VYOTE NDANI GONGA94
πΏππ£πππ‘πππ¦.....: ππππ ππππ ππ ππππππ ππ πππππ ππππ (ππππ£ππ πππͺπ£π€π£π) π©ππππ ππ πΊπππππππ SEHEMU YA 07
Usimulizi huu ni wa watu wazima. Chukua muda wako, tulia, kisha usome kwa utulivu kama machapisho yetu yanayoendelea moja kwa moja.
Kiukweli kwa hali halisi ya maisha ni kwamba watu ambao maisha yao ni duni wanaogopaga sana kutoka na watu ambao wana maisha mazuri, hii ni kwa sababu ya kushindwa kulinganisha hadhi, hivyo basi Nasma alivyokuwa anawaza kuhusu kija Raymond aliona kama vile anapoteza muda wake.
Ray alimaliza kupiga mswaki akaenda chumbani na kuchukua taulo halafu akazama bafuni akioga βMh yaani Rose atahisi nimesusa jamani wakati ninampenda sanaβ aliwaza akiwa bafuni anajipaka sabuni taratibu. Maana tangu jana usiku alikuwa hajamtakia hali mpenzi wake wa jijini Dar aitwaye Rose.
Ray alioga haraka haraka na kuweza kurudi chumbani, muda huo bado mama yake alikuwa amelala, ila mzee alikuwa akichunga mbuzi wake mitaa ya jirani kidogo kutoka pale nyumbani.
Ray alitoka nje akiwa ananukia, hasa, halafu akasimama mlangoni na kumuangalia binti aliyekuwa anamalizia kufagia uwanja βHeeeh kakaβ Nasma alianza mazoea
βNiniβ aliuliza Ray
βUnaoga kila saa?β alimuuliza
βKawaida, nimezoea, kule Dar kulivyo na joto lazima mtu uoge mara 3 mpaka 4 kwa sikuβ
βMungu wangu ni nyingi sanaβ alisema Nasma
βVipi wewe umeoga kweli tangu jana, maana nguo zilikuwa hizo hizoβ Ray aliuliza
βHamna, nimeoga, sema tu, nguo mimi ninazo mbili tu, hii ya kufanyia kazi, ila nikishaoga navaa hiyo nyingine nzuri nzuriβ
βMungu wangu, nguo mbili? Unalipwaga mshahara?β alimuuliza
βNalipwa, ila hivyo nyumbani kuna maisha magumu, mimi ndo mtoto ninayetegemewa na wazazi mshahara wangu huwa unatumwa kwao woteβ
βpole sanaβ alisema Ray binti akatikisa kichwa na kuinama kuendelea kufagia uwanja wake βUtaratibu wa chai vipi?β aliuliza Ray
βngoja namalizia usafi halafu nitatengenezaβ alisema binti
βvitafunwa je?β aliuliza
βKuna kiporo cha makandeβ
βHahahaaaβ¦..kwa huu mjengo nilijua maisha yamebadilika lakini kumbe wapi, embu niacheni kidogo bwana mimi ngoja nikalete vitafunwa nje huko.β Alisema Ray na kurudi ndani akachukua pochi pamoja na simu yake akatoka nayo mpaka njiani.
Alitembea tembea, kutafuta sehemu yakununulia chapati au vitafunwa vingine vitramu vitramu, akaona kama vile pale kijijini hakuna, ndipo akaanza kuelekea katika duka moja kununua mkate. Kabla hajafika akasikia sauti
βWe, Raymondβ ilitokea sauti nyuma yake, akatazama, ni Elinami pamoja na Doto walikuwa na mizigo ya majani wanapeleka nyumbani.
βNaaamβ aliitika na kusimama kuwasubiri mpaka wakafika pale
βHeh, ni wewe unanukia barabara nzima jamani?β Elinami alianza kumpamba lakini Ray alimtazama kwa aibu kidogo
βkawaida mbona?β alisema Ray na kumgeukia Doto aliyekuwa pembeni mwa Elinami
βShikamooβ alisema Doto huku akimkagua kuanzia juu mpaka chini
βMarahaba wewe ni yupi tena?β aliuliza
βDotoβ alisema binti
βDoto yupiβ¦.wale niliwaacha vidonchi juzi juzi wa kwa mama Saumu?β aliuliza
βndioβ
βDuuuh mnakuwa sanaβ alisema na kumgeukia Elinami βVipi natafuta sehemu wanayouza chapati chapati ntapata kweli humu kijijini?β aliuliza
βDah, ni mbali, karibia na sokoni muleβ¦.ina maana umeshasahau mitaa hii miaka michache tu mhβ alimuuliza binti
βHamna, maisha yamebadilika, mimi kipindi natoka huku kulikuwa hamna maendeleo hivi, nyumba kama hizi hapa, zote hazikuwepoβ alisema akizungusha mikono angani kuonyesha nyumba zilizokuwa zimejaa maeneo yale
βNdo hivyo lakini, wewe nyoosha na hii barabara, utapaona kumechangamka kidogo kuna kabango kameandika Rukia Foodβ alisema Elinami
βOk powa asanteβ Ray alisema, ndipo Elinami akamkonyeza kwa style fulani kwamba watawasiliana kwenye simu, halafu jamaa aliondoka zake akiwa anatabasamu.
