NILILETEWA MFANYAKAZI KUTOKA KIJIJINI 1--2
SEHEMU YA 1
ANZA NAYO SASA.......
Ndugu zangu, dada zangu mama zangu na watu wangu kwa ujumla kwanza kabisa nianze na funzo hasa hasa kwa hawa wanawake wanaopenda sana wadada wa kazi
Jamni sipo hapa kukufanya ujisikie vibaya au labda kuharibu kazi ya mtu, ila nipo hapa kukuambia kile ambacho kimenitokea mmi, unajua bwana unapotafuta mfanyakazi wa ndani
Unatakiwa ujue anapotokea, yani namaanisha mahali anapoishi wazazi wake, familia yake na yeye mwenyewe umjue ki undani ndio umuajiri kama mfanyakazi wako
Na sio unakurupuka kuajiri bila kujua anatokea wapi na ni mtu wa aina gani, guys mimi kama mimi naweza kusema kiherehere cha kuajiri dada wa kazi ndio kiliniponza
Kiherehere ambacho baadae nilikuja kujutia kabisa, na kuhaidi siku nyingine nijifunze kuchunguza kabla ya kukaribisha nyumbani kwangu, na nikaona sio mbaya kama nitawajuza
Na wanawake wenzangu ili na wao yasije kuwakuta kama yalivyonikuta mimi.....
jina langu kamili ni magreth lakini wengi wamezoea kuniita Maggie ikiwa ni kifupi cha jina langu, yes Maggie ndio jina ninalolikubali sana
Sasa Maggie mimi ni mwalimu wa shule za primary, ni miaka kama miwili toka niajiliwe na selikari, ukiachana na hayo nina mume na mtoto mmoja mdogo sana.
Yani ninaposema mdogo, muelewe, binti yangu ni mtoto wa miezi miwili yani bado mchanga hata mwili haujakaza vizuri, binti yangu anitwa princess.
Sasa bana ni miezi miwili toka nijifungue na ninaishi dar na familia yangu ipo huko kijijini kabisa, na kwa maisha ninayoishi na mume wangu sio ya kipato kikubwa sana
Lakini namshukuru mungu maisha yanatuendea vizuri kabisa, sasa tangu nijifungue nimekuwa nikifanya kazi mwenyewe hii ni kwa sababu ya kutokuwa na ndugu wa karibu
Wa kuja kuniangalia kipindi chote cha uzazi, so nikawa nafanya kazi hivyo hivyo ingawa nilikuwa baado sijaruhusiwa kufanya kazi, ila nilijikaza tu
Maana kama ningekaa tu ningejilemaza vibaya, so nikawa napiga kazi...
Basi siku nazo zikawa zinakimbia siku moja nilikuwa nafua fua vi nguo vya mtoto simu yangu ikaiita kwa wakati huo nilikuwa namiliki smart awee
Basi ninaichukua na kutazama mpigaji kwenye kioo cha screen, mpigaji alikuwa ni mama yangu basi nkampokelea
"Hello mama.."
"Maggie habari za huko...??"
"Salama, mama shkamoo..??"
"Marhabaa vipi hali, na mjukuu wangu anendeleaje..??"
"Naendelea vizuri ila ndio hivyo mama bado nina bleed sana sijui shida nini.."
Nilijieleza, jamani ni miezi miwili toka nijifungue lakini nina bleed tu jambo ambalo linanipa wasiwasi sana, so ikabidi nimwambie mama yangu maana yeye ni mtu mzima na hayo mambo anayajua vizuri kabisa.
"Kwani unajikanda vizuri kabisa..??"
Mama aliniuliza
"Aaah huo muda wa kujikanda nautoa wapi mama angu, maana kila muda kazi zimenibana walah..."
"Dah pole sana kama ningekuwa na nauli ya kuja ningekuja ila sasa sina na shambani mazao yamekauka natakiwa kuvuna so binti hakikisha unajikanda na maji ya moto, ili uchafu wote utoke kwani huna hata mdada wa kukusaidia kazi...??"
Mama aliniuliza
"Ah mama bwana, sasa mdada namtolea wapi harafu mdada wa kazi gani sasa..."
"Maggie saivi una majukumu mengi hapo unavyoona mtoto umuhudumie haya sijui huko shule utakuwa unaenda na mtoto, bado hujapika sijui mambo mengine utaweza kweli..."
