ð¿ðð£ððð¡ðððŠ.....: ðððð ðððð ðð ðððððð ðð ððððð ðððð (ðððð£ðð ðððªð£ð€ð£ð) ð©ðððð ðð ðºððððððð SEHEMU YA 07
Kiukweli kwa hali halisi ya maisha ni kwamba watu ambao maisha yao ni duni wanaogopaga sana kutoka na watu ambao wana maisha mazuri, hii ni kwa sababu ya kushindwa kulinganisha hadhi, hivyo basi Nasma alivyokuwa anawaza kuhusu kija Raymond aliona kama vile anapoteza muda wake.
Ray alimaliza kupiga mswaki akaenda chumbani na kuchukua taulo halafu akazama bafuni akioga âMh yaani Rose atahisi nimesusa jamani wakati ninampenda sanaâ aliwaza akiwa bafuni anajipaka sabuni taratibu. Maana tangu jana usiku alikuwa hajamtakia hali mpenzi wake wa jijini Dar aitwaye Rose.
Ray alioga haraka haraka na kuweza kurudi chumbani, muda huo bado mama yake alikuwa amelala, ila mzee alikuwa akichunga mbuzi wake mitaa ya jirani kidogo kutoka pale nyumbani.
Ray alitoka nje akiwa ananukia, hasa, halafu akasimama mlangoni na kumuangalia binti aliyekuwa anamalizia kufagia uwanja âHeeeh kakaâ Nasma alianza mazoea
âNiniâ aliuliza Ray
âUnaoga kila saa?â alimuuliza
âKawaida, nimezoea, kule Dar kulivyo na joto lazima mtu uoge mara 3 mpaka 4 kwa sikuâ
âMungu wangu ni nyingi sanaâ alisema Nasma
âVipi wewe umeoga kweli tangu jana, maana nguo zilikuwa hizo hizoâ Ray aliuliza
âHamna, nimeoga, sema tu, nguo mimi ninazo mbili tu, hii ya kufanyia kazi, ila nikishaoga navaa hiyo nyingine nzuri nzuriâ
âMungu wangu, nguo mbili? Unalipwaga mshahara?â alimuuliza
âNalipwa, ila hivyo nyumbani kuna maisha magumu, mimi ndo mtoto ninayetegemewa na wazazi mshahara wangu huwa unatumwa kwao woteâ
âpole sanaâ alisema Ray binti akatikisa kichwa na kuinama kuendelea kufagia uwanja wake âUtaratibu wa chai vipi?â aliuliza Ray
ângoja namalizia usafi halafu nitatengenezaâ alisema binti
âvitafunwa je?â aliuliza
âKuna kiporo cha makandeâ
âHahahaaaâŠ..kwa huu mjengo nilijua maisha yamebadilika lakini kumbe wapi, embu niacheni kidogo bwana mimi ngoja nikalete vitafunwa nje huko.â Alisema Ray na kurudi ndani akachukua pochi pamoja na simu yake akatoka nayo mpaka njiani.
Alitembea tembea, kutafuta sehemu yakununulia chapati au vitafunwa vingine vitramu vitramu, akaona kama vile pale kijijini hakuna, ndipo akaanza kuelekea katika duka moja kununua mkate. Kabla hajafika akasikia sauti
âWe, Raymondâ ilitokea sauti nyuma yake, akatazama, ni Elinami pamoja na Doto walikuwa na mizigo ya majani wanapeleka nyumbani.
