ππ¦ππ π π¨π¨ππ π π§ππ‘ππ *1 - - - - - 5* SEHEMU YA 1 MWANZO....... "Sitaki kuamini siku ya leo unaenda kula nyama choma kwenye lile soko la usiku.....kuna namna nahisi kama wanachoma nyama ya Mbwa..." Henry aliongea.
"Nyama ni nyama tu kikubwa iwe imeiva acha kutengeneza taharuki masikioni mwangu" Levi aliongea huku akizidisha kutembea.
"Tembea taratibu sasa lakini utake usitake Amelia ndio ameshakuwa mke wako. Nitahakikisha hamuachani yaani Mimi hapa nitawapambania kama watoto yatima vile wanaodai haki zao" Henry aliongea.
Levi alizidi kusikia hasira kuna namna alitamani kumpiga Henry lakini kwa kuwa ni Mjomba wake alivumilia.
"Amelia ni binti mrembo sana nipo radhi nipoteze macho yangu kutetea penzi lenu...." Henry alizidi kuongea, alipoona Levi hamjali aliamua kupaza sauti kabisa.
"Watuuuu, Levi ni Mume wa Amelia msikubali atembee na Dada zenu au watoto zenu... Mume wa mtu ni sumuuuuu" Henry alipaza sauti kwa nguvu zote hadi ushuzi ukampita.
Watu waliokuwa karibu yake walicheka, mbali na maneno yake ya kufurahisha sura yake iliwafurahisha pia.
Henry anakuja kushtuka akiwa pekee yake.... alianza kumtafuta Levi huku na kule bila mafanikio.
"Pata mtindi safi kwa afya yako....bei zetu ni nafuu kabisa karibu uulize bei...." Sauti hii ilisikika ndani ya soko la usiku.
Levi alisitisha kula nyama za kuchoma kuna namna alihisi kama zinanukia manyoya ya Mbwa hivi.
Aliangaza macho yake huku na kule hadi alipofanikiwa kumuona binti anayeuza mtindi.
"Karibu....karibu sana mteja wangu mzuri. Enhee nambie una kunywa hapa hapa au na kuwekea kwenye chupa ukanywe na familia yako. Hii kitu ni nzuri sana hata watoto wadogo wanakunywa ..." Isla aliongea mfulilizo bila kupumzika.
"Kama utakuwa unaongea hivi kila siku basi una kiadhibu kifua chako pamoja na mapafu....ni vyema ukiwa una zungumza taratibu" Levi alishauri kisha akavuta kiti kukaa.
Isla alishika chupa akampimia mtindi....
"Karibu, usiwe na hofu kunywa kuhusu bei tutaongea"
Levi aliachia tabasamu kimtindo kutokana na maneno anayoambiwa.
Alijikuta akinywa glass tatu.....
"Mtindi wako ni mzuri sana, mpole hongera mtu anaye tengeneza"
"Mama yangu ni kiwanda lakini Mimi ni Msambazaji....usijali nitampatia hongera zake"
"Nadaiwa shilingi ngapi?" Levi aliuliza
"Shilingi elfu kumi na tano..." Isla alizungumza uongo huku akikuna kichwa chake.
Levi aligundua binti huyu ana zungumza uongo hakutaka kumuumbua alimpatia shilingi elfu 20.
"Karibu tena....." Isla aliongea huku akiachia tabasamu.
Karibu Levi hajaongea chochote Henry alijitokeza.
"My dear usikubali maneno yake huyu nj Mume wa mtu, mke wake anaitwa Amelia" Henry alikurupuka akihisi Levi anataka kurusha nyavu....
ITAENDELEA........
SEHEMU YA 2
ENDELEA.......
Isla aliishia kukodoa macho tu hakuelewa ni kitu gani Henry ana zungumza.
"Tuondoke unazidi kuonekana kituko machoni kwa watu...." Levi aliongea kisha akaondoka.
"Huyu ni Mume wa mtu jitahidi kuziba masikio yako usije kuingia majaribuni" Henry alimsisitiza Isla kisha akamkimbila Levi.
"Nani kamuambia nahitaji Mume wa mtu? nipo hapa kupiga kazi na si kutamani Wanaume" Isla aliongea pekee yake kisha akaendelea kunadi biashara yake.
Upande wa Levi wakiwa na Henry wanafika nyumbani.
"Ulikuwa wapi" Vanessa (Mama yake Levi) aliuliza
"Kwani kuna kitu kimetokea baada ya Mimi kutoka" Levi aliuliza swali badala ya kujibu.
