*MCHUMBA WANGU WA UTOTONI KAWA MJEDA* *1-5* *__________________________________* *SEHEMU YA KWANZA* Siku zote Mchagua jembe siyo mkulima hiki kitendawili nakifahamu vizuri nilikiimba sana nikiwa mtoto
Sikutaka kuchagua kazi baada ya kumaliza Chuo Kikuu, degree yangu ya Ualimu haikunipa kiburi hata kidogo.
Najua mnaweza kunishangaa lakini nimefua sana nguo za masela ilimradi tu nipate chochote kitu. Nimejichanganya sana huku na kule, na hata imekuwa rahisi kwangu kufahamiana na watu wengi sana
Kama utani hivi lakini nilijikuta nikipata connection ya kufanya usafi Jeshini.
Halooooo sikutaka kujua nitalipwa shilingi ngapi, niliamini pindi nitakapofika huko kila kitu kitaenda sawa
Niliamini huenda huu ndio utakuwa mwanzo wa mafanikio yangu
Vigezo na masharti kuzingatiwa, nilipofika jeshini nilionesha vyeti vyangu Ufahulu wangu haukuwa mbaya wala mzuri sana.
Si unajua tena hii kazi nimeipata kwa connection basi kila kitu kilienda hivyo hivyo.
Kazi yangu Mimi ilikuwa ni kufua magwanda ya Kijeda.
Nguo za hawa viumbe hazifuliwi kiholela. Hivyo nilipatiwa mafunzo kwa wiki moja, sikuwa pekee yangu tulikuwa watu 45 ila wengi walukuwa na uzoefu tayari
Baada ya wiki moja la mafunzo kuisha tulianza kazi rasmi. Jeshi lina mambo ya mchaka mchaka nilisahau hata mambo ya make-up....wala saluni. Ilikuwa ni mwendo wa kipara tu. Vile na sura ya Baba sasa ilikuwa ni changamoto kuniita demu au manzi
Niwarudishe nyuma kidogo, enzi hizo niko kidato cha nne nilikuwaga na mahusiano па mwanafunzi mwenzangu....alikuwa mkorofi sana lakini kilaza aliyeshindikana. Yaani hata usomaji wake haukuwa na tofauti na ule wa mtoto wa darasa la kwanza
Mara nyingi alikuwa anapendelea kunyoa upara hadi tukambatiza jina la Mjeda Omary. Basi kwa kuwa nilikuwa demu wake sikuitwa Norah tena isipokuwa mke wa Mjeda
Baada ya kumaliza kidato cha nne kila mmoja alishika hamsini zake. Nilifahulu kwenda kidato cha tano lakini Omary alifeli, wala hata sikujuaga alifika wapi
"Norah......" Asubuhi moja nikiwa naelekea. kantini kupata chakula niliitwa
Niligeuka kwa haraka nimuone mtu anayeniita.
Mmmmh nilijikuta ni kikodoa macho tu baada ya kumuona Omary kilaza, mchumba wangu wa utotoni akiwa kavalia gwanda la Kijeda
Alipiga hatua kama tano hivi akanifikia
"Mchumba ni wewe Omary aliongea huku akiachia tabasamu, bado nilikuwa nimetekewa aisee alikusanya mikono yake miwili akanishika mabega yote
"Ni...ni...ni... Mimi.." Niliongea huku ni kitazama pete aliyokuwa amevaa kidoleni mwake kumaanisha ni Mume wa mtu
"Kaptein simu inaita Mjeda mmoja aliyekuwa kaambatana naye alizungumza
Eti Kaptein yaani huyu kilaza siyo tu Mjeda wa kawaida bali ni Kaptein? kwani jeshi linataka watu wenye nguvu au ufahulu mzuri??
Basi mie huyu tena sikutaka kuchunguza sana wakati nipo hapa kwa connection pia. Kwa kuwa Omary alikuwa bize kuzungumza na simu sikutaka kusimama nilitega mgongo niendelee na safari yangu lakini nilisubirishwa kwa lugha ngumu
"Wee k*ma unaondokaje bila Kaptein kukuruhusu...." Sauti ya Mjeda aliyeambatana na Omary ilinishtua
Itaendelea
Chapter 2
Basi nilisimama mpaka pale Omary alipomaliza kuongea na simu
"Norah mbona una haraka namna hiyo....nipe
namba zako tutakuwa tuna wasiliana" Aliniambia huku akinipatia simu yake nijaze namba
Nyie watu acheni tu kuna wale wanaomiliki kifaa cha mawasiliano halafu kuna wengine wanamiliki simu. Miongoni mwa watu wanaomiliki simu Omary ni mmoja wao
Niliandika namba zangu chapu chapu kisha ni kampatia.
Alifanya kama ana bipu hivi simu ikaita
"Namba yangu hiyo, baadae Omary aliongea kisha akaondoka na mwenzie
Nilimsindikiza kwa macho mpaka akatoweka kwenye upeo wa macho yangu.
Kuna wale wanao fanikiwa kwa kupita njia fupi, na kuna wale wanao fanikiwa kwa kupita njia ndefu. Sikutarajia kama Omary kilaza anaweza kufanikiwa mapema kabla yangu
Niliachana na hizi mambo, nilielekea kantini kupata chakula.
Sijui nasumbuliwa na umbeya au nini nilishindwa kuvumilia. Nilishika simu nikampigia Rafiki yangu Mage. Sikuwa tayari kukabwa na maajabu niliyoyaona kwa Omary
"Weee mbwa, unamkumbuka Mjeda kipara tuliyosoma naye kidato cha nne kwa sauti ya chini Niliongea
"Una muongelea bwana Omary shemeji yetu yule Mjeda kilaza"
"Huyo huyo
"Kapatwa na nini
"Si nilikuambia nimepata nafasi ya kufua magwanda ya Kijeda? basi kambi niliyopo Mimi na Omary yupo
"Yupo kufanyaje? ni mshona buti za Kijeda au ni mkata nyasi
"Hapana, ni Kaptein Mbwa wewe....najua huwezi kuamini lakini huo ndio ukweli wenyewe
"Unajua Mimi huwa sipendi utani, yaani yule
Omary ambaye kusoma yake ilikuwa ni kama tetemeko ni Kaptein? kama ni kweli Wallahi natembea uchi. Mimi hapa na degree yangu ya Uchumi sina kazi leo Omary Kilaza yupo Jeshini ana amrisha watu. Aisee muambie makalio yake "Mage aliongea kisha akakata simu
Nilijikuta ni kicheka, bila shaka alichukizwa na nguvu ya connection
Baada ya kumaliza zangu kunywa chai, nilielekea eneo langu la kazi.
Nashukuru watu niliopangwa nao hii wiki si wavivu, nilikuta wamemaliza kila kitu
Nilitarajia Omary atanitafuta lakini haikuwa hivyo.
Huwezi kuamini wiki mbili zilipita bila kunitafuta, nami sikutaka kujipendekeza ukizingatia mtu mwenyewe ni Mume wa mtu
Jumamosi moja nikiwa naanika vinguo vyangu kwenye kamba, nilishtuka baada ya kuhisi kama napulizwa sikioni. Niligeuka chapu ee bhana ee nilikutana na uso wa Omary
"Pole kwa kukushtua
"Watu wengine tuna presha bhana acha hiyo michezo
"Presha umeitoa wapi wewe na huku kipindi tunamaliza kidato cha nne ulikuwa mzima kabisa"
"Ni muda sasa tangu turmalize kidato cha nne, hapa kati kati nimepigwa na maisha nina uhakika nina presha" Niliongea huku ni kipambana kuanika boksa yangu
Nilishangaa tu Omary kanikwapua akaanika mwenyewe.