Alimtext Rose, Good morning babeβ alitum text kwa furaha lakini kwa bahati mbaya Rose hakujibu kabisa ile message akajua labda yuko bize na kazi yeye akaendelea na mishe zake
Kweli alifikia maeneo fulani akaona bango dogo limeandikwa Rukia Food, akatazama, akamuona mama mmoja mweusi mweusi akisukuma chapati
βShikamooβ alisilimia ikabidi yule mama atabasamu bila kuitikia salamu yake βVipi mbona unatabasamuβ aliuliza
βHahaaaβ¦..hivi Ray, wewe ni wa kunipa shikamoo mimi?β mama yule alimfahamu
βmhβ¦..mbona sijaelewa hapo kumbe najulikanaβ
βEmbu kwenda bwana,β¦.yani mkishatoka mjini ndo zenu, mnasalimia hadi wadogo zenu, au kisa tumezeeshwa na maisha sisi?β aliuliza
βMmmmh hapana, sister sorry sijakujua fulani hiviβ
βHumkumbuki dada mkuu wako ee?β aliuliza huku akimkazia macho, ndipo Ray akakumbuka na kucheka
βHahahaaaaaaβ¦β¦Sawa bana, jina la Rukia likanichanganya kumbe Mwanaidiβ¦ok sorry sana nimezeeka mpaka kumbukumbu zimeenda mbali
βAchana na mimiβ alisema huyo dada kwa jeuri, halafu akainuka βEmbu nipe zawadi yangu kutoka huko mjini, au ndo umemletea mama yako peke yakeβ alisema mwanamke yule
βHamna cha zawadi wala nini, sikia, nifungie chapati 3 mara 4, nikale raha mimiβ alisema Ray
βMh yaani chapati kumi na mbili?β aliuliza mwanaidi
βYaaapβ Ray alisema na kutoa noti ya 5000 kwenye pochi akamkabidhi, na yule dada alifanya hivyo βShilingi ngapi inakuwaβ aliuliza
β3600β alisema huyo dada maana chapati moja ilikuwa sh 300 tu
βOk iliyobaki kunywa sodaβ
βHayo ndo maneno, lakini kabla ya yote uoeeβ alisema mama huyo
Wote walibaki wakicheka huku akizidi kumuwekea chapati kwenye gazet. Akiwa anasubiri chapati pale ziwekwe vizuri, Doto alitokea akikimbia na kusimama pale, akamtazama Ray na kumuongelesha kwa sauti ndogo βUnisubiriβ alisema hivyo ili muuzaji asielewe kinachoendelea
Hata hivyo mwanamke huyo alimaliza akamuwekea vizuri na kumkabidhi Ray, wakaagana Ray aliondoka kwa mwendo wa taratibu huku akimsubiri Doto taratibu alikuwa anataka asikie kwamba ataambiwa nini
βDoto leo umekujua huku?βaliuliza
βNdio,naomba unipe chapati mbili haraka ninawahiβ alisema Doto
βsasa mbona kuna moja tu imebaki hizo zingine ni za kusubiriβ alisema mwanaidi
βBasi nipe hiyo hiyo, inatoshaβ aliongea kama vile ni mtu anawahi sana, kumbe alichokuwa anawahi ni kwenda kuongea na Ray.
πΏππ£πππ‘πππ¦.....: ππππ ππππ ππ ππππππ ππ πππππ ππππ
(ππππ£ππ πππͺπ£π€π£π)
π©ππππ ππ πΊπππππππ
SEHEMU YA 08
Alipatiwa chapati moja na kuondoka akikimbia akamuwahi Ray, huku akicheka na kuhema sana
βWe kaka, shikamooβ alimuamkia
βKila saa??β Ray aliuliza
βHamna jamaniβ¦si lazima nikuamkie kila saa kukuheshimu au hupendi?β aliuliza
βOk marahaba, shule vipi?β Ray alijifanya kukaza asijeonekana mrahisi
βShule nzuri, naona umeamua kuja kututembelea huku kijijiniβ alisema
βHahaaβ¦.nimekimbia maisha magumu Dar weweβ alisema Ray
βMmmh muongo, maisha magumu upendeze hivi?β aliuliza dotto
Ray alicheka kisha akamuambia βBy the way sitakaa sana, nitaondoka siku sio nyingiβ
βUnawahi nini? Au ndo wifi? Eeh naona, ila sawa kweli hawezi kuwa wifiβ alisema mtoto huyo aliyekuwa na uchangamfu uliozidi kipimo
βKwanini asiwe wifi?β Ray aliuliza
βHahaa.. wanaume wa Dar hizo mambo mh, kwani mnakuwaga nazo?β alimuuliza ikabidi Ray asimame na kumshangaa kidogo
βHiv wewe ni Doto au nakufananisha, mbona unaongea sana?β alimuuliza βMtoto wa juzi una maneno mengi hivi, kwanza wewe una miaka mingapi?β aliuliza
βkumi na sabaβ
βKumi na saba ndo uongee hivyo?β embu acha mambo yako, nambie kwanza mambo mazuri mazuri
βMazuri ni yapi kaka? Embu kwanza, kwani hayo niliyoongea sio mazuri? Mbona jamani watu wanayangβangβania wanasema ni matramuβ
βShitβ¦β¦β¦. Dotoβ¦.kimbia uende nyumbaniβ alisema Rayβ
βHaya sawa, basi nipe namba yako kakaβ
βElinami anayo kamuombeβ alisema Ray
βPoa byeβ
Binti alianza kukimbia mpaka akaenda nyumbani kwa Elinami huku akiwa ameificha chapati ili Elinami asishtuke kwamba alimfukuzia Raymond kule kibandani.
βEliiiβ alimuita mwenzake
βNini dogo?β alimwambia kwa kejeli
βUna message unisaidie nimtumie mtu?β aliuliza binti
Elinami alitoka na simu mkononi kisha akampatia binti mkononi βzipo chacheβ alisema na kuingia ndani kwake alikuwa anafanya fanya usafi kidogo
Kumbe ili ilikuwa ni gia ya binti kuiba namba ya Ray alitaka anagalao aibe namba ya Ray kwenye simu ya Elinami, hata hivyo bahati kama bahati ni kwamba Elinami alikuwa amesevu namba ya Ray hivyo hivyo kwa jina la Ray hivyo basi haikumpa taabu kuipata na kuiiba akaweka kwenye kisimu chake kidogo lakini kalikuwa ka-smartphone ka Samsung ambako ni version ya zamani halafu akamuita Elinami
βShogaaaβ alimuita βMi naenda kufua simu yako niweke hapa?β alimuambia
βNyooo, uweke simu yangu hapo? Je wakiibaβ alisema mtoto wa kike huku akitoka ndani na kuipokea simu yake
βAsante eeβ alisema Doto halafu akakimbia kuelekea nyumbani alipofika nyumbani hivi alikunywa kwanza chai na ile chapati yake
*
Upande wa Ray yeye muda huo alikuwa yuko mezani anakunywa chai na mama yake baba bado alikuwa anachungua mbuzi na kondoo wake, Ray alikula chapati mbili halafu akawa hoi na kuachana nazo halafu akatoka nje ya nyumba akamkuta Nasma akiwa ameketi kwenye ndoo akabaki anamshangaa
βHivi wewe mbona hauna raha muda wote?β alimuuliza
βSamahani kaka, ndo hivi nilivyo mimi nina raha sanaβ
βHaya kale chapati huko ndani halafu leo kwani una kazi ngumu sana?β alimuuliza
βhapana ninafua nguo za baba na mama, halafu nitapikaβ alimuambia
βOk basi, wewe nenda kanywe chai pale kuna chapati, ukishamaliza oga vizuri nikuone na nguo nyingine hiyo ni chafu sanaβ aliongea akimnyooshea kidole maana alijua uchafu tu ndo kilichokuwa kinamponza mpaka wazazi wakawa wanamdharau
βSawa kakaβ¦.nilikuwa na mpango huo piaβ alijitetea baada ya kuhisi amedharaulika.