"Amelia yupo mezani ana kusubiria mpate chakula, nadhani unaelewa hawezi kula bila wewe"
"Hajashikwa njaa vizuri, akishikwa na njaa ilivyo hawezi kunisubiria Mimi..." Levi aliongea kisha akaelekea mezani aliko Amelia.
"Jitahidi kula bila Mimi, jitahidi kufanya vitu vingi bila Mimi. Kama unaweza kwenda haja kubwa na ndogo bila kunisubiria basi hata vitu vingine jitahidi kufanya bila kunisubiria" Levi aliongea kisha akaelekea chumbani.
Amelia alimfuata pia kwa nyuma hakuona sababu ya kula pekee yake.
Kwa pamoja walipanda kitandani kulala....vile Levi alikuwa na usingizi wa siku mbili basi alilala kama mfu.
Amelia alitumia hii nafasi kwenda jikoni, alijifungia kisha akala kama anafukuzwa hivi.
Basi aliporudi kitandani alikoroma kama chatu aliyemeza ndama.
Kulivyo pambazuka asubuhi Levi aliwahi kuamka alijiandaa kwa ajili ya kwenda kazini.
Sauti ya Mama yake pamoja na Henry zikibishana kuhusu jungu la ubwaubwa kubaki tupu zilimfanya aachie tabasamu.
Alipiga hatua taratibu kisha akawasalimia.
"Eti wewe na mkeo ndio mmekula ubwabwa uliokuwa umesalia kwenye sufuria" Henry aliuliza.
"Ndiyo...." Levi aliongea kisha akaondoka, ni Daktari Mkuu katika Hospital ya Taifa hivyo ni kawaida yake kuwahi kwa ajili ya vikao vya asubuhi.
Akiwa ndani ya gari lake alifanikiwa kumuona Isla akizungumza na simu.
Hakutaka kumjali aliendelea na safari yake
Baada ya kufika Hospitali aliendesha vikao kisha ratiba nyingine ziliendelea.
"Kuna mgonjwa analeta fujo" Mlinzi alimpatia taarifa Levi.
Basi Levi alifanya chapu kwenda kusikiliza nini kinaendelea.
Alishangaa baada ya kumuona Isla akiwa kambeba mtoto mdogo kwa haraka tu alikuwa na miaka 5
"Mnasema hamuwezi kumpatia huyu Mtoto huduma bila kufungua file? kwani hilo file kufunguliwa kwa Mtoto mdogo kama huyu niliye muokota njiani ni mpaka hela?...sina hela huyu Mtoto ni wa kwetu sote toeni pesa zenu mfukoni tumsaidie" Isla aliendelea kufoka.
Levi alisogea taratibu akamuangalia Mtoto aliyekuwa mgongoni.
Moyo wake uliumia kwa sababu alikuwa tayari kapoteza maisha. Ni vile Isla hakujua.....
ITAENDELEA.........
SEHEMU YA 3
ENDELEA......
"Naelewa ni utaratibu wa kila hospitali, ili mgonjwa ahudumiwe ni lazima afungue file. Lakini nyie kama binadamu mlipaswa kuguswa na hili, mlipaswa kuhesabu kama mnatoa msaada hivi. Hakukuwa hata na haja ya Mimi kutolewa hospitalini...." Levi aliongea kisha akamtoa mtoto mgongoni.
Isla alipoa baada ya kuona msaada unapatikana. Alimfuata Levi kwa nyuma.
"Itakuaje sasa...." Alijikuta akiuliza.
"Hakuna haja ya kufungua file tena..."
"Kwanini..."
"Nifuate nitakuambia" Levi aliongea kisha akaingia ofisini kwake, Alimlaza mtoto kisha akamgeukia Isla
"Ahsante kwa kuonesha huruma hasa kwa mtoto kama huyu ambaye hata haumfahamu....tumechelewa kidogo"
"Una maanisha nini kusema tumechelewa kidogo..."
"Huyu Mtoto kapoteza maisha wakati mna bishana na watu wa mapokezi"
Isla aliachia kibao kikachapa shavu la Levi.
"Wale watu wa mapokezi ni wauaji..... nitaondoka na huu mwili mnachotakiwa kufanya ni kuniandikia kibali"
"Umefanya kazi kubwa, sehemu iliyobakia nitamalizia Mimi unaweza kuondoka" Levi aliongea.
