*KIJIJINI KWA BIBI* *1-----5* Na Mwaisa Story Sehemu Ya 1 ___________ MWANZO ____________ "njoo uingie bado gari iko wazi hii, mama kaa vizuri hapo mnatosha
watu wawili",ilikua sauti ya mpiga
debe aliyekuwa anaita abiria katika
stendi kuu ya daladala mkoani Dodoma(Jamatini).
Ni dhahiri kabisa mpiga debe huyo alikuwa amechoka kutokana na njaa na jua kali, pia muonekano wake ulijidhirisha alivyochoshwa na maisha. Mdomon alikuwa na sigara iliyokuwa inawaka na aliipeleka mdomoni kila alipogida kipakiti cha konyagi kilichokuwa na nembo ya kichwa cha jogoo, na kila alipogida konyagi hiyo aliimeza kwa tabu huku sura yake akiwa anaikunja kama anaumia koo. Alivaa shati na suruali ya rangi ya bluu iliyopauka na zaidi suruali yenyewe aliivalia chini ya makalio na kufanya kuonekana kwa nguo yake ya ndani iliyokuwa na rangi isiyoeleweka kutokana na kuvaliwa kwa muda mrefu au kukosa maji yenye sabuni ya unga kwa muda mrefu.
Na kichwani alikuwa na kofia ya kapelo yenye picha ya mmea kwa mbele na uso wake ulipambwa na macho makubwa malegevu yenye rangi nyekundu, alikuwa na pua pana ilienea vizuri juu ya mdomo wake uliokuwa mwekundu kama umeunguzwa na kemikali au moto, na masikioni alikuwa amevaa heleni ya duara kama mtoto wa kike na miguu ilikuwa na raba nyekundu ya kupanda iliyonakshiwa na mchoro wa nyota uliozungukwa na neno lililoandikwa "allstars".
Ndani ya daladala mojawapo pale
stendi anaonekana kijana mmoja
mtanashati, ingawa sio sana ila
mpangilio wake wa mavazi na usafi
ndo vimemfanya aonekane wa kipekee kuliko vijana wengine
ndani ya ile daladala.
Mpangilio wake mzuri wa mavazi ilitosha kumjua kabisa huyo kijana ni aina ya vijana wa kileo wanaokwenda na wakati. Alikaa kiti cha nyuma kabisa cha daladala huku masikioni akiwa amevaa headfones kubwa kama mpigaji mziki wa disco.
Baada ya muda wa dakika ishirini, ile daladala ilijaa kabisa na Dereva akaiwasha na safari ikaanza.
Ilitumia mwendo wa dakika 30, ile
gari ilisimama mbele ya majengo
marefu(ghorofa) yaliokuwa
yameandikwa UNIVERSITY OF
DODOMA.
kijana akatelemka na kumlipa konda nauli kisha akashika njia iliyokuwa ikielekea kwenye ghorofa lililokuwa na rangi nyeupe, alipolifikia alipanda ngazi mpaka ghorofa ya tatu na kuingia katika chumba ambacho inaonekana anaishi humo,
'niaje kayoza,? vipi umepata body
spray ya chastity,'" wenzake ndivyo
walivomlaki namna hiyo,hakujibu
kitu akawatupia begi,
"Alafu sio ustaharabu huo, muwe mnajifunza kusalimia ndipo muulize shida zenu" Kayoza aliongea huku akitoa shati
lake akabaki na vest iliyoruhusu kifua
chake kionekane kwa ufasaha zaidi, alafu akajitupa kitandani akachua
simu yake aina ya HTC desire,
akaenda upande wa ujumbe mfupi
wa maneno ambao kulikuwa na ujumbe mfupi uliongia muda mrefu uliopita ila hakuonekana kuujali, akaona huo ndio muda wa kuangalia huo ujumbe, alipousoma aliishia kutabasamu kwa dharau huku akisikitika, kisha akaandika
"usipoteze
muda wako kunifikiria, sina mpango
wa kuwa na mahusiano ya kimapenzi
muda huu" akautuma ule ujumbe katika jina alilosevu
KICHECHE.
"Vipi umekula" Rafiki yake mmoja alimuuliza huku alivaa fulana,
"Tayari, sasa nitaendaje mjini alafu nisile?" Kayoza alijibu huku akiutupia mto chini ya kitanda,
"Poa basi, mimi ndio naenda kutafuta msosi" Rafiki yake huyo aliongea huku akifungua mlango,
"Haina noma, Acha nijipumzishe kidogo" Kayoza alijibu.
Siku iliyofuata ilikua sikukuu ya
kitaifa, kwa hyo wanafunzi wengi
hawakuwa na ratiba ya kuingia
darasani.
Kayoza alichelelewa
kuamka hiyo siku, aliamka saa nne
asubuhi, akaingia bafuni, alipomaliza
kuoga akarudi katika chumba chao, ile kuingia ndani akakunja sura
ghafla baada ya kumkuta ndani msichana ambaye hakuwa akimpenda,
"mambo kayoza", ilikua sauti ya binti mrembo ambae
anawakimbiza wanawake wenzake
kwa uzuri wa umbo na sura, alikua
katika tatu bora katika shindano la urembo lililoshirikisha vyuo vyote vilivyopo Dodoma.
Huyu binti anaitwa Stellah
Malingumu, ni msichana wa miaka ishirini na moja ambaye alikuwa mwanafunzi chuoni hapo akichukua shahada ya ualimu katika masomo ya sayansi.
"poa, umeamkaje?",Kayoza akajibu
huku akijilazmisha kujua hali ya stellah ingawa hakutaka,
"aah safi, mbona meseji yako uliyonitumia jana sikuielewa?", Stellah nae akamtupia swali,
"kwani niliiandika kwa kutumia lugha
ya kichina?", Kayoza badala ya kujibu
nae akauliza, tena kwa jeuri,
" Ok, yaishe", stellah akaamua
kukatisha mabishano,
"Samahan naomba utoke nje mimi
nataka kuvaa", kayoza akaongea kwa
ustaharabu wa kinafki,
"mimi naondoka moja kwa moja, ila
naomba jioni tukutane mjini katika
maeneo ya nyerere square", Stellah
akamwambia Kayoza,
"kuna ishu gani?, alafu jioni, si bora
ingekua mchana ningekuja",Kayoza
akajibu. ,
"usiwe na wasiwasi mpenzi, kama
unahofu njoo hata na marafiki
zako",Stellah akamalizia huku akitoa tabasamu murua.
"Mimi sio mpenzi wako Stellah, rekebisha kauli zako" Kayoza alimuonya Stellah huku akiwa amekasirika,
"Sawa, nisamehe kwa hilo. Kwa hiyo jioni utakuja ama?" Stellah aliuliza tena,
" Jioni ya saa ngapi?", Kayoza akauliza,
"Saa moja na nusu tutakua pale tunawangojea, nitakua na Tausi",
"Poa, haina noma, nitakuja", Kayoza
akakubali mwaliko. Kama angejua
"Peke yako au?" Stellah aliuliza,
"Vipi kwani, mbona maswali mengi?" Kayoza aliuliza huku akiwa amehamaki,
"Inatakiwa nijue ili nipange ratiba zangu za matumizi vizuri" Stellah alijibu kwa upole,
"We panga unavyojua wewe, maana mimi nije peke yangu au na wenzangu hayo hayakuhusu na gharama zangu au wenzangu pia hazitokuhusu" Kayoza aliongea macho yakiwa makavu,
"Basi baba, hatugombani hapa" Stellah aliongea huku akitabasamu,
"Haya nenda nje mimi nivae" Kayoza alimwambia stellah,
"Kwani ukivaa mbele yangu kuna ubaya gani?" Stellah aliuliza kwa utani,
"Wewe mpumbavu nini?" Kayoza aliongea huku akimsukumia Stellah nje na kubaki ndani peke yake akisonya kwa hasira huku akiufikiria mualiko aliopewa na Stellah..
Ila angejua ambacho kitamtokea, basi asingekubali ule mwaliko.......
******ITAENDELEA******
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi