VYOTE NDANI GONGA94
NISAMEHE MAMA SEHEMU YA: 23
Usimulizi huu ni wa watu wazima. Chukua muda wako, tulia, kisha usome kwa utulivu kama machapisho yetu yanayoendelea moja kwa moja.
SONGA NAYO.................
Kaka akakaa chini kwanza yaani alika chini kabisa na kunyoosha miguu Kisha akaniambia
"Kaa chini "
Nikakaa na kumuangalia kwa makini kutaka kujua anatak kusema nini, nilipokaa akaanza kunishika kichwani, shingoni na mwili kiujumla, nilibaki nikimshangaa mwisho akauliza
"Uko sawa kweli??"
"Ndio "
"Una uhakika hata kichwa akiumi, usikii joto sana au baridi ?"
"We mbona sikuelewi ??"
" Mimi ndo sikuelewi, hivi unajua nilimtafuta kamili kiasi gani Mimi ?? Nilimtafuta kamili kwenye majivu Mimi niliangaika Sana ingawa walisema ameungua na kupoteza maisha lakini sikuchoka kumtafuta nimemtafuta takribani miaka miwili sijampata wewe inakuwaje unasema kamili anaishi umemuona wapi na Kama alikuwa anaishi muda wote huo na Nani anaishije ??"
Maneno ya Julius yalinifanya nijue kuwa Mimi na mama na baba ndo tuliamini kuwa kamili kweli amekufa, nikaanza kumuelezea kila kitu nilichoambiwa na yule rafiki yangu neema, Basi kaka akasema tutajitaidi twende usiku ndo itakuwa rahisi kuwapata.
Kweli jioni tukaenda kwa mwenyekiti wa serikali za mitaa na nashukuru alikuwa yule yule niliyemuacha na hakuwa amenisahau hata kodogo, tulipokeleww vizuri na kusema kilichotuleta.
" Ni kweli kamili yupo na nilikuwa bize nafanya utaratibu wa kumuamisha kwa yule mama anamtumia vibaya kama mlivyosikia na nilikuwa nimeanza mikakati hili apelekwe kwenye kituo Cha watu walemavu, nakumbuka nilijaribu Sana kukutafuta saada lakini nilipata taarifa kuwa umefariki kwenye uzazi hata sijui hi dunia inaenda wapi, lakini pia sikuwai kujua kuwa mna mkaka mkubwa hivi "
"Ndo hivyo Kaka angu alikuwa nchi za nje uko SI unajua alipata ufadhili akaenda kulelewa hivyo amerudi na anaishi tanzani, mda mrefu tu maana hata hapa alikuwa akija kumuona mama "
"Sawa Mimi naomba mje asubuhi Sasa hivi nitampelekea barua ya wito ja asubuhi tutakuwa na kikao kifupi kwaajili yenu naomba saa mbili kamili muwe hapa.
Tukaondoka nilikuwa na furaha Sana lakini Sasa niliwaza kamili akiniona atanikubali kweli maana alikuwa ni mkubwa na alikuwa akiona kila ubaya ninaofanya ukizingatia alikuwa na akili Sana ya kukalili mambo.
Asubuhi na mapema yaani kabla ya saa mbili tayali tulikuwa mbagala kwa mwenye kiti wa mtaa yaani nakumbuka nyumbai sijui tulitoka saa tisa maana Barabara ilikuwa nyeupe kabisa, na nakumbuka mwenyekiti na familia yake waliamka na kutukuta tumepaki gari nje na tumelala Ni ajabu lakini kiukweli hatukuweza kulala usiku huo tulikuwa tunaweza kuhusu kamili tu
" Ila njaa ishaanza kuniuma ujue "
Nilimwambia Julius tukiwa ndani ya gari
"Darasa la pili D punguza kula kula unataka unenepe Ufike wapi ??"