âNaaamâ aliitika na kusimama kuwasubiri mpaka wakafika pale
âHeh, ni wewe unanukia barabara nzima jamani?â Elinami alianza kumpamba lakini Ray alimtazama kwa aibu kidogo
âkawaida mbona?â alisema Ray na kumgeukia Doto aliyekuwa pembeni mwa Elinami
âShikamooâ alisema Doto huku akimkagua kuanzia juu mpaka chini
âMarahaba wewe ni yupi tena?â aliuliza
âDotoâ alisema binti
âDoto yupiâŠ.wale niliwaacha vidonchi juzi juzi wa kwa mama Saumu?â aliuliza
ândioâ
âDuuuh mnakuwa sanaâ alisema na kumgeukia Elinami âVipi natafuta sehemu wanayouza chapati chapati ntapata kweli humu kijijini?â aliuliza
âDah, ni mbali, karibia na sokoni muleâŠ.ina maana umeshasahau mitaa hii miaka michache tu mhâ alimuuliza binti
âHamna, maisha yamebadilika, mimi kipindi natoka huku kulikuwa hamna maendeleo hivi, nyumba kama hizi hapa, zote hazikuwepoâ alisema akizungusha mikono angani kuonyesha nyumba zilizokuwa zimejaa maeneo yale
âNdo hivyo lakini, wewe nyoosha na hii barabara, utapaona kumechangamka kidogo kuna kabango kameandika Rukia Foodâ alisema Elinami
âOk powa asanteâ Ray alisema, ndipo Elinami akamkonyeza kwa style fulani kwamba watawasiliana kwenye simu, halafu jamaa aliondoka zake akiwa anatabasamu.
Alimtext Rose, Good morning babeâ alitum text kwa furaha lakini kwa bahati mbaya Rose hakujibu kabisa ile message akajua labda yuko bize na kazi yeye akaendelea na mishe zake
Kweli alifikia maeneo fulani akaona bango dogo limeandikwa Rukia Food, akatazama, akamuona mama mmoja mweusi mweusi akisukuma chapati
âShikamooâ alisilimia ikabidi yule mama atabasamu bila kuitikia salamu yake âVipi mbona unatabasamuâ aliuliza
âHahaaaâŠ..hivi Ray, wewe ni wa kunipa shikamoo mimi?â mama yule alimfahamu
âmhâŠ..mbona sijaelewa hapo kumbe najulikanaâ
âEmbu kwenda bwana,âŠ.yani mkishatoka mjini ndo zenu, mnasalimia hadi wadogo zenu, au kisa tumezeeshwa na maisha sisi?â aliuliza
âMmmmh hapana, sister sorry sijakujua fulani hiviâ
âHumkumbuki dada mkuu wako ee?â aliuliza huku akimkazia macho, ndipo Ray akakumbuka na kucheka
âHahahaaaaaaâŠâŠSawa bana, jina la Rukia likanichanganya kumbe MwanaidiâŠok sorry sana nimezeeka mpaka kumbukumbu zimeenda mbali
âAchana na mimiâ alisema huyo dada kwa jeuri, halafu akainuka âEmbu nipe zawadi yangu kutoka huko mjini, au ndo umemletea mama yako peke yakeâ alisema mwanamke yule
âHamna cha zawadi wala nini, sikia, nifungie chapati 3 mara 4, nikale raha mimiâ alisema Ray
âMh yaani chapati kumi na mbili?â aliuliza mwanaidi
âYaaapâ Ray alisema na kutoa noti ya 5000 kwenye pochi akamkabidhi, na yule dada alifanya hivyo âShilingi ngapi inakuwaâ aliuliza
â3600â alisema huyo dada maana chapati moja ilikuwa sh 300 tu
âOk iliyobaki kunywa sodaâ
âHayo ndo maneno, lakini kabla ya yote uoeeâ alisema mama huyo
Wote walibaki wakicheka huku akizidi kumuwekea chapati kwenye gazet. Akiwa anasubiri chapati pale ziwekwe vizuri, Doto alitokea akikimbia na kusimama pale, akamtazama Ray na kumuongelesha kwa sauti ndogo âUnisubiriâ alisema hivyo ili muuzaji asielewe kinachoendelea
Hata hivyo mwanamke huyo alimaliza akamuwekea vizuri na kumkabidhi Ray, wakaagana Ray aliondoka kwa mwendo wa taratibu huku akimsubiri Doto taratibu alikuwa anataka asikie kwamba ataambiwa nini
âDoto leo umekujua huku?âaliuliza
âNdio,naomba unipe chapati mbili haraka ninawahiâ alisema Doto
âsasa mbona kuna moja tu imebaki hizo zingine ni za kusubiriâ alisema mwanaidi
âBasi nipe hiyo hiyo, inatoshaâ aliongea kama vile ni mtu anawahi sana, kumbe alichokuwa anawahi ni kwenda kuongea na Ray.