"Mpaka leo bado unavaa boksa ya saizi hii hakika haunenepi Omary aliongea
Sikutaka kuchangia chochote, kosa moja dogo tu naweza kumkaribisha shetani
"Ulitakiwa kuwa darasani na siyo hapa, endapo zitatoka nafasi za Ualimu nikumbushe Omary aliongea
Basi moyo wangu ulilipuka kujua Omary. anaweza kunifanyia connection
"Vipi huamini kama naweza kukufanyia hivyo,
"Naamini ni vile nimeshtuka Nilijiongelesha
"Ulivyo kuwa kidato cha nne ulikuwa mrembo sana ila kwa sasa umekuwa na sura tofauti sana "
"Nimekuaje"
"Umekuwa mbaya.
Chapter 3
"Yaani umekuwa mbaya halafu umekuwa na nguvu kama Samson wa Delila"
"Hebu ondoka zako sielewi hata hii kazi umeipataje. Vipi sasa hivi unajua kusoma vizuri bila kubabaika" Nilimuuliza
"Mpaka Kiarabu naongea, maisha hayana formula mchumba, darasa zima mlikuwa mnajua kusoma na kuandika pekee yangu tu nilikuwa natia huruma.....lakini naweza sema kwa sasa nimewaacha wote mbali"
"Sawa Mwanaume, naomba uondoke nahitaji kwenda kuoga, pia msalimie mkeo naweza kuiona pete kwenye kidole chako
"Tabia yako ya umbeya hujaiacha bado, sikutarajia kama ungeweza kuiona pete kwa urahisi namna hii bila kuobeshwa nimefurahi kukuona tutaendelea anyway kuonana" Omary aliongea akataka kuondoka lakini nilimsubirisha
"Naomba hela, sitarajii uninyime"
"Hela?....umeifanyia kazi ipi?...pamoja na kuwa mbaya tofauti na zamani umekuwa na katabia kakuomba pesa. Hivi unapata wapi ujasiri wa kumuomba pesa Mwanaume ilihali yeye hajakuomba chochote Kaptein Omary aliongea na kunifanya nione aibu
Sijui hata aliondoka saa ngapi lakini nilitamani niingie chini ya ardhi niligeuka huku na kule kuhakikisha hamna mtu aliyesikia. Nilijisikia amani kupita kiasi baada ya kugundua hamna mtu mwingine
"Kuanzia leo sitaki kabisa mazoea na huyu mtu, kawa na majibu magumu sana" Nilijiambia ndani ya moyo wangu kisha ni katoa vyombo nilivyokuwa nafulia
Siku zilikatika kama nne hivi bila kumtia machoni Omary, basi kuna Mjeda wa kike mrembo balaa yaani pamoja na kunyoa upara alikuwa mrembo sana. Ile anapita tu niliona watu wananong'ona. Sikutakar kupitwa na huu umbeya nilijisogeza karibu yao
"Yaani huyu demu ni kama kamuwekea Kaptein madawa ya kulevya. Chochote anachotaka anapatiwa ipo siku ataomba roho zetu na atapatiwa Mmbeya aliongea
"Si kaoa lakini au ni umalaya tu"
"Fimbo ya mbali haiui nyoka wala mende kwani hulijui hilo"
Mmmmh kabla sijajibu chochote Kaptein mwenyewe alipita basi tulifyata midomo yetu.
Nilijikuta nakuwa na hasira ghafla, yaani nilijiona kama nimemaliza kidato cha nne jana, nilihisi kama Omary kanidharau baada ya kujipata....
Nilichukua kioo ni kajitazama uso wangu, kama utani hivi lakini nilijiona mbaya eti nilishindwa kuelewa ni kwa sababu nimenyoa au ni nini
Nilikirudisha kioo kisha ni kaelekea mahali zilipoanikwa gwanda za Kijeda, nilianza kuanua moja baada ya nyingine. Sikuwa pekee yangu, nilishirikiana na watu watano.
Sijui kilitokea nini, kila gwanda nililoshika nianue lilianualiwa na mtu aliyekuwa nyuma yangu. Sikuwa na mood ya kucheza na hata sikuelewa ni nani huyo anataka kucheza na Mimi
"Oyaa sitaki ujinga Nilifoka kisha ni kageuka. Nilipoa kidogo baada ya kukutana na Omary. Sikuelewa hata ni lini na saa ngapi kawa mrefu namna hii kuliko hata Mimi.
