzito, na pumzi ya Amina ikawa nzito zaidi.
โKwa hiyo, Bi. Amina,โ Damian alianza kwa sauti ya taratibu lakini yenye mamlaka, โumerejea Tanzania baada ya miaka minane. Na sasa unataka kazi katika kampuni yangu?โ
Amina akajikaza, akiinua macho yake. โNdio, Bwana Damian. Niko tayari kufanya kazi kwa bidii. Hii nafasi itanisaidia kulea mwanangu.โ
Damian akasogea mbele, mikono yake ikiwa imejishika kiuno, macho yake yakimchoma.
โUnadhani ni rahisi hivyo? Wewe ni mwanamke yule yule aliyenidharau. Mwanamke uliyeniweka alama ya aibu moyoni kwa dola mia moja.โ
Amina akatikisa kichwa kwa uchungu. โHaikuwa kama unavyofikiriaโฆ haikua dhamira yangu kuwa pale, na nilipata aibu kubwa sana kwa kosa lile. Tafadhali, sihitaji mambo ya zamani kuharibu maisha yangu ya sasa.โ
Damian akainama karibu, sauti yake ikawa nzito kana kwamba ilikuwa siri hatari.
โBasi sikiliza sharti languโฆ Ikiwa unataka kazi hapa, lazima ukubali kuwa Secretary wangu binafsi. Utakuwa karibu nami kila saa, kila dakika.โ
Amina alishtuka, moyo wake ukipiga kwa nguvu.
โLakiniโฆ kuna watu wengi wenye sifa zaidi. Kwa nini mimi?โ
Damian alitabasamu kwa baridi, macho yake yakimwangalia moja kwa moja.
โKwa sababu nataka kukuona ukiteseka. Nataka kila siku uangalie macho yangu na ukumbuke kosa la usiku ule. Hii siyo kazi tuโni adhabu yako.โ
Amina alijua isingekua rahisi, lakini hakuwa na chaguo. Mtoto wake Adam alimhitaji, na kazi hii ilikuwa tumaini lao pekee.
Kwa sauti ya chini, akasema:
โNdioโฆ nakubali, lakini nina ombi mojaโฆโฆโฆnaomba niwe nakuja na kijana wangu mpaka pale nitakapo mtafutia shule nzuri.โ
Damian akatabasamu kwa ushindi.
โHaina shida. Lakini kumbukaโฆ sasa wewe ni mali yangu, Amina. Safari hii hutatoroka tena.โ
Amina aliondoka ofisini akiwa na moyo mzito, hajui kama amejifunga kitanzi cha maisha yake mwenyewe.
*FROM ONE NIGHT TO TRUE LOVE*๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐โจโจโจโจโจโจ
Sehemu ya 05
Siku ya kwanza ya Amina kuanza kazi rasmi kama secretary binafsi wa Damian ilikuwa yenye msukumo wa hisia. Aliamka mapema, akamwandalia Adam kifungua kinywa, kisha wakapanda gari kuelekea Noblefull Group.
Adam, kwa utundu wake wa kawaida, alikuwa na furaha isiyoelezeka.
โMama, najua siku moja boss wako atanipenda sana. Nina hisi hivyo.โ
Amina akatikisa kichwa, akijaribu kuficha wasiwasi wake. โLaiti ungejua anavyonichukia, Adamโฆโ
Katika ofisi ya juu, Damian alikuwa amekaa akipitia documents. Aliposikia mlango ukigongwa, alijiandaa kumkaripia mtuโlakini badala yake, uso mdogo wenye tabasamu ulijitokeza.
โGood morning, Sir!โ Adam aliingia bila hofu, akiwa amebeba mchoro mdogo aliouchorwa usiku wa jana.
โNimekuletea zawadi.โ
Damian akashangaa. โZawadi?โ
Adam akapeleka karatasi mbele ya mezani. Ilikuwa ni mchoro wa jengo refu lenye nembo ya Noblefull Group, na juu yake kulikuwa na familia ndogo: mtoto, mama na baba.
โHii ni wewe, mimi na mama,โ Adam alisema kwa fahari.
Kwa mara ya kwanza, moyo wa Damian ulitetemeka. Hakutaka kuonyesha, akajikaza na kurudi kwenye sura yake ya ukali.
โKwa nini unachora mimi kama baba yako?โ aliuliza, sauti yake ikijaribu kuwa kali kidogo yenye udadisi.
Adam akavuta pumzi na kusema kwa ujasiri:
โKwa sababu najua wewe ndiye baba bora zaidi kwa mama yangu. Hata kama yeye hataki kusema, mimi nahisi.โ
Wakati huo Amina aliingia, akabaki ameduwaa kuona Adam akiongea kwa uhuru mbele ya Damian.
โAdam! Nilikwambia usiingie ofisi ya boss bila ruhusa!โ aliwahi kusema, akimshika mkono.
Lakini Damian akamuinua mkono kidogo kuzuia.
โAcha. Nataka kujua zaidi kuhusu huyu kijana.โ
Macho yao yalipokutana, Damian alitabasamu kwa siriโtabasamu ambalo lilimchanganya Amina.
Kwa nini anaonyesha upande huu wa upole mbele ya Adam? alijiuliza kwa hofu.
Na moyoni mwa Damian, sauti ya ndani ikamwambia:
โMtoto huyuโฆ si wa kawaida. Kuna kitu ndani yake kinanieleza ukweli ambao sijataka kuamini.โ
JE UNAJUA NINI KILIENDELEA??
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi
Maoni