βSio kwamba nimesema hauogagi lakini nimekuambia uvae nyingine, wewe mbona mzuri ukiwa kila saa msafi basi utavutia saaanaaβ¦hujioni ulivyo mweupe?β alimuuliza, Nasma alitabasamu kwa furaha kwani mwanamke anapenda kusifiwa sana
Alitazama chini kichwa mwake wakiwa anawaza kwamba mh kanipenda au? Lakini ni kwamba jamaa alikuwa anamsaidia tu kimawazo, sio mapenzi.
Hata hivyo baada ya maneno hayo, Ray aliondoka akaenda mpaka pale baba yake alipokuwa anachunga mbuzi βMzee umeamkaje?β alimsalimia
βsalama umeamkaje wewe?β alimuuliza
βsijambo, emb niachie mbuzi hapa ukanywe chai kidogoβ alisema Ray na kusogea kwenye jiwe akaketi
βHuh, kuna chai na nini viporo mimi sili bwanaβ alisema
βHahaha, mzee unaringaβ¦ kule nimeleta chapati za kutoshaβ alisema kijana huyo
βHapo sawaβ mzee alisema akitabasamu na kuanza kuondoka kuelekea nyumbani.
Sasa alipomuacha Ray pale na mbuzi Ray alipata muda wa kupiga selfie za kutosha, halafu aliwatumia marafiki zake aliokuwa akifanya nao kazi huko jijini Dar.
Lakini pia alimtumia Rose na kuweka captions βUkwen kuko hivi utakuja kweli wewe mtoto mayai?β alisema na kumtumia, akaona imefika na kusomwa tayari, lakini haikujibiwa ikabidi ampigie simu aelewe labda ni ubize ama
βhallow Roseβ aliongea baada ya binti kupokea simu
βUsiniite tafadhali niache na maisha yanguβ Rose aliongea kwa hasira na kukata simu
Hilo suala lilimpa taabu sana Ray maana alimpenda yule mwanamke japo alikuwa akimsaliti mara kwa mara. Alimpigia simu tena na binti hakupokea simu kabisa ikabidi jamaa abaki akicheka maana hakuelewa kosa lake liko wapi βni hasira kisa sijamtafuta asubuhi atakuwa powa tuβ alijisemea Ray na kuchukua jiwe akamrushia kondoo aliyetaka kuondoka eneo lile.
Baada ya kumrushia jiwe, alisikia ujumbe umetumwa akaufungua ni namba mpya
βHello, uko pouwa?β
βNiko powa, nani?β alimuuliza
βMi Doto, ingia WhatsApp kuna kitu nimekutumiaβ alisema Doto
βOkβ Ray alijibu na kuingia WhatsApp moja kwa moja, alipongia hivi aliona ametumiwa ujumbe na Doto, akaingia kwenye msururu, alichokiona kutoka kwa Doto wala hakuaminiβ¦β¦β¦β¦..JE KAONA NINI?
Soma muendelezo kwa sh 1000
Njoo WhatsApp 0743433005
Umesoma kwa utulivu Β· dakika chache tu Asante Endelea kusoma chagua hapo chini
Umependezwa ?? Asante Soma Zaidi lovestory-last-born-na-bikira-ya-house-girl-shanga-kiunoni-burudan-simulizi-sehemu-ya
πΏππ£πππ‘πππ¦.....: ππππ ππππ ππ ππππππ ππ πππππ ππππ (ππππ£ππ πππͺπ£π€π£π) π©ππππ
ππ πΊπππππππ SEHEMU YA 15
πΏππ£πππ‘πππ¦.....: ππππ ππππ ππ ππππππ ππ πππππ ππππ (ππππ£ππ πππͺπ£π€π£π) π©ππππ
ππ πΊπππππππ SEHEMU YA 12
πΏππ£πππ‘πππ¦.....: ππππ ππππ ππ ππππππ ππ πππππ ππππ (ππππ£ππ πππͺπ£π€π£π) π©ππππ
ππ πΊπππππππ SEHEMU YA 21
πΏππ£πππ‘πππ¦.....: ππππ ππππ ππ ππππππ ππ πππππ ππππ (ππππ£ππ πππͺπ£π€π£π) π©ππππ
ππ πΊπππππππ SEHEMU YA 20
πΏππ£πππ‘πππ¦.....: ππππ ππππ ππ ππππππ ππ πππππ ππππ (ππππ£ππ πππͺπ£π€π£π) π©ππππ
ππ πΊπππππππ SEHEMU YA 25