"Umeanza "
"Sasa nimeanza Nini na nasema kweli unanenepa mno mdogo wangu fanya upungue upendezi "
Nikaona huyu ananipa somo Sasa nikatoka nje ya gari na kukaa chini ya mti majila ya saa mbili Bibi mindoli alifika pale alistuka aliponiona hakuamini Kama angeniona, pale lakini Kaka Julius alimsogelea huyo mama na kusema
"Waoooh ajabu Kama Ni wewe"
Nikamuomba atulie ingawa sikuwa naelewa anaongea kuhusu nini, Basi kikao kikaanza pale.
"Habari zenu jamani najua no asubuhi Sana lakini nimeona kikao hiki kifanyike wakati huu ili kiwai kuisha na kila mtu akaendelee na shughuli zake za utafutaji, kwanza kabisa saada na Julius naomba mtambue kuwa huyu ndo Bibi mindoli , Bibi mindoli huyu Ni sa ........."
" Nawajua tuendelee"
"Aaaah walikuja Jana na kuniambia kuwa wamepata taarifa kuwa ndugu yao Ni mzima na anaishi kwako, sikuona sababu ya kukataa ikiwa Ni kweli unaye ndugu yao, na wanamuitaji "
" Walikuwa wapi siku zote hizo? Wanajua nimemleaje ??"
Hapo Julius aliinuka kwa hasira na kumakaba yule mama kiukweli nilibaki nikishangaa tu yaani kwanini Kaka amekuwa na hasira sana tangu amemuona yule mama, tukasaidiana kumtoa asije akaua maana alimkapa kabali Moja matata
" Unazungumzika kuhusu tulikuwa wapi , unasema umetumia ghalama nyingi vipi kuhusu wewe kumtembeza barabarani kwenye jua akiomba omba kwaajili yako, mwenyekiti sikia huyu mwanamke ni mtu mzima lakini mpuuzi sana sana, Mimi sikuwai kuamini kuwa kamili amefariki lakini aliniaminisha alisema yeye ndie alimtoa mama kwenye lakini alipokuwepo kamili moto ulikuwa mkali mno alishindwa kumsaidia, lakini bado niliendelea kumtafuta akaonesha ushirikiano kuwa Yuko na Mimi , takribani miezi sita halafu Leo unaongea upuuzi gani namtaka kamili hapa laaah sivyo nitakuonesha upande wangu wa pili wa sarafu hapa sijauonesha kamili Yuko wapi "
Mwenyekiti akatuliza fujo na kumuuliza huyo Bibi
"Kamili Yuko wapi .."
"Ahahah mnafikili mtampata kirahisi mpaka nilipwe"
Nikasema kumbe huyu kabali haijamtosha nilimrukia na kuanza kumpiga hovyo hovyo watu wakanishika.
"Unapata wapi nguvu ya kunipiga we mtoto laana kabisa eeeh unapata wapi hiyo nguvu na ukuwai kumpenda kamili hata kidogo "
Muda huo huo kamili alikuwa akija kwa kusota mikononi ndio alikuwa amevaa ndala kiukweli alikuwa amekuwa mkaka kabisa jamani na kama angekuwa anasimama angekuwa na muonekano Kama wa toby hivi sema afya yake ilionekana kuzolota Sana uvumilivu ulinishinda nikamkimbilia ajabu akawa ananiogopa nikajua kabisa anakumbuka ubaya niliokuwa namfanyia lakini alifurahi Sana alipomuona Julius alikuwa akimkumbuka ingawa alimjua kwa muda mfupi tu.
"Umekuja kufanya Nini huku ??"
Aliuliza yule Bibi na kumfanya kamili aogope kabisa
"Wewe Bibi uo mdomo wako utakuponza "
Nilizungumza, kamili akaniita Dada saada
Niligeuka na kuitika Kisha kamili akamgeukia Bibi mindoli na kusema
" Si ulisema Dada saada na mama wamekufa kwaajali na nimebaki na wewe ambaye umeamua kunisaidia huyu Ni Nani ??"
Nilimgeukia Tena yule Bibi kwa hasira Nika..........
ITAENDELEA...
FORGIVE ME, MOM ππ
Umesoma kwa utulivu Β· dakika chache tu Asante Endelea kusoma chagua hapo chini
Umependezwa ?? Asante Soma Zaidi nisamehe-mama-sehemu-ya
