MIMI SIKUACHI🥰 Sehemu ya 38
Basi mimi nilikaa home siku 3. Nikapigiwa simu ya kwenda kusaini mkataba katika iyo bank. Na kweli nilienda nikasaini mkataba wa miaka 2. Na mshahara ulikuwa ni mrefu sana . Japo siwez kuutaja apa. Si unajua nilikuwa best student so nilikuwa nagombaniwa na makampuni. So mshahara ulikuwa mkubwa. Na wakanipa na nyumba ya kampuni. Walinipa na gari. Oyaaaa acheni tu maisha aya. Basi mimi nikahama na familia yangu .kutoka kule mzumbe chuoni. Nikaamia moro mjini sasa. Ili niwe karibu na sehmu yangu ya kufanya kazi.
Nikawa nasoma na maters chuoni. Na bado nikawa nafundisha vipindi vya usiku chuo. Napo mshahara unaingia. Na baada ya mwez. Nilipanua stationery yangu ikawa kubwa zaidi. Aseee maisha yalibadilika na pesa ikawa ingia nashukuru sana. Niliwahi kuishika pesa mapema tu. Japo sio kubwa ila kwangu ni kubwa mnoo. Basi maisha yakachange. Nikaenda kujifunza driving kujua kuendesha gari sasa .na baada ya miez 3. Mi nikajua fresh nimafanya na mpango wa kupata leseni nikapata .nikawa nadrive gari yangu mwenyewe. Mke wangu alipendeza sana. Alikuwa mdada wa kisasa. Na kila anachokitaka kwangu sio shida nampa.sababu naelewa tumetokea mbali sana na kanivumilia kawa mengi mnoo.
Baada ya miezi 6 . Cha kwanza nilijenga kwetu babati. Yani sikutaka masihara . Nilitaka kwnza mama na dada yangu wakae sehemu nzuri. Mana wao ndo wamenipambania sana kwenye suala zima la kusoma mpka leo mm nafika apa. Nilipo. So lazima niwakumbukea wao kwa kila kitu. Basi apo na pesa ukweni natuma sana. Yani kwa kina fatuma pia hakukuwa na shida. Yote nafanya na mke wangu afurahi . Na tuwe na amani. Basi bwana mwanangu akafikisha miaka 3. Ni kakubwa sasa kanaongea mnoo. Yani nikiludi nyumbani kanisimulia story kibao. Ni kanaongea kweli kweli. Mpaka nacheka. Mtoto wangu bwana. Nishamzoea . So hanipi shidaa. Na nilikuwa na familia yenye furaha. Sana. Maisha yakasonga na mda ukasonga . Na miaka ikakatika. Nikakuwa kiakiri na nikakomaa aswaaa .mpaka mwangu akafikisha miaka 5. Apo kalikuwa kapo nursery na apo mm na mke wangu tulianza ujenzi wa nyumba yetu . Uku uku moro mjini bwana. Sehemu moja inaitwa lukobe. Apo mm ni leacturer mzumbe. Na ni mfanya kazi wa bank uku mjini. Na tayari akili ilishapanuka nikawa nimejishikiza shikiza sehemu nyingi tu katika sector ya biashara
Apo sasa nilimwambia mke wangu .mtoto kashasogea ajiachie tu. Basi kweli . Nilikuwa nataka mtoto sasa. Mana araina sasa ni nursery na mwakani alikuwa anaanza standard one. So nilipnga apate mdogo wake mapema. Basi siku iyo nimetoka zangu job nimefika home nimechoka sana..nikaingia bafuni nikapiga maji nilipotoka mke wangu akaja kunifut maji uku.ananihadithia visa vya mwanangu nikaw anacheka sana. Mala simu yangu ikawa inaita . Mi nikaangalia aanyepiga ni bi mkubwa. Nikapokea simu. Mama akanmbia unaendeleaje baba yangu ww na familia yako. Niksema tunaendelea vizuri mama tunashukuru vp nyie na nyumbani mnaendeleaje. Mama akanmbi sie tunaendelea powa. Kuna mtu bwana uku anataka namba yako mnoo. Kila siku anakuja apa anataka namba yako . Yani ananitibua nikimuuliza ana shida gani na wewe hasemi mk nakasilika awa ni vijana wa ovyo isije kuwa wanataka kukusumbia mwanangu kukuomba ela mi sitaki bwana. Nikacheka kweli mma bwana. Nikasema mama uo ni uchoyo sasa mama angu. Ni nani kwani. Akanmbia si yule alex mtoto wa mzee mbinge. Nikasema ohhh alex. Mh nikaona mke wangu kastuka sana.
🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡🟡
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi