*MY WANGU❤️* *sehemu ya 98 na 99*
Basi bibi mie nikaanzaa safari ya kagera uo mdaa ulikuwa jioni . Nakumbuka gari ilitoka pale stand jioni saa 12. Nilikuwa na mawazo mnoo. Rahul ananiuliza mama tunaenda wapi. Namwamboa tunaenda kwa bibi na kwa babu . Mh nilikuwa na mawazo sana. Yani nilikuwa nawaza mnooo. Na mawazo yalinijaaa aswaaa . Nawaza vingi. Kwanza naludi nyumbani nipo kama chizi. Nimeishaa . Nimekondaaa mnoo. Mwili wangu sasa ni umezorota kwa mawazo. Na nimejawa na alama mwili mzima za kupigwa na mkia wa taa. Nilikuwa mnyonge sana wala sikuwa sawa. Yani sikuwa powa kabisaaa. Mpaka usiku saa 4 . Tukaingia msamvu. Apo ndo nikashuka nikae da kumnunulia chakula rahul. Nikpamda nae katika gari. Wala sokula mm. Yani sikula kabisaa. Mwanangu akalla. Nikamfunika na mbebeo yake. Na tukaendelea na safari.
Kesho yake saa 8 mchana mm ndo nashuka nyantakara. Nyieee nimeshuka mchana watu kama wote. Shoga yenu nilichukua mbebeo ya mwanangu nikajifunika mpka usoni kabisaaa yani . Ile watu wasinione.nikaanza kutembea kuelekea nyumbani. Uku nimembeba mwanangu. Naangalia mbele tu. Nakwambia . Naona aibu watu wataniona. Ila kuna baazi waliniona ila wala sikusalimia nikafika mpka nyumbani. Nikakuta mlango umefungwa na hakuna mtu . Ila dalili ya watu kuwepo niliiona nikahisi wazee watakuwa wameenda shambani Sasa mala zote mama huwa anaficha funguo chini ya kanyagio. Mi nikainua lile kanyagio pale kibalazani kweli nikakuta . Nikachukua funguo.nikafungua . Na nikaingia ndani. Mh ni miaka 5 ndo naludi nyumbani. Mh acheni tu
Basi bwana. Mie nikawa naangakia mazingira ya nyumbani. Bado kuna vitu alivyonunua mlige. Ila sofa ndo zimeanza kuchakaa. Ila ni kusafi sana na mama yangu ni msafi sana. Nikaingia mpaka chumbani kwangu. Mwanangu alichoka sana. Mi nikachukua maji nikaenda kumuogesha . Nilivyoludi nikamlaz kitandani kwangu. Hakuchukua mda akapitiwa na usingizi. Mi nikasogelea kabati langu nikawa naangalia yaaa nna nguo nikiziacha na zote alininunuliaga mlige. Nilijikuta nimekaaaa na nikaanza kulia . Moyo unaniuma snaaa. Hivi nikikutana na mlige mm namuangaliajee . Moyo unauma sanaa. Naangalia kwenye kabati naona vitu vingi kweli alivyoninunulia kipindi ikoo. Naangaliaaa mpaka begi langu la shule kipindi nasoma. Nililia sana na nikijutia sana. Yani vitu vilivyokuwa kwenye kabati ndo vilinikumbusha mbali.nilikumbuka furaha yangu kipindi nipo nae.
Nilikiwa ni mtu mwenye amani sana. Nikakuta mpka boksa zake. Kuna mda nilikuwa nikienda kwake. Nakuwa nazivaa naludi navyo. Matshirt yake yote yakikuwepo. Aseess moyo uliuma sanaaa . Nilijikuta nimekumbuka mbali. Mala nikasikia mlango wa sebleni kama umesukumwa . Nikajua ni mama sasa ndo kaludi . Basi mie nikatoka sas. Ndo namuona mama yangu. Nyie mama alinishangaaa sana nikaona machozi yanamtoka . Akanmbia faridah ndo umeisha hivyo mwanangu. Kweli wewe mkataa pema. Nyieee nilipiga magoti nikaanza kutambaaa nikimfata mama. Nikamwambia mama nisamehe mwanao.nisamehe mama. Ni majalibu tu yakinipata nisamehe mama yangu siludii. Nisamehe mama nimeshajifunza mimi. Mama alinambia faridah mm wala hujanikosea yupo uliomkosea sana ww. Ulipatwa n nn.
Mi sikumficha mama nikanza kumuahadithia maisha niliyokuwa naishi uku nalia. Asee mma mpka akawa ananifuta machozi. Akanmbia wewe ni mjinga sana faridaah . Yule baba alikupenda mnoo. Ila ukamuona mjinga . Ukababaika na watu wenye pesa zaid. Mbona ata mlige hayupo vibaya . Vihela anavyo. Ukamuona mjinga ukamuona hafai. Kisa mwarabu mwanangu ulipagawa na weupe. Umemsahau mwanaume aliyekusomesha . Amekusaidia mambo mangapi. Faridaaah nilijua lazima laana itakuludia . Baba wa watu kaja apa analia kama mtoto mpaka preshaaa. Amelazwa week nzima . Ikawa story yake tu .yaani apa. Mpaka akawa anataka kuhama na shule. Umemdhalilisha sana na kumtia aibu. Leo unadhalilika wewe faridah. Ona ulivyoisha ata tako hakuna. Umekuwa kama bibi . Yani wewe na mm mma yako mie mzuri. Zote ni tamaa faridaah na kujifanya unajua sana. Unataka vijana wenzio. Ukamuona mlige mkubwa aya kiko wapi.
Leo mwenzako kaolewa. Anatembela gari yusta. Ana maisha mazuri. Wazazi wake wanainjoy . Wewe unaludi na mtoto . Ata degree umeshindwa kumalizaa. Angalia mwenzako yusta anatembelea gali. Mlige kamfungulia maduka kibao apo balabalani yote anayasimamie yeye. Ana maisha mazuri . Kapendeza na kunenepa . We mpumbavu upo kuangaika loooh . Kiko wapi leo mwanangu . Eeeh nambie kiko wapi. Mwenzio yusta kashamzalia watoto wawili mlige. Kawapiga double double. Unahisi ni mjinga yule . Unazani haoni kama mlige mkubw . Ila mwenzio ana akiri ya maisha . Leo wazazi wake wana injoy apa kijijini . Mie nachekwa kwa ajili yako napata aibu kwa ajili yako .nadhalilika kwa ajili yako faridah. Ila nilishajishukulia sababu ww nilishakuona ni fungu la kukosa . We mtoto ni fungu la kukosa faridaah .ndo ipo hivyo.
Mimi nilibaki nalia tu. Mama aknmbia polee. Yusta mwenzio mwalimu anafundisha apo apo na mume wake. Mwnaume anapaki gari kushoto. Yeye anapaki gari kulia . Pole yakoo. Nyieeee moyo unauma . Nikawa nalia. Mama akanmbia na alivyo mwema yule baba nikikutana nae mapaka pesa ananipa mie ndo naona aibu nakataaa. Looh mtoto wewe. Leo kiko wapi mungu kakupiga kofi . Umeludi umekonda kama kuku . Muone kwanzaaa. Loooooh ata mie mama yako apa nalipa kuliko wewe. Loooh nyie mama alinichamba sana. Alinipa maneno kweli . Nilibaki kulia na majuto tu. Mala mwanangu ndo akatoka. Akja akanikumbatia . Ananifuta machozi. Mh mama akamchukua akatoka nae njee. Mi nalia jamni pale. Basi baada ya apo . Nikaingia chumbani . Na baada ya mda mama akaja . Akanmbia hongera mbegu umepata mwaya nimeenda nae dukani watu wote wanamsifia mwanao mzuri. Mh nilibaki kimyaaaa
🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi
Maoni