"Kwani unataka kusemaje mama..??"
Nilimuuuliza
"Ushauri wangu tafuta mdada wa kazi awe anakusaidia mambo madogo madogo, ni hilo tu.."
"Dah sawa mama basi mume akirudi nitaongea nae kama akikubali nitalifanyia kazi mara moj.."
"Ooho sawa, msalimie na huyo mjukuu.."
"Salamu zimeshafika mama..."
"Sawa hakikisha unafanya kama nilivyokwambia yani ujikande na maji ya moto..."
"Sawa mama..."
Basi mama akakata simu, nikaendelea na kufua, lakini akili yangu ilikuwa imebadilika kabisa kila muda nikaanza kumuwaza mdada wa kazi namna atakavyokuwa ananisaidia kazi
Basi nikafanya kazi kutwa nzima, princess alikuwa amelala so hakuwa akinisumbua, basi nikafanya yale yote mama aliyoniambia nikajikanda karibia lisaa limoja then nikatoka
Majira ya usiku mume wangu aliweza kurudi kutoka huko kwenye majukumu yake, baada ya kila kitu niliweza kumwambia mume wangu kuhusu suala la kuleta dada wa kazi..
"Babe, kuna kitu nataka kukwambia.."
Nilianzisha mazungumzo
"Ni kigu gani..??"
Mume wangu aliniuliza
"Ah ni kuhusu kuleta mdada wa kazi, maana kama unavyoona hapa kazi zimenielemea sana mume wangu.."
Nililijeleza
"Wazo zuri, lakini hakikisha unakuwa makini tu.."
Alisema mume wanngu, basi upande wanngu nilikuwa nafuraha sana kuniuliza sababu ya furaha nitakujibu kuwa ni mdada wa kazi
Basi baada ya maongezi mafupi na mume wangu tuliingia kulalaa, na muda wote huo sikuwa nawaza kabisa kama mume wangu ameniambia niwe makini.....
ITAENDELEA.......
SEHEMU YA 2
SONGA NAYO SASA.......
Na hatimae siku nyingine ikashika nafasi, niliamka na kuangaza chumba chote sikumuona mume wangu nilijua tu ameenda kazini
Basi nikanyanyuka na kumuangalia princess wangu π₯° baada ya hapo nikashuka mpaka sebleni, baada ya kufika sebleni nilikuta mume wangu akiwa ameniandalia kifungua kinywa
Ni kawaida yake kila akiondoka kwenda kazini lazima anaiandalie chai mama watoto wake, ni maamuzi yake binfsi msije mkasema namtumikisha mikazi
Wala sina hiyo tabia but ni mapenzi tu aliyonayo mume wangu juu yangu, na ukiangalia kwa wakati huu kazi ambavyo zenibana so lazima anisaidie bwana.
Basi mtoto wa kike nikasogea mezani ilikuwa ni majira ya saa tatu na niliamka na njaa sana so ikabidi nipashe kwanza utumbo harafu mambo mengine yafuate
Basi nilikunywa chai pale huku nikipekua pekua simu yangu huko online, nikiwa napekua pekea ndio nikakumbuka kuhusu mdada wa kazi ikabidi nimpigie mama yangu simu kumjuza
Kweli baada ya dakika moja simu yangu ilipokelewa nikaanza kuongea na mama yangu maneno mawili matatu hivi
"Mama, mkwe wako amekubali nilete mdada wa kazi sasa hata sijui huyo mdada namtolea wapi...??"
Nilimwambia mama
"Kwamba hujui wanapotafutwa au..??"
"Aah mama sio hivyo, huo muda wa kutoka hapa na kutafuta ndio sina kabisa maana mtoto bado mdogo sana kuanza kutembea naye itakuwa hatari.."
"Basi sawa, wacha nifanye mchakato huku nikipata nitakujuza.."
Mama aliniambia
"Sawa mama..."
Basi tuliagana na mama kisha nikakata simu, na kuendelea kunywa chai baada ya kumaliza kunywa chai nilielekea chumbani kwangu na kumkuta binti yangu bado kalala
Ikabidi nimufanyie usafi hivyo hivyo na usingizi wake, basi nilimuandaa vizuri kabisa kisha nikamrudisha akaendelea kulala, kisha nikaingia jikoni na kuandaa chakula laini
Ambacho wanatumia akina mama ambao wametoka kujifungu, basi ninapika pale chakula kikaiva, ninakiweka kwa hotpot kisha nikaelekea chumbani
Kumuchungulia princess kama atakuwa ameamka, nikamkuta bwana amelala, nikachukua nguo chafu na kwenda kuzifua kwenye machine
Nililifika na kuziweka kwenye machine nikaweka na sabuni ya maji kisha nikafunika na kuondoka, nikaendelea na kazi zingine
Baada ya nusu saa nikarudi na kwenda kuzitoa nguo kweny machine nikazisuuza na maji safi nikaanika kwenye kamba, baada ya kila kitu bila kusahau usafi wa vyombo na mwili
Nilikuwa nimechoka sana hivyo niliingia chumbani kupumzika, majira ya saa nane simu yangu iliita na mpigaji alikuwa mama
Nikampokelea bila shaka alikuwa akinipa taarifa za mdada wa kazi
"Hello mama.. "
"Acha maneno mengi, huyo mfanyakazi unayemtafuta amepatikana ila anauliza mshahara ni bei gani kwa mwezi..??"
Mama aliniuliza nikafikiria kisha nikamjibu
"Mama we mwambie tu aje, but sijajua kwa saivi maana kazi za hapa sio ngumu ki vile maana kama kufua ni kutumia machine vile vile kudeki nyumba napo kwa vifaa maalumu sio kuinama kabisa, labda kwenye kuosha vyombo na kupika
Lakini napo chakula hakina ugumu wa kupika we ongea nae mwambie maisha ya huko sio kama huku ila hakikisha unamwammbia msharaha tutakuja kuongea baada ya yeye kufika huku..."
"Sawa lakini anataka kujua mshahara..."
"Eeh jamani we mwambie kuw tutakuja kuongea huku, pia kuhusu nauli ni juu yangu we ongea nae vizuri akuelewe basi.."
"Sawa mama princess..."
Basi mama akakata simu, nikashusha pumzi ndefu, walah kuna watu wagumu kuelewa kabisa, basi siku hiyo sikuwa na kazi sana maana kazi zingine alinisaidia mume wangu
Muda ulienda ilipofika saa kumi na mbili siku hii mume wangu aliwahi kurudi nyumbani, nikiwa kama mke na mama wa familia nilifanya majuku yote kwa mume wangu kwa kumuandalia chakula anachokipenda
Naona mnawaza vibaya, namaanisha chakula na sio uzinifu π maana wabongo bana dah akili zenu mnazijua wenyewe, yani nimpe na huku mnaona niko bleed kweli?? Acheni kuwaza vibaya
Basi bwana wakati yote hayo yanaendelea mume wangu alikuwa na mtoto wake anaongea ongea mengine hata hayaeleweki kabisa ili mradi tu mtoto atabasamu basi πππΎ
"Mama p umefikia wapi kuhusu mdada wa kazi.."
Nikiwa naandaa chakula mume wangu aliniuliza, ikabidi nikae kwanza kisha nikamtazama usoni na kuzungumza
"Mume wangu, nimeongea na mama na ameniambia atanitafutia binti mmoja huko kijijini, sasa ndio yupo kwenye mkakati wa kuongea bei maana leo alinipigia na kuniambia ameshapatikana
Shida ni bei gani ya kuwa tunamlipa.."
"Kwahiyo umeshamwambia bei..??"
"Hapana maana kazi za hapa sio ngumu sana so nimeona akija ndio tutaongea vizuri..."
"Sawa lakini unazijua tabia za huyo binti yani yupoje yupoje ki tabia.."
Aliniuliza mume wangu, kwa kweli hili swali lilikuwa gumu sana maana hata tabia na mienendo ya huyo binti siijui kabisa
"Ah kwa kweli sifahamu kabisa tabia zake.."
"Sawa, ila nikuambie tu mshahara utakaomlipa huyo binti ni kuanzia 30 mpaka 60, maana kama ambavyo umesema kazi sio ngumu itabidi achukue kwenye hizo pesa amabzo nimetaja so utachagua wewe achukue 40, au 50..."
Mume wangu alizungumza, nilichofanya ni kumuitikia sawa, basi nikampakulia chakula tukala pale na kwenda kupumzika,....
ITAENDELEA.....
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi
Maoni