ð¿ðð£ððð¡ðððŠ.....: ðððð ðððð ðð ðððððð ðð ððððð ðððð
(ðððð£ðð ðððªð£ð€ð£ð)
ð©ðððð ðð ðºððððððð
SEHEMU YA 08
Alipatiwa chapati moja na kuondoka akikimbia akamuwahi Ray, huku akicheka na kuhema sana
âWe kaka, shikamooâ alimuamkia
âKila saa??â Ray aliuliza
âHamna jamaniâŠsi lazima nikuamkie kila saa kukuheshimu au hupendi?â aliuliza
âOk marahaba, shule vipi?â Ray alijifanya kukaza asijeonekana mrahisi
âShule nzuri, naona umeamua kuja kututembelea huku kijijiniâ alisema
âHahaaâŠ.nimekimbia maisha magumu Dar weweâ alisema Ray
âMmmh muongo, maisha magumu upendeze hivi?â aliuliza dotto
Ray alicheka kisha akamuambia âBy the way sitakaa sana, nitaondoka siku sio nyingiâ
âUnawahi nini? Au ndo wifi? Eeh naona, ila sawa kweli hawezi kuwa wifiâ alisema mtoto huyo aliyekuwa na uchangamfu uliozidi kipimo
âKwanini asiwe wifi?â Ray aliuliza
âHahaa.. wanaume wa Dar hizo mambo mh, kwani mnakuwaga nazo?â alimuuliza ikabidi Ray asimame na kumshangaa kidogo
âHiv wewe ni Doto au nakufananisha, mbona unaongea sana?â alimuuliza âMtoto wa juzi una maneno mengi hivi, kwanza wewe una miaka mingapi?â aliuliza
âkumi na sabaâ
âKumi na saba ndo uongee hivyo?â embu acha mambo yako, nambie kwanza mambo mazuri mazuri
âMazuri ni yapi kaka? Embu kwanza, kwani hayo niliyoongea sio mazuri? Mbona jamani watu wanayangâangâania wanasema ni matramuâ
âShitâŠâŠâŠ. DotoâŠ.kimbia uende nyumbaniâ alisema Rayâ
âHaya sawa, basi nipe namba yako kakaâ
âElinami anayo kamuombeâ alisema Ray
âPoa byeâ
Binti alianza kukimbia mpaka akaenda nyumbani kwa Elinami huku akiwa ameificha chapati ili Elinami asishtuke kwamba alimfukuzia Raymond kule kibandani.
âEliiiâ alimuita mwenzake
âNini dogo?â alimwambia kwa kejeli
âUna message unisaidie nimtumie mtu?â aliuliza binti
Elinami alitoka na simu mkononi kisha akampatia binti mkononi âzipo chacheâ alisema na kuingia ndani kwake alikuwa anafanya fanya usafi kidogo
Kumbe ili ilikuwa ni gia ya binti kuiba namba ya Ray alitaka anagalao aibe namba ya Ray kwenye simu ya Elinami, hata hivyo bahati kama bahati ni kwamba Elinami alikuwa amesevu namba ya Ray hivyo hivyo kwa jina la Ray hivyo basi haikumpa taabu kuipata na kuiiba akaweka kwenye kisimu chake kidogo lakini kalikuwa ka-smartphone ka Samsung ambako ni version ya zamani halafu akamuita Elinami
âShogaaaâ alimuita âMi naenda kufua simu yako niweke hapa?â alimuambia
âNyooo, uweke simu yangu hapo? Je wakiibaâ alisema mtoto wa kike huku akitoka ndani na kuipokea simu yake
âAsante eeâ alisema Doto halafu akakimbia kuelekea nyumbani alipofika nyumbani hivi alikunywa kwanza chai na ile chapati yake
*
Upande wa Ray yeye muda huo alikuwa yuko mezani anakunywa chai na mama yake baba bado alikuwa anachungua mbuzi na kondoo wake, Ray alikula chapati mbili halafu akawa hoi na kuachana nazo halafu akatoka nje ya nyumba akamkuta Nasma akiwa ameketi kwenye ndoo akabaki anamshangaa
âHivi wewe mbona hauna raha muda wote?â alimuuliza
âSamahani kaka, ndo hivi nilivyo mimi nina raha sanaâ
âHaya kale chapati huko ndani halafu leo kwani una kazi ngumu sana?â alimuuliza
âhapana ninafua nguo za baba na mama, halafu nitapikaâ alimuambia
âOk basi, wewe nenda kanywe chai pale kuna chapati, ukishamaliza oga vizuri nikuone na nguo nyingine hiyo ni chafu sanaâ aliongea akimnyooshea kidole maana alijua uchafu tu ndo kilichokuwa kinamponza mpaka wazazi wakawa wanamdharau
âSawa kakaâŠ.nilikuwa na mpango huo piaâ alijitetea baada ya kuhisi amedharaulika.
âSio kwamba nimesema hauogagi lakini nimekuambia uvae nyingine, wewe mbona mzuri ukiwa kila saa msafi basi utavutia saaanaaâŠhujioni ulivyo mweupe?â alimuuliza, Nasma alitabasamu kwa furaha kwani mwanamke anapenda kusifiwa sana
Alitazama chini kichwa mwake wakiwa anawaza kwamba mh kanipenda au? Lakini ni kwamba jamaa alikuwa anamsaidia tu kimawazo, sio mapenzi.
Hata hivyo baada ya maneno hayo, Ray aliondoka akaenda mpaka pale baba yake alipokuwa anachunga mbuzi âMzee umeamkaje?â alimsalimia
âsalama umeamkaje wewe?â alimuuliza
âsijambo, emb niachie mbuzi hapa ukanywe chai kidogoâ alisema Ray na kusogea kwenye jiwe akaketi
âHuh, kuna chai na nini viporo mimi sili bwanaâ alisema
âHahaha, mzee unaringa⊠kule nimeleta chapati za kutoshaâ alisema kijana huyo
âHapo sawaâ mzee alisema akitabasamu na kuanza kuondoka kuelekea nyumbani.
Sasa alipomuacha Ray pale na mbuzi Ray alipata muda wa kupiga selfie za kutosha, halafu aliwatumia marafiki zake aliokuwa akifanya nao kazi huko jijini Dar.
Lakini pia alimtumia Rose na kuweka captions âUkwen kuko hivi utakuja kweli wewe mtoto mayai?â alisema na kumtumia, akaona imefika na kusomwa tayari, lakini haikujibiwa ikabidi ampigie simu aelewe labda ni ubize ama
âhallow Roseâ aliongea baada ya binti kupokea simu
âUsiniite tafadhali niache na maisha yanguâ Rose aliongea kwa hasira na kukata simu
Hilo suala lilimpa taabu sana Ray maana alimpenda yule mwanamke japo alikuwa akimsaliti mara kwa mara. Alimpigia simu tena na binti hakupokea simu kabisa ikabidi jamaa abaki akicheka maana hakuelewa kosa lake liko wapi âni hasira kisa sijamtafuta asubuhi atakuwa powa tuâ alijisemea Ray na kuchukua jiwe akamrushia kondoo aliyetaka kuondoka eneo lile.
Baada ya kumrushia jiwe, alisikia ujumbe umetumwa akaufungua ni namba mpya
âHello, uko pouwa?â
âNiko powa, nani?â alimuuliza
âMi Doto, ingia WhatsApp kuna kitu nimekutumiaâ alisema Doto
âOkâ Ray alijibu na kuingia WhatsApp moja kwa moja, alipongia hivi aliona ametumiwa ujumbe na Doto, akaingia kwenye msururu, alichokiona kutoka kwa Doto wala hakuaminiâŠâŠâŠâŠ..JE KAONA NINI?
Soma muendelezo kwa sh 1000
Njoo WhatsApp 0743433005
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi
Maoni