Tulijikuta tumetazamana tu bila sababu ya msingi
Itaendelea
Chapter 4
"Uzuri wa macho yako tu ndio hujabadilika nahisi ndio yalinivuta kwa kipindi hicho hadi ni kakuandikia barua Kaptein Omary alijichekesha
'Kuna kitu nilikuwa natamani sana kukuambia, kwa kuwa umeanzisha mwenyewe hizi stori acha nipitie hapo hapo" Niliongea kisha nikaweka kapu la nguo chini
Omary alikaa kwa umakini kunisikiliza
'Enzi zile ulikuwa ni utoto, ni aibu hatal kuzungumza mbele za watu.... tulikuwa hatujui kuoga wala kuvuana nguo, kwa kifupi hata kuikatikia tu ilikuwa ni Mtihani. Hivyo sifurahishwi na namna unavyokuwa una kumbushia Niliongea
"Hapana hatukuwa watoto, na kumbuka nilikuwa naweza hata kukufikisha kileleni, unawezaje kusema tulikuwa watoto
Kabla sijamjibu yule Mjeda wa kike mrembo anayesemekana kuwa na uhusiano na Omary alipita karibu yetu
"Aiseee Kaptein wadada wembamba watakuua, yaani kila mdada mwembamba akipita mbele yako inasimama si ndiyo eeeh"
'Nachanganywa na Mdada mwenye vigezo kama vyako, yaani kitendo tu cha kupita mbele yangu tayari imesimama twende zetu basi Pisi kali kushinda wote hapa...... Omary alimwaga sifa
Sijui hata waliondokaje nilishtuka tu nipo pekee yangu na kapu la nguo
Nyie watu kama utani hivi lakini nilishtukia tu machozi yana poromoka sikuelewa hata ni sababu ipi inanifanya ni poromoshe machozi
maana 'Vipi umefiwa au nyege wamekuzidia kuna watu tangu wafike hapa Kambini huu ni mwaka wa pili sasa hawajawahi kutongozwa, basi kila ifikapo usiku wao ni kulia tu kisa nyege Sauti ya rafiki yangu Jane ilinishtua
Basi ndio nilizidisha kulia, hakuwa mchoyo wa kutoa faraja alinisogelea kisha akanikumbatia
"Sijui nini kinakusumbua lakini kila kitu kitakuwa sawa, huna haja ya kumwaga machozi mengi namna hiyo
"Kichwa changu kinauma, fanya mpango wa kuniombea ruhusa siku mbili....lakini kabla ya ruhusa naomba niende hospitali kwanza"
'Hebu acha kukimbilia hospitali kwanza, kwanini
kila ukikutana na Kaptein Omary huwa una vurugika? vipi anakutaka au wewe ndio unamtaka Jane aliuliza
Basi nilimsimulia enzi zetu za kidato cha nne
"Hebu acha kumpa muda wako kuanzia sasa, ule ulikuwa ni utoto na si mapenzi, hata kama yeye ndio alikutoa bikira hupaswi kuliweka akilini, vipi angekuwa ni Mlinzi wa getini au muokota makopo bado ungehuzunika hivi, futa machozi tuondoke" Jane alinitia nguvu na hata kichwa changu kilipona ghafla
Mida ya usiku nikiwa nimelala, nilikuja kuamshwa eti nahitajika ofisini kwa Kaptein Omary
Sikutaka kuleta maswali, katika kambi yetu hapa Kaptein ni mtu mkubwa sana.
Basi niliingia ofisini kwake nikiwa na shauku ya kujua ni kitu gani kaniitia
'Nitumie vyeti vyako, hata kama siyo kazi ya Ualimu nitakufanyia mpango
'Kwahiyo hicho tu ndio ulitaka kuniambia hadi ukaomba niamshwe"
"Ndiyo..."
'Huna haja ya kunipambania, ingawa sijiwezi lakini nina amini juhudi zangu hizi hizi zitaniweka mahali napotaka kuwa
'Kwahiyo hutaki ni kusaidie?..."