Basi Isla alisogea sehemu ulipo mwili wa mtoto aliyemsaidia
"Kama ungefanikiwa kuishi basi ningekufundisha namna ya kuandika na kuhesabu..... naomba unisamehe kwa hili lililokukuta. Kama utazaliwa mara ya pili basi nitakuwa Mama yako, nitahakikisha nakupa mapenzi yote unayo stahili" Isla aliongea kisha akaondoka. Levi aliumia kimtindo,
"Tuna shtumiwa kula ubwabwa uliobakia jana....hebu naomba uwaeleze tulilala njaa" Ujumbe wa Amelia uliingia kwenye simu ya Levi.
"Hivi ni Mwanamke wa aina gani hii nimeoa!" Levi alijiuliza asijue ni kitu gani anapaswa kujibu.
Basi mida ya usiku akiwa bado kazini kwake alijikuta akitamani kujua Isla anaendeleaje.
Japo ratiba ilikuwa imembana sana lakini aliondoka,
"Saa moja litatosha...." Alijisemea kisha akaondoka kama yupo hivi.
"Pata mtindi safi kwa afya yako, siku ya leo kutakuwa na punguzo kwa mtu atakaye nunua lita mbili....karibuni" Sauti ya Isla ilisikika.
"Huna haja ya kupaza sauti siku ya leo kwa sababu nitanunua mtindi wote..." Levi aliongea baada ya kumfikia.
Isla aliachia tabasamu kimtindo, siku ya leo hakuwa na mood nzuri hivyo itakuwa poa kama kweli Levi atayachukua yote.
Basi Levi aliamua kuwanunulia watu wa soko hili....hakuwa na shida na mtindi na wala hakutaka Isla ajitaabishe kwa siku ya leo.
"Sina uhakika kama umekula" Levi aliongea.
"Unataka kuninunulia chakula?...nichomee tu chips hapo mzambarauni nitashukuru sana" Isla aliongea kwa msisitizo.
Levi alifarijika kuona mtu huyu hajavurugwa kama alivyohisi.
Kwa pamoja walisogea mzambarauni.
"Mchomee chips mbili, moja weka mayai nyingine usitie chochote..." Levi aliongea
"Chips mbili? Mwanaume unalipia zote wewe?"
Levi alitikisa kichwa kuashiria ndiyo
Isla alijikuta amemkumbatia kisa chips mbili tu..........
ITAENDELEA........
SEHEMU YA 4
ENDELEA.........
Simu ya Levi ilianza kuita
"Nimepata dharula ya ghafla....hii ni pesa yako kwa ajili ya mtindi na hii ni kwa ajili ya chips utakazo chukua..."
"Mbona ni pesa nyingi sana...." Isla aliongea.
"Si pesa nyingi....hebu tuonane kwa wakati mwingine nilitoroka kazini" Levi aliongea kisha akaondoka.
"Jamaa ana roho nzuri sana huyu simjui hanijui lakini anajua kuhusu mahitaji ya watu" Isla alijisemea ndani ya moyo wake.
Basi baada ya kuchomewa chips zake aliondoka akiwa mwenye furaha.
"Hakuna haja ya kupika leo nimenunua vyakula vya kizungu...." Isla aliongea huku akimuonesha Mama yake vifuko vya chips
"Umekumbuka kumuambia huyo Mwanaume ahsante! vipi mmezungumza namna ya malipo" Mama Isla alizungumza.
"Mmmh huyu Mwanamke ana zeeka vibaya.... nimekosea kuwa mwema kwake, itapendeza akipika ugali " Isla aliongea kwa sauti ya chini kisha akaondoka na chips zote mbili.
"Huyu mtoto huyu, ni utani tu nilikuwa nafanya sielewi kwanini kachukulia vitu serious namna hiyo" Mama Isla aliongea pekee yake kisha akaelekea jikoni kupika ugali.
Upande wa Levi anarudi nyumbani mida ya saa kumi na mbili asubuhi akiwa kachoka balaa.... tofauti na kulala hakuwa akitamani kitu chochote.
"Ni siku ya saba sasa hunigusi, nakuhitaji Levi au unahisi Henry ndio ananitolea nyege zangu" Amelia aliongea, sauti yake ilikuwa ni kama kelele masikioni mwa Levi.
"Mwanaume wewe nadai haki yangu ya msingi...." Amelia alipaza sauti.
"Kiuno, mashine na korodani vyote havijiwezi....nimechoka hebu naomba uniache nilale hata kidogo..."
"Hapa huwezi kulala.... nitakuba....ka" Amelia aliongea.
Levi hakutaka kuongea chochote aliondoka akaelekea chumbani kwa Henry kulala.
"Utakujaje kulala kwenye chumba cha Mwanaume mwenzako....hebu ondoka nataka kupiga nye...to" Henry aliongea.
Levi ndio alizidi kuhisi kuvurugika kabisa... aliondoka zake akaingia kwenye gari.
Pesa haikuwa tatizo kwake aliona ni heri akalale lodge tu.
Aliuchapa usingizi mpaka saa tano asubuhi.
Wakati anatoka lodge alikutana uso kwa uso na Isla.
"Nyumbani kwangu kulikuwa na kelele na ndio maana niliamua nije kulala Lodge..." Levi alijikuta akijitetea.
"Kulala Lodge siyo dhambi na wala si kitu cha kujitetea...ni wachache sana wenye uwezo wa kulala sehemu kama hii, hakika una pesa sana wewe" Isla alimsifia Levi kisha akaendelea na safari yake.
Basi Levi alijikuta akikosa tu amani,
"Naomba tupate wote chai...." Alimpazia sauti
Isla kusikia chai alifunga breki,
"Aliko ni agiza Mama nitaenda baada ya kupata chakula..." Alijisemea ndani ya moyo wake.
Basi kwa pamoja walikaa katika Mgahawa wa Televisa kupata chai.
Kwa wakati huo huo Amelia akiwa na Vanessa (Mama yake Levi) waliingia pia kupata chai kwenye mgahawa wa Televisa.....
ITAENDELEA........
SEHEMU YA 5
ENDELEA.....
"Anataka chai ya maziwa na chapati lakini kwa namna alivyochoka itafaa kama utampatia supu ya pweza....kama haipo niambieni niingie jikoni mwenyewe nimpikie" Isla alimsemea Levi kwa Mhudumu.
Basi Levi ni kucheka kwa namna Isla anavyo mpambania.
Supu ya pweza ililetwa, kabla Levi hajaitia mdomoni Isla aliionja kidogo.
"Iko poa Mwanaume unaweza kula...."
"Ulifaa uwe Mama yangu kwa jinsi unavyo nijali najikuta namuona Mama yangu" Aliongea kwa utani.
"Mama na si mke!... vipi hujaoa bado?"
"Sina mke namaanisha bado nipo nipo kwanza ....hata mahusiano yenyewe tu sina. Nitafurahi kama utanipa company"Levi aliongea akiwa serious kidogo.
"Yaani unataka tuwe kwenye mahusiano ghafla namna hii?" Isla aliendelea kumchora maana anakumbuka vizuri siku anaambia kuwa huyu ni mume wa mtu.
"Ndiyo, kama mtu unaweza kufanya vitu vizuri sawa na Mama yangu inafaa zaidi kama utakuwa Mpenzi wangu"
"Mbwa huyu...." Sauti ya Vanessa ilisikika.
Ndipo Levi alishtuka baada ya kugundua Mama pamoja na mkewe walikuwa wakimsikiliza muda wote na mbaya zaidi walikuwa wamekaa karibu sana ni vile tu hakuwa amejua.
"Kaza moyo tuondoke..." Vanessa alimuambia Amelia.
Kwa jinsi Amelia alivyokuwa amevurugika aliondoka kwa kukimbia.
"Umejua kuniabisha mshe...nzi wewe" Vanessa aliongea kisha akatupia kipande cha sigara kwenye supu ya Levi, wala hakukaa alimkimbilia Amelia
"Kumbe una mke Mwanaume wewe? mpango wako ulikuwa ni Mimi kuchinjwa shingo si ndiyo au ulitaka nini kitokee kwangu" Isla aliuliza huku akitetemeka ni wazi kabisa alikuwa anaogopa kukutwa amekaa na Mume wa mtu.
"Naomba unisamehe..." Levi aliongea.
Isla hakutaka maelezo mengine aliondoka zake. Pamoja na Levi kumrudisha haikusaidia kitu.
Anarudi nyumbani akiwa kachoka kwa kiasi fulani. Bila sababu ya msingi alijikuta tu akiachia sonyo hasa akikumbuka uongo wa Levi.
Mida ya usiku ilipowadia aliingia kazini kama kawaida yake alianza kuitangaza biashara yake.
Ghafla tu alishtukia ana zibwa mdomo
"Huna haja ya kujinadi nitanunua mtindi wote...." Sauti ilisikika
Isla aligeuka nyuma amuone Mteja aliye mhurumia.
Alistaajabu baada ya kukutana na Levi..........
ITAENDELEA..........
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi
Maoni