VYOTE NDANI GONGA94
NISAMEHE MAMA SEHEMU YA: 20
Usimulizi huu ni wa watu wazima. Chukua muda wako, tulia, kisha usome kwa utulivu kama machapisho yetu yanayoendelea moja kwa moja.
SONGA NAYO.............
Nikaingia nikoni na kujifanya nasuuza glass ya maji, muda huo huo wifi akaingia
" Oooh afadhali nimekukuta , naomba nitengenezee juice ya ukwaju nataka Sasa hivi"
"Wewe mikono huna.."
"Jamani na hali yangu hi nawezaje kufanya kazi za kusimama mda mrefu au nimwambie Kaka ako"
"Hapana , hapana wifi usimwambie Kaka atanigombeza na kunifukuza usiseme wifi yangu nakuomba......chefu kaseme me kwani namuogopa kwanza in muda gani hiyo mpaka ushindwe kufanya kazi eeh ebu nikuulize una uhakika ya Kaka angu??"
Alistuka kidogo na kuniangalia usoni
" Unaongea vitu gani nawe kwanime nimeolewa na Nani ??"
"Nashangaa na Mimi uanimaindi Sana Mrs.........ju"
Huyo nikatoka nje akabaki akiniangalia , Sasa nikakumbuka kuwa Kaka kesho anatoka na ndio anasababishiwa ajali, nikatoka na kwenda duka la madawa na kununua dawa ya kumfanya mtu ahalishe hovyo hovyo nililipa pesa ndefu maana hizo dawa huwa azitolewi hivyo hovyo, nilipofika nyumbani nikaandaa chakula na kutenga mezani kwakuwa nilikuwa nikimpakulia chakula Bella na precious nikaamua nimpakulie na wifi yangu Kaka akasema
"Haya mahaba ungekuwa unampa kila siku wifi yako angenenepa kuliko wewe "
"Ndo naanza mahaba yaani kwa kaka na wifi mpaka pale nitakapopata shangazi wa pili mie nikavuta na sahani ya kaka na kumpaulia chakula hapo hapo nikamuwekea ile dawa kwani nilikuwa nimeifumba mkononi hakuna aliyekuwa anaelewa kabisa nikarudi jikoni na kunawa mikono kisha nikarudi kupata msos.
Usiku wa siku hiyo hatukulala yaani kwa jinsi Kaka alivyokuwa akiendesha yaani dakika mbili kitandani dakika mbili chooni.
Asubuhi dokta alikuja na kumuwekea dripu la maji na la nguvu na kumuomba apumzike kwa wiki Moja bila kufanya kazi yoyote.
Basi nikawa namuhudumia Kaka angu maana wifi ndio alikuwa akiigiza kuwa ujauzito unamsumbua Sana Sana nikiwa jikoni, napika chakula Cha jioni wifi alikuja na kuanza kunifangia fujo sijui alipanga Nini siku hiyo maana alifika na kuanza kunivuta nywele na Mimi kwaajili ya kujitetea nilimsukuma kwa nguvu Moja kwa Moja akaenda chini na kuangukia tumbo alipiga kelele hizo, zilimshtuka kila mtu niliogopa Sana na kumuangalia, damu zilianza kumtoka nilijua kabisa hapa mimba Basi tena.
Haraka tulimuwaisha hospital tukiwa Mimi Kaka na mama feki wa wifi yangu, toby alitaka Kuja lakini nilimkalia kwani sikuwa nikimuamini yule mama na Dickson kukaa ba Bella wangu.
Tulifika hospital na unauzito ulikuwa ushaharibika, alisafishwa na kupewa dawa kisha tukarudi nyumbani.
Asubuhi na mapema akaanza drama zingine, akiwa amepaki mabegi yake anayavuta kuyaleta sebleni Kaka akawa anamzuia
" Unaenda wapi mbona hatujagombana Nini kinaendelea jamani mama P ebu tulia tuongee "
Wote yulikusanyika sebleni na kuangalia tu
" Eti niendelee kubaki humu sijui Dada ako ndio ameshakutafutia mke mwingine ndomana Jana ameamua kumuua mwanangu "
" Unaongea kuhusu Nini wewe saada anahusika vipi"
"Kumbe ajakuambia, saada waambie Kama wewe ndio ulinisukuma jikoni "
"Lakini........",
Kabla sijamaliza kuzungumza jamani nilipewa bao Moja la uso matata Sana na Kaka Julius nilianza kuona nyota nilianza kulia lakini sio kwaajili ya kapigwa Ni kwaajili bellah anashuhudia mama yake ninavyopigwa nikamuomba Toby akawafungie watoto chumbani
"Tangu siku ile nkmerudi kutoka hospital dada ako ananiattack na kusema nazaa Sana nili nipate urithi Sasa Jana nilimfanya Nini mpaka anisukume ? Nilimwambia tu atengeneze juice ya embe akanijibu yeye sio house girl"
Mda huo Kaka amemkumbatia mkewe ambaye alikuwa akiongea uongo tu, akamuachia na kunifata tena na kunisogelea karibu zaidi na kusema
"Nikajua umebadilika kumbe bado nilikosea Sana kukusamehe, sikia Paki kilicho chako ondoka ondoka na kila kitu unachokiona Ni chako funguo zangu za dukani niachie "
Nilihisi ndoto niliumia Sana maana maneno ya kaka yalinikumbusha kuhusiana na mama na kamili nilitaka kujitetea lakini Kaka hakunipa hiyo nafasi wifi aliendelea kujiliza, mama feki akamchukua na kumtuliza kwenye Kochi niliita kwa hasira
" Toby paki kila kitu chako, "
nami nikaingia chumbani na kupaki vitu vyangu na vya Bella nikiwa na mihasira yangu nikakumbuka kuwa wifi itakuwa Kuna kitu kapanga siwezi kumuacha Kaka angu nikarudi chini na mabegi yangu na kuyaweka mlangoni na kutaka kuzungumza Tena
"Sitaki kusikia chochote kutoka kwako "
Alifoka Kaka Julius , lakini nilimfata na kumziba mdomo, nikasema utakaa kimya nikiwa naendelea kuongea ukiinua mdomo wako nafikili unanijua.
Hapo nilimkumbusha mbali maana nakumbuka nilishawai kumpiga Kaka Julius wakati tuko kwenye mahusiano enzi sa nyuma kabisa Tena nikimkanda kwelikweli.
Nikatoa simu na kuomba kila mtu awashe data video ya kwanza kuwarushia ilimuwa Ni ile ya wifi na dick wakiwa utupu wakitoka chumbani kwa kaka mpaka sebleni na mpaka maongezi yao na yule mama yao.
"Ni Nini hiki umetume, Julius nimesema dada ako ananichukia mpaka anatengeneza video za hizi Mimi nawezaje kufanya hivi na Kaka angu"
Kaka aka.....
ITAENDELEA....
Umesoma kwa utulivu Β· dakika chache tu Asante Endelea kusoma chagua hapo chini
Umependezwa ?? Asante Soma Zaidi nisamehe-mama-sehemu-ya