"Siyo kunisaidia tu kuanzia leo naomba uvunge kama hunijui Niliongea huku machozi yakinilenga
Omary alitaka kunishika nilimzuia,
"Sawa sikuwa na nia mbaya na wewe....machozi
yako sielewi yana sababishwa na nini lakini kama nimekukosea au niliwahi kukosea huko nyuma naomba unisamehe sana. Nisamehe pia kwa kukuamsha, kuanzia sasa na kuendelea nitavunga kama sikujui Omary aliongea unaweza kwenda
Basi sikutaka kuongeza neno lingine niliondoka, wakati nafungua mlango nilikutana na Mjeda pisi kali anaye sadikika kutoka na Omary, alisogea pembeni kisha nikaendelea na safari yangu.
Ni ujinga au nini hiki, moyo wangu ulikuwa unauma kana kwamba nimevunja ndoa
Itaendelea
Chapter 5
Nilipoingia chumbani nilijifunika gubigubi huku machozi yakiporomoka kimya kimya.
Kulivyobpambazuka asubuhi kila mmoja alishika majukumu yake. Magwanda ya leo yalikuwa mengi hatari.
Tulifua huku tukipiga stori, mara paap walikuja Wajeda watatu
"Vichaa wanaokaa chumba namba 34 tufuateni
"Mjeda mmoja aliongea
Basi moyo wangu ulishtuka sana siyo kidogo na hata tukatazamana na Jane Tulisimama kisha tukawafuata,
"Hii mkoba ni wa nani Tulitupiwa swali mara baada ya kufika
Kijasho chembamba kilinipita kwa sababu ulikuwa ni mkoba wangu
"Nyie was*nge nauliza kwa mara ya mwisho huu ni mkoba wa nani au mpaka Kaptein mwenyewe aje kuuliza ndio mtajibu kwa urahisi??" Mjeda mweusi kuliko wote alifoka
"Ni....ni...ni...ni wa kwangu" Niliongea
"Anza kuruka kichura chura, tunaelekea kwenye ofisi ya Kiongozi wa nidhamu"
Nilianza kuruka kichura chura kuelekea kwenye ofisi ya Kiongozi wa nidhamu, acha nimkute Mjeda pisi kali ndio Kiongozi eti wa nidhamu
"Mnaweza kuondoka
"Rosemary una uhakika utamalizana naye mwenyewe Mjeda mweusi aliongea akionekana kutamani kukabidhiwa kesi ambayo hata siijui
"Hili mbona naliweza mwenyewe, ondokeni" Mjeda Rosemary aliongea
Baada ya Wengine wote kuondoka niliamriwa kukaa kwenye kiti.
"Kwenye mkoba wako tumekuta pipi zilizo tengenezwa kwa madawa ya kulevya, ni haramu sana na ni kosa la jinai....hebu naomba ujielezee kwa kifupi"
Mmmmh macho yalinitoka kwa sababu sikuwa ni kielewa kitu nachoambiwa
"Unazingua kwa sababu katika hili Kaptein Omary hawezi kufanya chochote, sijui uhusiano wenu ni upi lakini jeshi limenipa mamlaka kama Kiongozi wa nidhamu kuhakikisha kila kitu kinaenda kwenye mstari naomba uongee haraka"
"Sijui chochote, ni kweli huo ni mkoba wangu lakini.... Kabla sijamaliza chochote nilishtukia nimepigwa ngumi ya pua damu zikaruka kuleeeee
Kitendo cha kuona damu nilichanganyikiwa, ile anataka kuniongeza teke mlango ulifunguliwa. Aliingia Kaptein Omary
"Rosemary ni kitu gani hiki unafanya naondoka naye huyu andaa maelezo ya kunipatia pindi nitakapo kurudia Omary aliongea akioneshwa kukasirika
Damu ziliniogopesha hata kutembea ikawa ni mtihani. Omary mchumba wangu wa kidato cha nne aliniweka mgongoni akaniwahisha hospitali
JE NINI KITAENDELEAAA
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi