HATARIIII SEHEMU YA "1"❤️❤️❤️❤️❤️❤️ Mwenzenu kwa majina tuseme naitwa skyler ni mzaliwa wa mwisho
basi bhana nilimaliza form four 2011 story yetu ianzie hapa tangia nmevunja ungo nikiwa form one sikuwahi kua na mahusiano kabisa hio ni kwa sababu kwetu walikua wanatuchunga sana sio wa kishua ila tulikua hakuna kutoka mpk ruhusa maalumu
pia changamoto ilofanya nisiwe na mahusiano nilikua nina kimwili kidogo sana nahisi wanaume walikua wanahisi bado mdg 🤣🤣🤣
sasa bhana baada ya kumaliza form four huyu dada angu mkubwa alinichukua niende kwake mjini mkoa tofauti na mkoa tunaoishi basi nilikaa huko mpk matokeo yalipotoka nilifaulu na nilifanikiwa kuchaguliwa shule ya kidato cha tano
Basi nikarudi nyumbani kwa mama kumuaga kwa ajili ya kwenda shule
Nakumbuka ilikua siku ya jumapili nilikua nmetoka mnadani nadhani mnaelewa nikisema mnada sasa mkoa niliokuepo ulikua na baridi sasa
namimi nina matatizo ya kifua basi niliporudi nyumbn mida km ya saa tatu usiku hivi nikabanwa na kifua nilikua nashindwa kupumua na kuongea mama angu akanipeleka hospital kipindi hicho baba angu bado mzima
walikua baba mama na kaka yangu tumefika tukaambiwa kuna mgonjwa wa ajali kaletwa daktari anamuhudumia kwahyo tusubiri basi bhana tumesubiri mwishoe nilizidiwa nikazimiaa sasa nilivozimia baba angu alikua mkali
mpaka akampiga nesi makofi ikabidi daktari aje kumbe alivomaliza kumshona mgonjwa alienda kulala🤣🤣🤣 basi alivokuja alinihudumia baba angu alimwambia asiondoke mpk niamke
kwahyo yule daktari bhanaa akakaa apo pembeni yangu mpk nilivoamka Uzuri nililazwa private ward hatukua na hali nzurii kiivo ila familia yetu inajali Sana maswala ya afya basi ile kuamka nikamuona mkaka kalala kwenye kiti kaegemea kitanda🤣🤣
nikamuamsha samahani dokta nilijua ni dokta sababu alivaa makoti yale ya kidaktari basi akaamka akasema thanks God umeamka we mtt kaaah baba ako alitaka kuniharibia kibarua changu
basi akasema unaitwa nani nikasema skyler akauliza una miaka mingapi nikamwambia 17 akasema unajisikiaje nikamwambia vzr ila mwili unauma akasema sababu ya kubanwa kifua kwa muda mrefu
Basi akaniangalia akanichoma sindano alikua ana biblia mkononi akanambia tuombe kheeeee mimi namshangaa tu alikua ni mkaka mzuri sio mrefu ni mfupi mweupe ana midomo mizuriiiiiiiiii🥰🥰🥰🥰🥰🥰🥰🥰🥰 alf msafiiiii alf anaongea kipole sana sanaaaaaa
basi akaomba anamaliza akaondoka ila nikajikuta namuwaza natamani sana sanaaa aje aniongeleshe na mimi kumbuka sikuwahi kua kwenye mahusiano apo ht siku moja nilishawahi kuto ng*zwa na rafiki ake kaka angu weeeee nilimsemea kwa baba fasta sana🤣🤣🤣🤣
na nilishawahi kuandikiwa barua na jirani yetu nikampelekea mama angu🤣🤣🤣 basi tangia apo nilikua nikuto ng*zwa nasemelea mpk baba akawa anasema nina akili za kitoto mpk namaliza form four nilikua nikito ng*zwa nasemelea🤣🤣
basi nilikaa hospital mpk kesho yake tena asubuhi nikaruhusiwa ila hakua yule dokta tumpe jina la Elias basi bhana nmerudi siku zikasonga hatimae siku za shule zikakaribia nikajiandaa huyo baba akanipeleka shule
Maisha ya shule yalikua magumu sababu sikuwahi kusoma boarding lkn nilizoea mpk ikafika likizo ya kwanza likizo fupi nikaenda kwa dada angu mkubwa sababu kwake ilikua ni mkoa mmoja na shule nilopangiwa.
Nilimmiss sana mama angu sababu mimi nmezoea kuishi nae lkn ndo hvo sikwenda likizo ilipoisha nikarudi shule nikasoma😣😣 mpk ikafika likizo kubwa ndo nikaenda kwa mama
Sasa nilipofika tu nyumbn nilikuta kaka angu anaumwa kipindi hicho kamaliza shule anasubiri Ajira sasa kesho yake mama akanambia mpeleke kaka ako hospital apo kijijini kwetu hospital ni hio moja ndo kubwa
nyingine ni Dispensary tu basi nilivofika tu nikakutana na yule yule dokta Elias😌❤️ akasema skyler vipi na leo umekuja na baba ako nikamwambia hapana kaka angu anaumwa akasema yuko wapi nikamwambia mapokezi
basi akanambia ngoja niwafanyie mpango muepukane na foleni kamlete nikaenda nikampeleka mpk chumba cha daktari me nikatoka nje akamchukua maelezo tukaenda maabara akapima tukarudisha majibu
basi bhana baada ya hapo wakati tunaenda kuchukua dawa kuna dawa tukaikosa wakasema twende tukamwambie dokta atuandikie tukanunue nikamuacha kaka nikaenda mwenyewe nmefika dokta😌❤️
akasema nilijua tu utarudi sababu nilishindwa kukupata ukiwa peke ako😌❤️❤️ nikaona niandike dawa ambayo haipo😌😌 ili urudi nikacheka🤣🤣🤣 ukweli nilikua napenda sana kumuangalia yule dokta😌😌❤️
basi akanambia sikuandikii dawa ila nakuandikia namba ya simu ukanitafute uniambie nikutajie jina la dawa🤣🤣🤣🤣 nikasema huyu akinito ng*za simwambii tena baba🤣🤣🤣 basi nikachukua namba 😌😌❤️❤️❤️itaendeleaaaa
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi
Maoni